Platform show

Platform show Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Platform show, Media/News Company, bujumbura, Bujumbura.

Platform Show TV is a popular media outlet from Burundi, Available on platforms like YouTube, Instagram, and Facebook, the channel provides entertainment, sports, and social news, keeping audiences informed

10/09/2026

FINALLY! VIDEO YA “MURIHE” YA MONIA FLEUR YATOKA RASMI

Hatimaye Video mpya ya “MURIHE” ya Monia Fleur imetoka rasmi, na ni miongoni mwa kazi zilizokuwa zikisubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa muziki wa Burundi.

Kutoka kwa jina la wimbo hadi kwenye video yenyewe, Monia Fleur ameendelea kuwapa mashabiki wake sababu nyingine ya kuendelea kumfuatilia. Kutolewa kwa video hii kunakuja wakati ambapo jina la msanii huyo limekuwa likizungumziwa sana kwenye mitandao ya kijamii.

Katika siku za hivi karibuni, kulikuwa na tetesi zilizozagaa kuhusu Monia Fleur kuwa mjamzito, jambo lililozua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki na wafuasi wake.

Sasa macho na masikio yote yako kwa video ya “MURIHE” je, Monia Fleur amewapa mashabiki kile walichokuwa wakikisubiri? 👀🔥

Video imetoka rasmi. MURIHE ipo hewani!
Gusa Link kwa comment

10/09/2026

Katika mahojiano kwenye kipindi cha Chita MAGIC kilichofanyika jijini Kigali 🇷🇼, msanii Vania Ice amewapongeza wasanii wenzake akiwemo Mo'W Kanzie , Monia Fleur , Natacha Burundi na Esther Nish , kwa namna wanavyojiamini na kujituma katika kazi zao za muziki.

Vania Ice amesema anavutiwa na namna wasanii hao wanavyojiamini pamoja na bidii wanayoweka katika kazi zao, akitaja Mo'W Kanzie kuwa miongoni mwa wasanii wanaofanya kazi kwa bidii nchini Burundi.

Kwa mujibu wa Vania Ice, ni vigumu kupuuza mchango wa Mo'W Kanzie katika matukio ya muziki yanayofanyika nchini humo, kwani anaonekana kushiriki katika takribani asilimia 80 ya matukio ya muziki yanayofanyika Burundi.

Vania Ice ameongeza kuwa kujiamini, kujituma na kujitokeza katika matukio mbalimbali ni miongoni mwa mambo yanayomtofautisha Mo'W Kanzie na kumfanya aendelee kuonekana katika tasnia ya muziki.

Aidha, Vania Ice amempongeza pia Natacha Burundi, akimsifu kwa namna anavyofanya kazi zake za muziki bila kujali watu watasema nini kuhusu yeye. Amesema Natacha anaendelea kuwa sehemu ya vizazi mbalimbali vya muziki, kuanzia kizazi cha zamani hadi kizazi cha sasa.

Vania Ice pia amewapongeza Monia Fleur, Esther Nish pamoja na wasanii wengine, akisisitiza kuwa anavutiwa na namna wanavyoendelea kujituma, kujiamini na kuweka nguvu katika kazi zao za muziki.

Baada ya sakata la beef kati ya Lolilo Simba  na Big Fizzo  kuendelea kuvuma katika mitandao ya kijamii, Lolilo sasa ame...
09/09/2026

Baada ya sakata la beef kati ya Lolilo Simba na Big Fizzo kuendelea kuvuma katika mitandao ya kijamii, Lolilo sasa ameonekana kujibu kupitia muziki.

Lolilo ameachia rasmi wimbo mpya unaoitwa “ICARA WIGE”, unaoelezwa kuwa ni mwendelezo wa majibizano yake na Big Fizzo baada ya wimbo “NIRUZE” kufanya vizuri na kuibua mjadala mkubwa.

‼️ICARA WIGE ni maneno ya Kirundi yanayomaanisha “kaa chini usome”, huku Lolilo akionekana kuendeleza ujumbe wake kuelekea kwenye beef hiyo.

Wimbo huo kwa sasa tayari unapatikana YouTube, kupitia ukurasa rasmi wa Lolilo Simba.

Sikiliza “ICARA WIGE” link iko kwa comment

alafu twambiye umeskiya vipi wimbo huu je beef kweli limejibiwa kisahihi

09/09/2026

Msanii wa Tanzania, Harmonize , amejibu tuhuma zinazomkabili kuhusu madai ya kuwadharau baadhi ya raia wa Burundi 🇧🇮 baada ya video za mapokezi yake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Katika tukio hilo, Harmonize alionekana akipokea maua na busu kutoka kwa mashabiki waliokwenda kumpokea uwanja wa ndege, lakini namna alivyoitikia tukio hilo imeibua mjadala mkubwa miongoni mwa baadhi ya Waburundi.

Tukio hilo limeendelea kujadiliwa huku wasani wa Burundi Lolilo Simba na Big Fizzo wakimkosoa Harmonize hadharani, wakisema wasanii wanaotembelea Burundi wanapaswa kuonyesha heshima kwa watu wanaowapokea.

Harmonize, hata hivyo, amejibu tuhuma hizo , akieleza upande wake kuhusu kilichotokea na namna alivyopokea mapokezi hayo.

Harmonize hivi karibuni alifanya tamasha nchini Burundi, likiwemo onesho la Gitega katika Good Bye Summer Vibes lililofanyika Stade Ingoma.

Tukio la mapokezi hayo limeendelea kuzua mjadala kuhusu namna wasanii wa nje wanavyopaswa kuhusiana na mashabiki na wenyeji wanapofanya ziara nchini Burundi.

Msanii wa Burundi, Monia Fleur , ametangaza jina la wimbo wake mpya  ambao utatoka ivi karibuni utaitwa MURIHE.
08/09/2026

Msanii wa Burundi, Monia Fleur , ametangaza jina la wimbo wake mpya ambao utatoka ivi karibuni utaitwa MURIHE.

08/09/2026

Sheila Kwamboka , maarufu k**a Kwambox, ni mwanahabari na mtangazaji maarufu wa Kenya 🇰🇪 ambaye ametoa ujumbe kuhusu video zinazosambaa mtandaoni zinazodaiwa kuwaonesha baadhi ya Wakenya wakiwapiga watu wanaotajwa kuwa ni raia wa Burundi 🇧🇮 .

Kwamboka amewataka wananchi kuwa makini na taarifa hizo, akisisitiza umuhimu wa kuhakiki taarifa na vyanzo vyake kabla ya kuziamini au kuzisambaza.

Katika ujumbe wake, amesema:

‼️ In a world of disinformation and propaganda please remember to verify the information and avoid information bias.

Kwamboka ameongeza kuwa ni muhimu watu kuwa wakosoaji wa taarifa na video zinazopatikana kwenye mtandao kuhusu suala hilo, akisema simulizi hatarishi linaanza kujengeka katika jamii na linaweza kuchochea ujinga na chuki.

Amesema yeye k**a Mkenya anaweza kuwahakikishia watu kuwa Waafrika wanapendwa na wanakaribishwa nchini Kenya , huku akisisitiza umuhimu wa kudumisha upendo na umoja.

Pia amewashauri watu kuhakiki vyanzo kabla ya kusambaza na kutumia taarifa kuhusu suala hilo.

Akihitimisha ujumbe wake, Sheila Kwamboka alisema:

**“I speak as a daughter of the soil. We are Burundians.”**

Msanii maarufu wa Kenya 🇰🇪, Bien-Aime Baraza , aliyekuwa mwanachama wa kundi la Sauti Sol, ameeleza wasiwasi wake kuhusu...
07/09/2026

Msanii maarufu wa Kenya 🇰🇪, Bien-Aime Baraza , aliyekuwa mwanachama wa kundi la Sauti Sol, ameeleza wasiwasi wake kuhusu hali ya raia wa Burundi 🇧🇮 wanaoishi nchini Kenya.

Kupitia ujumbe aliouchapisha Instagram, Bien alisema: “Leo ni Mmurundi nchini Kenya, kesho ni Mkenya mahali pengine.”

Kauli hiyo imekuja wakati mamia ya Warundi wanaoishi Nairobi leo hii walionekana kwenye Ubalozi wa Burundi, wakitafuta hati na nyaraka za kuwawezesha kurejea nchini kwao

Hatua hiyo imefuatia uamuzi wa Rais wa Kenya, William Ruto, wa kukomesha biashara ndogo ndogo zinazoendeshwa na wageni. Baadhi ya Warundi wameeleza hofu kuhusu usalama wao, huku serikali ya Kenya ikisisitiza kuwa wageni wenye vibali na nyaraka halali bado wana haki ya kufanya kazi nchini humo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Édouard Bizimana, pia ameitaka Kenya kuhakikisha usalama wa Warundi wanaoishi nchini humo. Amesema kuendelea kwa matamshi ya chuki dhidi ya Warundi kunaweza kuwa na athari kwa uhusiano kati ya Burundi na Kenya.

Kauli ya Bien imeibua mjadala kuhusu namna mataifa ya Afrika yanavyopaswa kuwalinda raia wa nchi nyingine wanaoishi ndani ya mipaka yao, akisisitiza kwamba kinachowakabili Warundi nchini Kenya leo kinaweza kumkabili Mkenya katika nchi nyingine kesho.

Mamia ya raia wa Burundi wamekusanyika katika Ubalozi wa Burundi jijini Nairobi, wakitafuta msaada na nyaraka za kusafir...
07/09/2026

Mamia ya raia wa Burundi wamekusanyika katika Ubalozi wa Burundi jijini Nairobi, wakitafuta msaada na nyaraka za kusafiria baada ya kuibuka hofu ya kutimuliwa nchini Kenya kufuatia tamko la Rais William Ruto kuhusu wafanyabiashara wa kigeni.

Taarifa zinaeleza kuwa umati mkubwa, hasa vijana, umeonekana nje ya ubalozi huo ukiwa na mizigo na mali zao, huku baadhi wakieleza hofu kuhusu mustakabali wao nchini Kenya.

Hatua hiyo imefuatia agizo la Ruto la kufungwa kwa biashara ndogo ndogo zinazoendeshwa na wageni wasio na vibali vya kufanya kazi. Tamko hilo limeibua wasiwasi mkubwa miongoni mwa raia wa Burundi, ambao wengi wao hujishughulisha na biashara ndogo ndogo jijini Nairobi.

Serikali ya Kenya baadaye ilitoa ufafanuzi kwamba hatua hizo zinalenga wageni wasio na vibali halali vya kufanya kazi, na kwamba hakukuwa na mpango wa kuwanyanyasa au kuwatisha raia wa nchi nyingine. Serikali pia imewataka raia wa Burundi na mataifa mengine ya Afrika Mashariki wenye hali isiyo rasmi kujisajili katika balozi zao.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Kenya pia imetangaza kipindi cha muda cha kuwaruhusu wahamiaji wa Afrika Mashariki wasio na nyaraka kurekebisha hali yao ya kisheria, huku ikisisitiza kuwa hakutakuwa na kuvumilia vitendo vya unyanyasaji au chuki dhidi ya wageni.

Inakadiriwa kuwa kuna takribani Warundi 16,000, wakiwemo wakimbizi na waombaji hifadhi, nchini Kenya, wengi wao wakiwa wanaishi na kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi jijini Nairobi.

07/09/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi akitangaza taarifa ya msiba wa Mhe. Hafidh Ameir Hassan ambaye ni Mume wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan

07/09/2026

Msanii wa Burundi, Lolilo Simba , ameendelea na mzozo wake wa kimuziki dhidi ya mwanamuziki Big Fizzo , huku akitoa kauli kali kuhusu safari ya Big Fizzo kwenye muziki.

Lolilo amesema kuwa kwa miaka yote ambayo Big Fizzo amekuwa akifanya muziki, hajawahi kusimama k**a msanii anayejitegemea kikamilifu, bali amekuwa akitegemea nguvu na ushawishi wa watu wengine katika safari yake ya muziki.

Kwa mujibu wa Lolilo, Big Fizzo aliwahi kutembeleya mgongo wangu kipindi cha awali , na hata sasa bado anaendelea, kwa kile alichodai, “kutembea kwenye migongo ya watu wengine” ili kuendelea kusalia kwenye muziki.

Kauli hiyo imekuja wakati ambapo beef kati ya Lolilo na Big Fizzo ikiendelea kushika kasi kwenye muziki wa Burundi, huku wasanii hao wakitupiana maneno kupitia nyimbo na kauli zao mbalimbali.

Lolilo anaonekana kusisitiza kuwa mafanikio ya msanii yanapaswa kujengwa kupitia uwezo na kazi yake mwenyewe, badala ya kutegemea jina, ushawishi au mafanikio ya watu wengine.

Beef hiyo imeendelea kuwavutia mashabiki wa muziki wa Burundi, ambao wanaendelea kufuatilia hatua inayofuata kutoka kwa kila upande.

Address

Bujumbura
Bujumbura
6314

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Platform show posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Platform show:

Shortcuts

Share