
26/07/2025
Leo mitandao ya kijamii imetikisika baada ya mke wa msanii Ibraah TZ 🇹🇿 kuposti picha mpya inayomuonesha akiwa mjamzito, 🤰 jambo ambalo limewafanya mashabiki na wafuasi wengi kushangaa na kujiuliza maswali mengi.
Hii inakuja siku 4 tuu baada ya harusi yao kufanyika rasmi, ambapo alimuoa mchumba wake kwa ndoa halali na ya hadhara.
Licha ya harusi hiyo kufanyika kwa heshima na hadhi, mke wake hakuwa bado ameweka wazi ujauzito huo mpaka leo alipovunja ukimya kwa picha 6 zilizobeba ujumbe mzito.
Katika picha izo, mke wa Ibraah anaonekana mtulivu, mchangamfu, na akibeba ujauzito wa wazi hali iliyowafanya watu wengi kusema:
‼️“Kumbe tayari ni mjamzito, na ndo maana harusi ikafanyika haraka?”
Wengine wamepongeza uamuzi wa wenzi hao kuweka maisha yao binafsi kuwa ya faragha hadi walipokuwa tayari kushiriki na umma.
Mpaka sasa, Ibraah TZ hajatoa kauli yoyote rasmi kuhusu ujauzito huo, lakini mashabiki wengi wanaamini kwamba huenda wameamua kuanza maisha ya ndoa kwa hatua kubwa na ya kujiamini.
Hongera kwa familia mpya ya Ibraah TZ na sasa, kinachosubiriwa ni mtoto!