19/10/2020
DRC: BURUNDI YA FICHUA NJAMA YA RWANDA DHIDI RDCONGO / by Madiba Mahoye
-----------------------------------------------------------------------------
Waziri wa ulinzi wa Burundi na wapiganaji wa zamani injinia Alain Tribert MUTABAZI, ameïshutumu Rwanda kwa kuwasajili kijeshi vijana wa Burundi kwa malengo ya kuihujumu kijeshi nchi ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Zowezi hilo limekua likiendeshwa na Rwanda tangu mapigano mapya ya zuke huko katika nyanda za juu za vilima vya Fizi - Minembwe, Uvira - Bijimbo na Mwenga, kwa malengo ya kuwasaïdia wanamgambo wa Gumino ikiwa ni watutsi wenye asili ya Rwanda k**a inavyo daïwa na raïa wa Congo.
Taarifa hizo pia zimezunguziwa kwenye kikao cha mawaziri wa ulinzi wa nchi za jumuia ya ukanda wa maziwa makuu, kikao kilicho fanyika tare 14 Oktoba mwaka huu kwa njia ya vidéoconférence, kikiendeshwa na waziri wa ulinzi wa Congo-Brazzaville akiwa ndie mwenyekiti wa baraza hilo.
Nchi za Zambia ,Uganda, Burundi, Tanzania, Rwanda , Angola , Afrika ya kati, Sudani Kusini zilikuwa wenyeji katika mkutano wa nchi hizo zikiwa zimewakilishwa na mawaziri wa ulinzi wa nchi hizo.
Katika mkutano huo wa mawaziri wa ulinzi,swala na mbinu za kumaliza uvunjifu wa amani katika ukanda wa maziwa makuu limepewa kipau mbele na kutafuta mbinu m'badala ili amani idumu. Mawaziri hao wa ulinzi pia wametizamia kwa pamoja jinsi ya kuongezea uwezo kwa kikosi cha kiukanda,FIB, ambacho kinatarajiwa kushika nafasi ya jeshi la MONUSCO linalo hudumu nchini DRC likiwa linamaliza muhula wa kusimamia amani nchi humo ifikapo Desemba mwishoni mwa mwaka huu.
Akizungumzia katika kikao hicho waziri Aimé NGOI MUKENA, waziri wa ulinzi wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, amekumbusha mawaziri wenzake wa ulinzi wa nchi za ukanda huu kufanya iwezekanavyo kwa kuziba pengo katika nyazifa zinazo baki kwenye ofisi hiyo n**i zote zifanyike k**a inavyo tarajiwa, huku waziri huyo akikazia kuimarishwa kwa kitengo kinacho husika na amani na usalama. Waziri NGOI MUKENA amependekeza DRC kuchukua tena nafasi ya uwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwenye muhula mwengine.
Rwanda imekua ikishotwa kidole mara kadha kwa kuyafadhili makundi ya watutsi wa kinyamulengo wenye malengo ya kujipatia nchi huru kutoka sehemu ya ardhi ya DRC tangu wakati wa uasi wa RCD Goma,iliokua ikiongozwa na Azarias RUBERWA myaka ya 1998 ambae ni waziri wa serikali za vijiji nchini. Kundi ambalo linalo fadhiliwa na Rwanda, ni kundi kundi la Gumino linalo ongozwa na kanali Michel Rukunda alias Makanika akishirikiana na waasi wa Burundi wa Red Tabara ambao wanayumbisha usalama siku hizi nchi Burundi kwa ushirikiano na Wanyarwanda, k**a zinazo ripoti duru zetu.
Itafahamika kuwa polisi ya Burundi imenya msako siku za hivi karibuni katika mikoa ya Gitega na Makamba na kuwak**ata mamia ya wanyamulenge ambao wamebainika kua ni wahamiaji haramu ambao wanaeshi bila vitambulisho nchini Burundi.
Wakuu wa mamlaka nchini Burundi wamekuwa na hofu dhidi ya watu wenye kuongea lugha ya kinyarwanda kutokana na uhusiano mdogo wa kidiplomasa kati ya nchi hizo mbili ulio haribika tangu wakati hayati raïsi Pierre NKURUNZIZA wa Burundi ajitangaze k**a mgombea kiti cha uraïsi katika uchaguzi wa mwaka wa 2015.
Burundi na Rwanda zimekua majirani wenye uhasamu mukubwa.