Imara média Imara média, c'est le media sous régionale pour la recherche de la paix et la réconciliation.

Marekani: RAIS DONALD TRUMP WA MARZKANI ATISHIA KUISHAMBULIA KIJESHI  NCHI YA NIGERIA./ Mahoye Madiba.""""""""""""""""""...
02/11/2025

Marekani: RAIS DONALD TRUMP WA MARZKANI ATISHIA KUISHAMBULIA KIJESHI NCHI YA NIGERIA./ Mahoye Madiba.
"""""""""""""""""""""""''''''''""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Rais Donald Trump wa Marekani, ameiagiza Wizara ya Ulinzi ya Nchi yake ‘Pentagon’ kujiandaa kwa uwezekano wa kuchukua hatua za Kijeshi nchini Nigeria, huku akiendelea kuishutumu nchi hiyo ya Afrika Magharibi kwa kufanya vitendo vya vurugu dhidi ya Wakristo — shutuma ambazo Nigeria imekanusha mara kadhaa.

Kupitia chapisho katika mitandao ya kijamii alilolielekeza kukosoa kile alichokiita “Mauaji makubwa ya Wakristo” nchini humo, Rais Trump aliandika kwamba Marekani “itasitisha mara moja misaada yote na usaidizi kwa Nigeria” na akaonya Serikali ya Nigeria “ichukue hatua haraka.”

Katika ujumbe wake mrefu, Trump alisema kuwa Marekani “huenda ikaingia katika nchi hiyo iliyopoteza heshima, ‘tukiwa tumebeba silaha,’ ili kuwaangamiza kabisa Magaidi wa Kiislamu wanaotekeleza uhalifu huu wa kikatili.”

“Ninaiagiza Wizara yetu ya Vita kujiandaa kwa hatua yoyote itakayohitajika,” aliandika Trump.

“Tukishambulia, itakuwa haraka — sawa na jinsi Magaidi hao wanavyowashambulia Wakristo! ONYO: SERIKALI YA NIGERIA ICHUKUE HATUA HARAKA!”

Tangazo hilo linakuja baada ya Trump kuishutumu Nigeria siku ya Ijumaa kwa kukiuka uhuru wa kidini, akidai kwamba “Ukristo uko katika hatari kubwa ya kutoweka nchini Nigeria” na kuitaja nchi hiyo k**a “Nchi ya Wasiwasi Maalum” chini ya Sheria ya Kimataifa ya Uhuru wa Kidini.

Tanzania: RAIS SAMIA SULUHU HASANI AHUTUBIA TAÏFA WAKATI WAMATANGAZO YA MATOKEO YA UCHAGUZI./ by Mahoye Madiba""""""""""...
01/11/2025

Tanzania: RAIS SAMIA SULUHU HASANI AHUTUBIA TAÏFA WAKATI WAMATANGAZO YA MATOKEO YA UCHAGUZI./ by Mahoye Madiba
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""'''"""""""""""""""'''
“Matukio yakiyofanywa katika miji ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza , Mbeya na Msongwe hayakuwa ya kiungwana wala ya kizalendo.
-
Uzalendo ni kujenga nchi wala si kubomoa.”
-Rais Mteule wa Tanzania Samia Suluhu Hassan punde baada ya kupokea cheti chake cha ushindi huko Dodoma.
-
Hii ndio mara ya kwanza kwa Rais Samia kuonekana hadharani tangu siku ya uchaguzi yalipotibuka maandamano ya vijana.
-
-

Tanzania: SADC YATOA KAULI KULINGANA NA GJASIA ZINAZO ENDELEA NCHINI TANZANIA./ by Mahoye Madiba."""""""""""""""""""""""...
01/11/2025

Tanzania: SADC YATOA KAULI KULINGANA NA GJASIA ZINAZO ENDELEA NCHINI TANZANIA./ by Mahoye Madiba.
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), imesema inaendelea kufuatilia kwa karibu matukio yanayoendelea katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuatia Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba 2025.

Katika Taarifa ya SADC iliyosainiwa na Profesa Arthur Peter Mutharika, Rais wa Malawi na Mwenyekiti wa Kamati ya SADC ya Masuala ya Siasa, Ulinzi na Ushirikiano wa Usalama, imesema inasikitishwa na kuendelea kwa vifo, majeruhi, na uharibifu wa mali binafsi na miundombinu ya umma.

SADC pia imesema inatoa wito kwa wadau wote kuwa na kiasi cha juu cha uvumilivu na kuepuka vitendo vyovyote vinavyoweza kuongeza vurugu na machafuko zaidi.

SADC imesema inathibitisha ipo tayari kusaidia, kupitia mifumo inayofaa, katika kuwezesha suluhisho la amani kwa changamoto zinazoikabili nchi kwa sasa.

Hivyo, imetoa wito wa kusitishwa mara moja kwa uhasama, na tunahimiza pande zote kuweka kipaumbele katika ustawi na maisha ya Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Tunasisitiza umuhimu wa kukumbatia mazungumzo ya amani na ya kujenga k**a njia bora ya kushughulikia malalamiko. Dhamira yetu ya pamoja inabaki kuwa kurejesha amani na utulivu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania” imesema taarifa ya SADC.

.

28/10/2025

Je fête mes 3 ans chez Facebook. Merci pour votre soutien, cela ne ce serait jamais fait sans vous.🙏🤗🎉

DRC - Kinshasa: AFISA WA JESHI LA JAMUHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO ASH*TAKIWA KWA KOSA LA KUPOSTI PICHA MITANDAONI AKIM...
28/10/2025

DRC - Kinshasa: AFISA WA JESHI LA JAMUHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO ASH*TAKIWA KWA KOSA LA KUPOSTI PICHA MITANDAONI AKIMBUSU MCHUMBA WAKE AKIWA AMEVALIA SARE ZA JESHI./ by .
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Béanche EBABI BONGOMA KOLI , ni afisaa wa jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwenye cheo cha adjudant amefikishwa mahak**ani ya jeshi inayo patikana mjini Kinshasa kwenye mtaa wa Gombe kwa kosa la kukeuka maadili ya kazi ( violation des consignes ).

Adjudent EBABI BONGOMA , ambae ni katibu msaïdizi kwenye ofisi ya makao makuu ya kitengo cha ujasusi jeshini alikutwa na hatiya ya kuposti picha zake na vidéo kwenye mtandao wa kijamii wa Tik Tok akiwa amevalia sare za jeshi huku akiwa anambusu mchumba wake ambae anataraji kufunganae ndoa.

Sherehe za ndoa zilitaraji kufanyika tarehe 31/10/2025 na mchumba wake nae pia akiwa ni mwanajeshi.
Kesi ya mwanajeshi huyo imeanza kusikilizwa tangu siku ya jumatatu tarehe 27/10/2025 kwenye kambi ya jeshi ya Luteni kanali KOKOLO ndani ya Jimbo la 14 la kijeshi kaskazini mwa jiji la Kinshasa.

Kwa upande wa mashtaka unadayi kuwa mstuhumiwa alienda kinyume na maagizo ya telegrmme ya mkuu wa majeshi inayo pigamarufuku kuposti picha aïdha vidéo kwenye mitandao ya kijamii shughuli zozote za jeshi jeshi ao mwanajeshi akiwa amevalia Sare za jeshi wala viashiria vya jeshi la FARDC.

, amesema hivo muendesha mashataka Lutenant Ghislain Lisama. Akionesha kua tabia hiyo inalidhalilisha jeshi.

Mshatikiwa EBABI BONGOMA KILI , mbele ya hakimu amekiri kua picha hizo anazitambua sababu ilikua ni katika maandali ya ndoa Yale anayo taraji kuifunga hivi karibuni akiwa na mchumba wake walipigwa picha hizo akitaji kutuma kwa ndugu wa familia yake ambae wako nchini Brasile. Lakini amekataa kuhusi na uvujishwaji wa picha hizo kwenye mtandao.

> amejitetea hivo.

Upande wa utetezi umeiyomba mahak**a kuialika studio ya Raus Studio kufika mahakani ili watoe maelezo.

Meja Christian Safari amemskiliza m'miliki wa studio hiyo ili atowe sababu za kusambaza picha hizo mitandaoni.

Upande wa mashataka umeomba mtuhumiwa apewe adhabu ya kifungo cha myaka 10jela.

Hukumu inasubiriwa kutolewa na mahaka tarehe 29/10/2025.

@ Towa maoni yako kwenye komenti kuhusiana na swala hilo

Namibia: RAÏSI WA NAMIBIA AMFUTA KAZI WAZI VIWANDA NA NISHATI KWA KOSA LA UZEMBE./ by Mahoye Madiba."""""""''''''''''"""...
27/10/2025

Namibia: RAÏSI WA NAMIBIA AMFUTA KAZI WAZI VIWANDA NA NISHATI KWA KOSA LA UZEMBE./ by Mahoye Madiba.
"""""""''''''''''"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""''''''""""""'"""""""''

Rais wa Namibia -Ndaitwah amemuondoa Natangwe Ihete kutoka nyadhifa zake k**a Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Viwanda, Madini na Nishati.

Ihete aliteuliwa kwa nyadhifa hizo mwezi Machi k**a sehemu ya utawala mpya wa -Ndaitwah. Anaendelea kuwa Mbunge, ilisema taarifa hiyo.

Namibia yenye rasilimali nyingi inalenga uzalishaji wake wa kwanza wa Mafuta ghafi ifikapo mwaka 2030 baada ya uvumbuzi kadhaa mkubwa katika miaka ya hivi karibuni. Inachimba Madini kadhaa k**a vile uranium na almasi.

Serikali ya Marekani, chini ya Rais , imefanya upatikanaji wa Madini muhimu kuwa msingi wa diplomasia yake barani Afrika, ikiwa ni pamoja na kupitia makubaliano ya amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya yenye utajiri wa rasilimali mwaka huu.

@

Cameroun - Yaoundé : MATOKE YA UCHAGUZI YATOLEWA NA BARAZA LA KATIBA, HUKUVUTUGU EIKIRIPOTIWA ./ bya Uhariri."""""""""""...
27/10/2025

Cameroun - Yaoundé : MATOKE YA UCHAGUZI YATOLEWA NA BARAZA LA KATIBA, HUKUVUTUGU EIKIRIPOTIWA ./ bya Uhariri.
""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Baraza la Katiba nchini limemtangaza Rais Paul Biya kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais kwa kupata asilimia 53.66 ya kura,huku mpinzani wake mkuu na aliyekuwa mshirika wake wa zamani, Bakary, akipata asilimia 35.19.

, ambaye ametawala tangu mwaka 1982, anaendelea kushikilia madaraka baada ya uchaguzi ulioshirikisha zaidi ya wapiga kura milioni nne, huku ushiriki ukiwa asilimia 57.76. Hata hivyo, matokeo hayo yanapingana na madai ya aliyedai kushinda kabla ya matokeo rasmi kutangazwa.

Taatifa kutoka mjini Yaoundé za srma kua maandamano ya kypinga matokeo ya uchaguzi ya maanza mapema alfajiri ya jumatatu hii, huku upinzani ukidaï kuwa kura ziliibiwa .

Vyombo vya usalama vimekua vikikabiliana na waandamanaji wa fwasi wa mpinzani wa raïsi bwana .
Mpizani huyo ameskika akisema kuwa makaazi yake yameshambuliwa kwa risasi na vyombo vya usalama vya nchi hiyo.
-
@

RDC-Bukavu : WATU 14 WARIPOTIWA KUFA BAADA YA MOTO MKALI KUTEKETEZA MAJUMBA./ by Mahoye Madiba."""""""""""""""""""""""""...
27/10/2025

RDC-Bukavu : WATU 14 WARIPOTIWA KUFA BAADA YA MOTO MKALI KUTEKETEZA MAJUMBA./ by Mahoye Madiba.
""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Ilikua usiku wa manani wakati watu wote wakiwa kweye usingizi, ndipo moto mkali ulipozuka na pembezuni ya kanisa Funu Nuru kwenye barabara ya Maendeleo( Avenue Maendeleo) mtaa wa Mosala mjini . Hadi sasa chanzo cha moto huyo bado hakijajulikana.

Mkuu wa mamlaka ya eneo hilo amesibitisha tukio hilo huku akitoa idadi ya watu 14 ndio wamefariki huku akisema kua idadi hiyo inaweza ikaongezeka.

Huzuni imetanda kwenye nyuso za wakaaji wa asubuhi ya jumatatu hii, huku harakati za kuwasaka majeruhi na mwili mingine ya wahanga wa ajali hiyo zikiwa zimeanza.

Igahamike kua tukio k**a hilo la moto lilirupotiwa jumaa pili maeneo ya Lugushwa tarafa la kwenye umbali wa takribani nyumba 400 ziliteketea.

HADITHI YA GRACE MACHEL - MAMA WA TAIFA MARA MBILI./ by Mahoye Madiba.""""""""""""""""""""''''"""''""""'''"'''''""""""""...
27/10/2025

HADITHI YA GRACE MACHEL - MAMA WA TAIFA MARA MBILI./ by Mahoye Madiba.
""""""""""""""""""""''''"""''""""'''"'''''"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Bara la Afrika limelojaa simulizi za Mashujaa na Malkia wa kweli, jina la linang’ara kwa mwangaza wa pekee. Mwanamke huyu si wa kawaida. Ndiye Mwanamke pekee katika historia ya Afrika aliyepewa hadhi ya kuwa Mama wa Taifa katika nchi mbili tofauti, Msumbiji na Afrika Kusini.

Hadithi yake inaanza katika anga la mapambano, akiwa upande wa Rais wa Kwanza wa Msumbiji huru, . Grace aliishi naye k**a Mke na Mshirika wa karibu katika vita vya kujenga taifa jipya. Lakini bahati mbaya, mwaka 1986, Ndege ya Samora ilianguka, ikachukua uhai wake na Grace akabaki Mjane, akiwa na masikitiko na kumbukumbu nzito.

Miaka ilivyosonga, upepo wa mabadiliko ulianza kuvuma kusini mwa Afrika. , Mfungwa wa kisiasa maarufu zaidi duniani, aliachiliwa kutoka Gerezani mwaka 1990 baada ya miaka 27 ya kifungo. Lakini tofauti na matarajio ya wengi, ndoa yake na Winnie Mandela haikustahimili upepo wa muda wakaachana rasmi mwaka 1996. Na ndipo historia ilipoanza kuandika ukurasa mpya wa huba.

Julai 18, 1998, siku ambayo Mandela alitimiza miaka 80 hakuchagua sherehe ya kifahari pekee, bali alichagua upendo. Alimuoa , Mwanamke wa hekima, mwenye utulivu, na aliyebeba majeraha ya Afrika lakini pia matumaini yake.

hakujali umri, hakujali siasa, hakujali sura za dunia. Alijali moyo, moyo wa Grace. Na hivyo, Bi. Grace Machel akawa First Lady wa Afrika Kusini, akiwa tayari ameshawahi kuwa Mama wa Taifa wa Msumbiji.

Alikuwa Mrembo, Jasiri, na mwenye roho ya kipekee. Kwa maneno ya wengi: “Huyo Bi. Grace alikuwa mwanamke haswa, Mzee Mandela hakufanya makosa kabisa.”

Leo hii, historia inamtambua si tu k**a Mjane wa Mashujaa wawili, bali k**a Mama aliyeishi kwenye kivuli cha vichwa vizito lakini bado aliangaza kwa mwanga wake mwenyewe.

Toa maoni yako

Le vice gouverneur honorable maître Jean Jacques Elekanao devant la presse locale répondant aux questions des Journalist...
15/10/2025

Le vice gouverneur honorable maître Jean Jacques Elekanao devant la presse locale répondant aux questions des Journalistes de la ville de Baraka et de Fizi.

15/10/2025

de Baraka Kivu.

Adresse

Bukavu

Téléphone

+243975571265

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Imara média publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Partager