Classic Media Ente10nment

Classic Media Ente10nment Maison de production Audiovisuelle et l'impression Général

“Miaka 10 iliyopita ulikataa kuchukua pesa kutoka kwangu kwa ajili ya collabo, ulijitolea kuifanya bure.” – Diamond Plat...
24/06/2025

“Miaka 10 iliyopita ulikataa kuchukua pesa kutoka kwangu kwa ajili ya collabo, ulijitolea kuifanya bure.” – Diamond Platnumz

“Nilipokuwa nikijaribu kupata nafasi huko Nigeria miaka 10 iliyopita, ulitoa beti (verse) ambayo ilibadilisha kabisa maisha yangu ya muziki. Ulilipia nauli yako mwenyewe, ukaja Tanzania tukarekodi. Tulipouliza kuhusu malipo, ukasema hakuna shida – ni sawa tu. Kila wakati kwako imekuwa ni kuhusu kukuza wengine. Unapenda kuwaona wengine wakikua, na ndiyo maana umekuwa mkubwa zaidi – 001 wa Afrika. Wanasema hakuna mtu mzuri, lakini wewe ni mzuri ndugu yangu. Hakuna anayeweza kujifanya kuwa mzuri kwa miaka 10. Mungu aibariki familia yako.” – Amesema Diamond Platnumz

Omo, si leo tu bwana – miaka 10 iliyopita? Dah! Kumbe 001 amekuwa akiinua wengine toka zamani. Ni miaka 10 na bado anaendelea kufanya hivyo.

Funzo: Davido anastahili kila kitu kizuri anachopata.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa Iran imejibu mashabulizi ya ufyatuaji vifaa vyao vya Nyuklia, huku akiliita s...
23/06/2025

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa Iran imejibu mashabulizi ya ufyatuaji vifaa vyao vya Nyuklia, huku akiliita shambulizi hilo kuwa dhaifu dhidi yao.

Trump kupitia mtandao wake wa "X" ameeleza kuwa shambulio hilo walilitarajia na wamelikabili kwa ufanisi mkubwa na kueleza kuwa makombora 14 yalirushwa na Iran dhidi yao na walifanikiwa kuyazuia na kusema hakuna mtu aliye athirika na shambulizi hilo na Marekani ipo katika mwelekeo sahihi.

"Iran imejibu rasmi Ufyatuaji wetu wa Vifaa vyao vya Nyuklia kwa jibu dhaifu sana, ambalo tulitarajia, na tumekabiliana kwa ufanisi sana. Kumekuwa na makombora 14 yaliyorushwa-13 yaliangushwa, na 1 "iliwekwa huru," kwa sababu ilikuwa inaelekea katika mwelekeo usio na tishio.

Nimefurahiya kuripoti kwamba HAKUNA Waamerika waliodhurika, na hakuna uharibifu wowote uliofanyika. Muhimu zaidi, wameiondoa yote kwenye "mfumo" wao, na kwa matumaini, hakutakuwa na CHUKI zaidi. Ninataka kuishukuru Iran kwa kutupa taarifa ya mapema, ambayo iliwezesha hakuna maisha ya watu kupotea, na hakuna mtu kujeruhiwa.

Pengine Iran sasa inaweza kuendelea na Amani na Maelewano katika Eneo hili, na kwa shauku nitahimiza Israel kufanya vivyo hivyo. Asante kwa umakini wako kwa jambo hili"Alisema Trump.

TESSA GEORGESûrement le personnage le plus détesté du film.Agaçante. Froide. Parfois même cruelle sans le vouloir.Elle n...
16/06/2025

TESSA GEORGE

Sûrement le personnage le plus détesté du film.
Agaçante. Froide. Parfois même cruelle sans le vouloir.
Elle nous rappelle cet agent administratif insensible à nos urgences.
Ce médecin rigide qui attend le paiement avant de toucher à notre mère en détresse.
Ce genre de personne qui applique les règles sans jamais entendre la détresse.

Tessa George n’a rien fait de mal.
Et pourtant, elle a tout fait .

Mais la vraie leçon, elle est ailleurs.
Tessa nous apprend une vérité inconfortable :
Peu importe la sincérité de ton histoire, la noblesse de tes intentions, ou la clarté de tes explications ,
il y aura toujours des gens comme elle.
Des gens qui ne t’écouteront pas.
Qui ne te croiront pas.
Qui ne te soutiendront pas.

Et ce n’est pas grave.
Parce qu’on ne peut pas plaire à tout le monde.
Et surtout, on ne doit pas vivre pour être compris par tout le monde.
Goatdirector Filmmaker Ismail

UTALIPIA 165,000/=  KUPIGA PICHA NA DIAMOND PLATNUMZ LONDONUnaambiwa Tiketi Za Kusalimiana Na Kupiga Picha Na SIMBA 🦁  J...
14/06/2025

UTALIPIA 165,000/= KUPIGA PICHA NA DIAMOND PLATNUMZ LONDON

Unaambiwa Tiketi Za Kusalimiana Na Kupiga Picha Na SIMBA 🦁 Jijini London Ni Kiasi Cha £55 Ambazo Ni Takribani Tsh 165,000/=.

Tiketi Hii Inampa Nafasi Ya Kipekee Shabiki Kukutana Na (Meet & Greet) Kusalimiana Na Kupigana Nae Picha K**a Kumbukumbu. Na Tukio Hili Linatajwa Kufanyika Leo Jijini London.

Ukiachilia Mbali Hivo Tiketi Pia Za Onesho Hilo Kubwa Lililofanyika Ukumbi Wa Royal Albert Hall Zilikuwa Zinanzia Tsh 90,000/= Na Kuendelea . Hivyo Hii Inaonesha Thamani Na Mafanikio Makubwa Ya Star Huyu Wa Muziki Duniani. ( Swipe)

Safari ya kompyuta zote za Mac ambazo zinatumia chip/processor ya Intel imefika mwisho; na mwisho wake ni mwaka huu. Mfu...
12/06/2025

Safari ya kompyuta zote za Mac ambazo zinatumia chip/processor ya Intel imefika mwisho; na mwisho wake ni mwaka huu.

Mfumo wa macOS 26 Tahoe ambao umetambulishwa siku ya jana, utakuwa ni mfumo wa mwisho kukubali kompyuta ambazo zinatumia chip ya Intel. Ina maana kuwa, kuanzia 2026 Apple haitakuwa inatoa updates katika kompyuta hizo.

Mwaka huu Mac hizi zimepona na utakuwa mwaka wake wa mwisho:
💻 16-inch MacBook Pro ya mwaka 2019
💻 Intel 13-inch MacBook Pro ya mwaka 2020,
🖥️iMac 2020,
🖥️ na Mac Pro 2019

K**a una mpango wa kununua Mac ni muhimu kuepuka Macs hizi ili kuepuka kulazimika kubadili Mac baada ya miaka michache.

K**a unauza Mac, ni muda wa kuanza kufikiria Mac za Apple Silicon ambazo zinatumia chip za Apple badala ya chip za Intel.

_____________
#
Goatdirector Filmmaker Ismail
Classic Media Ente10nment

💔💔 I know Tems will be somewhere now wondering why Classic Media Ente10nment did not post about her on her birthday. She...
11/06/2025

💔💔 I know Tems will be somewhere now wondering why Classic Media Ente10nment did not post about her on her birthday. She is probably sad and thinks we forgot about her.

But the truth is, throughout the entire day today, I’ve been trying to picture the African music industry without Tems, and it just didn’t make sense. Tems is unarguably the biggest female artist to ever be born in Nigeria.

She came into the game with just talent and changed everything.

She didn’t need a big record label to sign her and invest billions in her music before she could be loved.

She didn’t need to show her body, even though she has very good raw materials behind her for us to watch her videos.

She came with just hard work and talent and changed everything for the Nigerian music industry. She was producing her own music in her room for the love of it and it made her who she is today!

She became the first Nigerian female artist to win two Grammy Awards in the 21st century.

She will be the first Nigerian to perform at the Club World Cup halftime show.

Rihanna loves her.

Beyoncé loves her.

Wizkid loves her.

And Music Base Africa, as the most Afrocentric African blog on Facebook, and all its admins love Tems.

She is a role model and an example for our young girls to follow!

Today, she turned 30 years old!

If you are a fan of her work and a true African, gather here and wish her a happy birthday!❤️

Happy Birthday, Temilade! 🎉🎉

Top 10 Investments To Become Rich 🤑💸• Index funds (set and forget)• Rental properties (cash flow + appreciation)• Your o...
10/06/2025

Top 10 Investments To Become Rich 🤑💸

• Index funds (set and forget)
• Rental properties (cash flow + appreciation)
• Your own business (scalability)
• REITs (real estate without the hassle)
• Dividend stocks (passive income)
• High-yield savings (liquidity + security)
• Private equity (long-term growth)
• Yourself (skills, network, knowledge)
• Side hustles (extra income + tax benefits)
• Peer-to-peer lending (alternative income)

You need to Start early & stay consistent!

Mwanamitandao maarufu anayeshikilia rekodi ya kuwa na wafuasi wengi TikTok, Khabi Lame amek**atwa nchini Marekani 🇺🇸 na ...
08/06/2025

Mwanamitandao maarufu anayeshikilia rekodi ya kuwa na wafuasi wengi TikTok, Khabi Lame amek**atwa nchini Marekani 🇺🇸 na baadae kufukuzwa nchini…

Raia huyu wa Italy 🇮🇹 mwenye asili ya Senegal 🇸🇳 amek**atwa na maafisa wa uhamiaji nchini Marekani 🇺🇸 kwa kosa la kuzidisha muda wa kukaa nchini humo (overstay)…

Khabi Lame, miaka 25, mwenye followers Milioni 162 Tiktok, aliteuliwa mwezi February 2025 kuwa Balozi wa UNICEF… Alikuwa nchini Marekani 🇺🇸 tangu mwezi April…

01/06/2025
Huku Jaku boy kamzawadia mkewe Mercedes benz kule Mary mchepuko karudi rumande kwa kukosa dhamana huku akiwa anakabiliwa...
01/06/2025

Huku Jaku boy kamzawadia mkewe Mercedes benz kule Mary mchepuko karudi rumande kwa kukosa dhamana huku akiwa anakabiliwa na mashtaka karibu kumi ikiwamo kutishia kuua kisa kumgombea Mwijaku ambaye ni mume wa mtu🥹

Lakini pia safari yake ya elimu imeshaishia pale na sasa anatazamia kifungo au pengine na faini juu

Mabinti wadogo na michepuko woteee mna kitu kikubwa cha kujifunza hapo

1. Mume wa mtu ni k**a bolt/uber/kiti cha bus! Hata ushinde navyo siku nzima jioni ni mahesabu nyumbani

2. Mume wa mtu HAPENDWI

3. Mume wa mtu ni wa MSIMU

4. Mume wa mtu HAZALIWI MTOTO

5. Kubwa kabisa
MUME WA MTU HAPIGANIWI
🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Sasa JICHANGANYE
Goatdirector Filmmaker Ismail

Wataalamu wanasema, wanaume wana uwezekano mkubwa wa kufa kabla ya wakati wao kuliko wanawake.Sababu huenda zikawa hizi ...
01/06/2025

Wataalamu wanasema, wanaume wana uwezekano mkubwa wa kufa kabla ya wakati wao kuliko wanawake.

Sababu huenda zikawa hizi ;

1. Mtindo wa Maisha (Lifestyle)
Kuna idadi KUBWA ya Wanaume wenye lifestyle za uvutaji sigara, kunywa pombe, kutumia dawa za kulevya, kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) na shinikizo la damu, kidukari n.k

Mambo hayo huchangia kwa kiasi kikubwa, wanaume kufa mapema kuliko wanawake – ikielezwa kuwa hufa mapema kwa miaka minne kuliko wanawake. Pia wanaume wana uwezekano wa karibu 60% kufa kabla ya umri wa miaka 75 kutokana na ugonjwa wa moyo, saratani ya mapafu, ugonjwa wa ini.

Wanatoa mfano wa janga la Covid 19, wanaume wengi walifariki kuliko wanawake ikichangiwa na Kinga za mwili.

2. Uchunguzi WA afya

Wanaume hawana ujuzi na pia nafasi ya kutosha ya kushughulikia afya zao, hawazungumzi kuhusu afya na kuchukua hatua kulingana na dalili. Wengi inapita miaka bila kuonana mtaalamu wa afya."

"Ni tofauti kwa wanawake. Wao hujikuta wanapata huduma za uzazi wa mpango, chunguzi za mlango wa kizazi na ktk UZAZI na hiyo inamaanisha wanawake wengi huonana mara kwa mara na wahudumu wa afya kwa njia ambayo wanaume hawaipati."

3. Majukumu;
Utofauti wa majukumu hasa linapokuja suala la kazi Wanaume wengi hujihusisha na ajira mbalimbali, ujenzi, ufundi , udereva, Michezo, viwandani nk
Kazi hizi ni ngumu na huambatana na mambo Mengi k**a ajali, majeraha, nk Vile vile mtu anayefanya kazi hizi mara chache sana kuwa na mapumziko, iwe ni kwa uchunguzi wa afya au kupumzisha mwili.

4. Robo 3 ya wanaojiua ni wanaume
Presha wanayoibeba ya majukumu km mwanaume, wkt mwingine kukosa/kutokuwa na kazi na matatizo ya kifedha, pamoja na matatizo ya mahusiano, ni kichocheo kikubwa cha kuwepo kwa viwango vya juu vya kujiua vinavyotokea kwa wanaume.

Kua makini wanaume hatufanyagi Ujinga huu wakati wa Mahusiano!Wanaume katika mapenzi hutumia akili zaidi kuliko moyo. Ku...
01/06/2025

Kua makini wanaume hatufanyagi Ujinga huu wakati wa Mahusiano!

Wanaume katika mapenzi hutumia akili zaidi kuliko moyo. Kuna maamuzi mwanaume akifanya, na vitu anakufanyia, badala ya kufurahia na kuhisi ni mapenzi, hebu jiulize: kwa nini ananifanyia hivi?

Kwa mfano, k**a mwanaume hajakuoa, ni ngumu sana kumshirikisha mwanamke katika mali zake. Labda anajenga au ana biashara anayoanzisha, hatashirikisha mwanamke mpaka awe na hakika kuna faida atakayopata.

Hivyo basi, k**a huna ndoa naye na anakwambia tujenge, unapaswa kuwa makini sana. Mara nyingi, hayo si mapenzi ya kweli. Na inapaswa uogope zaidi ukimuuliza tuandike majina yetu mawili kwenye kiwanja au nyumba, akakujibu kuwa haiwezekani kuandika majina mawili. Ukiona hivyo, tahadhari!

Au akikujibu, "Tutabadilisha mbeleni," ogopa zaidi. Na k**a akikwambia, "Ina maana huniamini? K**a huniamini kwenye vitu vidogo, tunaweza kujenga familia kweli?" hapa ndio unapaswa kutetemeka zaidi. Wanaume hawako tayari kuwekeza kwa mwanamke ambaye si mke ni mpenzi tu mara nyingi mpaka kuwa na kitu.

Mfano mwingine ni pale mwanaume anakwambia mfanye biashara ya pamoja, wewe utoe pesa, lakini kila kitu anasimamia yeye—kuanzia mkataba wa mwenye nyumba hadi TIN namba, halafu anasema biashara ni "yetu." Muombe utumie TIN namba yako, halafu sikiliza majibu yake!

Nimalizie kwa kusema hivi: si kila tabasamu ni la furaha, na si kila mwanaume anayejifanya mkweli ni wa kweli. Sikushauri kufanya vitu vya pamoja kabla ya ndoa, lakini k**a ni lazima, hebu fanyeni mambo kwa uwazi, na majina ya wote yawepo kwenye mali mnayoshirikiana. Wale wanaosema, "Mwanaume wangu ni tofauti," endeleeni, labda kweli ana pembe!

NB: K**a hujaelewa rudia tena kusoma kichwa kikiwa kimetulia!

Adresse

Bukavu

Heures d'ouverture

Lundi 09:00 - 17:00
Mardi 09:00 - 17:00
Mercredi 09:00 - 17:00
Jeudi 09:00 - 17:00
Vendredi 09:00 - 17:00
Samedi 09:00 - 17:00
Dimanche 09:00 - 17:00

Téléphone

+243970074377

Site Web

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Classic Media Ente10nment publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter L'entreprise

Envoyer un message à Classic Media Ente10nment:

Partager