06/12/2025
Rwanda na Congo wamesaini mkataba wa amani kwa upatanishi wa Trump hapo jana December 4, 2025, Mkataba huo wa amani umesainiwa baada ya mafanikio ya Doha process na Washington Peace deal process ambao mchakato wake ulisainiwa kwa mara ya kwanza tarehe 27 Juni 2025 jijini Washington DC na mawaziri wa mambo ya nje wa nchi hizo tatu.
Mkataba huu ni maboresho (ratified) ya ule mkataba wa Washington Peace deal process na maazimio ya Doha process.
Mkataba huu, unafahamika k**a "2025 Democratic Republic of the Congo–Rwanda peace agreement (Au “Washington Accord of peace and prosperity”).
Wadau wakuu wa kikanda walioalikwa kushiriki k**a “guarantors" ni Kenya na Burundi huku Tanzania imeachwa nje.
Tanzania ndio key master wa siasa za maziwa makuu kwa miaka 40 sasa, ila kinachoonekana sasa nafasi hiyo imechukuliwa na Kenya.
Kwa sasa eneo la Afrika Mashariki, Marekani kaamua kuipa nafasi ya "Geopolitical Credibility" Kenya kuwa ndio mshirika wao mkuu wa kimkakati katika military, economic na diplomacy kiasi cha kuifanya Kenya kuwa Guarantor mkuu wa kusimamia mchakato mzima wa amani ya Kongo, isitoshe Donald Trump kamualika Ruto mwaka 2028 kuwa mgeni kwenye Mashindano ya dunia ya Olimpiki yatakayo fanyika Las Angelas.
Huku Burundi waalikwa Kuwa k**a mshirika wa usalama upande wa DRC,
Kwa mantiki hii kwasasa Marekani inaichukulia Kenya k**a “anchor state” ya eneo hili kuliko nchi zote za maziwa makuu.
Imeatolewa na Goatdirector Filmmaker Ismail
Classic Media Ente10nment