20/05/2026
Rapa Billnass alishinda tuzo za muziki Tanzania (TMA) kwa mara ya kwanza na kutoa nyimbo zilizopata namba kubwa katika majukwaa ya kidijitali kuliko zote za mwanzo baada ya kufunga ndoa na Nandy.
Ikiwa ni takribani miaka tisa tangu alipotoka na wimbo wake, Raha (2014), Billnass alishinda tuzo ya TMA kwa mara ya kwanza katika kipengele cha Msanii Bora wa Kiume wa Hip Hop 2022.
Katika TMA 2015 na 2021, hakushinda ila baada ya kuingia tu katika ndoa, basi ikawa baraka kwa kushinda mbele ya wakali wa Hip Hop k**a Fid Q, Joh Makini, Country Wizzy na Kala Jeremiah.
Utakumbuka ushindi huo ulikuja baada ya Billnass kufanya vizuri na wimbo wake, Puuh (2022) ulioweka rekodi k**a wimbo wa Bongofleva uliosikilizwa zaidi Boomplay Music 2023 ukiongoza chati kwa wiki sita.
Hadi sasa wimbo huo aliomshirikisha Jay Melody, ndio wimbo pekee wa Billnass aliosikilizwa zaidi Boomplay, pia ndio wimbo wake ambao video yake imefanya vizuri zaidi YouTube ikiwa imetazamwa zaidi ya mara milioni 17.
Na mwaka huo wa ndoa, Billnass alikuwa msanii wa pili wa Hip Hop Bongo aliyetazamwa zaidi YouTube, video zake zilitazamwa zaidi ya mara 25.9, huku akiwa ametanguliwa na Darassa aliyetazamwa mara milioni 28.6.