Lemera News Tunapatikana DRCongo, Kivu-kusini, Uvira/Lemera. Taarifa za habari zenye ukweli na uhakika, tembelea Lemera News

https://youtube.com/channel/UCXaLExJsr5w02xuOUJjovTA Lemera News, tupo kwaajili ya kukuletea habari za dunia popote ulipo kwa muda muafaka.

Ulivyoziona hizi mechi za kirafiki za Leopards, ni upi ushauri wako kwa Sébastien Desabre kuelekea Michuano ya kombe la ...
10/06/2026

Ulivyoziona hizi mechi za kirafiki za Leopards, ni upi ushauri wako kwa Sébastien Desabre kuelekea Michuano ya kombe la dunia?

07/06/2026

Tunakusalimu popote ulipo, ndugu msikilizaji na ufuatiliaji wa Lemera News.
Tukutakie pia Jumapili njema.

ANATAFUTWAAnaitwa Mashauri, kijana mwenye umri wa miaka takribani 35 , mzaliwa wa kijiji cha Kiliba tarafani Uvira ambay...
09/05/2026

ANATAFUTWA

Anaitwa Mashauri, kijana mwenye umri wa miaka takribani 35 , mzaliwa wa kijiji cha Kiliba tarafani Uvira ambaye kwa sasa ni mkazi wa kijiji cha Katanga tarafani Fizi.
Taarifa zinaeleza kwamba aliondoka nyumbani kuelekea mjini Bukavu tangu mwishoni mwa mwezi uliopita kwa lengo la kununua pikipiki.
Familia inaeleza kwamba kijana wao alifika mjini Bukavu na kufanya shughuli zake vizuri akiwa salama mpaka alivyorudi mpaka kijiji cha Nyangezi tarafani Walungu akiwa na pikipiki yake hiyo aliyonunua lakini mpaka sasa hajafika nyumbani.
Inasemekana kwamba kupotea kwake kumeanzia Nyangezi.
Kwa sasa ni wiki mbili tangu alipotoweka, na simu yake haipatikani.

Inaombwa kwa yeyote mwenye taarifa yoyote kuhusu kijana huyu, aweze kuwasilisha taarifa hizo kwa Familia yake au anaweza kuwasiliana na kupitia njia zetu zote za mawasiliano.

Picha hizi ilipigwa 2016.

Msikilizaji...Neno lolote kwa liwali wa jimbo la Kivu-kusini tafadhali!!!Vipindi vyetu na ratiba zetu zitaendelea wakati...
01/05/2026

Msikilizaji...

Neno lolote kwa liwali wa jimbo la Kivu-kusini tafadhali!!!

Vipindi vyetu na ratiba zetu zitaendelea wakati ambao eneo la makao makuu ya Lemera News litaondoka mikononi mwa adui mvamizi.

Hujambo ndugu popote ulipo Unalo lolote la kumwambia Rais wa zamani wa nchi, Joseph Kabila kuhusiana na hali ya taifa wa...
01/05/2026

Hujambo ndugu popote ulipo

Unalo lolote la kumwambia Rais wa zamani wa nchi, Joseph Kabila kuhusiana na hali ya taifa wakati wa utawala wake na baada ya utawala wake???

DR CONGO Bertrand Bisimwa, ahimiza heshima kwa mashujaa wote wa harakati za ukombozi waliotoweka kwenye uso wa dunia, bi...
26/02/2026

DR CONGO

Bertrand Bisimwa, ahimiza heshima kwa mashujaa wote wa harakati za ukombozi waliotoweka kwenye uso wa dunia, bila kutaja majina ya mashujaa hao.

DR CONGO Mkuu wa majeshi ya kundi la magaidi wa AFC-M23, Sultan Makenga, anaripotiwa kunusurika kifo baada ya kujeruhiwa...
26/02/2026

DR CONGO

Mkuu wa majeshi ya kundi la magaidi wa AFC-M23, Sultan Makenga, anaripotiwa kunusurika kifo baada ya kujeruhiwa vikali katika shambulio la ndege isiyo na rubani lililotekelezwa na vijana Wazalendo katika halmashauri ya Rubaya tarafani Masisi jimboni Kivu-kaskazini.
Makenga amejeruhiwa huku maafisa wengine wengi wa vikosi vya AFC-M23 wakiwa wamepoteza maisha katika tukio hilo ambalo waasisi hao mpaka sasa hawajatangaza wazi matokeo.
Mpaka sasa, serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo pia haijazungumza chochote kuhusiana na taarifa hizo.

DR CONGO Inasemekana kwamba, msemaji wa kijeshi wa AFC-M23, W***y Ngoma, amefia tarafani Masisi karibu na halmashauri ya...
25/02/2026

DR CONGO

Inasemekana kwamba, msemaji wa kijeshi wa AFC-M23, W***y Ngoma, amefia tarafani Masisi karibu na halmashauri ya Rubaya, kwa mujibu wa ripoti ya kundi hilo la magaidi.
Lakini taarifa kutoka vyanzo vyetu, zinaeleza kwamba Gaidi huyo alikuwa amepoteza maisha tangu muda mrefu katika shambulio la ndege isiyo na rubani, alipokuwa tarafani Uvira kwa mara ya mwisho, yeye pamoja na maafisa wengine wengi wa ngazi za juu wa kundi hilo wakiwemo wengine wa jeshi la Rwanda na baadhi ya maafisa wa wizara ya ulinzi ya serikali ya dikteta Paul Kagame.

19/02/2026

Hali sio nzuri sana hapa Lemera.

Magaidi wa kundi la waasi la M23 na jeshi la Rwanda wanaendelea muligana na jeshi la taifa (FARDC) wanaoshirikiana na vijana wazalendo.
Mpaka sasa watu kadhaa wakiwemo raia wa kawaida wasio na hatia, wamesha poteza maisha, katika halmashauri za Lemera na Kigoma katika utawala wa Wafuliiru.

DR CONGO Askari zaidi ya 700 wa nchi ya Afrika kusini wanaohudumu katika vikosi vya Monusco, wanatarajia kuanza kurudi n...
08/02/2026

DR CONGO

Askari zaidi ya 700 wa nchi ya Afrika kusini wanaohudumu katika vikosi vya Monusco, wanatarajia kuanza kurudi nchini kwao ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2026, k**a inavyoeleza barua ya Rais Cyril Ramaphosa iliyotumwa kwa katibu mkuu wa umoja wa matiafa, Antonio Gutteres

Adresse

Lemera

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Lemera News publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter L'entreprise

Envoyer un message à Lemera News:

Raccourcis

Partager

Type