28/08/2026
🇨🇩 TSHISEKEDI ATANGAZA MAZUNGUMZO YA KITAIFA, AWEKA MASHARTI KUHUSU MADARAKA NA AFC/M23
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Félix-Antoine Tshisekedi, ametangaza kufunguliwa kwa mazungumzo ya kitaifa yatakayofanyika ndani ya DRC, akisema lengo ni kuimarisha umoja wa taifa, kujenga amani na kuhusisha nguvu mbalimbali za kijamii katika mustakabali wa nchi.
Katika hotuba yake kwa taifa, Tshisekedi amesisitiza kuwa mazungumzo hayo hayatalenga kugawana madaraka au nafasi za serikali, na kwamba taasisi zilizopo pamoja na mfumo wa kikatiba vinapaswa kuheshimiwa.
Rais Tshisekedi pia ameweka msimamo kuhusu ushiriki wa AFC/M23, akilikataa kundi hilo katika mfumo alioutangaza na kulielezea k**a nguvu inayosaidia Rwanda katika kile ambacho serikali ya Kinshasa inakitaja kuwa uchokozi dhidi ya DRC.
Hatua hiyo inafungua mjadala kuhusu nani atashiriki katika mazungumzo hayo, ajenda zitakazojadiliwa na namna yatakavyosaidia kufikia suluhisho la kudumu la mgogoro wa kisiasa na kiusalama nchini Congo.
Bonyeza hapa ili utu follow Meca Media
Meca Media Facebook
Soma zaidi: www.Mecamediaafrica.com
Mwandishi: Mangwa