Emission Sanaa ya Nyumbani

Emission Sanaa ya Nyumbani Emission Radio Notre Dame de Tanganyika RNDT 99.6 MHz
KWAHUDUMA ZAMATANGAZO MAWASILIANO+243972069631

19/04/2025

Lini mara yako ya mwisho kusikiliza vipindi vya Sanaa vya nyumbani Uvira ?

TANGAZO KWA WASIKILIZAJI"Habari familia ya ÉMISSION SANAA YA NYUMBANI Tunapenda kuwataarifu kuwa kipindi chetu hakitapit...
24/03/2025

TANGAZO KWA WASIKILIZAJI

"Habari familia ya ÉMISSION SANAA YA NYUMBANI Tunapenda kuwataarifu kuwa kipindi chetu hakitapita hewani leo kutokana na tatizo la kiufundi lililojitokeza. Tunaomba radhi kwa usumbufu huu na tunafanya kila jitihada kurekebisha hali hii ili tuweze kurudi hewani haraka iwezekanavyo. Asanteni kwa uelewa wenu na endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi

17/03/2025

TUMA UJUMBE WAKO TUWEZE KUUSOMA MDA HUU

MSANII NOVA KIMENDE ATAKUWA LIVE NDANI ÉMISSION SANAA YA NYUMBANI KWA SIKU YA LEO USIKOSE KUSIKILIZA NAPIA TOWA MAONI YA...
17/03/2025

MSANII NOVA KIMENDE ATAKUWA LIVE NDANI ÉMISSION SANAA YA NYUMBANI KWA SIKU YA LEO USIKOSE KUSIKILIZA NAPIA TOWA MAONI YAKO

Msanii jdd amempoteza mama yake mzazi hapo jana  Pole kwa msanii wetu 💪🏿
14/03/2025

Msanii jdd amempoteza mama yake mzazi hapo jana

Pole kwa msanii wetu 💪🏿

10/03/2025

Washa redio now tuko live

Usikose kusikiliza kipindi sanaa ya nyumbani kumi jioni hadi kumi na moja jioni mualikwa ni msanii mr alimasi usikose ku...
10/03/2025

Usikose kusikiliza kipindi sanaa ya nyumbani kumi jioni hadi kumi na moja jioni mualikwa ni msanii mr alimasi usikose kumuuliza chochote kitu

Usikose kusikiliza kipindi sanaa ya nyumbani kesho na saa kumi jioni hadi kumi na moja jioni waalikwa ni father drago na...
02/03/2025

Usikose kusikiliza kipindi sanaa ya nyumbani kesho na saa kumi jioni hadi kumi na moja jioni waalikwa ni father drago na wachekeshaji wawili Jay og na esco DRC usikose kusikiliza vipaji vya nyumbani @

DELCAT IDENGO Alikuwa rasta aliyejichora tattoo ya Congo kwenye kuta za kifua chake. Kila kinywa chake kilipofunguka, ms...
18/02/2025

DELCAT IDENGO
Alikuwa rasta aliyejichora tattoo ya Congo kwenye kuta za kifua chake. Kila kinywa chake kilipofunguka, msingi wa mahubiri yake ulijikita juu ya haki na Amani. Alikuwa mwanaharakati aliyeishi ndani ya falsafa na maono ya "Patrick Lumumba."

Alichukizwa kuona Congo DRC ina laana ya Rasilimali. Yaani utitiri wa madini katikati ya watu maskini. Hili lilimumiza sana.

Alikuwa mwanamuziki aliyeamini, kuimba mapenzi wakati Congo haina amani, ni kuionyesha dunia kiwango cha upumbavu unaopatikana ndani ya akili yako."

DELCAT IDENGO kila alipozama booth. Microphone ilitumika k**a nyenzo ya kuwasilisha hasira kali zinazoishi juu ya kifua chake.

Alikemea watawala dhulumati, na kufokea mabeberu wanaokwamisha amani ya Congo. Ujasiri wa kuimba kile ambacho jamii ina njaa ya kukisia. Ulimtengenezea jina, hadhi, na heshima kwenye mji wa Goma. Alikuwa ni mfalme wa kivu ya kaskazini."

Siku kadhaa zlizopita, aliingia booth akaachia wimbo wenye mahadhi ya rege akauita "bunduki." Wimbo ukikemea uwepo wa M-23 ndani ya Congo.

Baadhi ya mistari katika wimbo ule wenye mahadhi ya 'sweet rege' ni maneno haya.

Jambo wavamizi/
mmetufanya wakimbizi/
Najua mnatuogopa/
ila roho yenu ngumu imewaleta hapa/
Mtaishia hapa hapa/
Hiii ni nchi ya wa congo man/
Hapa ni macho kwa macho/
Hakuna kukimbia tena."

"DELCAT IDENGO." Hakujua anawatisha binadamu walioenda "Goma" wakiwa hai kimwili lakini kifkra walishajifia. Hakuna kitu hatari k**a kupambana na mwanadamu ambaye ni mfu wa fikra.

"Kuwatungia wimbo M-23. Ni k**a kukilazimisha kifo kije kazini wakati kimechukua likizo ya kuua."

Alfajiri ya leo goma imetikisika. Rastafarian, mwanamuziki, aliyeamini kwenye harakati za ukombozi wa Congo. Mdomo wa bunduki umehitimisha safari ya uwepo wake chini ya jua kikatili.

Ameuawa baada ya kupigwa risasi katika jiji la Goma na watu inaosadikika ni waasi wa M-23.

"DELCAT IDENGO" alitamani kuona siku moja Congo ina amani ya kudumu. Watu wana gonga cheer's huku wakitafuna kuku, wanapotazama kiuno cha "Fally Ipupa." Bahati mbaya amelala mauti, akiwa hajashuhudia ndoto aliyoitamani, ikigeuka kuwa simulizi ya kweli."

IMEANDIKWA NA Mufaridji Ngarambi Fei @

MCHEKESHAJI WA UVIRA KITWERA AMEVURUGWA  SOMA ALICHO ANDIKA"Uvira kwa Nini amujuwi samahani yetu sisi? 🚨Munaleta wa Arti...
13/02/2025

MCHEKESHAJI WA UVIRA KITWERA AMEVURUGWA SOMA ALICHO ANDIKA
"Uvira kwa Nini amujuwi samahani yetu sisi? 🚨Munaleta wa Artiste 3 tena wachekeshaji wazuri👌 Ila akuna ata muchekeshaji mmoja wa uvira ambaye atawakaribisha k**a muzalendo wa nyumbani 👈kisha nyuma unasema ooooooh mweye amuendaki mbali ,na wakutufanya Sisi tuende mbali zaidi ni nyinyi Ila uvira tukileta wasanii wa kubwa Sisi munatubaguwa kisha unawaza kesho ni kienda lomba collabo nao nasema Niko wa uvira 👈 wataelewa nini,sibatasema uvira tulikuwa atukuona wa comédiens 😭Kisha kesho goma inaendelea kutushinda aseme Sanaa yao inalipa , Calvin Mulingu wa kivu star njo alitowa fido drc👌kumukutanisha na wa artistes wa kubwa ,mukuwe najuwa kutuprepare sasa tulisha komala ,kicheche Tanzanie 🇹🇿 alifika apa akucheza na mtu juu yenu ,tena munatushusha mbele yake akatuona wa ovyo 😭ba congolais ya uvira 👈 déjà uvira ilisha kuwa ville,apa munapashwa tayarisha bangine ba comédiens ya uvira benye batapokeya benzabo, ata aiko miye Ila kukuwe tu !bauvira nabo njo besoin yang 👏 nama affiche zabo nabo zitoke za bote kwa pamoja njo vile banatoshaka talent za kunyumba 👈

NB: nawakati munawa invite Ku radio ita na bale bakunyumba kisha journaliste ana baambia aba njo nasiye betu banguvu apa🫷pale unatupa valeur,ata na kufanya collabo aita kuwa nguvu ju nabo batajuwa k**a nikifanya nauyu naweza kumubeba shabiki, uvira 👈 tuache bujinga,,

REMARQUE : problème Moya batu ya uvira tunakuwaka nayo ni iyi: unaleta artiste kutoka inje ya inchi ao inje ya uvira 👈 akifika uvira unashindwa kuonganisha mtoto wa nyumbani ju ya buduru Yako, kesho naye akomale ,mukuwe natuacha Ila ujuwe tu k**a ulisha fanya dépensé Yako kwa ule mtu ulileta aita punguka savile wenge mugere na mtoto wa nyumbani naye aende mbele zaidi 👈

Ivi amuko nasikiya haya baraka nayo yende natuzidi Ku comédie?? Leo Jackson wa kizazi kipya anakuwa juu zaidi 👈🤣🤣aiko anajuwa cheza ,apana ni watu kumusukuma mbele tu! Basi k**a munapenda twende nyuma kila Siku akuna shida 👈

K**a nilisema makosa naomba samahani sana"

Usikose kusikiliza kipindi sanaa ya nyumbani kumi jioni hadi kumi na moja  zadbi baleine na gang boy watakuwa nyumbani u...
10/02/2025

Usikose kusikiliza kipindi sanaa ya nyumbani kumi jioni hadi kumi na moja zadbi baleine na gang boy watakuwa nyumbani
usipange kukosa

Ujambo mpenzi msikilizaji wa kipindi Sanaa ya Nyumbani 🤚Uongozi wa kipindi unao furaha ya kukutangazia WATANGAZAJI WAPYA...
09/02/2025

Ujambo mpenzi msikilizaji wa kipindi Sanaa ya Nyumbani 🤚
Uongozi wa kipindi unao furaha ya kukutangazia WATANGAZAJI WAPYA wa kipindi chenu mkipendacho bahada ya mtangazaji RAMA KELLY RK kwenda mapumzikoni kwa mda usio fahamika.
Kuanzia sasa hawa ndio watakuwa watangazaji wapya wa kipindi na page yetu hii:
MBOTO MEA ALEXIS
JACKSON MUHOLEZA JM
PHILIPPE TANDURA
MUFARIDJI NGARAMBI FEI

Tuwatakie kazi njema na karibu kwenye kipindi matata 🔥

Adresse

Mairie
Uvira

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Emission Sanaa ya Nyumbani publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter L'entreprise

Envoyer un message à Emission Sanaa ya Nyumbani:

Partager