
22/04/2025
Waanga wa ugonjwa wa Kipindupindu Kazimia wanufaika kwa msaada
Baada ya visa Congo vya Kipindupindu kuongezeka katika mji wa Kazimia ndani ya sekta ya NGANDJA atimaye shirika la médecin du monde limeweza kuwajia waanga kwa ajili ya msaada.
Kwake kiongozi wa PRECODESA katika mtaa wa afya wa KAZIMIA Bwana SHOMARI IBÙCHWA TRÉSOR amesema kwamba waanga wameweza kunufaika kwa ndoo moja, dumu moja pamoja Na mti mmoja wa sabuni.
" Baada ya visa vya Kipindupindu kuongezeka katika mtaa wa afya wa Kazimia, shirika la médecin du monde limeweza kuwaletea waanga msaada huu wa ndoo, dumu kwa ajili ya kuteka maji Na wamepata Pia Mti mmoja wa sabuni kwa ajili ya kufuwa Na kuoga kwa ajili ya kijikinga Na ujonjwa huo hatari wa Kipindupindu. Japo kuwa visa vimeisha ila hii ni kwa ajili ya kuwapa pole waanga" alieleza.
Mwishowe ameongeza kutoa ushauri ili kupunguza Na kukomesha ugonjwa huo
"Ni kwa masikitiko makubwa Sana kwani kuna baadhi ya watu wengine walikuwa wakishikwa Na ugonjwa huo wanachukuwa mganga nyumbani kwao"