Shirko

Shirko Awadh Salim popularly known as Shirko, the best Musician/producer well recognized in East Africa.

Major hits: Nawewe tu, Najua ft Berry black, Kidogo Diamond ft P.Square, Nibebe, Natamba & founder of Yamoto Band (Aslay, E.Bella, Beka flavour & Mbosso)

Tutege skio pale kwenye nyumba ya kutunga sheria na matekelezo ya tarehe 1   zitaskika sauti zao manguli wa sanaa ya mch...
29/10/2025

Tutege skio pale kwenye nyumba ya kutunga sheria na matekelezo ya tarehe 1 zitaskika sauti zao manguli wa sanaa ya mchanga wa bahari
naskia kuna orodha ya wasanii 70 wanaowania kutumbuiza kule ila acha tuskie kikao cha wanne hao leo wakiwa na kwenye ya ✍🏻

31st October kalenda limeshapigwa pini na nafasi ya kutumbuiza inaletwa kwako na mvunja steji maalum kwenye nafasi ya bu...
24/10/2025

31st October kalenda limeshapigwa pini na nafasi ya kutumbuiza inaletwa kwako na mvunja steji maalum kwenye nafasi ya burudani Dazlah binafsi Ntakuwepo mimi pale nyuma nikitoa maelekezo na kupiga samasolt ambazo naziona tu kwenye ndoto nikiwa na jet li. Oyaa don’t miss out this 6th edition niπŸ”₯ watu wakiendelea na ngonjera ya majibuzano pale kwenye page zao weka alama ya kukumbuka hii tarehe. Bango linajieleza kwenye viingilio na ticket zinapatikana kwete tovuti ya www.pwaniinnovationweek.com/tickets
fans

21/10/2025

πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

Binadamu wanachagua kudharau vizuri na kufanya au kuwaaminisha wengine kuwa havipo. Usifiche ulichojaaliwa kwa faida ya ...
20/10/2025

Binadamu wanachagua kudharau vizuri na kufanya au kuwaaminisha wengine kuwa havipo. Usifiche ulichojaaliwa kwa faida ya kuonekana na wanaopenda pamoja na watakao heshimu neema yako, ubunifu au zawadi kutoka kwa aliyekuumba. Ukiondoka duniani maskini kwa kutegemea vile ulivyoaminishwa kuwa ndo utajiri kesho utajutia kwanini hukutumia neema, ujuzi au ubunifu wako sababu tu ulikatishwa tamaa na watu weye husda au wasiokuwa na taaluma ya kuelewa tunu yako na wale ambao uliwaamini kuwa bila wao kukushauri wewe hufanyi lolote. Ukiendelea kuishi hivyo, utapitwa kimaendeleo, kimanufaa, kiubora na watu ambao wanafanya chini ya kiwango au daraja aliyokuinua nayo Mungu na utaona wanafanikiwa we unakaa kinyonge. Kisha hao hao ambao waliokuaminisha cha kwako ni cha kawaida sana na kukukatisha tamaa, wakisifie cha mwingine ambacho sio bora k**a chako mradi tu kukufanya uwe muoga wa kutojiamini na kuthubutu kufanya. Acha dunia ione ubunifu wako na ubora na heri au tunu aliyokupa Mungu kwa ubunifu au taaluma binafsi sababu kweli mficha uchi hazai.

Pumzika salama shujaa, mzalendo ulielibeba taifa kwenye kifua. Unaondoka na mioyo ya wananchi ambao hawatawahi kusahau u...
16/10/2025

Pumzika salama shujaa, mzalendo ulielibeba taifa kwenye kifua. Unaondoka na mioyo ya wananchi ambao hawatawahi kusahau ujasiri wako katika kila hatua ya kuleta upendo kwenye ncha ya amani na usawa nchini. Unaondoka tena huku bado nchi inahitaji busara yako, ulezi na usimamizi wako. BABA RAILA pumzika kwa amani.

Pole sana brother kwa yaliyokusibu Mungu atakujaalia upate yale uliyotapoteza ambayo yamebeba kazi zako muhimu. Vijana w...
14/10/2025

Pole sana brother kwa yaliyokusibu Mungu atakujaalia upate yale uliyotapoteza ambayo yamebeba kazi zako muhimu. Vijana wetu tunaoishi nao tunaishi nao kwa wasi wasi hujui leo na kesho utanusurika ama utakuwa miongoni mwa wanaopata matatizo k**a hayo. Vijana wetu wenyewe majirani zetu wenyewe imekuwa sio poa tena tukikutana nao. Pole sana brother Beka Ruga

Wachana na huyo alie haribu picha huko nyuma skia hii!..Kutupa au kukiondoa kisicho thamani nawe kwenye maisha yako kuli...
14/10/2025

Wachana na huyo alie haribu picha huko nyuma skia hii!..

Kutupa au kukiondoa kisicho thamani nawe kwenye maisha yako kulingana na nafsi yako inavyopenda au kuchagua kuachana kitu, ni namna moja ya kumnufaisha mwingine ambae anaejua kutumia hicho ambacho hakikufai. Na huo ndio mfumo wa maisha. Usije kuchukia kwanini (kile ulicho kitupa au kukidharau) kinamfaa na kumnufaisha mwingine na kikakufanya ukajenga uadui na chuki hususan kwa mtu usiemjua kisa kinachomfaa yeye ni kile ambacho hakikukufaa wewe kipindi unacho.

13/10/2025

Kuna muda tunatakiwa kufurahia kila hatua k**a zawadi ya kupumua, kwenye kukosa au kutusua, yote kujipiga kifua kuwa kila muda wako ni muda sahihi wa kutimiza au kujenga mafanikio yako hatua kwa hatua. Ukija kuelewa kuwa hii yote ni kwa ajili ya maisha yako binafsi utakuwa serious. Kwa dalili au sababu gani? Ulitoka kwenye kizazi pasipo kushikana na kiumbe mwingine, pumzi yako hausaidiani kupumua na mwingine, mapigo ya moyo yako hayaendi kumdundia mwengine kwenye kifua chake na siku ya kwenda kuzikwa shimo lako halitaweka nafasi ya mtu mwingine. Its all about you and your decisions. Tunaharibu kuingiza wengine kwenye vitu ambavyo vinataka tumalizane navyo sisi wenyewe ndio maana kwenye maamuzi tunakosa kuamua haraka tunasita na heri nyingine hazina subira.

08/10/2025

Special appearance kidogo pale ku support ndugu zangu wa Tukiachilia mbali salam hapo kwenye hiyo video la muhimu tuwape support kwenye link hapo chini. Dude ni
πŸ‘‡πŸΌπŸ‘‡πŸΌ

https://youtu.be/CSpFqHlArhY?si=h9iPkasYpJGHPHty

Maisha yako na afya yako pamoja na pumzi jumla uhai vina thamani kubwa sana kiasi usiwahi kuvidhalilisha kisa kusemwa au...
03/10/2025

Maisha yako na afya yako pamoja na pumzi jumla uhai vina thamani kubwa sana kiasi usiwahi kuvidhalilisha kisa kusemwa au kuharibiwa au husda ya binadamu wenye wivu ambao unasababishwa na hofu yao kuwa ipo siku ukubwa wako, ubora wako au thamani yako itakuja kuwafedhehesha mmoja mmoja sana kwa waliyokufanyia ili usijitambue umuhimu wa uliyojaaliwa kisa masimango yao.
Jumaa Mubarak

Shukrani za dhati kwa waandalizi na wafanikishaji wa PWANI GOT TALENT (PGT) inayofanyika pale SWAHILI POT nilipata fursa...
29/09/2025

Shukrani za dhati kwa waandalizi na wafanikishaji wa PWANI GOT TALENT (PGT) inayofanyika pale SWAHILI POT nilipata fursa ya kuhusishwa na kutoa ushirikiano kwenye ukaguzi wa vipaji awamu ya kwanza, k**a JAJI kwa vipaji mbali mbali vilivyopo Mombasa. Imenipa
Moyo sana kuona vipaji vipo na vinajitahidi kutumia fursa kuonyesha walichokua nacho kujaribu kutafuta nafasi mbali mbali kwa kutumia uwezo wao. Kizazi kipya hakijaniangusha kimenipa sura nyingine ya ukuaji wa sanaa tunayoitegemea miaka ya baadae. Sikujutia masaa yangu 11 kusimamia ukaguzi huu wa vipaji vilivyohusisha wana sanaa wa vitengo mbali mbali takriban 70 nikishirikiana na wenzangu mwanzo hadi mwisho. Mungu wabariki wasanii wetu na sanaa yetu kwa ujumla.

Address

London

Opening Hours

Monday 11am - 10pm
Tuesday 11am - 10pm
Wednesday 11am - 10pm
Thursday 11am - 8pm
Friday 2pm - 5am
Saturday 2pm - 8pm
8pm - 5am

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shirko posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Shirko:

Share

Category