Shirko

Shirko Awadh Salim popularly known as Shirko, the best Musician/producer well recognized in East Africa.

Major hits: Nawewe tu, Najua ft Berry black, Kidogo Diamond ft P.Square, Nibebe, Natamba & founder of Yamoto Band (Aslay, E.Bella, Beka flavour & Mbosso)

Ijumaa nyingine pale ZANZIBAR 🤲🏼 kauli mbiu “SUBRA”
08/08/2025

Ijumaa nyingine pale ZANZIBAR 🤲🏼 kauli mbiu “SUBRA”

INNA LILLAAHI WA INNAA ILEYHI RAAJIUUNNatangulia kumshukuru Mungu kwa kila neema aliyotujaalia na baraka zake nyingi zil...
04/08/2025

INNA LILLAAHI WA INNAA ILEYHI RAAJIUUN

Natangulia kumshukuru Mungu kwa kila neema aliyotujaalia na baraka zake nyingi zilizo tuzunguka. Leo hii huzuni imetanda kwenye mioyo yetu kuanzia kwenye familia jamaa na marafiki. Alhamdulillaah leo Tumefiwa na Baba yetu (Babaake AMOURY ) wengi munafahamu vyema mimi na ndugu yangu AMOURY tumetoka wapi tumeishi vipi kwa miaka hadi leo. Tumefunga safari hadi Zanzibar hususan kwa minajili ya kumjulia hali mgonjwa hospitali ila kwa qadari yake Muumba alitupangia hadhari ya msiba na pasipo budi tunasema Alhamdulillaah. Tutazika mwili wa marhum Zanzibar Bububu kwa abiola, insha Allaah kwa wale wakatao kuwa nasi tutajumuika pamoja kwenye maziko ila kwa wale ambao wapo mbali basi tunatarajia dua kwa wingi insha Allaah. Allaah analeta viumbe wake wema na kwa qudra zake anawachukua. Kwa atakaeipata taarifa hii basi amfikishie mwingine.

Pindi Mungu anavyokujaalia uwezo binafsi k**a kiambatanishi cha kipaji bora, kikawiana vizuri sana na ujuzi wa kufunzwa ...
30/07/2025

Pindi Mungu anavyokujaalia uwezo binafsi k**a kiambatanishi cha kipaji bora, kikawiana vizuri sana na ujuzi wa kufunzwa na mtu, kwa kusikia, kusoma au kujifunza mwenyewe kwa kujaribu mawazo yako mwenyewe na ukayajulia matumizi yake yakakuletea faida kwenye harakati zako za kazi na maisha binafsi amini sio kitu cha kuchukulia kawaida kabisa. Unafaa kuthamini kitu hicho kwa moyo wako wote kukilinda kwa akili yako yote pasina kudharau hata chembe ya tunu hiyo.

Tuwe makini sana baada ya kuwa na zawadi hii kwenye maisha yetu, wengi tunapenda tuonekane bora kwa kufanya mbele ya wengi ilimradi tupate sifa tujihisi bora miongoni mwa watu bora duniani tukisahau kuwa kuna wengi ambao wanatamani hata robo ya tuliyojaaliwa. Wengine wanatumia mapesa mengi angalau wapate kidogo ya kile tulicho nacho. Wengine walishapoteza thamani ya ukubwa wa tuliyojaaliwa na wanatamani wapate kuwa navyo tena ila haviji mara mbili kiurahisi.

Mara ya kwanza kinakuja na usipokigundua na kukithamini kikiondoka ni lazima kikukosti kitu cha thamani ndio kije tena sio kwa asilimia zote. Kuna hata hata ya kuzungukwa na vijicho na roho za wivu sehemu ambazo hutarajii roho mbaya ya kutamani ulicho nacho zikajenga “kwanini yeye na sio mimi?” kwenye mioyo yao. Ila huwezi kuwajua sababu wengi ni wale ambao wapo karibu nawe na huwezi kukaa bila wao.

Tukijifunza kuthamini na kulinda vinavyotufanya tujihisi kuwa na thamani na furaha kwenye mioyo yetu basi tujifunze na kuvilinda sababu tunapokuja kuvipoteza, wengi watatukimbia, watatukataa, watatudharau, watatuona hatuna thamani na hatustahili kuwa na wao na huo ndio mwanzo wa upweke na kukata tamaa maishani.

25/07/2025

😢 my brother 🙏🏼 tumeonana tena ndani ya Zanzibar. Mungu aendelee kukubariki.

With my brother   siku ya jana ilikuwa ya furaha sana. Ni miaka imepita  Alhamdulillaah 🙏🏼 tumekutana tena.
23/07/2025

With my brother siku ya jana ilikuwa ya furaha sana. Ni miaka imepita Alhamdulillaah 🙏🏼 tumekutana tena.

Another good day, Thank you God.
20/07/2025

Another good day, Thank you God.

Leo nataka muniambie kile ambacho wengi wenu mnatamani ningelikuwa nimechagua kipi kati ya hizi option tatu.1. Ningeliba...
19/07/2025

Leo nataka muniambie kile ambacho wengi wenu mnatamani ningelikuwa nimechagua kipi kati ya hizi option tatu.

1. Ningelibakia kuwa narap (dancehall)
2. Ningelibakia kuwa Music producer
3. Niwe tu natumbuiza kupiga Violin (violinist performer)
4. Bonus option - au nifanye tu vyote japo ni ngumu sana ku manage vyote!!!

Weka kwenye comment hapo👇🏼

Nakumbuka miaka nikiwa Zanzibar nlienda kumtembelea rafiki yangu mitaa flani kipindi hicho tena ndo umaarufu sana yaani ...
18/07/2025

Nakumbuka miaka nikiwa Zanzibar nlienda kumtembelea rafiki yangu mitaa flani kipindi hicho tena ndo umaarufu sana yaani hadi ile unajistukizia kukatiza mitaa na kila mtu vile alikua anatamani kukuona, kukaa nawe, kusalimiana nawe. Hadi ukiamua kwenda sehemu zenye watu wengi unakuwa attention kiasi kwamba ilikua changamoto miaka hiyo hadi ukienda sehemu ulioalikwa k**a harusi, birthday misiba hadi mskitini ndo watu wanakushangaa wanaacha shughuli zao wanakutazama au kukusema au kuona sijui wewe ni odd one out. Kuna muda msanii anatamani aishi k**a binadamu wa kawaida sababu ndio uhalisia wake kazi nyingine na maisha ndani ya kazi zao ni k**a biashara maigizo ila dhehebu, jaamii nyingine tunazoishi nao na tabia ngozi na mazoea yanawafanya watu wenye umaarufu na ushawishi duniani kujiona tofauti na binadamu wa kawaida. Ndio maana wengi wanaamua wakae tu kujitenga sababu jamii zetu hizi zinaishi kwa mazoea ya kushangaa shangaa sana na kufikia hadi mtu kukuchukia au kukudharau na hajawahi kuishi na wewe akakujua vizuri wewe ni mtu wa aina gani. Hii inawatokea wasanii wengi sana kuwa unaingia mskitini hata k**a khatibu au anaehutubia siku hiyo mada yake ilikuwa tofauti na akakuona wewe basi anaamua kuishi na wewe na utatafuta pakutokea lakini hakuna mada itakuhusu wewe. Ila kwa sababu kila mtu anaishi maisha anayotaona sahihi kwake na kila mmoja anatetea ugali wake hamna kulaumiana mwisho wa siku tunasalimiana na maisha yanaendelea. Ijumaa njema kwenu 🤲🏼 Mungu awabariki sana.

Address


Opening Hours

Monday 11:00 - 22:00
Tuesday 11:00 - 22:00
Wednesday 11:00 - 22:00
Thursday 11:00 - 20:00
Friday 14:00 - 05:00
Saturday 14:00 - 20:00
20:00 - 05:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shirko posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Shirko:

Shortcuts

  • Address
  • Opening Hours
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share