Banza Media

Banza Media "Burudani | Gossip | Lifestyle
đź“© DM for Ads & Collabs
🎬 New content daily"

Muigizaji wa Fast & Furious, Vin Diesel, ameashiria kupitia Instagram kuwa huenda nyota wa soka Cristiano Ronaldo (CR7) ...
13/12/2025

Muigizaji wa Fast & Furious, Vin Diesel, ameashiria kupitia Instagram kuwa huenda nyota wa soka Cristiano Ronaldo (CR7) akaonekana katika muendelezo ujao wa filamu hiyo. Kauli hiyo imezua mjadala na hamasa kubwa kwa mashabiki wa filamu na soka duniani, kutokana na umaarufu mkubwa wa CR7. Endapo itatimia, itakuwa hatua kubwa katika tasnia ya burudani.

Guinness World Records Yathibitisha Kupokea Ushahidi wa Jaribio la TruphenaShirika la Guinness World Records limethibiti...
13/12/2025

Guinness World Records Yathibitisha Kupokea Ushahidi wa Jaribio la Truphena

Shirika la Guinness World Records limethibitisha kupokea na kuanza mchakato wa tathmini ya ushahidi wa jaribio la kihistoria lililofanywa na mwanaharakati wa mazingira kutoka Kenya, Truphena Muthoni, aliyedai kukumbatia mti kwa muda wa saa 72 mfululizo.

Kupitia chapisho rasmi kwenye mitandao ya kijamii, Guinness World Records imeeleza kuwa jaribio hilo limechochewa na mapenzi ya dhati kwa miti pamoja na mchango wake muhimu katika mfumo wa ikolojia. Hatua hiyo imepokelewa kwa maoni chanya na mvuto mkubwa kutoka kwa watu mbalimbali duniani, ikiwa ni ishara ya kuongezeka kwa uelewa na uhamasishaji wa masuala ya uhifadhi wa mazingira.

Hata hivyo, Guinness World Records imesisitiza kuwa hadi sasa, rekodi inayotambuliwa rasmi bado ni ya saa 48, ambayo Truphena aliweka awali jijini Nairobi. Kuhusu jaribio la saa 72, uamuzi wa mwisho utafikiwa baada ya ushahidi wote kukamilika kuwasilishwa na kufanyiwa tathmini kwa mujibu wa taratibu na kanuni za Guinness World Records.

Wakati mchakato huo ukiendelea, hatua ya Truphena inaendelea kupongezwa k**a mfano wa ujasiri, kujitolea na dhamira ya dhati katika kulinda mazingira, sambamba na kutoa matumaini mapya katika juhudi za kimataifa za kuhifadhi sayari kwa vizazi vijavyo.

Uchambuzi wa Verse ya Ibraah kwenye Wimbo IPO SIKUVerse ya msanii Ibraah () katika wimbo IPO SIKU, alioshirikishwa na , ...
13/12/2025

Uchambuzi wa Verse ya Ibraah kwenye Wimbo IPO SIKU

Verse ya msanii Ibraah () katika wimbo IPO SIKU, alioshirikishwa na , imeonekana kuchukua nafasi kubwa katika mitandao ya kijamii, hususan TikTok na Instagram nchini Tanzania. Verse hii imekuwa kivutio kikuu cha wimbo huo, hali iliyosababisha kuongoza kwa challenges nyingi za TikTok pamoja na kutumiwa sana k**a sauti (sound) kwenye post na reels za Instagram.

Kwa mujibu wa mwenendo wa mitandao ya kijamii, verse ya Ibraah imeonekana kuwa ndiyo sehemu inayovutia zaidi wasikilizaji, jambo linaloonyesha uwezo wake wa kuwasilisha hisia na ujumbe unaogusa jamii. Umaarufu huu haujatokea kwa bahati mbaya, bali ni matokeo ya ubora wa uandishi, delivery yenye hisia, pamoja na sauti inayobeba mvuto wa kipekee.

Kwa upande wa nyimbo za mapenzi, Ibraah ameendelea kuthibitisha kuwa ni msanii mwenye uthabiti na ubora wa hali ya juu. Kwa muda mrefu hajawahi kuwaangusha mashabiki wake katika eneo hili la muziki, na verse yake kwenye IPO SIKU ni ushahidi mwingine wa uwezo wake katika kuwasilisha mapenzi kwa lugha rahisi lakini yenye uzito wa kihisia.

Kwa hitimisho, verse ya Ibraah kwenye IPO SIKU si tu sehemu ya wimbo, bali imekuwa chombo cha utamaduni wa kidijitali, kikiongoza mitindo (trends), changamoto (challenges), na matumizi ya sauti katika mitandao ya kijamii, jambo linalothibitisha ushawishi wake mkubwa katika muziki wa kizazi cha sasa.

HARMONIZE AMJIBU MAJIZO, ATOA KAULI NZITO KUHUSU DIAMONDMwanamuziki Harmonize ameibuka na kutoa kauli nzito baada ya Maj...
12/12/2025

HARMONIZE AMJIBU MAJIZO, ATOA KAULI NZITO KUHUSU DIAMOND

Mwanamuziki Harmonize ameibuka na kutoa kauli nzito baada ya Majizzo kumtaja k**a msanii aliyeibuliwa na Diamond Platnumz.

Harmonize amesema alimtafuta Majizzo na kumshauri kuacha kumtaja Diamond k**a mtu aliyemtoa kimuziki, akisisitiza kuwa Diamond hastahili heshima hiyo ingawa anatambua mchango wake kwenye safari yake ya muziki.

Msanii huyo amesema kuwa yeye ni “msanii mkubwa” kiasi kwamba Diamond anatakiwa kuomba msamaha kwake badala ya kutajwa kuwa mtu wake wa kumbukumbu. Amekiri kuwa kwa sasa hawezi kumheshimu Diamond kutokana na namna ambavyo, kwa mujibu wake, amekuwa akitumia jina lake vibaya.

Aidha, Harmonize amemshutumu Diamond kwa kuwa chanzo cha anguko la lebo yake ya Konde Gang. Amesema Diamond alikuwa anatoa ahadi zisizotekelezeka kwa wasanii waliokuwa chini ya lebo yake, akiwahadaa kuwa atawaunga mkono wakiondoka Konde Gang.

Akitolea mfano, Harmonize amemgusia msanii Angella, aliyedaiwa kuahidiwa kolabo na Zuchu—ahadi ambayo hadi leo haijatimia. Vilevile, Harmonize amefunguka kuwa Diamond alimlipa mwanasheria wa Ibraah wakati msanii huyo alipokuwa akitafuta njia ya kujitoa katika lebo ya Konde Gang.

Harmonize ametahadharisha kuwa kuanzia sasa atamchukulia hatua za kisheria mtu yeyote atakayehusisha jina lake na Diamond Platnumz bila msingi.

Je uko tayari?
11/12/2025

Je uko tayari?

Ili Ndo jibu la  Kwa Mashabiki Wanao muandama mtandaoni Ame post picha Mpya na kuwajibu Mashabiki kupitia Wimbo wake  (M...
11/12/2025

Ili Ndo jibu la Kwa Mashabiki Wanao muandama mtandaoni

Ame post picha Mpya na kuwajibu Mashabiki kupitia Wimbo wake (MIMI)
Hii imekuja baada ya diamond platnumz kusapoti CCM Ambayo ina Raisi Samia Ambae alitangazwa k**a rais ila Uku wananchi wengi hawajakubaliana na matukio

Msanii  ameonekana Akiwa makao makuu ya  Kwa mara ya Kwanza Akiwa na manager na producer wake  Nchini Dubai Warner music...
09/12/2025

Msanii ameonekana Akiwa makao makuu ya Kwa mara ya Kwanza
Akiwa na manager na producer wake Nchini Dubai

Warner music Africa ni kampuni ya usambazaji Wa Muziki Inayo simamia wasanii Wengi Afrika Akiwemo Msanii kutoka Tanzania Ambae Yuko chini ya usimamizi Wa kampuni Iyo Kwa Miaka sasa
Pia inakuunganisha na wasanii wakubwa,inasaidia kumpeleka Msanii international na connection nyingi za kibiashara ya Muziki

Wenda marioo akawa Msanii Wa pili Tanzania kujiunga na kampuni Iyo baada ya kufanya vizuri mwaka huu

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, , amerejea nchini Tanzania pamoja na mke wake .priscy baada ya kuwa nje ya nchi kwa mud...
01/12/2025

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, , amerejea nchini Tanzania pamoja na mke wake .priscy baada ya kuwa nje ya nchi kwa muda tangu kabla ya Uchaguzi wa Oktoba 29, 2025. Wawili hao walikuwa wakitokea Nigeria na kupita Kenya kabla ya kuwasili jana jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kurejea, Jux alitembelea duka lake la African Boy, ambalo lilivamiwa na waandamanaji wakati wa vurugu za uchaguzi na kuporwa mali zote. Ikumbukwe kuwa tangu tukio hilo, msanii huyo hakuwa amerejea nchini.

Kupitia ukurasa wa African Boy, kampuni imetoa ujumbe wa matumaini ikisema:

“African Boy inarudi upya—ikiwa bora zaidi kuliko ilivyowahi kuwa

Dunia ya muziki imeingia katika majonzi kufuatia kifo cha gwiji wa reggae kutoka Jamaica,   aliyefariki akiwa na umri wa...
25/11/2025

Dunia ya muziki imeingia katika majonzi kufuatia kifo cha gwiji wa reggae kutoka Jamaica, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 81. Taarifa ya msiba huu ilithibitishwa na mkewe, ambaye alieleza kuwa msanii huyo aliaga dunia baada ya kupata mshtuko na baadaye kuugua homa ya mapafu.

Jimmy Cliff anabaki kuwa mmoja wa wanamuziki walioipa hadhi na kuitangaza reggae duniani. Kupitia vibao maarufu k**a “Many Rivers to Cross,” “You Can Get It If You Really Want,” na “The Harder They Come,” aliweza kuigusa mioyo ya watu na kueneza ujumbe wa upendo, amani na ustahimilivu kwa vizazi mbalimbali.

Mbali na muziki, Jimmy Cliff pia aling’ara katika uigizaji, hususan kupitia filamu ya The Harder They Come (1972), ambayo ilichangia pakubwa kuutambulisha muziki na utamaduni wa Jamaica katika anga za kimataifa.

Wapenzi wa muziki na viongozi wa tasnia mbalimbali duniani wameendelea kutuma salamu za rambirambi, wakimtaja Jimmy Cliff k**a nembo ya reggae, msambazaji wa utamaduni wa Jamaica, na msanii aliyeacha alama isiyofutika.

Sauti yake itaendelea kuishi katika kumbukumbu na muziki wa mashabiki wake duniani kote.

Pumzika kwa amani, Jimmy Cliff. 💚💛❤️

Address

Kiambu Road
Kiambu Road
1234

Telephone

+254745736132

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Banza Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Banza Media:

Share