Chronicles media

Chronicles media Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Chronicles media, News & Media Website, Kilifi.

Utawala wa kijeshi wa Burkina Faso umeivunja tume ya uchaguzi nchini humo ukiitaja kuwa ni ufujaji wa fedha.Badala yake ...
18/07/2025

Utawala wa kijeshi wa Burkina Faso umeivunja tume ya uchaguzi nchini humo ukiitaja kuwa ni ufujaji wa fedha.

Badala yake wizara ya mambo ya ndani itashughulikia uchaguzi katika siku zijazo, runinga ya serikali ya RTB iliripoti.

Tangu utawala huo ulipoingia mamlakani mnamo Septemba 2022, viongozi wake wa mapinduzi wameanzisha mageuzi makubwa, ikiwa ni pamoja na kuahirishwa kwa uchaguzi ambao ungesababisha kurejea kwa utawala wa kiraia.

Uchaguzi mkuu ilitarajiwa kufanyika mwaka jana, lakini serikali ya kijeshi iliongeza muda wa mpito kwa demokrasia hadi Julai 2029, na kumruhusu kiongozi Kapteni Ibrahim Traoré kusalia madarakani na kuwa huru kugombea uchaguzi ujao wa urais.

Shirika la habari la AFP linamnukuu Waziri wa Utawala wa Wilaya Emile Zerbo akisema kwamba tume ya uchaguzi "iligharimu" serikali takriban dola 870,000 kwa mwaka.

Kufuta tume hiyo "kutaimarisha udhibiti wetu wa mchakato wa uchaguzi na wakati huo huo kupunguza ushawishi wa kigeni", aliongeza Zerbon.

Welcome 🇰🇪 , You see every year we impose extra tax on beer and wine.Now EABL Exits Kenya, Diageo Cites Losses, CMA Halt...
22/06/2025

Welcome 🇰🇪 , You see every year we impose extra tax on beer and wine.

Now EABL Exits Kenya, Diageo Cites Losses, CMA Halts NSE Trading.

In Texas, beer are same price as water and definitely cheaper than coffee, ice tea, ice cream and bread.

Here in the paradise of Kenya🇰🇪 a beer is a staggering ksh 250 and you hope to keep EABL as one of your biggest employers!

In both Russia and USA, beer is affordable for every human being. In our case, it is for the upper middle class, drug dealers and slayqueens. Sad 😔

When you have time go visit DON BAY CLUB (RABAI MWEMBENI)
Let’s go support this community projects on this day.

RR OFFICIALS
James Ngala
Job Chilibasi
Fadhili Bavyombo
Mr Bado Kuhu Safi

Kampuni ya Apple imetoa onyo kwa watumiaji wake dhidi ya kulala karibu na simu zao za iPhone 📲 wakati zinachajiwa, hasa ...
17/06/2025

Kampuni ya Apple imetoa onyo kwa watumiaji wake dhidi ya kulala karibu na simu zao za iPhone 📲 wakati zinachajiwa, hasa ikiwa zimefunikwa kwa blanketi au kuwekwa chini ya mito ya kulalia.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hali hiyo inaweza kusababisha joto kujikusanya kwenye simu na hatimaye betri yake kuongezeka joto kupita kiasi. Jambo linaloweza kusababisha majeraha na hata ajali ya moto.

Apple inasisitiza kuwa ni muhimu kuchaji simu kwenye sehemu ngumu,iliyowazi na yenye mzunguko mzuri wa hewa. Aidha, inashauri kuepuka kutumia nyaya na chaja ambazo hazijathibitishwa rasmi na Apple, kwani zinaweza kuongeza hatari ya kuharibika kwa vifaa au kusababisha majanga.

The easiest way to remove Kasongo is either a referendum, impeachment or mass action.The current opposition had decided ...
16/06/2025

The easiest way to remove Kasongo is either a referendum, impeachment or mass action.

The current opposition had decided those aren't viable options, so it's frothing wantam kasongo mus GO, all the way, for the next two years.

Well, unless CJ Maraga change the script.

Otherwise..

TANZIA …Habari zahivi punde..Gavana wa kaunti ya kilifi Gideon Maitha Mung'aro amepata pigo baada ya kuondokewa na baba ...
15/06/2025

TANZIA …Habari zahivi punde..

Gavana wa kaunti ya kilifi Gideon Maitha Mung'aro amepata pigo baada ya kuondokewa na baba mzazi aliyefariki dunia leo ikiwa ni siku ya kuwasherehekea wazazi wakiume duniani.

Gideon Baya Mung’aro ambaye ameaga dunia akipokea matibabu katika hospitali ya serekali mjini Kilifi - Kilifi County Hospital.
Tunatoa pole zetu Mola awekaribu nanyi nyote mulioguswa familia ndugu na marafiki lakini na wanakilifi sote.

03/01/2024

Warahisishie kazi unaowaomba msaada, usiwape kazi ya kuwaza majibu au njia ya kukusaidia. Nenda ukiwa na majibu pengine wao watabaki kukusaidia.

Mfano 1:
Una kipaji cha mziki, unaenda kwa mtu unamuambia “Naomba unishike mkono”. Unampa yeye kazi tena ya kuwaza kukushika mkono’ ni nini?. Omba huo msaada mahususi, eleza bayana namna unayotaka usaidiwe mtu aone k**a anaweza au hawezi. Unaweza kusema “Naomba niongezee pesa ya kwenda studio / Naomba nisaidie kufikisha nyimbo zangu redio au jambo lingine.

Mfano 2:
Unatafuta kazi, unaniambia kaka “Nitafutie kazi yoyote”. Bro kazi yoyote ni kitendawili, kwa sababu ukweli ni kwamba kuna kazi huwezi kufanya. Rahisisha kwa kueleza angalau kazi kadhaa unazoweza kufanya, ikiwezekana niambie ofisi fulani kuna nafasi na anayehusika ni fulani (tafuta mawasiliano yake ikiwezekana).

10/08/2023

Siku moja baada ya Benki ya Dunia kutangaza kusitisha utoaji wa mikopo mipya kwa Serikali ya Uganda baada ya kujiridhisha kuwa sheria ya Nchi hiyo inayopinga ushoga ambayo imelaaniwa na Mataifa mengi ya magharibi ikiwemo Marekani pamoja na Umoja wa Mataifa, inakinzana na maadili ya Beki hiyo, Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema Uganda inaweza kujiendesha na kupiga hatua kimaendeleo bila mikopo.

Museveni amesema “Benki ya Dunia na Waigizaji wengine wanataka kutulazimisha tuache imani, tamaduni, kanuni na Mamlaka yetu ya kujitawala kwasababu ya pesa zao, wanatuweka tabaka la chini Waafrika wote”

“Hatuitaji kupewa presha na Mtu yoyote na kutufundisha jinsi ya kutatua matatizo yetu kwenye Jamii zetu, wao ndio tatizo kubwa kwetu”

Sheria hiyo mpya ya Uganda inatoa hadi hukumu ya kifo kwa ‘ushoga uliokithiri’ ikiwemo kusambaza Virusi Vya UKIMWI kupitia ngono ya mashoga.

Hadi mwishoni mwa mwaka jana 2022, Benki ya Dunia ilitoa dola za Marekani bilioni 5.4 kufadhili miradi ya maendeleo nchini Uganda ikiwemo miradi mingi ya afya na elimu ambayo Benki hiyo inasema inaweza kuathiriwa na sheria mpya iliyopitishwa nchini humo na uamuzi wa kusitishwa kwa mikopo wa Benki hiyo.

Tupe maoni yako msomaji wetu hapo chini...

Fuatilia ukurasa wetu kwa karibu ili kupata taarifa zaidi na matukio.

Benki ya Dunia imesitisha mikopo nchini Uganda kufuatia sheria ya kupinga mapemzi ya jinsia moja ambayo kimsingi inakinz...
09/08/2023

Benki ya Dunia imesitisha mikopo nchini Uganda kufuatia sheria ya kupinga mapemzi ya jinsia moja ambayo kimsingi inakinzana na maadili ya Benki hiyo. Benki ya Dunia imetangaza kusitisha mikopo mipya kwa Uganda kutokana na sheria tata iliyowekwa nchini humo dhidi ya LGBTQ.

Benki hiyo iliyopo mjini Washington, DC Merekani ilisisitiza na kusema kwamba itasitisha ufadhili wa miradi nchini Uganda ikisubiri tathmini ya hatua ilizoanzisha ili kulinda walio wachache kijinsia dhidi ya ubaguzi na kutengwa katika miradi yake.

Maoni yako wewe msomaji wetu ni yapi...

Fuatilia kwa karibu ukurasa wetu ili kupata taarifa zaidi na matukio.

I have reached 400 followers! Thank you for your continued support. I could not have done it without each of you. 🙏🤗🎉
11/12/2022

I have reached 400 followers! Thank you for your continued support. I could not have done it without each of you. 🙏🤗🎉

Address

Kilifi

Telephone

+254793772989

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Chronicles media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share