16/04/2026
Shirika linalosimamia haki za mziki The Kenya Copyright Board (KECOBO) limetoa malipo mapya kwa wahitaji wa kutumia nyimbo sehemu tofauti tofauti ambapo malipo hayo yanatafanya kazi mpaka 2028.
Malipo hayo yanawalenga watumiaji wa mziki k**a DJs, wafanya biashara kwenye maeneo yao na wenye vituo vya habari.
Marekebisho ya malipo hayo DJs wanatakiwa kulipia kibali kwa garama ya 30,000 kwa muda wa miaka miwili au 1,000 kwa kila event kuruhusiwa kucheza mziki.
Shule za kujifunza muziki pamoja na aina yoyote ya chuo kinachohusu uimbaji vinatakiwa kulipia angalau 20,000.
Malipo hayo pia yamegusia sehemu mbalimbali ambapo ni pamoja na Nightclubs, Casino, Bars, Restaurants, Hetels na AirBnBs watatakiwa kulipa asilimia 60% ya malipo yao kwa permit ya biashara.
Private member’s clubs wanatakiwa kulipia mpaka 100,000 kwa hapa mjini na 75,000 maeneo mengine.
Concert organisers wanatakiwa kulipia 50,000 kwa local events na 100,000 kwa international events, huku live bands na watumbuizaji watatakiwa kulipa 50,000 hapa mjini na 20,000 maeneo mengine.
Vituo vya habari wanahitajika kulipia mpaka asilimia 4% ya kipato chao ambapo kwa 500,000 kwa national radio na 400,000 national TV.
Watumiaji wengine supermarkets, salons na magari watalipia kulingana na ukubwa wa biashara na pesa ya chini kabisa watalipia 3,000.
Follow RAHAI MEDIA