Radio Safina 90.7FM & 99.9FM

Radio Safina 90.7FM & 99.9FM Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Radio Safina 90.7FM & 99.9FM, Radio Station, Kenyatta Street, Ebby towers 5th Floor, Kitale.

π—ͺπ—”π—£π—˜π—Ÿπ—˜π—Ÿπ—˜π—­π—œ π—ͺπ—”π— π—žπ—”π— π—”π—§π—” π— π—§π—¨π—›π—¨π— π—œπ—ͺ𝗔 π— π—žπ—¨π—¨ π—ͺ𝗔 π—ͺπ—œπ—­π—œ π—ͺ𝗔 π—žπ—”π—›π—”π—ͺ𝗔 π—žπ—œπ— π—œπ— π—œπ—‘π—œMaafisa wa upelelezi wamemnasa mtuhumiwa mkuu wa wizi wa k...
08/12/2025

π—ͺπ—”π—£π—˜π—Ÿπ—˜π—Ÿπ—˜π—­π—œ π—ͺπ—”π— π—žπ—”π— π—”π—§π—” π— π—§π—¨π—›π—¨π— π—œπ—ͺ𝗔 π— π—žπ—¨π—¨ π—ͺ𝗔 π—ͺπ—œπ—­π—œ π—ͺ𝗔 π—žπ—”π—›π—”π—ͺ𝗔 π—žπ—œπ— π—œπ— π—œπ—‘π—œ

Maafisa wa upelelezi wamemnasa mtuhumiwa mkuu wa wizi wa kahawa katika eneo la Kimimini na kurejesha shehena kubwa ya kahawa iliyokuwa imeibwa.

Wizi huo ulifikia kilele usiku wa Novemba 25, 2025, baada ya genge la takriban wahalifu 50 kuvamia kiwanda cha Sowek Kenya Company Limited, kukata uzio, kuwafunga walinzi na kutoroka na magunia tisa ya kahawa.

Siku moja kabla, majambazi wengine walivamia Kiwanda cha Ushirika wa Wakulima wa Kiungani na kuiba takribani magunia 25 ya kahawa ya P1 baada ya kutoboa ukuta na kupenya kwenye eneo la kukausha.

Kupitia uchunguzi wa kisayansi, polisi walimk**ata Gregory Kingasia Wekesa, anayejulikana kwa kununua kahawa kutoka vyanzo visivyo halali. Alik**atwa na jumla ya magunia 18 ya kahawa, yakiwemo kilo 500 ndani ya nyumba yake na kilo 1,300 nyingine zikiwa nje zikikauka.

Mtuhumiwa anazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kimimini huku akitarajiwa kufikishwa mahak**ani.

Jamii za Wachache na Waliotengwa Wataka Idara Maalum ya SerikaliJamii za wachache na waliotengwa katika Kaunti ya Trans ...
25/10/2025

Jamii za Wachache na Waliotengwa Wataka Idara Maalum ya Serikali

Jamii za wachache na waliotengwa katika Kaunti ya Trans Nzoia zimeitaka serikali kuunda Idara Maalum ya Serikali itakayoshughulikia maslahi yao.

Wakizungumza mjini Kitale wakati wa ushiriki wa umma kuhusu Mswada wa Jamii za Wachache na Waliotengwa wa 2025, wawakilishi kutoka jamii tisa zikiwemo Ogiek, Bongomek, Konyi, Cherangany, Cabiny, Sengwer, Wahindi na wazee wa Mau Mau walisema hatua hiyo itasaidia kushughulikia changamoto zao ipasavyo.

Mwakilishi wa Konyi, Gregory Ngeywa, aliishukuru serikali kwa kuunda Kitengo cha Masuala ya Wachache katika Ofisi ya Rais lakini akasisitiza haja ya kuwa na idara huru.

Washiriki waliitaka serikali kutoa fidia kwa dhuluma za kihistoria, kuwatafutia makazi waliotimuliwa na kuhakikisha sheria zilizopo zinatekelezwa.

Josephat Barasa, mwakilishi wa watu wenye ulemavu, alipendekeza wachache wachaguliwe moja kwa moja kwenye debe badala ya kuteuliwa na vyama vya siasa.

Wengine k**a Johnson Masai na Martin Simwota waliitaka serikali kuhakikisha usawa katika ajira, uwezeshaji kiuchumi, na uwakilishi wa kweli katika mabunge ya kaunti.

22/10/2025

Equity Bank Kenya has broken new ground in impact transparency with the launch of its inaugural Sustainable Development Impact Disclosure (SDID) Report, a data-driven framework in partnership with J.P. Morgan, that aligns finance with the Sustainable Development Goals and quantifies progress through measurable outcomes.

16/10/2025

Jinsi Wakenya walivyovunja usalama wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA), wakimiminika hadi kwenye njia ya kurukia ndege wakati wa kuwasili kwa mwili wa Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga, huku maelfu ya waombolezaji wakivamia sehemu zilizokuwa zimewekewa vizuizi kwa hamu ya kuona jeneza lilipokuwa likishushwa kutoka kwenye ndege.

16/10/2025

Umati mkubwa wa watu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) uliwavuruga maafisa wa usalama muda mfupi baada ya kuwasili kwa mwili wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani, Raila Odinga. Wanafamilia, marafiki na waombolezaji waliokuwa na hisia kali walivunja maeneo yaliyokuwa yamezuiwa wakisukumana kwa nguvu wakitaka kumuona jeneza lilipokuwa likitolewa.

Former Prime Minister Raila Odinga collapses and dies while talking a morning walk in India
15/10/2025

Former Prime Minister Raila Odinga collapses and dies while talking a morning walk in India

Ruto Azindua Vikao vya Kitaifa vya Mradi wa NYOTARais William Ruto ameagiza makatibu wakuu kuongoza vikao vya viongozi m...
05/10/2025

Ruto Azindua Vikao vya Kitaifa vya Mradi wa NYOTA

Rais William Ruto ameagiza makatibu wakuu kuongoza vikao vya viongozi mashinani kuhusu mradi wa National Youth Opportunities Towards Advancement (NYOTA) katika kaunti zote 47 kuanzia Jumatatu.

Vikao hivyo vitafanyika kwa wakati mmoja kote nchini vikihusisha viongozi waliochaguliwa, maafisa wa utawala wa serikali ya kitaifa (NGAO), na timu ya NYOTA.

β€œTunataka kuhakikisha vijana walio katika ngazi ya chini ya uchumi wanapata nafasi za kazi kwa uwazi na usawa,” ilisema taarifa kutoka Ikulu.

Katika Kaunti ya Trans Nzoia, kikao kitaongozwa na Katibu Mkuu Dkt. Korir Sing’oei katika Kitale National Polytechnic. Jijini Nairobi, kikao kitafanyika Kariokor Social Hall kikiongozwa na Katibu Mkuu Nixon Korir.

β€œLengo letu ni kuhakikisha hakuna kijana anayesahaulika,” alisema Dkt. Sing’oei.

Vikao hivyo vitaanza saa 9AM asubuhi Jumatatu kote nchini.

Polisi Bungoma wamewak**ata washukiwa 7 na kuk**ata mali nyingi za wizi zikiwemo TV, laptop, spika na pikipiki 2. Washuk...
20/09/2025

Polisi Bungoma wamewak**ata washukiwa 7 na kuk**ata mali nyingi za wizi zikiwemo TV, laptop, spika na pikipiki 2. Washukiwa watafikishwa mahak**ani Sept 22. Polisi wanaahidi kuendeleza msako dhidi ya uhalifu.

Harooooo πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚Wanasabato wote wawe na ibada njema.Wakilisha kanisa la kwako ambalo utashiriki ibada siku ya leo.
06/09/2025

Harooooo πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Wanasabato wote wawe na ibada njema.
Wakilisha kanisa la kwako ambalo utashiriki ibada siku ya leo.

Mwanamziki wa Rwanda Gloriose Musabyimana maarufu k**a Gogo aliyejulikana kwa wimbo 'I need blood of Jesus' ameaga dunia...
04/09/2025

Mwanamziki wa Rwanda Gloriose Musabyimana maarufu k**a Gogo aliyejulikana kwa wimbo 'I need blood of Jesus' ameaga dunia.
RIP Gogo

Full Time EPL, Liverpool 1-0 Arsenal.Mara ya mwisho Arsenal kushinda kwenye uwanja wa Anfield dhidi ya Liverpool kwenye ...
31/08/2025

Full Time EPL, Liverpool 1-0 Arsenal.

Mara ya mwisho Arsenal kushinda kwenye uwanja wa Anfield dhidi ya Liverpool kwenye EPL ilikuwa Septemba 2, 2012 na Mikel Arteta alicheza mechi yote akiwa mchezaji wa Arsenal.

Liverpool imefanikiwa kufunga bao kwenye mechi 37 mfululizo za EPL kwa mara ya kwanza katika historia.

Na Mfalme Sam atalala na viatu leo

Mohamed Hrimat wa Morocco achukua tuzo ya mchezaji bora wa mashindano ya CHAN.Tumpe maua yake.
30/08/2025

Mohamed Hrimat wa Morocco achukua tuzo ya mchezaji bora wa mashindano ya CHAN.
Tumpe maua yake.

Address

Kenyatta Street, Ebby Towers 5th Floor
Kitale
30200

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Safina 90.7FM & 99.9FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category