Magnet Radio

Magnet Radio Powered by IPO SIKU MEDIA{ISM}

Magnet Radio~Stick With Us! ISM~Your Getaway to Digital Excellence!
(1)

 Gavana wa Jiji kuu la Nairobi Johnson Sakaja amekanusha madai kuwa alitoa shilingi milioni 2 kwa aliyekuwa Rais wa Bung...
20/06/2025


Gavana wa Jiji kuu la Nairobi Johnson Sakaja amekanusha madai kuwa alitoa shilingi milioni 2 kwa aliyekuwa Rais wa Bunge la Mwananchi Calvince Okoth maarufu Gaucho.

Ripoti ziliibuka kuwa kabla ya maandamano ya jumaatano, gavana huyo alikutana na viongozi kadhaa, akiwemo Gaucho na jamaa mmoja maarufu Swaleh, na kuwapa Shilingi milioni 2 fedha za kuwafadhili wahuni kwenye maandamano hayo.

Katika kujieleza kwa haraka, Sakaja amejitenga na tuhuma hizo na kufafanua kuwa siku hiyo hakuwepo Jijini, akitoa ushahidi, bosii huyo wa Jiji kuu la Kenya amefichua kwamba alikuwa amesafiri kule Lugari na hakuitisha mkutano huo unaodaiwa.

"Uongo huo wa wazi. Jumapili, nilikuwa Lugari kwa Kanisa na nikarudi Nairobi Jumatatu alasiri kupitia Kitale. Sijaona Gaucho tangu alipohudhuria Uzinduzi wa Mukuru Housing au Swaleh kwa miezi mingi," Sakaja alifafanua.

 Wakenya wa tabaka mbali mbali wameweka picha zao mitandaoni wakiwa wamevaa barakoa, k**a ishara ya kuonyesha mshik**ano...
20/06/2025


Wakenya wa tabaka mbali mbali wameweka picha zao mitandaoni wakiwa wamevaa barakoa, k**a ishara ya kuonyesha mshik**ano na Boniface Kariuki, Mchuuzi wa Maski aliyepigwa risasi na polisi wakati wa maandamanoo ya Juni 17, 2025.

Naibu wa Rais aliyebanduliwa Rigathi Gachagua naye pia ameonekana akiwa amevaa barakoa hii leo, akiwa kwenye ziara yake ya kisiasa huko Meru, huku pia gavana wa Trans Nzoia George Natembeya pia akivalia maski akiwa afisini mwake.

Wito wa kampeni hii ulitolewa na mwanaharakati ambaye pia ni mchekeshaji maarufu wa humu nchini Eric Omondi.

 Rais William Ruto amesema amelazimika kufanya maamuzi 'magumu' ili kuhakikisha mageuzi yenye manufaa kwa wananchi.Ikumb...
19/06/2025


Rais William Ruto amesema amelazimika kufanya maamuzi 'magumu' ili kuhakikisha mageuzi yenye manufaa kwa wananchi.

Ikumbukwe katika siku za hivi karibuni Rais amekuwa akishinikiza haja ya kukabili migawanyiko na siasa anazozitaja kuwa za 'ukabila' na 'chuki' hasa baada ya kuwapo kwa serikali jumuishi yaani broad-based government kufuatia ushirikiano na Raila Odinga.

 Maafisa wawili wa polisi Masinde Barasa na Duncan Kiprono, wanaoshtakiwa kwa kumpiga risasi mchuuzi wa maski wakati wa ...
19/06/2025


Maafisa wawili wa polisi Masinde Barasa na Duncan Kiprono, wanaoshtakiwa kwa kumpiga risasi mchuuzi wa maski wakati wa maandamano ya kumtaka Naibu mkuu wa Polisi Eliud Lagat kujiuzulu, katikati mwa jiji kuu la Nairobi mnamo Jumanne, wamefikishwa katika Mahak**a ya Milimani jijini Nairobi.

 Rais William Ruto ametoa mchango wa Shilingi Milioni 2 kwa familia ya Albert Ojwang inayoomboleza.Ojwang alifariki akiw...
16/06/2025


Rais William Ruto ametoa mchango wa Shilingi Milioni 2 kwa familia ya Albert Ojwang inayoomboleza.

Ojwang alifariki akiwa mikononi mwa polisi katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Nairobi, siku chache baada ya kuk**atwa kwa kilichotajwa k**a kumharibia jina Naibu jenerali mkuu wa Polisi kupitia mtandao wa kijamii.

Mchango wa Rais unalenga kusaidia familia kwa gharama za mazishi na mahitaji mengine ya haraka.

 Muhtasari wa hotuba ya Waziri wa Mambo ya Ndani Kipchumba Murkomen kwenye Jumba la Harambee, Jijini Nairobi.-Katika kip...
16/06/2025


Muhtasari wa hotuba ya Waziri wa Mambo ya Ndani Kipchumba Murkomen kwenye Jumba la Harambee, Jijini Nairobi.

-Katika kipindi cha miaka 2 ijayo, zaidi ya vituo 1000 vya polisi nchini Kenya lazima vitakuwa na kamera za CCTV. OCS wa kila kituo atawajibika kwa uendeshaji, na kwa hitilafu yoyote kwenye kamera.

-Makurutu wanaume na wanawake wanatakiwa kufundishwa kwa viwango vya juu iwezekanavyo, umahiri na uadilifu ili kuheshimu Haki za Binadamu, Uhuru wa kimsingi na utu.

-Mswada wa marekebisho ya IPOA utatoa mifumo zaidi ya sheria ambayo itaimarisha time hiyo kutekeleza majukumu yake ya kikatiba.

-Kitabu cha Matukio (OB) kitawekwa kidigitali na pia Mpango wa Polisi wa Jamii.

- Ukaguzi wa mara kwa mara na mapitio ya utendaji na Ubia na wadau wengine ili kuboresha taaluma ya polisi

-Waliohusika na mauaji ya Albert Ojwanga watawajibishwa na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria.

 Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen anahutubia wakenya, kuhusu mipango ya kuimarisha usalama zaidi, haya yana...
16/06/2025


Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen anahutubia wakenya, kuhusu mipango ya kuimarisha usalama zaidi, haya yanajiri siku chache tu baada ya kifo cha mwanablogu na mwalimu Albert Ojwang akiwa mikononi mwa Polisi.

 Mwanariadha wa Emmanuel Wanyonyi alikuwa na matokeo mazuri katika mbio za Stockholm Diamond League, akishinda mita 800 ...
16/06/2025


Mwanariadha wa Emmanuel Wanyonyi alikuwa na matokeo mazuri katika mbio za Stockholm Diamond League, akishinda mita 800 kwa wanaume katika muda bora zaidi duniani kufikia sasa mwaka huu Dakika 1 na sekunde 41.95

Huu ni ushindi wake wa pili mkubwa katika msururu wa mbio za Diamond League na ishara ya umahiri wa wanariadha wa Kenya katika mbio za masafa ya kati.

 OCS wa Kituo Kikuu cha Polisi Samson Talaam na Konstebo wa Polisi James Mukhwana wameiomba Mahak**a Kuu kusitisha masht...
16/06/2025


OCS wa Kituo Kikuu cha Polisi Samson Talaam na Konstebo wa Polisi James Mukhwana wameiomba Mahak**a Kuu kusitisha mashtaka dhidi yao yanayohusiana na mauaji ya mwalimu na mwanablogu Albert Ojwang anayedaiwa kufariki akiwa mikononi mwa polisi.

Wakiwakilishwa na wakili Danstan Omari, maafisa hao wanasema utaratibu wa kuk**atwa kwao na Mamlaka Huru ya Uangalizi wa Polisi (IPOA) ulikuwa na dosari, huku wakisisitiza kuwa uchunguzi ulitakiwa kufanyika kabla ya kesi.

 Rais William Ruto amewakashifu wale wanaotaka ajiuzulu na kusema hawana maslahi mema na nchi. Wakosoaji na wapinzani wa...
16/06/2025


Rais William Ruto amewakashifu wale wanaotaka ajiuzulu na kusema hawana maslahi mema na nchi. Wakosoaji na wapinzani wamekuwa wakitema cheche za kumtaka ang'atuke kwa kile wanachosema ni kushindwa kuongoza nchi.

Kwa upande wake Rais Ruto anasema k**a wana tatizo na yeye basi yuko tayari kukabiliana nao, akisisitiza kuwa wanaomkosoa wanafanya hivyo kwa maslahi yao binafsi wala siyo kwa wakenya.

 Afisa mkuu wa Kituo cha Polisi cha Central, Nairobi, Samson Talaam, amewasilishwa katika Mahak**a ya Milimani kuhusiana...
16/06/2025


Afisa mkuu wa Kituo cha Polisi cha Central, Nairobi, Samson Talaam, amewasilishwa katika Mahak**a ya Milimani kuhusiana na kifo cha mwanablogu Albert Ojwang.

Talam, alifuatwa na kuk**atwa siku ya Ijumaa baada ya msako mkali.

Polisi walidai kuwa Talam alijaribu kukwepa kuk**atwa kwa kuzima simu zake za rununu tangu Alhamisi.

Familia yake, hata hivyo, ilikanusha madai hayo.

Afisa mwingine wa polisi wa k**e aliyelengwa katika kesi hiyo alipatikana na kuhojiwa kwa muda wote wa Ijumaa kabla ya mpango uliopangwa.

 Afisa Mkuu wa Kituo Kikuu cha Polisi cha Central jijini Nairobi, Samson Talam, amek**atwa mjini Eldoret, baada ya msako...
13/06/2025


Afisa Mkuu wa Kituo Kikuu cha Polisi cha Central jijini Nairobi, Samson Talam, amek**atwa mjini Eldoret, baada ya msako wa siku nzima.

Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai ilidai kuwa alitoroka katika jaribio la kukwepa kuk**atwa baada ya kuhisishwa na kifo cha mwanablogu Albert Ojwang.

Mamlaka yalisema Talam alikuwa amezima simu yake ya rununu siku ya Alhamisi huku maafisa wa polisi wakimkaribia.

Hatimaye alipatikana, akak**atwa, na kukabidhiwa kwa Mamlaka Huru ya Kusimamia Polisi (ipoa) kwa ajili ya kufanyiwa kazi zaidi.

Kuk**atwa kwake kunafikisha watatu idadi ya watu walio kizuizini kuhusiana na kifo cha Ojwang, ambaye alifariki akiwa mikononi mwa polisi chini ya hali ya kutiliwa shaka.

Afisa mwingine wa k**e aliyehusishwa na kesi hiyo pia alihojiwa kwa saa kadhaa siku ya Ijumaa na anatarajiwa kuhojiwa zaidi.

Address

St Marys Kibomet-Kitale
Kitale

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Magnet Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Magnet Radio:

Share