Etau Television

Etau Television Etau is the Turkana’s Premium Channel for Sports, Music, News, education, Culture & Entertainment.

11/10/2025

"Utamaduni wa jamii yetu ya Turkana, hasa wafugaji wa kuhamahama wanachangia uharibifu wa misitu. Wanahitaji kuhamasishwa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa." ~ Mbunge, Turkana North, Ekuwom Nabuin
!

11/10/2025

"K**a usalama haitarekebishwa, Chakula na pesa watu hawatapata, mambo ni ONE_TERM." ~ MCA, LOKICHAR, SAMWEL LOMODO
!

10/10/2025

"Machafuko tunayoshuhudia eneo la Kainuk yanahusiana na biashara, haswa mahali ambapo magari yatapumzika wakati wa safari na uchimbaji wa dhahabu." - Waziri, Beatrice Askul Moe

09/10/2025

"Don't Punish Our People because of your differences with some leaders." ~ Governor, Jeremiah Lomorukai
!

08/10/2025

Margret Kipchumba, mkazi wa Kalokol, Kaunti ya Turkana, ameibua wasiwasi kwamba mtoto wake alitekwa nyara na watu wanaoshukiwa kuwa maafisa wa polisi katika eneo la Tot Kaunti ya Elgeyo Marakwet akiwa kwenye baa Moja na marafiki wakiburudika. Mshukiwa alik**atwa kwa misingi kuwa alikuwa anamiliki silaha haramu (Bunduki). Margret hata hivyo amemlaumu chifu wa eneo hilo kwa kumsaliti mtoto wake kwa polisi bila hatia.

"K**a Mtoto Wangu Yuko hai Mnipe na k**a amekufa Mleteni Mwili yake nizike Mimi Mwenyewe." ~ Margret Kipchumba, Mama Mzazi
!

07/10/2025

The influence of Dynamics in cultural traditions and customs.
!

06/10/2025

"Shule za maeneo kame zinakumbwa na changamoto nyingi, mgao ukisitishwa wataumia zaidi. " ~

06/10/2025

Askofu Mkuu wa ACK, Dkt Jackson Ole Sapit katika ziara yake Kaunti ya Turkana ametoa wito kwa wakazi kukomesha mila na desturi zinazowanyima watoto haki ya kupata elimu.
Kwa kauli, Ole Sapit ameitaka serikali ya kaunti hii kuhakikisha inawekeza zaidi katika elimu kwani kuna uhaba wa madarasa hasa za shule ya chekechea, ukosefu wa maji safi ya kunywa na ukosefu wa Mradi wa kulisha watoto shuleni.
!

04/10/2025

Rais wa Madagascar Andry Rajoelina alisema siku ya Ijumaa yuko tayari kusikiliza malalamishi ya vijana wa GEN Z wanaoandamana kote nchini kutafuta suluhu la matatizo yanayokabili taifa hilo. Hata hivyo, Rajoelina alipuuza wito wa kumtaka ajiuzulu kutoka kwa waandamanaji.

"Hakuna anayefaidika na uharibifu wa taifa. Niko hapa, nimesimama hapa tayari kusikiliza, tayari kunyoosha mkono wa usaidizi na zaidi ya yote, tayari kuleta suluhisho kwa Madagascar," Rajoelina alisema katika hotuba iliyotangazwa kwenye ukurasa wake wa Facebook.
!

01/10/2025

Wakazi wa eneo la Kakwanyang Kaunti ya Turkana wamemkashifu Dkt Alfred Areman, Mkuu wa shule ya Upili ya Talent High kwa kufuja mali na kutatiza maendeleo ya shule hiyo. Wanavijiji hao wanaitaka Tume ya Kuajiri walimu (TSC) kuchukua hatua za haraka kwa kumwondoa na kumteua mkuu mpya.

" Mwalimu anaiba kengele pia, wakati wa chakula cha mchana ukifika mwanafunzi anapiga milusi kuashiria ni wakati wa kula." ~

Aidha, tume hiyo ya TSC tawi la Turkana imeunda bodi ya kuchunguza madai dhidi ya Dkt Areman kisha kumchukulia hatua za kisheria.
!

30/09/2025

Titans Fc walipandishwa ngazi, mahasidi wamepatana Divisheni ya kwanza. Ngarambe itambe!

30/09/2025

Wababe wa soka Kaunti ya Turkana Hillside FC wazidi kunyoosha misuli wakijiweka tayari kuwakabili wapinzani wao vilivyo kwa michuano za Divisheni ya kwanza ambayo inatarajiwa kuanza hivi karibuni.
!

Address

Lodwar

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Etau Television posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Etau Television:

Share