02/06/2026
Mwakilishi Wadi ya Ganda Hon. Oscar Wanje amekemea vikali hatua ya kunyanyaswa, kutishiwa na kudhulumiwa kwa wafanyibiashara wa pombe ya mnazi Malindi, akitaja kwamba biashara hiyo ni chanzo kikubwa cha kipato kwa familia nyingi tangu jadi.
Kauli yake inajiri baada ya wafanyibiashara wengi wa Mbuzi Wengi, mjini Malindi kuk**atwa na maafisa wa polisi hapo jana, huku biashara yao ikipata hasara kubwa. Mheshimiwa Oscar Wanje katika kauli yake, amesema kwamba endapo ni swala la leseni, au sheria, basi swala hilo wafanyibiashara na jamii - watumizi, wahusishwe na kuelemishwa kwa njia ya mazungumzo ili kuhakikisha biashara hii ambayo ni kitega uchumi cha familia nyingi iendelee tu k**a biashara nyingine.
"Ikiwa kuna maswala ya liseni, au sheria, yashughulikiwe kwa njia ya mazungumzo na kufuata taratibu za kisheria, si kwa dhulma au matumizi mabaya ya mamlaka.'' ~ Oscar Wanje
Swala la unyanyasaji kwa wafanyibiashara hawa limezua hisia mseto huku wakazi wa Malindi na Pwani kwa jumla wakikosoa hatua ya kuk**atwa kwa wachuzi hao, na pia matumizi mabaya ya mamlaka dhidi yao.
Wengi wa wakazi wa Pwani wanauliza kwa nini biashara ya Mugoka isidhibitiwa k**a wanavyotaka biashara ya mnazi idhibitiwe vikali?
Kwa nini biashara ya mugoka inauzwa usiku na mchana bila kudhibitiwa?
Kwa nini wauzaji Mugoka na Miraa hawak**atwi usiku?
Wakazi wa Malindi na Pwani wamemuunga mkono kiongozi Oscar Wanje wakisema kwamba Mnazi si biashara tu, ni kitambulisho cha jamii ya pwani - kitambulisho cha uasili wa Wapwani.