Husband Pocket Stories

Husband Pocket Stories Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Husband Pocket Stories, News & Media Website, Kilifi.

03/01/2024

Warahisishie kazi unaowaomba msaada, usiwape kazi ya kuwaza majibu au njia ya kukusaidia. Nenda ukiwa na majibu pengine wao watabaki kukusaidia.

Mfano 1:
Una kipaji cha mziki, unaenda kwa mtu unamuambia “Naomba unishike mkono”. Unampa yeye kazi tena ya kuwaza kukushika mkono’ ni nini?. Omba huo msaada mahususi, eleza bayana namna unayotaka usaidiwe mtu aone k**a anaweza au hawezi. Unaweza kusema “Naomba niongezee pesa ya kwenda studio / Naomba nisaidie kufikisha nyimbo zangu redio au jambo lingine.

Mfano 2:
Unatafuta kazi, unaniambia kaka “Nitafutie kazi yoyote”. Bro kazi yoyote ni kitendawili, kwa sababu ukweli ni kwamba kuna kazi huwezi kufanya. Rahisisha kwa kueleza angalau kazi kadhaa unazoweza kufanya, ikiwezekana niambie ofisi fulani kuna nafasi na anayehusika ni fulani (tafuta mawasiliano yake ikiwezekana).

10/08/2023

Siku moja baada ya Benki ya Dunia kutangaza kusitisha utoaji wa mikopo mipya kwa Serikali ya Uganda baada ya kujiridhisha kuwa sheria ya Nchi hiyo inayopinga ushoga ambayo imelaaniwa na Mataifa mengi ya magharibi ikiwemo Marekani pamoja na Umoja wa Mataifa, inakinzana na maadili ya Beki hiyo, Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema Uganda inaweza kujiendesha na kupiga hatua kimaendeleo bila mikopo.

Museveni amesema “Benki ya Dunia na Waigizaji wengine wanataka kutulazimisha tuache imani, tamaduni, kanuni na Mamlaka yetu ya kujitawala kwasababu ya pesa zao, wanatuweka tabaka la chini Waafrika wote”

“Hatuitaji kupewa presha na Mtu yoyote na kutufundisha jinsi ya kutatua matatizo yetu kwenye Jamii zetu, wao ndio tatizo kubwa kwetu”

Sheria hiyo mpya ya Uganda inatoa hadi hukumu ya kifo kwa ‘ushoga uliokithiri’ ikiwemo kusambaza Virusi Vya UKIMWI kupitia ngono ya mashoga.

Hadi mwishoni mwa mwaka jana 2022, Benki ya Dunia ilitoa dola za Marekani bilioni 5.4 kufadhili miradi ya maendeleo nchini Uganda ikiwemo miradi mingi ya afya na elimu ambayo Benki hiyo inasema inaweza kuathiriwa na sheria mpya iliyopitishwa nchini humo na uamuzi wa kusitishwa kwa mikopo wa Benki hiyo.

Tupe maoni yako msomaji wetu hapo chini...

Fuatilia ukurasa wetu kwa karibu ili kupata taarifa zaidi na matukio.

Benki ya Dunia imesitisha mikopo nchini Uganda kufuatia sheria ya kupinga mapemzi ya jinsia moja ambayo kimsingi inakinz...
09/08/2023

Benki ya Dunia imesitisha mikopo nchini Uganda kufuatia sheria ya kupinga mapemzi ya jinsia moja ambayo kimsingi inakinzana na maadili ya Benki hiyo. Benki ya Dunia imetangaza kusitisha mikopo mipya kwa Uganda kutokana na sheria tata iliyowekwa nchini humo dhidi ya LGBTQ.

Benki hiyo iliyopo mjini Washington, DC Merekani ilisisitiza na kusema kwamba itasitisha ufadhili wa miradi nchini Uganda ikisubiri tathmini ya hatua ilizoanzisha ili kulinda walio wachache kijinsia dhidi ya ubaguzi na kutengwa katika miradi yake.

Maoni yako wewe msomaji wetu ni yapi...

Fuatilia kwa karibu ukurasa wetu ili kupata taarifa zaidi na matukio.

I have reached 400 followers! Thank you for your continued support. I could not have done it without each of you. 🙏🤗🎉
11/12/2022

I have reached 400 followers! Thank you for your continued support. I could not have done it without each of you. 🙏🤗🎉

Address

Kilifi

Telephone

+254793772989

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Husband Pocket Stories posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share