WILD ROCKY TV

WILD ROCKY TV UCHANGANUZI WA MASUALA NYETI YANAYO FUNGAMANA NA MAISHA MAMBO LEO

24/05/2025

💞Kuna tofauti kubwa sana ya “Kuwa na Mtoto” na “Single Mother”, kuwa na mtoto ni ile hali ya mwanamke kuzaa, lakini kuwa Single Mother ni ile hali ya mwanamke, kwanza kuzaa, kuishi na mtoto wake, kumhudumia kwa kila kitu na hata k**a anapata msaada wa mwanaume aliyezaa naye lakini hayuko na huyo mwanaume na anabeba majukumu ya Mama na Baba kwa mtoto wake.
Mwanamke unapokutana na mwanaume, ukamuambia una mtoto akakubali akakuambia kuwa hamna shida labda hata akakuambia kuwa na mimi nina mtoto usichekelee kwanza. Ni lazima ujiulize kuwa kakukuta na mtoto au single mother? Labda nifafanue, unaweza kuwa na mtoto lakini huishi naye, umemuacha kijijini kwa Mama yako, au anaishi na Baba yake. Hapa ni k**a una mtoto lakini kiuhalisia ni k**a vile huna tu ni mwanamke ambaye hajazaa.
Kwamba mwanaume akikukuta katika hali hii anaweza hata kusahau k**a una mtoto, anaweza kuja kwako wakati wowote, mnaweza kutoka wakati wowote bila kuwaza nyumbani au dada wa kazi, anaweza kuamka asubuhi akakuambia twende zandibar, unaweza kutoka kazini ukapitia kwake ukakaa wiki bila kurudi kwako ni simu unampigia tu Mama yako au X wako kuulizia hali ya mtoto.
Lakini single mother, unaishi na mtoto wako, huwezi mleta leta tu mwanaume kizembe zembe kwako, huwezi toka tu ukasafiri wiki na mwanaume, huwezi toka tu kazini ukapitia baa ukarudia kwa mwanaume ukakaa wiki bila kurudi nyumbani. Kila kitu utakachokifanya lazima uangalie mwanao kala, kavaa, anaumwa, ameenda shule, kaoga, yaani unakua Mama.
Hata k**a hamuishi na huyo mwanaume au haji kwako kabisa, lakini zile pilikapilika za umama anaziona, wakati mwingine mnataka kupiga mechi dada wa kazi anapiga simu mtoto anawaka moto mnalazimisha kuacha mechi mnaondoka. Sasa unaona utofauti, mwanaume anapokuambia sijali k**a una mtoto jiulize ni k**a hajali kwakua umezaa au hajali kwakua ni single mother. Usifurahie kichwa kichwa kwani kuna wengine hawajui majukumu.
Unaingia kwenye ndoa akiona pilika pilika za kuwa Mama ananza kuhisi humpendi, anaanza kukuona k**a mchafu flani, anaanza kuhisi kuwa labda mtoto ni kikwazo. Mara anakuambia simtaki mtoto mpeleke kwa Mama yako! Lakini ishu inakuja je wewe unajikubali k**a single mother au mwanamke tu mwenye mtoto? Sijui k**a mmenielewađź•´đź•´đź•´

UCHANGANUZI WA MASUALA NYETI YANAYO FUNGAMANA NA MAISHA MAMBO LEO

20/10/2022

đź’žMHESHIMU HUYU BINTI SIKU AKIKUACHA UTACHANGANYIKIWA!đź’ž

👉Kuna baadhi ya wanaume, binti akishamkubali kimapenzi na kukolea, akaonyesha kuwa anampenda sana basi anaanza kumnyanyasa, kumpiga na kumdharau, anaanza kuona k**a yeye ndiye kampa huyo binti maisha. Kana kwamba kabla ya kukutana nayeye binti alikua hana maisha, alikua takataka hajielewi🤔.

K**a vile hana familia na k**a vile akimuacha hawezi kuishi. Yaani unakutana na mwanaume anavyomnyanyasa binti wawatu basi unaweza kudhani huyu ndiye yule jamaa ambaye anashikilia koki ya bomba la pumzi hivyo siku akiamua kulizima basi ndo binti anaishia hapo🤣.

Nikukumbushe tu ndugu yangu, huyo binti alikua na maisha kabla yako. Yaani mpaka unamuona amependeza, ukavutiwa naye alikua anakula, analala, anavaa ndo hata ukamtamani. Yaani hiyo miaka mitano ya kukaa naye ni kidogo ukilinganisha na miaka 20 ambayo alikua bila wewe.

Hivyo k**a aliweza kuishi miaka ishirini bila wewe kwanini ashindwe sasa🤔. Anaweza kutoishi bila wewe na kukunyenyekea na kukupenda si sababu eti kuwa maisha yake yatakoma kwakua kaachana na wewe. Ubaya nikuwa, mwanamke unayemnyanyasa hivi siku akikuacha utachanganyikiwa, narudia, ukijiona unamnyanyasa mwanake siku akikuacha utachanganyikiwa!🤣🤣🤣

20/10/2022

K**a huna mpango wa kumuoa muambie binti wa watu, huna haja ya kwenda kujitambulisha kwao wakati una maisha mengine, haikufanyi kuwa mjanja wala mwanaume Zaidi kutoa kishika uchumba ili tu akukubali kimwili.

Hata k**a unaona kwamba huwezi kupata mwanamke bila kumdanganya ila si kwa kiwango cha kwenda mpaka kwao. Unatakiwa kujua kuwa, unapoenda kwa mwanamke ukajitambulisha bila kumuoa, aibu unayompa ka wazazi wake, marafiki na ukoo wake ni kubwa.

Najua unaona sifa kwakua ukishaondoka basi kila kitu kwako kinakua sawa ila ulishawaza kuhusu yeye. Vipi maisha yake baada ya hapo yatakuaje, ni wanaume wangapi wanamtaka lakini anawakataa kwakua anajiona k**a yeye ni mchumba wa mtu? Acha hizo mambo usifike huko sio ujanja!

07/09/2022

KUNA MUDA TUNAJITAHIDI SANA KUYALINDA na KUYATETEA MAHUSIANO YADUMU.

Tuko tayari kupoteza ili wao wapate, tuko tayari kutengwa na kusemwa vibaya na jamaa zetu ili KUWALINDA na KUWATETEA wawe salama na wasidharaulike tunaamua kuwalinda na kila mtu atakayeonekana adui wa MWILI na ROHO kwake.

Kwa ufupi tunafanya mengi ya HATARI na yanye GHARAMA kwa ajili yao. Wakati mwingine tunaaminika tumeshikwa AKILI au hatuna PAKWENDA, hatujitambui nk (fasili za watu).

Unayempenda yeye hakupendi, unayemtetea yeye hajali, unayemhitaji yeye hakuhitaji nk. Mara nyingi tunateswa na kunyanyaswa na wale tunaowathamini na tunaowapenda kwa dhati.

Kuna wakati tunawaasamehe, tunajishusha na kubeba makosa yao ili wao wabaki salama na maisha yaendelee lakini wanafanya makosa yaleyale yanayotuumiza.

Ifike wakati tukubali kuachia vitu hata k**a tulivitesekea sana kuvipata maana si kila kitu kinahitaji uvumilivu vingine vinahitaji kuviachilia ili ubaki salama.

07/09/2022

HII NI KWA WALE MABINTI WA NIACHIE MWANAUME WANGU!

K**a uko kwenye mahusiano ya kawaida tu, halafu kila siku kazi yako nikuwapigia wanawake wengine kuwaambia achaneni na mume wangu wakati huyo mwanaume hajakuoa! Narudia hajakuoa, ni mpenzi tu labda hata mnaishi naye bila ndoa au kajitambulisha tu kwenu lakini hakuna ndoa basi jua kuwa huyo si mwanaume wako.

Huyo mwanaume bado anatafuta mwanamke wa kuwa naye, hana ndoa bado anaweza kuolewa yoyote kati ya hao unaowapigia simu! Najua unajiambia mimi kwao nafahamika! Unajuaje k**a hao wengine nao hawafahamiki! Ananihudumia kwa kila kitu, kwani hao wengine vipi hawahudumii!

Katoa mahari kwani huko kwingine anashindwa kutoa! Muda mwingi niko naye si ni kwakua wewe ni king’ang’anizi! Ninachotaka kusema hapa ni hivi, huyo mwanaume si mume wako, hata k**a humuachi badala ya kujipa kazi ya kupigia wanawake wenzako simu yhembu amka, waza hivi asiponichagua mimi nimejiandaaje na maisha yangu!

Wengi wakishaanza kufumania badala ya kuamka kujifikiria wao ndiyo kwanza wanabeba mimba ili kimshukilia mwanaume! Dada nani kakuambia wewe pekee ndiyo mwenye kizazi, ndiyo kwanza utasikia kmapa mwanaume mtaji, anahangaika na mawifi kwa waganga, mara kujipendekeza kwa Mama mkwe ili apendwe yeye!

K**a ukishaanza kumfumania na unaona kuwa humuachi, badala ya kuhangaika na simu kupigia hao wengine kutaka wakuachie mwanaume wako kana kwamba ni maparachichi hayo basi hangaika kutafuta maisha yako binafsi. K**a huna kazi tafuta, k**a mlipanga kuzaa acha, kuwa makini na siku zako, fanya Biashara hata ukiachwa unakua umepoteza muda tu ila hujapoteza maisha!

07/09/2022

UFANYACHO LEO KINAWEZA KUAMUA KESHO YAKO NA HATIMA YA FAMILIA YAKO

Kila jambo unalotenda kwa mtu au katika jamii yako kwasababu ya mamlaka, cheo, nguvu ulizonazo zinaweza kuathiri uzao wako au wewe mwenyewe (kwa uzuri au ubaya)

Unamkumbuka Hamani, makosa yake kutaka kuwaua wayahudi yaligharimu jamii yake yote pamoja na yeye waliuawa. (Mchuma janga hula na wakwao)

Unamkumbuka Yeroboamu aliyekuwa mfalme wa Israel alivyomuasi Mungu na Mungu akajilipiza juu ya mwanae wa kiume akamuua. (Makosa ya baba yaligharimu maisha ya mtoto)

Unamkumbuka Mfalme Ahabu na Jezbel mkewe, makosa yao ya utalawa mbaya yaligharimu uzao wao wote na wao kuuwawa. (Mungu alijilipiza kwa mabaya yao)

Unamkumbuka mfalme Daud alivyoyakumbuka mema ya Jonathan yakawa neema kwa mtoto wa Jonathan ingawa Jonathan hakuwa hai alirejeshewa mali za babu na baba ake (Wema ni akiba utamfaa hata mwanao hata k**a wewe usipokuwepo).

Unatenda nini sasa kwa mtu au watu unaoishi nao. Je hawatajilipiza kwa mabaya yako? Maisha yako yasije kuacha kisasi juu ya wanao au makosa yako yakakugharimu wewe na uzao wako au familia yako.

Usiwaimize watu ukikumbuka wewe ni mwanadamu na una familia inaahitaji kuishi.

07/09/2022

SOME WARNING SIGNALS YOU MUST PAY ATTENTION TO IN YOUR RELATIONSHIP!

ANGER: If he/she easily gets angry when you have a little misunderstanding, he/she doesn't tolerate jokes, be conscious before you committed to him/her.

THREATENING YOU: If he/she threatening to leave you when you have a little argument, he/she will threatening and may leave you in marriage, be wise.

BEATING YOU: If he beat you up every time, if he slaps you during an argument, he will do the worst in marriage. Be wise.

LACK OF COMMUNICATION: If you are the only one that does all the calling, caring, messaging, texting... It depicts that you are forcing yourself on him/her. A man/woman that truly loves you will show it through his/her actions, he/she will not make excuses, they will find time to connect with you no matter how busy their schedule is. He/she will see you as their priority...Be sensitive.

WOMANIZER: If he womanizes, if you always see him with different girls, if he cheats on you on countless occasions, he may not change if you marry him. Look well before you leap.

HIDING YOU: If he/she hides you if he/she is not proud of you, if he/she fails to introduce you to his friends and family, it possible you are not his/her only option... Be wise.

MUMMY'S BOY/MUMMY'S GIRL: If he/she is a Mummy's boy/girl, if he/she can't make decisions by himself/herself, if he/she must consult his/her mum at all times before he/she can talk to you, his/her mum will influence him/her in marriage. Be wise.

LACK OF MATURITY: If he/she still behaves like a child, if he/she is not mature Spiritually, Emotionally, Mentally, Financially, etc. Marriage is not for kids, marriage is for mature. Be wise.

LACK OF VISION: If he/she doesn't have visions, goals, and dreams, such a man/woman can not be responsible, you will be the one taking all the responsibility if you marry him/her. A woman without vision will be a liability to a man, and a man with no vision will be a burden to a woman.

07/09/2022

K**A UKO HIVI UNAMLAZIMISHA MPENZI WAKO KUCHEPUKA!

Hujawahi kumfumania au ulishamfumania ukasamehe, lakini kila siku akichelewa kurudi utasikia ulikua na wanawake/wanaume zako! Akoongea na simu utasikia ni wanawake/wanaume zako, akisalimiana na mtu basi utasikia ni wanawake/wanaume zako, akifanya chochote kile basia kili yako inakuambia ni wanawake/wanaume zake nma unanuna.

Hata huna ushahidi au ushahidi wenyewe ni wakuuungaunga lakini unalazimishia ana wanawake/wanaume zake! Dada yangu, huyo mwanaume ni suala la muda tu, atakuchoka, yaani hizio kelele zitamlazimisha kuchepuka. Hata k**a mtu alikua malaya kaamua kuacha basi anaona hivi naachia nini k**a mtu kila sikua ananishutumu.

Kwake ataona ni bora tu kwenda kutafuta amani nnje na k**a mnavyojua wanawake/wanaume hawatafuti amani kwa wanawake/wanaume wenzao.

Siku akiipata basi hutakua na haja ya kukisiakisia labda alikua na wanawake/wanaume wake kwani utamuona huyo wanawake/wanaume wake! K**a una tabia hii jua shida si wanawake/wanaume bali ni wewe hujiamini na una kisirani, badilika kabla huyo mwanaume hajakuacha.

07/09/2022

AMKA NA HII; Ujinga ni pale ambapo unatembea na mwanaume, anakushirikisha katika mambo yake yote, wakati mwingine anakupa mpaka kusimamia vitu vyake, wakati ana mke wake au kuna mwanamke wanaishi naye hata k**a hawajafunga ndoa.

Anamdharau huyo mwanamke, anamuongelea vibaya kuwa hamtaki anakupenda wewe, lakini jioni anaenda kulala kwa huyo huyo mwanamke. Hamuachi kila siku anamuambia ni kwasababu ya watoto na wewe unakubali. Unajiona spesho kwakua muda mwingi anatumia kwako na si kwa huyo mwanamke au vitu vingi unajua wewe.

Lakini kuna shida moja, katika hivyo vitu vyote anavyokushirikisha, hakuna hata kimoja, narudia, hakuna hata kimoja ambacho kina jina lako. Kila kitu kuna majina yake au majina ya watoto, wewe ndiyo unasimamia, labda ni mshauri mkubwa lakini hakuna hata kimoja kina majina yako. Halafu anajishaua anakupenda, mwenyewe unamuona mume kabisa kila siku kutuma status kumchamba mke wake.

Dada wewe ni tambara la daki, kazi yake ni kufutia miguu lakini haliingii ndani na k**a likiingia basi litafuta ndani kisha litarudishwa nnje, halivuki ndani. Umuhimu wako ni anapokuomba ushauri, anapokutumia kusimamia biashara zake lakini si kukuweka ndani. K**a akishaamlizana na wewe anarudi kwa mwanamke wake kulala naye basi jua kuwa unatumika tu!

25/08/2022

Don't envy!

• Someone graduated at the age of 22, but waited 5 years before securing a good job.

• Someone became a CEO at 25, and died at 50.

• While another became a CEO at 50, and lived to 90 years.

• Someone is still single, while someone from his school group has become grandfather.

• Obama retired at 55 & Trump started at 70.

• Everyone in this world works based on their time zone.

• People around you might seem ahead of you & some might seem to be behind you.

• But everyone is running their own race, in their own time.

• Do not envy them.

• They are in their time zone, and you are in yours.

So, relax.

You're not late.
You're not early.
You are very much on time.

20/08/2022

AINA ZA HASIRA ZA WANAWAKE

1. Kuna mwanamke ambaye akikasirika, huishia kulia tuu!

2. Lakini mwingine akichukia, anaongea saanaa muda wote hadi ikukere!

3. Mwanamke mwingine akikasirika, ananuna, haongei! Mtapishana tu kimya kimya. Mawasiliano kibubu-bubu. Shavu limejaa k**a Kobra!

4. Mwingine akishikwa na hasira, period ya ghafla ghafla inafuata!

5. Wako wanawake ambao, ole achukie! Atakachokishika usipokimbie anakutandika nacho, majuto baadaye! Baba mmoja alipigwa 'Pedi' ilotumika, kufuatia kung'ang'ania tendo, huku mwenzi wake yuko katika hali hiyo!

6. Mwanamke mwingine akikasirika, hasira zake zinaishia kwenye kuvunja-vunja vyombo. Au saa nyingine kugombeza-gombeza wafanyakazi na watoto! Dizaini hii, huwa ni wale waliokosa kukidhiwa haja za kihisia na waume zao!

7. Mwanamke mwingine ole akasirike. Mtajuana kitandani panapo majaaliwa! Nakwambia utaungama yote!

8. Kuna ambao wakitibuliwa, hukimbilia kufunga mabegi na kuondoka!

9. Wapo ambao wakikasirika, wanagoma kupika!

10. Wengine wakichukia, wanaamua kwenda kulala kimyaaa!!

11. Wanawake wengine wakikasirika, tumbo linakata, na pengine mpaka kuharisha!

13. Wako ambao wakishikwa na hasira, huingia maombi na kuugua kusikoweza kutamkwa. Uchungu ukiisha, wananawa uso na kwenda sokoni.

14. Yuko ambaye akishikwa na hasira, hucheka saaanaaa.... Hutajua k**a amekasirika! Dizaini hii ni hatari sana, maana anaweza kukudhuru kiurahisi.

WEE UKO KUNDI GANI?

20/08/2022

HATUA ANAZOPITIA MTU ANAYEMWACHA MWENZIE.

Baada ya kuachana, aliyeachwa hudhani yeye pekee ndiye mwenye maumivu. Hujiona ameshindwa na aliyemwacha ni mshindi. Ukweli ni kuwa maumivu hujiri pande zote mbili k**a kweli nyote mlipendana na kuzoeana.

Zifuatazo ni hatua ambazo mtu anayemwacha mwenzie huzipitia;

KIPINDI CHA AHUENI AU NAFUU

Wazo la kuachana na mtu haliji ndani ya dakika moja. Ukiona mwenzio anafanya uamuzi wa kuachana na wewe leo, ujue pengine alishawaza hivyo muda mrefu uliopita. Inawezekana alishafanya tathmini yake ya kina na kujiridhisha kuwa hapaswi kuendelea nawe.

Wakati mwingine mtu anakosa ujasiri wa kutamka kwamba mfike mwisho, lakini ukitazama matendo yake unagundua anataka nini.

Inapotokea uhusiano umefika mwisho na mtu akatamka au nia yake ikaeleweka, huwa nafuu kubwa. Angalau, kile ambacho kilikuwa kinamtesa, akifikiria jinsi gani atakifanya sasa kimekuwa. Anakuwa ameshusha mzigo mkubwa sana na kupata ahueni ya kutosha.

Hatua ya ahueni huchukua muda mchache. Mara nyingi hudumu kuanzia siku 3-7 lakini pia inaweza kudumu kwa kipindi kirefu zaidi kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine. Mazingira ya mtu na mtu huamua kipindi cha ahueni kidumu kwa muda gani.

2. UHURU
Katika kipindi hiki, sasa anao uhakika kuwa uhusiano umefika mwisho. Anafurahia maisha yake mapya bila uwepo wa aliyetamani kuachana naye. Anaishi huru bila migogoro ambayo ilitawala uhusiano wake uliopita. Ni kipindi ambacho anaweza kujenga ujamaa na watu ambao mwenzi wake wa zamani alikuwa hapatani nao, pengine mwanzoni aliwakwepa kwa sababu ya kulinda hisia za aliyekuwa mwandani wake. Zaidi, atakuwa huru kufanya kila alichotamani kabla lakini alishindwa kwa sababu ya uwepo wa mpenzi wake

3. TATHMINI
Katika kipindi hiki anaanza kumkumbuka mpenzi wake aliyepita. Anakumbuka mazuri yake na huenda akaanza kupuuza mabaya yake. Anajiuliza yuko wapi, anafanya nini, na nani, anaendeleaje, je, ameshapata mpenzi mwingine? Anakuwa na shauku ya kujua kitu gani kinaendelea katika maisha ya

Address

DIANI
Mombasa

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when WILD ROCKY TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share