04/05/2026
Simba 🦁Diamond Platnumz amewasuprise Mashabiki Ufaransa Kwenye Show Ya Fallyipupa Kwa Ajili Ya Kutumbuiza Wimbo Wao "Inama" Kwa Mara Ya Kwanza Pamoja.
Diamond anakuwa Msanii Wa Kwanza kutoka Afrika Mashariki Kutumbuiza Mbele Ya Mashabiki Zaidi Ya Elfu 80 Nchini Ufaransa.
Kumbuka Leo Inakuwa Siku Ya Pili (2) Mfululizo Kwa Fally Ipupa Kufanya Onesho Lake Hili Katika Uwanja Wa Stade De France Unaochukua Mashabiki Zaidi Ya 80K. Fally Ipupa Ameweka Historia Kwa Kuuza Tiketi Zote (Sold-Out) Katika Siku Zote Mbili Mfululizo, Ambapo Kiingilio Cha Chini Kilikuwa Ni Tsh 195,000/=.
Tamasha Hili Ni Maalumu Kwa Ajili Ya Kusherehekea Miaka 20 Ya Mafanikio Ya Muziki Wake (Fally Ipupa).