Mombasa InfoDrop

Mombasa InfoDrop We spotlight truth, amplify local voices, and hold power to account.

Mombasa InfoDrop is a bold, independent digital news platform delivering real-time updates, human interest stories, and in-depth investigative reports from Kenya and beyond.

Maafisa wa Idara ya Upelelezi ya Jinai (DCI) wamemk**ata mshukiwa anayehusishwa na matamshi ya uchochezi yaliyosambaa kw...
27/05/2026

Maafisa wa Idara ya Upelelezi ya Jinai (DCI) wamemk**ata mshukiwa anayehusishwa na matamshi ya uchochezi yaliyosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, huku maudhui yake yakitajwa kuwa ya kuchochea vurugu na kuhatarisha mshik**ano wa wananchi pamoja na utulivu wa taifa.

Mshukiwa huyo mwenye umri wa miaka 33, Evans Onyango Kawala maarufu k**a Kidero Jasuba, alik**atwa katika eneo la Shujaa Mall, Kayole, kufuatia operesheni maalum iliyotekelezwa na maafisa wa Kikosi cha Operations Support Unit (OSU).

Kwa sasa anazuiliwa na anaendelea kufanyiwa taratibu za kisheria kabla ya kufikishwa mahak**ani.

DCI imewaonya wananchi dhidi ya kutoa matamshi ya uchochezi au kusambaza maudhui yanayoweza kuchochea vurugu, kueneza chuki au kuhatarisha amani na umoja wa kitaifa. Idara hiyo imesisitiza kuwa vitendo vya aina hiyo ni makosa makubwa ya jinai, na wahusika watakabiliwa na hatua kali za kisheria kwa mujibu wa sheria.

Lulu Hassan
27/05/2026

Lulu Hassan

27/05/2026
26/05/2026

TUNAHITAJI viongozi wanaotenda kwa hekima, busara na nidhamu wakati wote. Kilichotokea hakikubaliki kabisa kwa hadhi ya Mbunge wa Mvita. Mvita inastahili uongozi wa heshima, utulivu na mfano mwema kwa vijana na jamii kwa ujumla.

25/05/2026

LULU YA JAMII- Kila mmoja ni lulu atika jamii by Lulu Hassan

MABADILIKO MAKUBWA YAFANYIKA KATIKA HUDUMA YA POLISI KENYANaibu Inspekta Jenerali wa Huduma ya Polisi Kenya, Eliud Lagat...
24/05/2026

MABADILIKO MAKUBWA YAFANYIKA KATIKA HUDUMA YA POLISI KENYA

Naibu Inspekta Jenerali wa Huduma ya Polisi Kenya, Eliud Lagat, ametangaza mabadiliko mapya ndani ya kikosi hicho katika waraka uliotolewa tarehe 24 Mei 2026.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mak**anda na maafisa mbalimbali wamehamishwa katika vitengo tofauti huku wengine wakielekea likizo ya kustaafu.

Miongoni mwa walioguswa na mabadiliko hayo ni Noah Kirwa Maiyo ambaye amehamishwa kutoka nafasi ya Kamanda wa PEU kwenda Makao Makuu ya Polisi Kitengo cha Vigilance.

Aidha, Juda Mathews Gwiyo ambaye alikuwa Naibu Kamanda wa PEU amepelekwa likizo akisubiri kustaafu rasmi.

Katika mabadiliko hayo pia, William Sawe amehamishwa kutoka kitengo cha Recce Sub Unit na kuwa Kamanda mpya wa PEU huku George Kirera akiteuliwa kuwa Naibu Kamanda wa PEU.

Josphat Sirma naye amehamishwa kutoka nafasi ya Naibu Kamanda wa Recce Sub Unit na kuwa Kamanda wa kitengo hicho.

Vilevile, Rere Kipkoech amehamishwa kutoka Deputy SOB1 kwenda Makao Makuu ya Polisi Kitengo cha Vigilance.








NAIROBI - This girl was rescued from trafficking, currently at jogoo road police station.
24/05/2026

NAIROBI - This girl was rescued from trafficking, currently at jogoo road police station.

24/05/2026

Hali ya Taharuki Kilifi: Mwanamume Aliyevunja Ulinzi na Kumkaribia Rais Ruto Adhibitiwa
Kijana mmoja alizua hali ya taharuki ya muda katika Kaunti ya Kilifi baada ya kufanikiwa kupenya katikati ya maafisa wa usalama na kuelekea moja kwa moja jukwaani alipokuwa akihutubia Rais William Ruto.Tukio hilo lilifanyika wakati wa ibada na hafla ya shukrani iliyoandaliwa kwa heshima ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana (Youth Affairs PS), Fikirini Jacobs.

Jinsi Tukio Lilivyojiri
Mwanamume huyo alijitokeza ghafla kutoka kwenye umati mkubwa wa watu na kuanza kupiga hatua kwa kasi kuelekea jukwaani huku Rais akiwa katikati ya hotuba yake. Hatua hiyo ilisababisha sintofahamu ya sekunde kadhaa na kumlazimu Kiongozi wa Nchi kukatiza hotuba yake ghafla.

Maafisa wa Kitengo cha Ulinzi wa Rais (Presidential Security Unit) walivamia jukwaa haraka na kumkaba koo kijana huyo kabla ya kumwondoa eneo hilo.Kauli ya Rais Ruto: Pamoja na taharuki hiyo, Rais Ruto aliwasihi walinzi wake wasimuumize kijana huyo akisema: “Wachana na huyo kijana.”

Rais Atuliza Umati kwa Utani
Baada ya kijana huyo kuondolewa kwa amani, Rais alituliza anga kwa kucheka na kutupia utani uliowavunja mbavu waliohudhuria:“Huyo kijana hana shida yoyote. Nafikiri amejifunza kutoka kwa Fikirini Jacobs kwamba usipitwe na fursa yoyote (not to miss any opportunity).

Nitashughulikana naye baadaye,” Rais alisema huku kukiwa na vicheko kutoka kwa umati.Muda mfupi baada ya tukio hilo, usalama uliimarishwa zaidi jukwaani na hafla hiyo iliendelea k**a ilivyopangwa bila matatizo mengine. Hadi sasa, nia hasa ya kijana huyo haijajulikana wazi na maafisa wa usalama hawajatoa taarifa rasmi.

Mfalme wa Morocco, Mohammed VI, amewasamehe mashabiki wa Senegal waliokuwa wamefungwa jela kufuatia vurugu na machafuko ...
24/05/2026

Mfalme wa Morocco, Mohammed VI, amewasamehe mashabiki wa Senegal waliokuwa wamefungwa jela kufuatia vurugu na machafuko yaliyotokea baada ya fainali ya AFCON 2025 kati ya Senegal na Morocco mjini Rabat.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu ya Morocco, msamaha huo umetolewa kuelekea maadhimisho ya Eid al-Adha na umetajwa kuwa wa “kibinadamu” pamoja na kuimarisha uhusiano wa kindugu kati ya Morocco na Senegal.

Mashabiki hao walik**atwa baada ya vurugu kuzuka kufuatia maamuzi tata ya VAR wakati wa fainali hiyo yenye utata mkubwa katika historia ya AFCON. Baadhi yao walikuwa wamehukumiwa vifungo vya kati ya miezi mitatu hadi mwaka mmoja kwa makosa ya uharibifu wa mali, vurugu dhidi ya maafisa wa usalama na kujaribu kuvamia uwanja.

WAMEPANDISHA FERRY KIMYA KIMYA Kenya Ports Authority CHARGES ARE NOT THERE ON THE WEBSITE
22/05/2026

WAMEPANDISHA FERRY KIMYA KIMYA Kenya Ports Authority CHARGES ARE NOT THERE ON THE WEBSITE

MAAFISA WA TANZANIA WAPIGWA MARUFUKU MAREKANI KWA TUHUMA ZA KUMTESA BONIFACE MWANGI NA MWANAHARAKATI WA UGANDAMarekani i...
22/05/2026

MAAFISA WA TANZANIA WAPIGWA MARUFUKU MAREKANI KWA TUHUMA ZA KUMTESA BONIFACE MWANGI NA MWANAHARAKATI WA UGANDA
Marekani imechukua hatua kali dhidi ya afisa mwandamizi wa polisi nchini Tanzania, Faustine Jackson Mafwele, kwa madai ya kuhusika katika ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya wanaharakati wawili maarufu wa Afrika Mashariki.

Mwanaharakati wa Kenya, Boniface Mwangi, pamoja na Agather Atuhaire kutoka Uganda, walik**atwa mwaka jana walipokuwa Tanzania kufuatilia kesi ya uhaini dhidi ya kiongozi wa upinzani Tundu Lissu.

Wawili hao walidai walizuiliwa kwa siri kwa siku kadhaa, wakateswa na hata kufanyiwa ukatili wa kingono kabla ya kuachwa karibu na mipaka ya nchi zao.

Kupitia taarifa iliyotolewa na ofisi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, Marekani imesema kuna ushahidi wa kuaminika unaomhusisha Mafwele na mateso hayo.

Sasa afisa huyo amepigwa marufuku kuingia Marekani.

Address

Mombasa
80100

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mombasa InfoDrop posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share