
18/04/2025
"Asipopadilika, hatutamwona Mbappe tuliyemjua" - Daniel Riolo amesema.
Mchambuzi wa kandanda Mfaransa Daniel Riolo ameonya kwamba Kylian Mbappe anapoteza umahiri wake katika klabu ya Real Madrid wasipoleta mabadiliko makubwa.
Matamshi hayo yanafuatia baada ya mwanasoka huyo kuondoka mapema baada ya jeraha la mguu katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku Arsenal wakiwapa mapingwa hao mara 15 kichapo cha 5-1 kwa jumla ya mabao katika robo-fainali.
Riolo anasisitiza kuwa mwanasoka huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye alijizolea sifa kemkem huko Paris Saint-Germain kwa kuiongoza vyema safu ya ushambulizi, amepungukiwa na makali ambayo yalimtambulisha wakati moja. Kulingana na mchambuzi huyo huyo wa kandanda, kipaji cha Mbappe kinazimwa na mfumo na mbinu wa uchezaji kandanda wa Madrid, ambao wakati huu unawazuia mashabiki kumshuhudia mshambulizi huyo akiwa kwenye upora wake.
Mtaalam huyo alieleza kwenye After Foot on RMC (kupitia Kandanda ya Kikabila):
"Anajitahidi kuongeza mchango wake, akifunga mabao mengine thelathini mwaka huu, ambayo mengine ni ya kupendeza, wakati mengine ni ya msingi. Kwa kuzingatia msimamo wake wa mbele, ni kawaida kufunga. Lakini ataendelea kupoteza talanta yake katika nafasi hii hadi lini?
Riolo alihitimisha:
"Aidha atagundua umbo la kweli - ambalo yuko mbioni - kuchukua tena nafasi ambayo ilimzolea umaarufu, au anaendelea na nafasi huu wake wa 9 na kufanya kazi k**a mshambuliaji wa kati, na hatimaye utapunguza uwezo wake wa ushambulizi mwenyewe.”
"Tulikuwa na mchezaji wa ajabu kutoka umri wa miaka 17 hadi 25, jambo ambalo ni la kupongezwa. Hata hivyo, mabadiliko usipofanuwa, hatutamuona Mbappe tuliyemheshimu."
Ukosoaji huu unafuatia kuondolewa kwa Real Madrid kwenye Ligi ya Mabingwa ya UEFA Ulaya, baada ya kushindwa nyumbani kwao na Arsenal.
Mchezo huo wa marudiano uliofanyika Santiago Bernabeu Aprili 16, tulishuhudia Mbappe akipadilishwa na Brahim Diaz baada ya kupata jeraha la kifundo cha mguu.