Brainset Swahili

Brainset Swahili Tazama • Sikiliza • Jifunze
-
Idhaa inayokuletea makala, tafiti na habari, kwa lugha nyepesi zaidi.
-
Ukweli k**a ulivyo

° instagram.com/brainsetswahili

Putin atoa rambirambi kwa Iran kufuatia ‘mauaji ya kikatili’ ya KhameneiRais wa Urusi, Vladimir Putin, ametuma rambiramb...
01/03/2026

Putin atoa rambirambi kwa Iran kufuatia ‘mauaji ya kikatili’ ya Khamenei

Rais wa Urusi, Vladimir Putin, ametuma rambirambi kufuatia kuuliwa kwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei, shirika la habari la serikali ya Urusi TASS linaripoti.

Putin amekitaja kifo cha Khamenei kuwa ni “mauaji ya kikatili yaliyokiuka misingi yote ya maadili ya kibinadamu na sheria za kimataifa.”

20/02/2026

Mistari myeusi na myeupe ya pundamilia si urembo tu wa asili; ni zana muhimu ya kisayansi inayomsaidia kuishi katika mazingira magumu ya savana. Hizi hapa ni sababu kuu tatu zinazowasilishwa na;

Brenda Karegi, Allan Wetungu, Powell Kipchumba na Isaac Kipngetich.

19/02/2026

Hatma ya mtandao wa TikTok hapa Kenya ni ipi? Wengi wamechanganyikiwa na habari kwamba huenda baadhi ya maudhui yasipatikane au yakadhibitiwe zaidi — na hii inatokana na mpango wa Bunge la Kenya kuanzisha sera kali za udhibiti.

Unaunga mkono mpango huu, au unaupinga.

Hii hapa taarifa inayowasilishwa na wanahabari wa Brainset Swahili; Allan Wetungu, Brenda Kingi na Neema Chepkorir

Ramadhan Kareem!
18/02/2026

Ramadhan Kareem!

Mtindo wa kulala unaweza kuathiri ubora wa ndoto na mzunguko wa jinamizi.Utafiti kutoka Yuzuncu Yil University School of...
11/02/2026

Mtindo wa kulala unaweza kuathiri ubora wa ndoto na mzunguko wa jinamizi.

Utafiti kutoka Yuzuncu Yil University School of Medicine uligundua kuwa karibu 40% ya watu wanaolala upande wa kushoto waliripoti jinamizi za mara kwa mara, ikilinganishwa na chini ya 15% ya watu wanaolala upande wa kulia.

Watafiti walipendekeza kuwa sababu za kisaikolojia k**a vile mkao wa moyo na shughuli za mfumo mkuu wa neva zinaweza kuathiri usindikaji wa hisia wakati wa usingizi wa REM.

10/02/2026

Ukiona vyaelea, vimeundwa! Hii haina mfanowe. Idhaa inayoendeshwa na vijana, walionoa vipaji na kuwa videdea. Hii ni Brainset Swahili. Fuatilia kwnenye mitandao yote. Tazama, Sikiliza, Jifunze.

Mbona Isaac Koech aliamua kuketi staili hii jamani?😅Brainset Swahili katika harakati za kufanya research.
09/02/2026

Mbona Isaac Koech aliamua kuketi staili hii jamani?😅

Brainset Swahili katika harakati za kufanya research.

08/02/2026

Rais mteule wa Uganda, Yoweri Museveni, ataapishwa tarehe 12, Mei 2026, baada ya kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa Januari 15, 2026. Huu utakuwa mwaka wa 41, na muhula wa saba tangu aingie madarakani mwaka 1986.

Wasimuliaji - Allan Wetungu , Powell Kipchumba na Isaac Koech Kipngetich

Hii ni Brainset Swahili, na wewe ni sehemu ya safari yetu. Baki nasi.
07/02/2026

Hii ni Brainset Swahili, na wewe ni sehemu ya safari yetu. Baki nasi.

06/02/2026

Uzuri wa kweli haupo kwenye kioo, bali kwenye ulimi wako. Imam Ali (AS) alitufundisha kuwa nusu ya uzuri wa mwanadamu ni namna anavyozungumza. Lakini tahadhari: k**a alivyosema Rumi, ulimi usiodhibitiwa unaweza kuwa adui wa nafsi yako. Linda maneno yako, linda uzuri wako.

05/02/2026

Huyu ni Mariam Swalehe, mwanahabari hapa Brainset Swahili. Wewe shabiki ni sehemu ya safari yetu. Baki nasi!

04/02/2026

Rais wa Kenya William Ruto amecheza wimbo maarufu wa Kenya “Donjo Maber” wa msanii Iyanii.

“Donjo Maber” unapendwa hasa na vijana wa Gen Z.

Amecheza wakati wa mkutano wake na vijana katika Kaunti ya Kisumu Februari 2, 2026.

Rais anaendeleza mpango wa maendeleo ya vijana unaoitwa “Mradi wa Nyota” ambao anasema utainua vijana kiuchumi.

Address

Nairobi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Brainset Swahili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share