12/09/2025
Ikiwa unahitaji kutumia muda wa maisha yako kuwa pamoja na yule mtu ambae umesema unampenda basi ni lazima uelewe kwamba si kila siku itakuwa nzuri kwenu. Zipo siku za migogoro, siku ngumu, siku za huzuni na shida pia.
Hivyo jifunze kusamehe na kusahau, mahusiano ni zaidi ya picha na zile romantic movies za kihindi na kikorea ambazo huwa unazitazama.
Mahusiano ni zaidi ya hadithi za Romeo and Juliet ambazo huwa tunahadithiwa, mahusiano ni zaidi ya tamthilia nzuri za kufikirika ambazo huwa tunazipenda na kuzitunza kichwani.
Mahusiano ni zaidi ya kiu za nafsi zetu ambazo huwa tunapata shauku ya kuzitimiza ili kumudu hisia. Mahusiano ni zaidi ya mategemeo yetu ambayo huwa tunayaweka juu ya mtu ili aje awe k**a tunavyodhani ..
Msione watu wanalia, msione watu wanajinyonga ukweli ni kwamba ikiwa hakuna atakaejua majukumu yake mbele ya mwenzi wake basi wote wataishia tu kulalamika na kulaani kizazi hiki. Kizazi ambacho baba na mama bado wapo kwenye ndoa ila binti/kijana wao tayari kashaenda kwenye ndoa tatu na kuachika.
Kwani mnahitaji niwape ushahidi gani wa kuaminika. Hamuoni hata wale ambao hawakuyafahamu mahusiano kwa kina walikimbilia kufanya *harusi* za gharama kubwa na mwishoe mikono yao ikaishia kusaini talaka kwa udhalili na uchungu mkubwa ???
Ugumu wa kuitwa mke/mume wa fulani ulianza pale walipomaliza Fungate π€
Ukweli tusioutilia maanani ni kwamba, harusi ni ya siku moja ila ndoa ni ya milele.
Hata hivyo kila tunda bovu hudondoka kwa wakati wake ππ½ na adhana haina maana kwenye jamii ya viziwi 𦻠π€
Ikiwa wewe hutajifunza kwa kuona mifano ya wengine, basi ipo siku wengine watajifunza kwa kukuona wewe mfanoππ½β. Kuna maisha baada ya hizi (Nakupenda - nakupenda pia) ambazo huwa tuna
Karibu mdundo kwenye channel ya mafunzo na ushauri πππ
https://mdundo.com/a/15130
Misemo ya hekima