Kambi Ya Wateule

Kambi Ya Wateule Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Kambi Ya Wateule, Digital creator, N/A, Nakuru.

Bwana Yesu Kristo asifiwe na karibu sana kwenye hii group,lengo kuu likiwa ni tujifunze Neno La Mungu litupe nuru maishani mwetu ,maarifa na hekima ya Mungu,kuimarisha uhusiano wetu na Mungu kupitia maombezi ,maombi na sadaka zetu [+254]0792593648 .

Nehemia 2:6-7 Mfalme akaniuliza, (malkia naye ameketi karibu naye), Safari yako itakuwa ya siku ngapi? Nawe utarudi lini...
15/01/2026

Nehemia 2:6-7 Mfalme akaniuliza, (malkia naye ameketi karibu naye), Safari yako itakuwa ya siku ngapi? Nawe utarudi lini? Hivyo mfalme akaona vema kunipeleka; nami nikampa muda. Tena nikamwambia mfalme, Mfalme akiona vema, na nipewe nyaraka kwa maliwali walio ng’ambo ya Mto, ili waniache kupita mpaka nifike Yuda;halleluyah mtu wa Mungu, Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya sasa hivi leo biblia inatukumbusha kwamba kabla ya kuanza lolote lile mtafute Mungu kwa maombi naye atakufanikisha k**a tu Nehemia Hallelujah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡

Nehemia 2:6-7 Mfalme akaniuliza, (malkia naye ameketi karibu naye), Safari yako itakuwa ya siku ngapi? Nawe utarudi lini? Hivyo mfalme akaona vema kunipeleka...

Nehemia 1:4 Hata ikawa niliposikia maneno hayo, nikaketi, nikalia, nikaomboleza siku kadha wa kadha; kisha nikafunga, ni...
14/01/2026

Nehemia 1:4 Hata ikawa niliposikia maneno hayo, nikaketi, nikalia, nikaomboleza siku kadha wa kadha; kisha nikafunga, nikaomba mbele za Mungu wa mbinguni;Hallelujah mtu wa Mungu, Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya sasa hivi leo biblia inatukumbusha kwamba Nehemia alilia, akafunga, na akaomba aliposikia habari za uharibifu.hivyo rafiki Sio kila mzigo ni wa kukatisha tamaa,baadhi ya mizigo ni maagizo ya kiungu.
Mungu huturuhusu kuhisi maumivu ili tuwe sehemu ya suluhisho lake.Halleluyah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡

Nehemia 1:3-4 Wakaniambia, Watu wa uhamisho, waliosalia huko katika wilaya ile, wamo katika hali ya dhiki nyingi na mashutumu; tena ukuta wa Yerusalemu umebo...

Hesabu 12:3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.Halleluyah ...
13/01/2026

Hesabu 12:3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.Halleluyah mtu wa Mungu, Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya sasa hivi Rafiki, leo biblia inatukumbusha kuhusu upole na unyenyekevu na biblia inazungumzia Musa aliyekuwa mpole na jinsi Mungu anamshuhudia na zaidi kumtetea na kuweka wazi kwamba Musa alikuwa spesheli kwake na hivyo Mungu anatufundisha nini ?Bonyeza link kisha sikiliza kwa youtube hallelujah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡

Hesabu 12:3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.

Zaburi 34:12​-14 Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, Apendaye siku nyingi apate kuona mema? Uuzuie ulimi wako na maba...
12/01/2026

Zaburi 34:12​-14 Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, Apendaye siku nyingi apate kuona mema?
Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila.Uache mabaya ukatende mema,
Utafute amani ukaifuatie.Halleluyah mtu wa Mungu, Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya sasa hivi, leo biblia inatukumbusha Njia ya maisha mema hallelujah kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡

Zaburi 34:12-14 Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, Apendaye siku nyingi apate kuona mema? Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila.Uach...

Yeremia 18:6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile k**a mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema BWA...
10/01/2026

Yeremia 18:6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile k**a mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema BWANA. Angalieni, k**a udongo ulivyo katika mkono wa mfinyanzi, ndivyo mlivyo ninyi katika mkono wangu, Ee nyumba ya Israeli.halleluyah mtu wa Mungu, Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya sasa hivi, leo biblia inatukumbusha kwamba Mungu ana mamlaka ya kutuumba ,kuturekebisha na kutuongoza kulingana na mapenzi yake k**a vile mfinyanzi anavyoufanyia udongo hivyo jiachilie mikononi mwa Mungu na hautajutia hallelujah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡πŸ‘‡

Yeremia 18:1-2 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa BWANA, kusema, The word which came to Jeremiah from the LORD, saying,[2]Ondoka, ukashuke mpaka ...

Mwanzo 15:6 Akamwamini BWANA, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.halleluyah mtu wa Mungu popote pale ulipo, Bwana Yes...
09/01/2026

Mwanzo 15:6 Akamwamini BWANA, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.halleluyah mtu wa Mungu popote pale ulipo, Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya sasa hivi ,leo biblia inatufunza kumwamini Bwana ni kumtii Jinsi Ibrahimu Alimwamini Bwana na kutii yote Mungu aliyomwagiza kufanya vivyo hivyo nasi k**a ibrahimu inatupasa kumwamini Mungu na kutii Neno lake ili tukaafikie baraka zetu hallelujah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡πŸ‘‡

Mwanzo 15:6 Akamwamini BWANA, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki. And he believed in the LORD; and he counted it to him for righteousness.

Zaburi 23:1-2 BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,Kando ya maji...
08/01/2026

Zaburi 23:1-2 BWANA ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,Kando ya maji ya utulivu huniongoza.halleluyah mtu wa Mungu ,Bwana yesu asifiwe na habari ya sasa hivi leo zaburi 23 inatufundisha kumtumaini Mungu kikamilifu, kujua kuwa yupo nasi katika kila hali, na kwamba upendo na ulinzi Wake havikomi.halleluyah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡πŸ‘‡

Zaburi 23:1-2 BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

Yohana 16:33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeu...
07/01/2026

Yohana 16:33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.halleluyah mtu wa Mungu, Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya sasa hivi, leo biblia inatukumbusha kwamba amani hupatikana ndani ya Kristo, dhiki ni lazima katika dunia, na ushindi tayari umepatikana kupitia Yesu Kristo na hivyo Dunia inaweza kumsumbua mkristo, lakini haiwezi kumshinda Kristo aliye mshindi.Halleluyah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡

Yohana 16:33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.

Mathayo 8:25-26 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia.Akawaambia, Mbona mmekuwa ...
06/01/2026

Mathayo 8:25-26 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia.Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu.Halleluyah mtu wa Mungu,Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya Mwaka mpya, leo biblia inatukumbusha kwamba Hofu ni dalili ya kutoamini uwepo na uwezo wa Kristo katikati ya dhoruba.Imani ya kweli haimaanishi kutokuwepo kwa dhoruba, bali kumwamini Yesu katikati ya dhoruba.na hivyo ndivyo wanafunzi walihitaji kufanya sawia nasi huu mwaka twahitaji kuwa na imani kwa Yesu katikati ya changamoto badala ya kuogopa hallelujah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡πŸ‘‡

Mathayo 8:23-27 Akapanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata. And when he was entered into a ship, his disciples followed him.[24]Kukawa msukosuko mkuu bahar...

Yohana 15:5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi nin...
05/01/2026

Yohana 15:5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote. Hallelujah mtu wa Mungu, Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya Mwaka mpya, leo biblia inatukumbusha kwamba iwapo tunahitaji kufanya neno lo lote mwaka lazima tukae ndani ya Yesu na Yesu ndani yetu hivyo husifanye lolote 2026 pasipo na Yesu Kristo hallelujah na kuwa na siku ya baraka. πŸ‘‡πŸ‘‡

Yohana 6:17-21 wakapanda chomboni, wakaanza kuivuka bahari kwenda Kapernaumu. Nako kumekwisha kuwa giza, wala Yesu hajawafikia.Na bahari ikaanza kuchafuka kw...

Isaya 43:1-2 Lakini sasa, BWANA aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nime...
03/01/2026

Isaya 43:1-2 Lakini sasa, BWANA aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito,haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.Halleluyah mtu wa Mungu,Bwana yesu asifiwe na habari ya mwaka mpya,kwenye neno la Mungu leo ,biblia inatukumbusha kwamba Mungu anawamiliki watu wake, anawapenda, na hawapaswi kuogopa kwa sababu yuko pamoja nao katika kila hali mwaka huu wa 2026 Halleluyah na kuwa na siku ya baraka . πŸ‘‡πŸ‘‡.

Isaya 43:1-2 Lakini sasa, BWANA aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, we...

Isaya 43:18-19 Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litac...
01/01/2026

Isaya 43:18-19 Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.Halleluyah mtu wa Mungu ,Bwana Yesu Kristo asifiwe na habari ya Mwaka mpya,tunapoanza mwaka huu mpya wa 2026 Mungu anatwambia tuyasahau yaliyopita maana anataka kutenda jambo jipya maishani mwetu na anataka tuinue imani yetu na tulione hilo analolitenda na kisha tutafanikiwa,Mwaka wa 2026 tembea kwa imani sio kwa hofu,tembea kwa tumaini na wala sio majuto ,tembea na Mungu na wala sio peke yako na utakula mema ya nchi. πŸ‘‡πŸ‘‡

Isaya 43:18–19 (NIV) Msiyakumbuke mambo ya kale wala msiyaangalie mambo ya zamani. Tazama, nafanya jambo jipya; sasa linachipuka, je, hamlioni?”—Join this ch...

Address

N/A
Nakuru
N/A

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kambi Ya Wateule posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kambi Ya Wateule:

Share