Masomo ya Misa ya kila siku

  • Home
  • Masomo ya Misa ya kila siku

Masomo ya Misa ya kila siku This is a religious page that enables you to find daily Mass readings. Welcome all and God bless you. Spiritual counselor and Coach.

Motivation and spiritual Career Advisor.

MASOMO YA MISA, DESEMBA 7, 2025JUMAPILI, JUMA LA  2 LA MAJILIOSOMO 1Isa. 40:1 – 11Somo la 1Isa 11:1-10Siku ile: litatoka...
06/12/2025

MASOMO YA MISA, DESEMBA 7, 2025
JUMAPILI, JUMA LA 2 LA MAJILIO

SOMO 1
Isa. 40:1 – 11

Somo la 1
Isa 11:1-10
Siku ile: litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda. Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana; na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayas**iayo kwa mas**io yake; bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya. Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa kujifungia. Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza. Ng'ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani k**a ng'ombe. Na mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika pango la fira. Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua Bwana, k**a vile maji yanavyoifunika bahari. Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 72:1-2, 7-8, 12-13, 17

(K) Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi,
Na wingi wa amani hata mwezi utakapokoma.

Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako,
Na mwana wa mfalme haki yako.
Atawaamua watu wako kwa haki,
Na watu wako walioonewa kwa hukumu. (K)

Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi,
Na wingi wa amani hata mwezi utakapokoma.
Na awe na enzi toka bahari hata bahari,
Toka Mto hata miisho ya dunia. (K)

Kwa maana atamkomboa mhitaji aliapo,
Na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi.
Atamhurumia aliye dhaifu na maskini,
Na nafsi za wahitaji ataziokoa. (K)

Jina lake na lidumu milele,
Pindi ling'aapo jua jina lake liwe na wazao;
Mataifa yote na wajibariki katika yeye, Na kumwita heri. (K)

SOMO 2
Rum 15:4-9

Ndugu zangu, yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini. Na Mungu mwenye saburi na faraja awajalie kunia mamoja ninyi kwa ninyi, kwa mfano wa Kristo Yesu; ili kwa moyo mmoja na kwa kinywa kimoja mpate kumtukuza Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Kwa hiyo mkaribishane ninyi kwa ninyi, k**a naye Kristo alivyotukaribisha, ili Mungu atukuzwe. Kwa maana nasema, ya kwamba Kristo amefanyika mhudumu wa agano la kutahiriwa kwa ajili ya kweli ya Mungu, kusudi azithibitishe ahadi walizopewa baba zetu; tena ili Mataifa wamtukuze Mungu kwa ajili ya rehema zake; k**a ilivyoandikwa, Kwa hiyo nitakushukuru kati ya Mataifa, Nami nitaliimbia jina lako.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO
Lk 3:4,6

Aleluya, aleluya
Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake,na wote wenye mwili watauona wokovu wa Mungu.
Aleluya

INJILI
Mt 3:1-12

Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. Kwa sababu huyo ndiye aliyenenwa na nabii Isaya, akisema, Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake. Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi lake la singa za ngamia, na mshipi wa ngozi kiunoni mwake; na chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu. Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani; naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao. Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? Basi zaeni matunda yapasayo toba; wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto. Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni. Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto. Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

06/12/2025

MASOMO YA MISA DESEMBA 6, 2025
JUMAMOSI, JUMA LA 1 LA MAJILIO

SOMO 1
Isa. 30:19-21, 23-26

Bwana Mungu Mtakatifu wa Israeli asema; watu watakaa katika Sayuni huko Yerusalemu; wewe hutalia tena; hakika yake atakuonea rehema nyingi kwa sauti ya kilio chako; as**iapo ndipo atakapokujibu.

Na ingawa Bwana atawapeni chakula cha shida na maji ya msiba, lakini waalimu wako hawatafichwa tena, ila macho yako yatawaona waalimu wako; na mas**io yako yatas**ia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.

Naye atatoa mvua juu ya mbegu zako, upate kuipanda nchi hii; na mkate wa mazao ya nchi, nayo itasitawi na kuzaa tele; katika siku hiyo ngo’ombe zako watakula katika malisho mapana. Ng’ombe pia na wanapunda wailimao nchi watakula chakula kilichokolea, kilichopepetwa kwa ungo na kwa pepeo.

Na juu ya kila mlima mrefu, na juu ya kila kilima kilichoinuka, itakuwapo mito na vijito vya maji, katika siku ya machinjio makuu itakapoanguka minara. Na tena nuru ya mwezi itakuwa k**a nuru ya jua, na nuru ya jua itaongezeka mara saba, k**a nuru ya siku saba, katika siku ile Bwana atakapofunga mapigo ya watu wake, na kuliponya pigo la jeraha yao.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 147:1-6 (K) Isa. 30:18

(K) Heri wote wamngojao Bwana.

Msifuni Bwana, maana ni vema kumwimbia Mungu wetu,
Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri.
Bwana ndiye aijengaye Yerusalem,
Huwakusanya waliotawanyika wa Israeli. (K)

Huwaponya waliopondeka moyo,
Na kuziganga jeraha zao.
Huihesabu idadi ya nyota,
Huzipa zote majina. (K)

Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu.
Akili zake hazina mpaka,
Bwana huwategemeza wenye upole,
Huwaangusha chini wenye jeuri. (K)

SHANGILIO
Isa. 33:22

Aleluya, aleluya.
Bwana ndiye mwamuzi wetu; Bwana ndiye mfanya sheria wetu; Bwana ndiye mfalme wetu; Ndiye atakayetuokoa.
Aleluya.

INJILI
Mt. 9:35-10:1, 6-8

Siku ile: Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.

Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika k**a kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apelike watenda kazi katika mavuno yake.

Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.

Akawaambia, afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

04/12/2025

© 2021 Radio Maria Tanzania Dar es Salaam P.O.Box 34573, Plot Namba 125, Mikocheni Industrial Area, Dar es Salaam, Tanzania

28/11/2025
Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Timoth Chakundya, Nicholus Everlyn Mwita, Andreus Simion,...
27/11/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Timoth Chakundya, Nicholus Everlyn Mwita, Andreus Simion, Titus Akungwi

27/11/2025

Good morning the people of God.
Tujue Rangi ya Liturujia ya maajilio(kwa kiswahili) ... Tuone wanafunzi wachangamfu🖐️

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI, NOVEMBA 30 2025* *DOMINIKA YA KWANZA YA MAAJILIO, MWAKA A* *RANGI YA LITURUJIA: URUJUANI 💜*...
27/11/2025

*MASOMO YA MISA YA JUMAPILI, NOVEMBA 30 2025*

*DOMINIKA YA KWANZA YA MAAJILIO, MWAKA A*

*RANGI YA LITURUJIA: URUJUANI 💜*
*MATENDO YA ROZARI 📿: MATENDO YA UTUKUFU*

*MADA YA DOMINIKA:*
```KUWA MACHO!```

*_Masomo yote matatu ya Dominika hii yanahimiza kuhusu kukesha, sio k**a hali ya huzuni katika kumsubiri Bwana/jaji kwenye mwisho wa maisha yetu, lakini k**a mwamko wa uwepo wa Bwana leo. Somo la kwanza linatuambia juu ya ulimwengu mpya ambao utaanza na kuja kwa Bwana. Injili inatuhimiza tuwe macho ili tuweze kumkaribisha wakati wa "ujio" wake. Somo la pili linatualika kufungua macho yetu ili kutambua ishara za siku mpya ambayo tayari imeanza._*

*ANTIFONA YA KUINGIA*
_Ee Bwana, nakuinulia roho yangu, nakutumainia wewe, ee Mungu wangu, usiniache niaibike. Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda; wote wanaokutumainia hawatatiwa haya._

*KOLEKTA*
```Ee Mungu mwenyezi, twakuomba, uwajalie waamini wako ari ya kumlaki kwa matendo ya haki Kristo wako anayekuja, ili, akiisha kuwaweka kuumeni kwake, wapate kuumiliki Ufalme wa
mbinguni. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.```

*SOMO LA KWANZA*
*ISAYA 2: 1-5*

_Bwana atayakusanya mataifa yote katika amani ya milele ya ufalme wa Mungu_

*_Somo katika kitabu cha Nabii Isaya_*

Haya ndiyo aliyoyaona Isaya, mwana wa Amosi, kuhusu Yuda na Yerusalemu. Itatukia siku za mwisho ya kuwa mlima wa hekalu la BWANA utawekwa imara juu ya milima, na kuinuliwa juu kupita vilima. Mataifa yote watauendea kwa wingi. Na makabila mengi watafika huko, wakisema, "Haya, tuupande mlima wa BWANA, tuiendee nyumba ya Mungu wa Yakobo, ili atufundishe njia zake, nasi tufuate mapito yake." Maana toka Sioni sheria itatokea, na neno la BWANA kutoka Yerusalemu. Naye atafanya hukumu kati ya mataifa., atawaamua makabila mengi. Nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao
kuwa mapanga; taifa halitainua upanga iuu ya taifa jingine, wala hawatajifunza ufundi wa vita tena. Enyi watu Wa nyumba ya Yakobo, njoni, tutembee katika mwanga wa BWANA!

*_Neno la Bwana_*

*ZABURI YA KUITIKIZANA*
*ZABURI 122:1-2,4-5,6-7, 8-9 (K. 1)*

*KIITIKIO: _Twende nyumbani kwa Bwana, tukiimba kwa shangwe_*

Nalifurahi waliponiambia,
Twende nyumbani kwa Bwana."
Sasa miguu yetu imesimama
ndani ya malango yako, ee Yerusalemu.

*KIITIKIO: _Twende nyumbani kwa Bwana, tukiimba kwa shangwe_*

Ndiko wanakopanda makabila,
makabila ya Bwana,
k**a ilivyo sheria ya Israeli,
Ya kulitukuza jina la Bwana.
Humo vimewekwa viti vya hukumu,
viti vya nyumba ya Daudi.

*KIITIKIO: _Twende nyumbani kwa Bwana, tukiimba kwa shangwe_*

Uombeeni Yerusalemu amani:
wakupendao wawe salama.
Amani na iwe ndani ya kuta zako,
baraka kwa nyumba zenu!

*KIITIKIO: _Twende nyumbani kwa Bwana, tukiimba kwa shangwe_*

Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu,
nitasema, "Amani kwako."
Kwa ajili ya nyumba ya Bwana, Mungu wetu,
nitakuombea upate fanaka.

*KIITIKIO: _Twende nyumbani kwa Bwana, tukiimba kwa shangwe_*

*SOMO LA PILI*
*WARUMI 13:11-14a*

_Wokovu wetu u karibu zaidi._

*_Somo katika barua ya Mtakatifu Paulo kwa Warumi_*

Ndugu zangu: Mnautambua wakati, saa ya kuamka katika usingizi imefika. Kwa maana sasa wokovu wetu u karibu zaidi
kuliko wakati tulipoanza kusadiki. Usiku umekwisha, mchana umekaribia. Basi, tuyavue matendo ya giza na tuzivae silaha za mwanga. Tuenende kwa adabu k**a inavyopasa mchana, si kwa ulafi au ulevi, si kwa ufisadi wala uasherati, si kwa ugomvi wala wivu. Bali, mvaeni Bwana Yesu Kristo.

*_Neno la Bwana_*

*SHANGILIO LA INJILI*
*ZABURI 85:8*

*Aleluya! Aleluya!*

Utuonyeshe wema wako, ee Bwana; utuletee wokovu wako.

*Aleluya!*

✝️ *INJILI* 📖
*MATHAYO 24:37-44*

_Kesheni, muwe tayari._

*+ _Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Mathayo_*

Wakati ule: Yesu aliwaambia wafuasi wake, "Kwa ujio wa Mwana wa Mtu itakuwa k**a ilivyokuwa siku za Nuhu. Kwa maana siku zile zilizotangulia gharika kuu, watu waliendelea kula na kunywa, kuoa na kuolewa mpaka siku Nuhu alipoingia katika safina. Wasituhumu mambo mabaya hata gharika kuu ikawaghafilisha na kuwachukua wote. Ndivyo kutakavyokuwa pia kuja kwake Mwana wa Mtu. Wakati ule watu wawili watakuwako shambani; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa. Wanawake wawili watakuwa katika kusaga; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa. Kwa hiyo kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu. Basi, fahamuni haya; k**a mwenye nyumba angelijua saa ajapo mwizi, angelikesha asimpe nafasi ya kuvunja nyumba yake. Kwa hiyo nanyi muwe tayari, kwa kuwa Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoidhania."

*_Injili ya Bwana_*

MASOMO YA MISA, NOVEMBA 27, 2025ALHAMISI, JUMA LA 34 LA MWAKA WA KANISA SOMO 1.Danieli 6:12-28Ndipo wakakaribia, wakasem...
27/11/2025

MASOMO YA MISA, NOVEMBA 27, 2025
ALHAMISI, JUMA LA 34 LA MWAKA WA KANISA


SOMO 1.
Danieli 6:12-28

Ndipo wakakaribia, wakasema mbele ya mfalme katika habari ya ile marufuku ya mfalme; Je! Hukuitia sahihi ile marufuku, ya kwamba kila mtu atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme, atatupwa katika tundu la simba? Mfalme akajibu, akasema, Neno hili ni kweli, k**a ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi isiyoweza kubadilika.

Basi wakajibu, wakasema mbele ya mfalme, Yule Danieli, aliye mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda, hakujali wewe, Ee mfalme, wala ile marufuku uliyoitia sahihi, bali aomba dua mara tatu kila siku.

Basi mfalme alipos**ia maneno haya alikasirika sana, akakaza moyo wake ili kumponya Danieli; akajitaabisha kumwokoa hata jua likachwa.

Ndipo watu wale wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia mfalme, Ee mfalme, ujue ya kuwa ni sheria ya Wamedi na Waajemi, lisibadilike neno lo lote lililo marufuku, wala amri yo yote iliyowekwa na mfalme.

Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akanena, akamwambia Danieli, Mungu wako unayemtumikia daima, yeye atakuponya.

Likaletwa jiwe, likawekwa mdomoni mwa lile tundu; naye mfalme akalitia muhuri kwa muhuri yake mwenyewe, na kwa muhuri ya wakuu wake, lisibadilike neno lo lote katika habari za Danieli.

Kisha mfalme akaenda nyumbani kwake, akakesha usiku kucha, akafunga; na vinanda havikuletwa mbele yake; na usingizi wake ukampaa.

Asubuhi mfalme akaondoka mapema, akaenda kwa haraka mpaka penye lile tundu la simba.

Naye alipolikaribia lile tundu, akamlilia Danieli kwa sauti ya huzuni; mfalme akanena; akamwambia Danieli, Ee Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je! Mungu wako, unayemtumikia daima, aweza kukuponya na simba hawa?

Ndipo Danieli akamwambia mfalme, Ee mfalme, uishi milele.

Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi nalionekana kuwa sina hatia; tena, mbele yako, Ee mfalme, sikukosa neno.

Basi mfalme akafurahi sana, akaamuru wamtoe Danieli katika lile tundu. Ndipo Danieli akatolewa katika lile tundu, wala dhara lo lote halikuonekana mwilini mwake, kwa sababu alikuwa anamtumaini Mungu wake.

Mfalme akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomsh*taki Danieli, wakawatupa katika tundu la simba, wao, na watoto wao, na wake zao; na wale simba wakawashinda wakaivunja mifupa yao vipande vipande, kabla hawajafika chini ya tundu.

Ndipo mfalme Dario akawaandikia watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, waliokaa juu ya uso wa dunia; Amani na iongezeke kwenu.

Mimi naweka amri, ya kwamba katika mamlaka yote ya ufalme wangu watu watetemeke na kuogopa mbele za Mungu wa Danieli; maana yeye ndiye Mungu aliye hai, adumuye milele, na ufalme wake ni ufalme usioharibika, na mamlaka yake itadumu hata mwisho.

Yeye huponya na kuokoa, hutenda ishara na maajabu mbinguni na duniani, ndiye aliyemponya Danieli na nguvu za simba.

Basi Danieli huyo akafanikiwa katika enzi ya Dario, na katika enzi ya Koreshi, Mwajemi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 100 (K) Ufu. 19:9

(K) Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwanakondoo.

Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote,
Mtumikieni Bwana kwa furaha;
Njoni mbele zake kwa kuimba. (K)

Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)

Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru;
Nyuani mwake kwa kusifu;
Mshukuruni, lihimidini jina lake. (K)

Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)

SHANGILIO
Zab. 25:4 , 5

Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, unijulishe njia zako, unifundishe mapito yako.
Aleluya.

INJILI
Lk. 21:20-28

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo jueni ya kwamba uharibifu wake umekaribia. Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio katikati yake wakimbilie nje, na walio katika mashamba wasiuingie. Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapitilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa. Ole wao wenye miamba na wanaonyonyesha katika siku hizo!

Kwa kuwa kutakuwa na shida katika nchi, na hasira juu ya taifa hili. Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata majira ya Mataifa yatakapotimia.

Tena, kutakuwa na ishara katika jua; na mwenye, na nyota; na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake; watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazama mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu z ambinguni zitatikisika. Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi. Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

MASOMO YA MISA NOVEMBA 26, 2025 JUMATANO, JUMA LA 34 LA MWAKASOMO 1Dan. 5:1-6,13-14.16-17,23-28Belshaza, mfalme, aliwafa...
26/11/2025

MASOMO YA MISA NOVEMBA 26, 2025
JUMATANO, JUMA LA 34 LA MWAKA

SOMO 1
Dan. 5:1-6,13-14.16-17,23-28

Belshaza, mfalme, aliwafanyia wakuu wake elfu karama kubwa, akanywa divai mbele ya elfu hao. Belshaza, alipokuwa akionja ile divai, akaamuru wavilete vile vyombo vya dhahabu na fedha, ambavyo baba yake, Nebukadreza, alivitoa katika hekalu lililokuwako Yerusalemu; ili kwamba mfalme, na wakuu wake, na wake zake, na Masuria wake, wapate kuvinywea. Basi wakavileta vile vyombo vya dhahabu, vilivyotolewa katika hekalu la nyumba ya Mungu lililokuwapo Yerusalemu; na mfalme, na wakuu wake, na wake zake, na Masuria wake, wakavinywea. Wakanya divai, wakaisifu miungu ya dhahabu, na ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mwe. Saa iyo hiyo vikatokea vidole vya mkono wa mwanadamu, vikaandika katika chokaa ya ukuta wa nymba ya enzi ya mfalme, mahali palipokikabili kinara; naye mfalme akakiona kitanga cha ule mkono ulioandika. Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana.

Ndipo Danieli akaletwa mbele ya mfalme. Na mfalme akanena, akamwambia Danieli, Je! Wewe ndiwe Danieli yule, aliye mmoja wa wana wa Yuda waliohamishwa, ambao mfalme, baba yangu, aliwaleta huku toka Yerusalemu? Nimes**ia habari zako, kwamba roho ya miungu imo ndani yako, na kwamba nuru na ufahamu na akili bora zimeonekana kwako. Nimes**ia habari zako, kwamba waweza kuleta tafsiri, na kufumbua mafumbo; haya! K**a ukiweza kulisoma andiko hili, na kunijulisha tafsiri yake, utavikwa mavazi ya rangi ya zambarau, na kuwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utakuwa mtu wa tatu katika ufalme.

Ndipo Danieli akajibu, akasema, mbele ya mfalme; Zawadi zako zishike wewe mwenyewe; na thawabu zako mpe mtu mwingine; walakini nitamsomea mfalme maandiko haya, na kumjulisha tafsiri yake. Basi umejiinua juu ya Bwana wa mbingu; nao wamevileta vyombo vya nyumba yake mbele yako; na wewe, na wakuu wako, na wake zako, na Masuria wako, mmevinywea; nawe umeisifu miungu ya fedha nay a dhahabu, na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe; wasioona, wala kus**ia, wala kujua neno lolote; na Mungu yule, ambaye pumzi yako I mkononi mwake, na njia zote ni zake, hukumtukuza. Ndipo kile kitanga cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa.

Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; Mene, Mene, Tekeli, na Peresi. Na tafsiri ya maneno haya ni hii; Mene, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha. Tekeli, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka. Peresi, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Dan. 3:62-67 (K) 59

(K) Msifuni na kumwadhimisha Bwana milele.

Jua na mwezi, mhimidini Bwana;
Msifuni na kumwadhimisha milele.
Nyota za mbinguni, mhimidini Bwana;
Msifuni na kumwadhimisha milele. (K)

Manyunyu yote na ukungu, mhimidini Bwana;
Msifuni na kumwadhimisha milele.
Pepo zote, mhimidini Bwana;
Msifuni na kumwadhimisha milele. (K)

Moto na hari, mhimidini Bwana;
Msifuni na kumwadhimisha milele.
Kipupwe na musimu, mhimidini Bwana;
Msifuni na kumwadhimisha milele. (K)

SHANGILIO
1Pet. 1:25

Aleluya, aleluya,
Neno la Bwana hudumu hata milele, na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.
Aleluya.

INJILI
Lk. 21:12-19

Yesu aliwaambia wanafunzi wake; Watawak**ata na kuwaudhi; watawapeleka mbele ya masinagogi, na kuwatia magerezani, mkipelekwa mbele ya wafalme na maliwali kwa ajili ya jina langu. Na hayo yatakuwa ushuhuda kwenu. Basi, kusudieni mioyoni mwenu, kutofikirifikiri kwanza mtakavyojibu; Kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga. Nanyi mtasalitiwa na wazazi wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu. Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu. Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu. Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

26/11/2025

Hamjambo, we are about to usher in the period of advent.

22/11/2025

*SOMANUTIK AB MISA NE TILIL NEBO JUMAPILI, TARIKIT 23/11/2025*

*JUMAPILI NEBO LET (NEBO 34) EN KENYIT AB C NEBO KANISA*

*SUKUKUU NEBO JEISO KRISTO LAITORYAT AB NG'WONY*

*NGORYEET NEBO MISA: NE LEEL 🤍*
*YAUTIK CHEBO ROSARI 📿: CHEBO KALASUNET*

*SOMANET NE TAI*
*2 SAMUEL 5: 1-3*

*_Somanet ne tai koyob kitabutab aeng' nebo Samuel_*

Ki pwa anyun pororyosyek tugul che po Israel ole mi Daudi eng' Hebron ak komwachi koleenji, “Keero, acheek anyun ko ki koweguk ak poortang'ung'.
Eng' peetuusyek che ki kosiirto ye ki laitoryat Saulo ne kiboiywech, ko inyee ne ki indochini Israel ye kimandoi ak komang'u eng' lugoosyek tugul. Ak ki leenjin `Kamuktaindet ne Toroor, ‘Ibae piikyuk Israel ak iegu pounindetap Israel.’ ”
Ki pwa anyun poisyek tugul che po Israel ole mi laitoryat eng' Hebron; ak ki yai `Laitoryat Daudi arorutyet kobooto icheek eng' Hebron eng' taitap Kamuktaindet ne Toroor, ak ki iil `icheek Daudi koek laitoryat koboi Israel.

_*Niton ng'olyotab Cheptalel: Kiwekyini Cheptalel kongoi*_

*TYENDAB KALASUNET*
*TYENWOGIGAP KALASUNET 122: 1-2, 3-4ab, 4cd-5 (W. 1)*

*WOLUNET: _Ongebe kootap Kamuktaindet ne Toroor eng' poiboiyet _*

Ki abaibaitu ye kimwaiwo icheek kole, “Ongebe kootap Kamuktaindet ne Toroor.”
Tonondos keelyekyok eng' ormariichoguk, ee Jerusalem.

*WOLUNET: _Ongebe kootap Kamuktaindet ne Toroor eng' poiboiyet _*

Jerusalem, ne teegat ko uu nganaseet ne tuiyot.
Ole togoste pororyosyek, pororyosyegap Kamuktaindet ne Toroor,

*WOLUNET: _Ongebe kootap Kamuktaindet ne Toroor eng' poiboiyet _*

Paornateet eng' Israel, si komwa kongoi agobo kainetap Kamuktaindet ne Toroor.
Amu ki kinde olooto ng'echerogap laitornatet che po kirwooget, ng'echerogap laitornatet che po kootap Daudi.

*WOLUNET: _Ongebe kootap Kamuktaindet ne Toroor eng' poiboiyet _*

*SOMANET NE BO AENG'*
*KOLOSAIK 1: 12-20*

*_Somanetab aeng' koyob baruetab koyoktoindet Paulo ne kisirjin Kolosaik_*

Ogoochini kongoi Kwanda, ne kiyaech keegu che nyoljin keyamde poroteetap che tiliileen eng' lapkeiyet; ne kisarwech kemang'une kimnateetap mesundeito, ak kouutech keebe laitornatetap Weeriit ne po chamyennyi; ne ki tinyei eng' ineendet katyagennyo, nyoetap kaat ne po tengekwogikyok.
Ineendet itoondap Kamuktaindet ne ma taagu, ineendet ne kisip kesich eng' kiit age tugul ne ki kitoi keyai; amu ki kitoi keyai tuguuk tugul eng' ineendet, che mi kipsengwet ak che mi ng'wony, tuguuk che taagu ak tuguuk che ma taagu, anan laitornatosyek, anan kiptainatosyek, anan pounatosyek anan kimnatosyek; ki kitoi keyai tuguuk tugul eng' ineendet ak ko po ineendet; ak po tai ineendet eng' tuguuk tugul, ak namegei tuguuk tugul eng' ineendet.
Ak ineendet metitap poorto, nooto kaniset: ineendet taunet, taunindetap che ki mong' eng' che ki pek; si kobiit koek ne oo eng' tuguuk tugul.
Amu ki chamak komyee keele komeny nyiyet tugul eng' ineendet; si kotuiyechigei tuguuk tugul ineendet, ye kingo kagoyai kaalyeet eng' korotiigap kimurtoiyondennyi; eng' ineendet, ngo tuguuk che mi ng'wony anan tuguuk che mi kipsengwet.

_*Niton ng'olyotab Cheptalel: Kiwekyini Cheptalel kongoi*_

*KATORORETAB LOGOIYWEK CHE MYACH*
*MARIKO 11: 9, 10*

_Aleluya! Aleluya!_

Iberuurot ineendet ne nyoonei eng' kainetap Kiptaiyat! Iberuurot laitornatet ne nyoonei ne po kwandanyo Daudi.

_Aleluya!_

✝️ *INJILI* 📖
*LUKA 23: 35-43*

_*Logoiywek che myach kouu ye kisir Luka ne Tiliil: Ilosunot ee Kiptaiyat*_

Ak kitonondos piik kogeerei. Ak kororechi ineendet pounik kole, Kisaru alak; ingosargei ibak ngo Kristo niito, ne lewenot ne po Kamuktaindet. Ak kichurochur ak icheek kiplugotinik ineendet, kobwanei ye mi ineendet, kogoochin s**i, koleen, Ngo ii Laitoryatap Yahudik, isarugei.
Ak ki mi siruutik metinnyi parak, che mwaei koleen, NI KO LAITORYAT NE PO YAHUDIK. Ak kichurachur ineendet age eng' kiptengeginichooto kiga kigartaat, kole, “Tos ma ii Kristo inyee? Sarugei ak isarwech ak acheek.”
Ago ki wol age, ak koger kong' kole, “Meiywei Kamuktaindet, agot inyee, ak imi kagikyinonooto? Ago po iman nenyo; amu kagigoonech ko uu poisyonikyok: ago ma yai chiichi kiy ne ma nyolu.”
Ak ki le, “Jeso, ibwaata ye tuun inyone eng' laitornateng'ung'.” Ak ki leenji `Jeso ineendet, Amwaun iman, ale, Kitebye tuwai rani eng' Paradiso.

*_Logoiywek che myach chebo Cheptalel: Neng'ung'et katororet ee Kristo_*

22/11/2025

Shallom. Were you aware that we are starting the last week tomorrow as per to the church calendar. Wangapi walikuwa wakijua🖐️

Address

Nandi Hills

Telephone

+254716792020

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Masomo ya Misa ya kila siku posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share