Masomo ya Misa ya kila siku

  • Home
  • Masomo ya Misa ya kila siku

Masomo ya Misa ya kila siku This is a religious page that enables you to find daily Mass readings. Welcome all and God bless you.

You will come out of the deserts of your life..... Amen
24/09/2025

You will come out of the deserts of your life..... Amen

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 24, 2025JUMATANO, JUMA LA 25 LA MWAKASOMO 1Ezr. 9:5-9Wakati wa sadaka ya jioni, mimi Ezra nilii...
24/09/2025

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 24, 2025
JUMATANO, JUMA LA 25 LA MWAKA

SOMO 1
Ezr. 9:5-9

Wakati wa sadaka ya jioni, mimi Ezra niliinuka baada ya kunyenyekea kwangu, nguo yangu na joho yangu zimeraruliwa, nikaanguka magotini nikakunjua mikono yangu mbele za Bwana, Mungu wangu; nikasema, Ee Mungu wangu, nimetahayari, naona haya kuinua uso wangu mbele zako, Mungu wangu; kwa maana maovu yetu ni mengi, hata yamefika juu ya vichwa vyetu, na hatia yetu imeongezeka na kufika mbinguni. Tangu siku za baba zetu tumekuwa na hatia kupita kiasi hata leo; na kwa sababu ya maovu yetu sisi, na wafalme wetu, na makuhani wetu, tumetiwa katika mikono ya wafalme wa nchi hizi, tumepigwa kwa upanga, tumechukuliwa mateka, tumenyang’anywa mali zetu, tumetiwa haya nyuso zetu, k**a hivi leo. Na sasa kwa muda kidogo tumeneemeshwa na Bwana, Mungu wetu, hata akatuachia mabaki yaokoke, akatupa msumari katika mahali pake patakatifu. Mungu wetu atutie nuru machoni mwetu, tuburudike kidogo katika kufungwa kwetu. Maana sisi tu watumwa; lakini Mungu wetu hakutuacha katika utumwa wetu, bali ametufikilizia rehema zake, mbele ya wafalme wa Uajemi, ili kutuburudisha, tuisimamishe nyumba ya Mungu wetu, na kuitengeneza palipobomoka, atupe ukuta katika Yuda na Yerusalemu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Tob. 13:2-4, 6 (K) 1

(K) Amehimidiwa Mungu aishiye milele.

Kwa maana hurudi, na kurehemu tena;
Hushusha hata kuzimu, na kuinua tena;
Wala hakuna awezaye kujiepusha na mkono wake. (K)

Enyi bani Israeli, mshukuruni mbele ya mataifa
Yeye ambaye ametutawanya katikati yao. (K)

Kuko huko utangazeni ukuu wake,
Mwadhimisheni mbele ya wote walio hai;
Kwa kuwa Yeye ndiye Bwana wetu,
Naye Mungu yu Baba wetu,
Naye Mungu yu Baba yetu milele. (K)

SHANGILIO

Aleluya, aleluya,
Ee Mungu, tunakusifu, tunakukiri kuwa Bwana. Jamii tukufu ya Mitume inakusifu.
Aleluya.

INJILI
Lk. 9:1-6

Yesu aliwaita wale Thenashara, akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi. Akawatuma wautangaze ufalme wa Mungu, na kupoza wagonjwa. Akawaambia, Msichukue kitu kwa safari yenu, fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, wala mmoja wenu asiwe na kanzu mbili. Na nyumba yoyote mtakayoingia kaeni humo, tokeni humo. Na wale wasiowakaribisha, mtokakpo katika mji huo yakung’uteni hata mavumbi ya miguuni mwenu, kuwa ushuhuda juu yao. Wakaenda, wakazunguka katika vijiji, wakihubiri Injili, na kupoza watu kila mahali.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Kwa ajili ya wale wangependa kuenda kitu bio kwa kiswahili.
23/09/2025

Kwa ajili ya wale wangependa kuenda kitu bio kwa kiswahili.

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 23, 2025JUMANNE, JUMA LA 25 LA MWAKASOMO 1Ezr. 6:7-8, 12, 14-20Mfalme Dario alimwandikia liwali...
22/09/2025

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 23, 2025
JUMANNE, JUMA LA 25 LA MWAKA

SOMO 1
Ezr. 6:7-8, 12, 14-20

Mfalme Dario alimwandikia liwali wa ng’ambo wa mto, na wenzake; Waacheni liwali wa Wayahudi na wazee wa Wayahudi, waijenge nyumba hii ya Mungu mahali pake. Tena, natoa amri kuwaagiza ninyi mtakayowatendea wazee hao wa Wayahudi kwa kazi hii ya kuijenga nyumba ya Mungu; katika mali ya mfalme, yaani, katika kodi za nchi iliyo ng’ambo ya Mto, watu hao wapewe gharama zote kwa bidii, ili wasizuiliwe. Na Mungu huyu, aliyelifanya jina lake likae pale, na aangamize wafalme wote, na watu wote, watakonyosha mikono yao kulibadili neno hili, na kuiharibu nyumba hii ya Mungu, iliyoko Yerusalemu. Mimi, Dario, nimetoa amri; na ifanyike kwa bidii nyingi. Nao wazee wa Wayahudi wakajenga, wakafanikiwa, kwa masaada wa kuhubiri kwao Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido.

Wakajenga, wakaimaliza kazi yao, kwa maagizo ya Mungu wa Israeli, na kwa amri ya Koreshi, na Dario, na Artashasta mfalme wa Uajemi. Nyumba hiyo ik**alizika siku ya tatu ya mwezi Adari, katika mwaka wa sita wa kutawala kwake mfalme Dario. Na wana wa Israeli, na makuhani, na walawi na watu wengine katika hao waliohamishwa, wakaiweka wakfru nyumba ya Mungu kwa furaha. Na katika kuiweka wakfu nyumba ya Mungu, wakatoa sadaka, ng’ombe mia, na kondoo waume mia mbili, na wanakondoo mia nne; tena wakatoa mbuzi waume kumi na wawili, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli wote, kwa hesabu ya kabila za Israeli. Wakawaweka makuhani katika kura zao, wakawaweka na Walawi vilivyoandikwa katika chuo cha Musa. Kisha, wana wa uhamisho wakaifanya Pasaka, mwezi wa kwanza, siku ya kumi nan ne ya mwezi. Kwa maana makuhani na Walawi walikuwa wamejitakasa wote pamoja; wote walikuwa hali ya tohara; wakachinja pasaka kwa ajili ya wana wote wa uhamisho, na kwa ajili ya ndugu zao makuhani, na kwa ajili ya nafsi zao.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

ZABURI YA KUITIKIZANA
Zab. 122:1-5 (K) 1

(K) Nalifurahi waliponiambia, na twende nyumbani kwa Bwana.

Nalifurahi waliponiambia,
Na twende nyumbani kwa Bwana. (K)

Miguu yetu imesimama
Ndani ya malango yako, ee Yerusalemu!
Ee Yerusalemu uliyejengwa
K**a mji ulioshik**ana. (K)

Huko ndiko walikopanda kabila,
Kabila za Bwana;
Ushuhuda wa Israeli,
Walishukuru jina la Bwana.
Maana huko viliwekwa viti vya hukumu,
Viti vya enzi vya mbari ya Daudi. (K)

SHANGILIO
1Pet. 1:25

Aleluya, aleluya,
Neno la Bwana hudumu hata milele, na neno hilo ni neno lile jema lililohubiriwa kwenu.
Aleluya.

INJILI
Lk. 8:19 – 21

Walimwendea Yesu mama yake na ndugu zake, wasiweze kumkaribia kwa sababu ya mkutano. Akaletewa habari akiambiwa, Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kuonana nawe. Akawajibu akasema, Mama yangu na ndugu zangu ndio hao walisikiao neno la Mungu na kulifanya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

22/09/2025

MASOMO YA MISA, SEPTEMBA 22, 2025
JUMATATU, JUMA LA 25 LA MWAKA

SOMO LA KWANZA
Ezr. 1:1-6

Ilikuwa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalame wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwambia roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia akisema, Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi: Bwana Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu, ulioko Yuda. Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Mungu wake na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu. Na mtu awaye yote aliyesalia mahali popote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu.

Ndipo wakaondoka wakuu wa mbari za mababa, wa Yuda na Benyamini, na makuhani, na Walawi, naam, watu wote ambao Mungu amewaamsha roho zao kukwea, ili kuijenga nyumba ya Bwana, iliyoko Yerusalemu. Na watu wote, waliokaa karibu nao pande zote wakawatia nguvu mikono yao, kwa vyombo vya fedha, kwa dhahabu, kwa mali, na kwa wanyama, na vitu vya thamani, zaidi ya vile vilivyotolewa kwa hiari ya mtu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

ZABURI YA KUITIKIZANA
Zab. 126 (K) 3

(K) Bwana alitutendea mambo makuu.

Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni,
Tulikuwa k**a waotao ndoto.
Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko,
Na ulimi wetu kelele za furaha.
Ndipo waliposema katika mataifa,
“Bwana amewatendea mambo makuu”. (K)

Bwana alitutendea mambo makuu,
Tulikuwa tukifurahi.
Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa,
K**a vijito vya Kusini. (K)

Wapandao kwa machozi
Watavuna kwa kelele za furaha.
Ingawa mtu anakwenda zake akilia,
Azichukuapo mbegu za kupanda,
Hakika atarudi kwa kelele za furaha,
Aichukuapo miganda yake. (K)

SHANGILIO LA INJILI
Yak. 1:18

Aleluya, aleluya,
Kwa kupenda kwake mwenyewe, Baba alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe k**a limbuko la viumbe vyake.
Aleluya.

INJILI
Lk. 8:16 – 18

Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Hakuna mtu ambaye akiisha washa taa huifunika kwa chombo, au kuiweka uvunguni, bali huiweka juu ya kiango, ili waingiao wapate kuona nuru yake. Kwa maana hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa ambalo halitajulikana na kutokea wazi. Jiangalieni basi jinsi msikiavyo; kwa kuwa mwenye kitu atapewa, na yule asiye na kitu atanyang’anywa hata kile ambacho anadhaniwa kuwa nacho.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo

22/09/2025

Tumsifu Yesu Kristo wakristo.

20/09/2025

September 21, 2025
Twenty-fifth SUNDAY in Ordinary Time

✝️ MASS READINGS

🙏 First Reading
AMOS 8:4-7

A reading from the Book of Prophet Amos

Hear this, you who trample upon the needy and destroy the poor of the land! "When will the new moon be over," you ask, "that we may sell our grain, and the sabbath, that we may display the wheat? We will diminish the ephah, add to the shekel, and fix our scales for cheating! We will buy the lowly for silver, and the poor for a pair of sandals; even the refuse of the wheat we will sell!" The LORD has sworn by the pride of Jacob: Never will I forget a thing they have done!

The Word of the Lord.

🙏Responsorial Psalm
PSALMS 113:1-2, 4-6, 7-8

:
PRAISE THE LORD WHO LIFTS UP THE POOR.
or:
R. ALLELUIA

Praise, you servants of the LORD,
praise the name of the LORD.
Blessed be the name of the LORD
both now and forever.

:
PRAISE THE LORD WHO LIFTS UP THE POOR.

High above all nations is the LORD;
above the heavens is his glory.
Who is like the LORD, our God, who is enthroned on high
and looks upon the heavens and the earth below?

:
PRAISE THE LORD WHO LIFTS UP THE POOR.

He raises up the lowly from the dust;
from the dunghill he lifts up the poor
to seat them with princes,
with the princes of his own people.

:
PRAISE THE LORD WHO LIFTS UP THE POOR.

🙏Second Reading
1 TIMOTHY 2:1-8

A reading from the first letter of Saint Paul to Timothy

Beloved:
First of all, I ask that supplications, prayers, petitions, and thanksgivings be offered for everyone, for kings and for all in authority, that we may lead a quiet and tranquil life in all devotion and dignity. This is good and pleasing to God our savior, who wills everyone to be saved and to come to knowledge of the truth. For there is one God. There is also one mediator between God and men, the man Christ Jesus,
who gave himself as ransom for all. This was the testimony at the proper time. For this I was appointed preacher and apostle— I am speaking the truth, I am not lying —, teacher of the Gentiles in faith and truth.

It is my wish, then, that in every place the men should pray,
lifting up holy hands, without anger or argument.

🙏Alleluia
2 CORINTHIAN 8:9

R. Alleluia, alleluia.
Though our Lord Jesus Christ was rich, he became poor,
so that by his poverty you might become rich.
R. Alleluia, alleluia.

✝️Gospel
LUKE 16:1-13

A reading from the Holy Gospel according to Saint Luke

Jesus said to his disciples, "A rich man had a steward who was reported to him for squandering his property. He summoned him and said, 'What is this I hear about you?
Prepare a full account of your stewardship, because you can no longer be my steward.' The steward said to himself, 'What shall I do, now that my master is taking the position of steward away from me? I am not strong enough to dig and I am ashamed to beg. I know what I shall do so that,
when I am removed from the stewardship, they may welcome me into their homes.' He called in his master's debtors one by one. To the first he said, 'How much do you owe my master?' He replied, 'One hundred measures of olive oil.' He said to him, 'Here is your promissory note.
Sit down and quickly write one for fifty.' Then to another the steward said, 'And you, how much do you owe?' He replied, 'One hundred kors of wheat.' The steward said to him, 'Here is your promissory note; write one for eighty.' And the master commended that dishonest steward for acting prudently. "For the children of this world are more prudent in dealing with their own generation than are the children of light. I tell you, make friends for yourselves with dishonest wealth, so that when it fails, you will be welcomed into eternal dwellings. The person who is trustworthy in very small matters is also trustworthy in great ones; and the person who is dishonest in very small matters is also dishonest in great ones. If, therefore, you are not trustworthy with dishonest wealth, who will trust you with true wealth? If you are not trustworthy with what belongs to another, who will give you what is yours? No servant can serve two masters. He will either hate one and love the other, or be devoted to one and despise the other. You cannot serve both God and mammon."

The Gospel of the Lord.

✝️Or
LUKE 16:10-13

A reading from the Holy Gospel according to Saint Luke

Jesus said to his disciples:
"The person who is trustworthy in very small matters is also trustworthy in great ones; and the person who is dishonest in very small matters is also dishonest in great ones. If, therefore, you are not trustworthy with dishonest wealth, who will trust you with true wealth? If you are not trustworthy with what belongs to another, who will give you what is yours? No servant can serve two masters. He will either hate one and love the other, or be devoted to one and despise the other. You cannot serve both God and mammon."

The Gospel of the Lord....

We say thanks alot to God for the World Champions in Tokyo Japan. Ni kwa neema ya Mungu pamoja na ukak**avu pia. Safari ...
20/09/2025

We say thanks alot to God for the World Champions in Tokyo Japan. Ni kwa neema ya Mungu pamoja na ukak**avu pia. Safari ya mbinguni ni sawa kabisa na hayo mashindano. Ukitaka kushindana jikakamue na uweke kila kitu mbele zake Mungu. Tusisahau kesho ni Jumapili. Tumalize siku kwa sala kisha tujiandae kuenda kesho kumpokea Kristo.

20/09/2025

Celebrating my 3rd year on Facebook. Thank you for your continuing support. I could never have made it without you. 🙏🤗🎉

20/09/2025

MASOMO YA MISA YA JUMAPILI

DOMINIKA YA ISHIRINI NA TANO KATIKA KIPINDI CHA KAWAIDA MWAKA C

SEPTEMBA 21 2025

RANGI YA LITURUJIA: KIJANI💚

MADA YA DOMINIKA:

JINSI YA KUWA MSIMAMIZI MWEREVU WA MALI ZA ULIMWENGU HUU.

_Je! Tunaweza kuwaita matajiri wa wakati wa Amosi ni werevu? Walikuwa matajiri kwa kudanganya maskini, hawakuheshimu "'siku takatifu" na walijishughulisha na tamaa zao za ubinafsi. Katika macho ya watu hakika walikuwa na werevu, lakini machoni pa Mungu walijiangamiza. Hii ndio tunafundishwa na somo la kwanza. Yesu anatuambia katika Injili kuwa sisi ni "werevu" ikiwa tunatumia mali za ulimwengu huu kusaidia wengine. Kwa njia hii tunapata kitu cha kipekee chenye thamani, urafiki na maskini. Kuelewa ukweli huu, ambao ni mgumu sana kukubali, tunahitaji sala. Paulo anatuambia hili katika somo la pili.

ANTIFONA YA KUINGIA*

_Mimi ndimi wokovu wa watu, asema Bwana. Katika shida yoyote wataniita, nami nitawasikiliza; nami nitakuwa Bwana wao hata milele._

KOLEKTA
Ee Mungu, uliyaweka maagizo yote ya sheria takatifu katika upendo kwako na kwa jirani: utujalie kuzishika amri zako, tupate kustahili kuufikia uzima wa milele. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao...

SOMO LA KWANZA
Amosi 8:4-7

Bwana alinena dhidi yao wanaonunua watu maskini kwa fedha.

Somo katika kitabu cha Nabii Amosi

Sikilizeni haya, enyi mnaomkanyaga mnyonge, na kuwaangamiza watu maskini wa nchi; ninyi mnaosema: Sikukuu ya mwezi mwandamo itakwisha wakati gani, tupate kuuza ngano? Nayo siku ya Sabato, tupate kufungua ghala ya ngano? Tutapunguza vipimo, tutapandisha bei, tutageuza mizani ziwe za uongo! tutauza hata makapi ya ngano, tupate kuwanunua watu maskini kwa fedha, na wanyonge kwa jozi ya viatu! Bwana ameapa kwa utukufu wa Yakobo: Hakika sitasahau kamwe matendo yao.

Neno la Bwana.

ZABURI YA KUITIKIZANA
Zaburi 1 13:1-2,4-6,7-8(K 1a na 7a)

K. Msifuni Bwana, humwinua mnyonge kutoka mavumbini.

au: Aleluya.

Enyi watumishi wa Bwana, sifuni,
lisifuni jina la Bwana.
Jina la Bwana litukuzwe / tangu sasa na hata milele.
K.

Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote;
utukufu wa Mungu ni juu ya mbingu.
Ni nani aliye k**a Bwana,
Mungu wetu, aketiye juu kabisa,
ainamaye atazame chini mbinguni na duniani?
K.

Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,
kutoka jalalani humpandisha maskini,
amketishe pamoja na wakuu,
pamoja na wakuu wa watu wake.
K.

SOMO LA PILI
1Timotheo 2:1-8

Maombezi yatolewe kwa ajili ya watu wote kwa Mungu, ambaye ataka watu wote waokolewe.

Somo katika barua ya kwanza ya Mtakatifu Paulo kwa Timotheo.

Mpendwa: Kwanza kabisa ninayowaomba hasa ndiyo, dua na sala, maombezi na shukrani zitolewe kwa ajili ya watu wote, kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tupate raha na utulivu kwa kuishi maisha ya uchaji wa Mungu na ya mwenendo mwema. Hayo ni mema, tena yampendeza Mungu, mwokozi wetu, ambaye anataka watu wote waokolewe, na watambue yaliyo kweli. Kwa maana kuna Mungu mmoja, na mpatanishi baina ya Mungu na
wanadamu ni mmoja, ndiye mwanadamu Kristo Yesu, huyo alijitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya watu wote. Ndio ushuhuda nyakati zake. Kwa hiyo nimewekwa mimi niwe mtangazaji na mtume, tena mwalimu wa mataifa katika imani na ukweli. Hayo maneno yangu ni kweli, si uongo. Kila mahali mnaposali napenda wanaune wainue mikono kwa utakatifu, si kwa hasira na ubishi.

Neno la Bwana.....

SHANGILIO LA INJILI
2 Wakorintho 8:9

Aleluya. Aleluya.
ljapokuwa Yesu Kristo alikuwa tajiri, alijifanya fukara kwa ajili yenu, ili ninyi mpate kutajirika kwa ufukara wake.

INJILI
Luka 16:1-13

_Hamwezi kumtumikia Mungu na fedha._

Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Luka..

Wakati ule: Yesu aliwaambia wafuasi wake, Tajiri mmoja alikuwa na karani naye alish*takiwa kwake kwamba anatapanya mali zake. Akamwita, akamwambia, Je, nasikia nini juu yako? Toa hesabu ya ukarani wako, kwa maana huwezi kuwa karani tena, Karani huyo akasema moyoni mwake, 'Nifanyeje? Maana, Bwana wangu ananiachisha kazi ya ukarani. Kulima, siwezi, na kuomba k**a maskini naona haya. Najua la kufanya, ili baada ya kutolewa katika ukarani, wanikaribishe nyumbani kwao. Akawaita wadeni wa bwana wake mmoja mmoja, akamwambia wa kwanza, 'Una deni gani kwa bwana wangu? Naye akajibu, Mapipa mia ya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako ya deni; kaa upesi, andika, hamsini. Kisha akamwambia mwingine, Nawe una deni gani? Akasema, Mifuko mia ya ngano.' Akamwambia, Twaa hati yako ya deni, andika, themanini. Bwana akamsifu karani mdanganyifu kwa sababu alifanya werevu. Maana wana wa dunia hii ni werevu katika mahusiano yao kuliko wana wa mwanga. Nami nawaambieni, jifanyieni rafiki kwa mali inayoharibika, ili mnapoishiwa nayo wawapokee katika makao ya milele. Aliye mwaminifu kwa mambo madogo ni mwaminifu pia kwa mambo makubwa; kadhalika asiye mwaminifu kwa mambo madogo, si mwaminifu kwa mambo makubwa. Basi, k**a hamwi waaminifu kwa mali isiyo haki, nani atawakabidhi mali ya kweli? Na k**a hamwi waaminifu kwa mali ya mwingine, nani atawapa yenu wenyewe? Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili, ama atamchukia wa kwanza na kumpenda wa pili au atamjali wa kwanza na kumdharau mwingine. Hamwezi
kumtumikia Mungu na fedha.

Injili ya Bwana.... Sifa kwako Ee Kristo

20/09/2025

MASOMO YA MISA, JUMAMOSI YA JUMA LA ISHIRINI NA NNE, KIPINDI CHA KAWAIDA, MWAKA I, KUMBUKUMBU YA WAT. ANDREA KIM TAEGON, PADRE, NA WENZAKE, MASHAHIDI, SEPTEMBA 20, 2025
RANGI YA KILITURJIA: NYEKUNDU ♥️

SOMO LA KWANZA
1 TIMOTHEO 6:13—16

Shika amri bila kuivunja hadi Bwana atakaporudi.

Somo katika barua ya kwanza ya Mtakatifu Paulo kwa Timotheo

Mwanangu: Ninakuamuru mbele ya Mungu aliye asili ya kila uhai na mbele ya Kristo Yesu, aliyetoa ushahidi mzuri mbele ya Ponsio Pilato, utimize agizo hili bila waa na bila lawama mpaka kutokea kwake Yesu Kristo. Wakati wake mwenye heri atalidokeza tokeo lake aliye peke yake mtawala, Mfalme wa wafalme, Bwana wa bwana, Yeye peke yake hawezi kufa. Amekaa katika mwanga usiosogeleka. Hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na enzi ya milele ni yake. Amina.

NENO LA BWANA... TUMSHUKURU MUNGU

ZABURI YA KUITIKIZANA
ZABURI 100:1—2, 3, 4, 5 (K. 2b)

K. Njoni mbele za Bwana mkiimba kwa furaha.

Mshangilieni Bwana, nchi yote.
Mtumikieni Bwana kwa furaha.
Njoni mbele zake kwa kuimba. K.

Jueni kwamba ndiye Mungu.
Ndiye aliyetuumba,
nasi tu watu wake.
Taifa lake na kondoo wa malisho yake. K.

Ingieni malangoni mwake kwa shukrani,
nyuani mwake kwa masifu,
mshukuruni, lisifuni jina lake. K.

Kwa maana Bwana ndiye mwema,
wema wake wadumu milele,
uaminifu wake unadumu kizazi hata kizazi. K.

SHANGILIO LA INJILI
TAZAMA LUKA 8:15

K. Aleluya. W. Aleluya.
K. Heri wale ambao baada ya kulisikia neno la Mungu, wanalishika kwa moyo mzuri na mwema, wanazaa matunda kwa uvumilivu.
W. Aleluya.

SOMO LA INJILI
LUKA 8:4—15

Ile mbegu iliyoanguka kwenye udongo mzuri, ni wale ambao wanalishika hilo neno na kuzaa matunda kwa uvumilivu.

† Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Luka

Wakati ule: Watu wengi sana walikusanyika wakimkimbilia kutoka mjini, hapo Yesu akasema kwa mfano, "Mpanzi alikwenda shambani kupanda mbegu. Katika kupanda, nyingine zilianguka kando ya njia, zikakanyagwa, na ndege wa angani wakazila. Nyingine zikaanguka penye mwamba, zikaota, na kunyauka kwa kukosa unyevu. Nyingine zikaanguka kati ya miiba, na miiba ikaota mara, ikazisonga. Tena nyingine zikaanguka katika udongo mzuri, zilipoota, zikazaa mara mia zaidi." Aliposema hayo, alipaza sauti akisema, "Mwenye masikio ya kusikilizia, na asikie." Kisha wafuasi wake wakamwuliza maana ya mfano huu. Akajibu, "Ninyi mmejaliwa kuyajua mafumbo ya ufalme wa Mungu; lakini wengine hupewa mifano, 'wapate kuona wasione, wapate kusikia wasielewe.' Basi, maana ya mfano huu ni hii. Mbegu ni neno la Mungu. Wale wa kando ya njia ndio walisikiao, kisha Shetani akaja, akaliondoa neno mioyoni mwao, wasije wakasadiki na kuokoka. Waliopo penye mwamba ndio watu wenye kulisikia neno, na kulipokea kwa furaha, lakini hawana mizizi; husadiki kwa muda tu, lakini wakati wa kujaribiwa wanashindwa. Zilizoanguka kati ya miiba, ndio watu waliolisikia neno, wakaenda na kusongwa na shughuli na mali na anasa za maisha, wasitoe mavuno. Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu, wenye kulisikia neno, na kulishika kwa moyo mzuri na mwema, wakatoa mavuno kwa uvumilivu."

INJILI YA BWANA... SIFA KWAKO EE KRISTO

17/09/2025

Address

Nandi Hills

Telephone

+254716792020

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Masomo ya Misa ya kila siku posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share