12/08/2026
HERI YA SIKU YA VIJANA DUNIANI 2026!
Leo tunapoadhimisha International Youth Day, ninatoa wito kwa jamii, viongozi na wadau wote kutambua jambo moja muhimu: kuwekeza kwa vijana si matumizi, ni uwekezaji wa kujenga maisha, familia, uchumi na mustakabali wa taifa.
Vijana wetu wana ndoto. Wana vipaji. Wana nguvu, ubunifu na mawazo yanayoweza kubadilisha jamii. Kile wanachohitaji ni nafasi, maarifa, ujuzi, mitaji, mentorship na watu wanaowaamini.
Kupitia Shangaishi Foundation, tumeendelea kuwekeza katika Vijana Tumekuwa tukifungua nafasi za mafunzo na uwezeshaji, kuunga mkono makundi ya vijana, kushirikiana na sekta ya boda boda katika mafunzo na uongozi, kukuza vipaji vya Mpira na muziki na kuwekeza katika elimu kwa sababu tunaamini elimu ndiyo msingi wa fursa za kesho.
Leo, tunasema wazi: hatutaki vijana wa kusubiri fursa, tunataka vijana wenye uwezo wa kutengeneza fursa. Hatutaki vipaji vibaki mitaani bila kuonekana; tunataka vipaji vipate jukwaa. Hatutaki ndoto zizimwe kwa kukosa nafasi; tunataka vijana wapate uwezo wa kuziishi ndoto zao.
Dunia ya leo inahitaji vijana wenye maarifa, ubunifu, uwezo wa kutumia teknolojia na ujasiri wa kutatua changamoto za jamii. Kaulimbiu ya International Youth Day 2026, โDifferent Contexts, Common Aspirations,โ inatukumbusha kuwa licha ya mazingira tofauti, vijana wengi wanashiriki matumaini ya kupata elimu bora, kazi zenye staha, fursa na sauti katika maamuzi yanayohusu maisha yao.
Kwa hiyo, uwekezaji mkubwa zaidi tunaoweza kufanya leo ni kumwamini kijana. Kumfundisha. Kumuelekeza. Kumpa nafasi. Kumwezesha. Na pale anapoanguka, kumsaidia kusimama tena.
Kwa vijana wote wa Taita Taveta na Kenya kwa ujumla: msikubali kuambiwa kwamba nyinyi ni viongozi wa kesho pekee. Mna nafasi ya kuongoza, kubuni na kubadilisha dunia kuanzia leo.
Shangaishi Foundation itaendelea kuamini katika nguvu ya vijana, kwa sababu tunaamini kwamba tukiwajenga vijana leo, tunajenga jamii imara na yenye matumaini kesho.
Ndio mwanzo tu mkoko unaalika maua na safari hii ya Transforming Communities Beyond Boarders itafikia Kila mtu hatua kwa hatua.Vijana wote Nawapenda sana Tuko pamoja โค๏ธ
Christopher Shangaishi Mwanjala
Founder, Shangaishi Foundation