25/12/2025
Mzee wa Kimila wa jamii ya Maasai Alaigwanan Godson Ole Nduya Kijiji Cha Terrat Simanjiro Manyara,amesema Moja ya sababu ya vijana kunywa pombe kupitiliza na kupelekea maadili kuporomoka ni kukata tamaa.
Ole Nduya ameyazungumza hayo wakati akifanya mahojiano na Orkonerei Fm Radio kwenye kipindi Cha Kurunzi maalumu linaloruka kila ijumaa Saa 2:30 Asubuhi mada ya wiki hii ikisema "Unywaji wa pombe kupitiliza unachangia vipi mmomonyoko wa maadili?"
Wewe Unadhani kipi kinafanya watu kunywa pombe kupita kiasi?