Orkonerei FM Radio

Orkonerei FM Radio ๐Ÿ“ป Orkonerei FM 94.3
Sauti ya Jamii โ€“ Redio ya kwanza ya kijamii ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ
Terrat โ€“ Simanjiro, Manyara

13/09/2025

Mgombea Urais kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Luhaga Joelson Mpina, leo Jumamosi Septemba 13, 2025 akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupitishwa rasmi na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi amesema kuwa anatarajia kuibuka mshindi kwa zaidi ya asilimia 70 katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Mpina amesema kuwa yeye na Chama chake wamejipanga, ambapo amesema kwamba licha ya kubakia na siku 45 za kufanya kampeni lakini zinawatosha kuzunguka kwenye majimbo yote ya kiuchaguzi.

11/09/2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa mvua za Vuli kwa kipindi cha Oktoba hadi Desemba 2025, ikiwataka wananchi na mamlaka mbalimbali kujiandaa kwa changamoto na fursa zitakazotokana na mvua hizo.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladslaus Changโ€™a, alisema mvua za Vuli mwaka huu zinatarajiwa kuanza kwa nyakati tofauti kulingana na maeneo ya nchi, huku baadhi ya mikoa ikitarajiwa kupata mvua za wastani na mingine chini ya wastani.

Maeneo yatakayopata mvua

Kaskazini na Kati: Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara itaanza kupata mvua wiki ya pili ya Novemba 2025, zikitarajiwa kuisha Januari 2026. Hapa mvua zitakuwa za wastani hadi chini ya wastani.

Magharibi na Kaskazini-Magharibi: Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Mara na kaskazini mwa Kigoma inatarajiwa kuanza kupata mvua wiki ya pili ya Oktoba 2025. Mikoa ya Simiyu na Shinyanga itaanza wiki ya nne ya Oktoba. Mvua zitadumu hadi Januari 2026.

Pwani na Visiwa: Mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, kaskazini mwa Morogoro pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba itapokea mvua kuanzia wiki ya pili ya Novemba hadi Januari 2026, ambazo pia zinatarajiwa kuwa za wastani hadi chini ya wastani.

Dkt. Changโ€™a amewataka wakulima kutumia taarifa hizo kupanga shughuli zao za kilimo kwa kuzingatia ushauri wa wataalamu na kupanda mazao yanayofaa kwa hali ya hewa inayotarajiwa. Aidha, alisisitiza matumizi ya mbegu bora ili kuongeza tija.

Kwa upande wa wafugaji, alishauri kuandaa malisho na maji mapema, huku mamlaka za maji, nishati na miundombinu zikihimizwa kuchukua hatua za tahadhari ili kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo.

โ€œNi muhimu wananchi, kufuatilia kwa karibu taarifa za hali ya hewa na kuchukua tahadhari stahiki. TMA itaendelea kutoa taarifa za mara kwa mara ili kuhakikisha usalama na ustawi wa jamii,โ€ alisema Dkt. Changโ€™a.

10/09/2025

Katibu mkuu wa chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara Ndg.Amos Shimba amesema chama hicho kitazindua kampeni zake kiwilaya Tarehe 15 mwezi September,2025 Orkesumet.

Katika uzinduzi huo wataanza kuwanadi Wagombea wa Udiwani wa Kata zote 18 na Ubunge Simanjiro Ndg James Millya.

10/09/2025

โ€œJaribu kufikiria mgombea anapeleka sukari ya kilo mbili mbili kwenye maboma usiku na fedha ndogo ndogo elfu kumi, lakini tukumbuke akishinda anakaa madarakani kwa miaka mitano โ€” sasa gharama hizi atazirudishaje?โ€ ๐Ÿ—ณ๏ธ

Afisa Uchunguzi wa TAKUKURU Simanjiro, Faustin Mushi, akizungumza kwa njia ya simu na Dorcas Charles kuhusu rushwa kwenye uchaguzi.

๐Ÿ‘‰ Sikiliza zaidi kupitia Kurunzi Maalum, kila Ijumaa saa 2:30 asubuhi.

10/09/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Amos Gabriel Makalla ameunda Tume Maalum kufuatilia sakata la machinjio ya Ngorbob, Kata ya Matevesi โ€“ Arumeru, kufuatia malalamiko ya wananchi licha ya mradi huo kukamilika kwa gharama ya zaidi ya Milioni 800.

Tume hiyo, ambayo haitahusisha watendaji wa Arumeru ili kuepuka mgongano wa maslahi, imepewa wiki mbili kuchunguza uhalali wa mradi, ushirikishwaji wa wananchi na iwapo sheria za mazingira zilizingatiwa

Wakati Msimu wa kiangazi (Kutokuepo kwa Mvua) ukiendelea kujongea kwenye maeneo mbalimbali, je, jitihada za serikali za ...
09/09/2025

Wakati Msimu wa kiangazi (Kutokuepo kwa Mvua) ukiendelea kujongea kwenye maeneo mbalimbali, je, jitihada za serikali za kusambaza maji zinaonekana kwenye eneo lako?

Tuambie Maji yanapatikana kwa urahisi kiasi Gani hapo Ulipo ?

Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Mwl. Fakih Lulandala, amekagua gwaride na kufunga rasmi mafunzo ya jeshi la akiba (Mgambo) ...
09/09/2025

Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Mwl. Fakih Lulandala, amekagua gwaride na kufunga rasmi mafunzo ya jeshi la akiba (Mgambo) yaliyofanyika katika kijiji cha Okutu, kata ya Naberera.

Jumla ya vijana 53 wamehitimu mafunzo hayo, wakiwemo wanawake 7 na wanaume 46. Akisoma risala kwa mgeni rasmi, MG Yusufu Noah alisema mafunzo hayo yamewawezesha vijana kujifunza mbinu za kivita, ukakamavu na utiifu, pamoja na namna ya kukabiliana na adui.

Aidha, ameiomba Serikali kuwapa kipaumbele vijana hao kujiunga na majeshi mbalimbali pindi nafasi zitakapopatikana.

Mkuu wa Wilaya Lulandala amewataka viongozi wa taasisi za umma na binafsi kuwapa nafasi wahitimu hao kwenye ajira za muda mfupi au mrefu, hususan kwenye kazi za ulinzi wa mali na usalama.

Kadhalika amewaasa wahitimu wa Mafunzo hayo โ€œNendeni mkawe mstari wa mbele katika kudumisha amani na usalama katika jamii na kupambana na changamoto zote za dharura zitakazojitokeza zenye viashiria vya kuvunja amani"Lulandala.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania walieleza, na sasa macho yetu yamethibitisha ๐ŸŒ˜โœจ. Kupatwa kwa mwezi kimeanza na kitasali...
07/09/2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania walieleza, na sasa macho yetu yamethibitisha ๐ŸŒ˜โœจ. Kupatwa kwa mwezi kimeanza na kitasalia hadi saa 6 usiku. September 7,2025 kuelekea September 8,2025.Umeuona huu uzuri wa anga leo?

Ndio huu hapa saa 2 usiku!

05/09/2025

Mgombea Urais kupitia Chama cha CUF, Gombo Samadito Gombo, akiwa kwenye kampeni mkoani Shinyanga, amesema kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, hana makosa bali ni mpigania haki na demokrasia nchini.

Akihutubia wananchi, Gombo alisema:
โ€œMkinichagua kuwa Rais, nitamtoa Lissu gerezani kwa sababu ni msema kweli na mtetea haki. Nitamteua aingie kwenye Kamati ya kusimamia mchakato wa Katiba Mpya.โ€

05/09/2025

Mgombea Urais kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, ameahidi kuwa endapo atachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu ujao, serikali yake itaanzisha rasmi Fao la Uzee kwa wazee wote nchini.

Akizungumza kwenye kampeni mikoa ya Kanda ya Kaskazini ikiwemo Tanga na Kilimanjaro, amesema fao hilo litakuwa sehemu ya sera mahsusi za kuwatambua, kuwathamini na kuwawezesha wazee kuishi maisha yenye heshima, usalama na ustawi hata baada ya kustaafu au kushindwa kujitafutia kipato.

Ameongeza kuwa serikali ya CHAUMMA itaweka utaratibu maalumu wa utoaji wa fao hilo, likiwemo kwa wazee wasiokuwa watumishi wa umma, ili kuwasaidia kifedha na kiuchumi.

Cc

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Ndg. Gracian Makota, ameongoza kikao kazi na SUMA JKT pamoja ...
04/09/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Ndg. Gracian Makota, ameongoza kikao kazi na SUMA JKT pamoja na wakuu wa idara na vitengo kujadili tathmini ya ujenzi wa jengo jipya la Halmashauri.

Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Mwenyekiti wa Halmashauri ambapo Makota alieleza kuwa tathmini hiyo inalenga kubaini mapungufu yaliyopo ili kuhakikisha jengo linakamilika kwa ubora unaotakiwa.

Aidha, Makota alitangaza kuundwa kwa kikosi kazi cha wataalamu watakaofuatilia changamoto zilizopo kwenye mradi huo na kuja na suluhisho la kudumu.

Mwisho, aliwashukuru wadau wote walioshiriki kikao hicho na kuwasihi SUMA JKT kuendelea kushirikiana na Halmashauri katika miradi mingine itakayojitokeza.

Cc

Orkonerei FM Radio imepokea Silver Award (Nishani ya Fedha) kwenye Global Youth & News Media Prize for Journalism 2025 โ€“...
04/09/2025

Orkonerei FM Radio imepokea Silver Award (Nishani ya Fedha) kwenye Global Youth & News Media Prize for Journalism 2025 โ€“ tukio kubwa la kimataifa linalotambua vyombo vya habari vinavyoshirikisha vijana kwenye habari za ki-jamii.

Katika mashindano haya yaliyoandaliwa na Global Youth & News Media kwa kushirikiana na washirika 15 duniani, mashirika 19 pekee kutoka nchi 16 yalitambuliwa โ€“ na Orkonerei FM Radio pekee kutoka Afrika Mashariki! ๐ŸŒ

Tuzo hii imetolewa kwa kutambua mchango wa vipindi vyetu vinavyowawezesha vijana (miaka 18โ€“28+) kushiriki moja kwa moja katika mijadala ya utawala bora, mazingira, ustahimilivu wa kiuchumi na haki za binadamu. Kupitia redio, na mitandao ya kijamii, vijana wamepata nafasi ya kusikika โ€“ na hata viongozi wa jamii wameanza kuwaita kwenye majukwaa rasmi baada ya kuwasikia hewani.

Tunawashukuru sana:
๐Ÿ™Œ Vijana wote waliokuwa sehemu ya safari hii
๐Ÿ™Œ Timu ya Orkonerei FM Radio
๐Ÿ™Œ Wasikilizaji na jamii yetu ya Terrat, Simanjiro na kwingineko

Huu ni ushindi wa pamoja. Asanteni kwa kutuamini na kutusikiliza kila siku ๐Ÿ’š


Address

P O Box 12785 Arusha
Arusha
27613-16

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Orkonerei FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category