Orkonerei FM Radio

Orkonerei FM Radio 📻 Orkonerei FM 94.3
Sauti ya Jamii – Redio ya kwanza ya kijamii 🇹🇿
Terrat – Simanjiro, Manyara

25/12/2025

Mzee wa Kimila wa jamii ya Maasai Alaigwanan Godson Ole Nduya Kijiji Cha Terrat Simanjiro Manyara,amesema Moja ya sababu ya vijana kunywa pombe kupitiliza na kupelekea maadili kuporomoka ni kukata tamaa.

Ole Nduya ameyazungumza hayo wakati akifanya mahojiano na Orkonerei Fm Radio kwenye kipindi Cha Kurunzi maalumu linaloruka kila ijumaa Saa 2:30 Asubuhi mada ya wiki hii ikisema "Unywaji wa pombe kupitiliza unachangia vipi mmomonyoko wa maadili?"

Wewe Unadhani kipi kinafanya watu kunywa pombe kupita kiasi?

19/12/2025

Jeshi la Polisi nchini kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani limezindua operesheni maalumu ya ukaguzi wa mabasi ya abiria ili kudhibiti ajali msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.

Mkuu wa Operesheni, ACP Joseph Mwakabonga, amewaonya madereva wanaokimbiza magari ili kusafirisha abiria wengi kwa muda mfupi.

Shirika la kutetea haki za abiria (SHIKUHA) limewataka abiria kulipa nauli halali kisheria na kuepuka tiketi za karatasi ambazo ni kinyume na utaratibu.

18/12/2025

Diwani wa Kata ya Komolo Wilaya ya Simanjiro, Ndugu Saning’o Kipoon Somi, ametembelea Kijiji cha Kitiangare kwa lengo la kusikiliza changamoto mbalimbali zinazokabili kijiji hicho.

​Katika ziara hiyo Diwani amepokea kero na mapendekezo ya maendeleo kutoka kwa viongozi na wakazi, akiahidi ushirikiano wa dhati na mamlaka husika.

​Amekagua eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa zahanati, hatua itakayomaliza adha ya huduma za afya kwa wananchi wa Kitiangare.

​

18/12/2025

Meya wa Jiji la Arusha, Maximilian Iranque, amezungumzia ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe, aliyoifanya siku ya Leo alhamisi tar.18, Disemba 2025 ikiwa na lengo la kukagua miradi inayotekelezwa Jijini Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumatatu Disemba 15, 2025 amefungua na kuongoza Kikao cha kusikiliza...
15/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumatatu Disemba 15, 2025 amefungua na kuongoza Kikao cha kusikiliza kero na changamoto za bodaboda na Bajaji Mkoa wa Arusha, Kikao kilichofanyika kwenye Viwanja vya Makumbusho ya Azimio la Arusha.

Katika salamu zake za utangulizi, Makalla aliyeambatana na Wakuu wote wa Wilaya za Mkoa wa Arusha, ameahidi na kuwahakikishia wananchi wa Mkoa wa Arusha kuwa utakuwa utamaduni wake mara zote katika Utumishi wake Mkoa wa Arusha kuwafikia na kuwasikiliza wananchi na Makundi mbalimbali ya Kijamii ili kuondoa kero zinazowakabili, akiagiza pia Wakuu wa Wilaya kufanya ziara za kuwatembelea, kuwasikiliza na kutatua kero za wananchi.

15/12/2025

Kikao Cha kupokea mapendekezo ya Kuepo kwa ofisi ndogo ya Mbunge wa Simanjiro Kilichofanyika katika ofisi ya Kata ya Terrat Leo Disemba 15,2025 ambapo katibu wa Mbunge huyo Kanda ya Magharibi (Simanjiro Proper) Ndg Papaye Ole Njidai ameomba kikao hicho kuridhia mambo haya.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Manyara Ndg Peter Toima amepongeza Uamuzi wa Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Ndg James Millya wa ...
15/12/2025

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Manyara Ndg Peter Toima amepongeza Uamuzi wa Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Ndg James Millya wa kufungua ofisi yake ya pili Kata ya Terrat -Simanjiro itakayohudumia ukanda wa Simanjiro Proper.

Akizungumza mbele ya kikao Cha kujadili maadhimio ya kulipokea wazo la ofisi ndogo ya Mbunge Terrat Leo Disemba 15,2025,Toima amesema ulikuwa ni Uamuzi mzuri na wa busara ambao umefanywa na mbunge na kumpongeza mteule wa nafasi ya katibu wa Mbunge ukanda huo Papaye Ole Njidai.

Toima amewashauri wakaazi wa Terrat wasimuachie mbunge pekee ajenge ofisi hiyo Bali washiriki Pamoja katika ujezi wa ofisi hiyo kwa kila mtu kutoa anachoweza kwani ofisi hiyo itatumika kuwahudumia wakaazi wa Terrat na Simanjiro kwa ujumla.

"Kila mmoja achangie msimuachie mbunge peke yake kwani ofisi hii itawahudumia ninyi...Ili kufanikiwa ni kuacha makundi ya kisiasa mshikamane kwa Ushirikiano" amesema Toima

Baadhi ya viongozi wa vijiji ndani ya Kata na wakaazi wameridhia Ombi hilo na kwamba zoezi la kuandika barua ya kuomba eneo iwasilishwe haraka kwani wanatamani kuwa na ofisi hiyo.

12/12/2025

Mbunge wa Simanjiro (CCM) na Naibu waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki James Millya amemteua Ndg. Papaye Ole Njidai kuwa katibu wa ofisi ya Mbunge ukanda wa Terrat (Simanjiro Proper).

Ole Millya amezinduas ofisi hiyo na kumteua siku ya leo Desemba 12,2025 akiwa Terrat Simanjiro Mkoa wa Manyara.

08/12/2025

Waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt.Mwigulu Nchemba amesema siku ya kumbukizi ya uhuru wa Tanzania tarehe 9 Des.2025 iwe siku ya mapunziko na watu wote kupumzika nyumbani.

Waziri mkuu amesema hayo akitoa salamu za Rais wa Tanzania kuelekea siku hiyo.

08/12/2025

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro wametakiwa kubuni vyanzo vipya vya mapato visivyoumiza wananchi, huku wakisisitizwa kusimamia ukusanyaji na matumizi sahihi ya fedha hizo kuleta tija kwenye maendeleo ya wananchi.

Wito huu umetolewa na Jackson Kisaka mwanasheria wa mkoa wa Manyara, wakati akizindua Baraza Jipya la Madiwani alhamis Tarehe 04 Disemba 2025, Orkesumet.

Cc

Diwani wa Kata ya Msitu wa Tembo, Kaleya Melita Mollel, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanji...
05/12/2025

Diwani wa Kata ya Msitu wa Tembo, Kaleya Melita Mollel, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro kwa kura 24 za ndiyo kutoka kwa Madiwani waliohudhuria kikao kilichofanyika Orkesumet.

​Uchaguzi huo pia umemhakikishia Mwanjaa Jacob (Diwani Viti Maalum, Tarafa ya Terrat) nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri, ambaye naye alipata kura zote 24. Uchaguzi ulihusisha madiwani wote 24 wanaotokana na CCM wa kata 18 na viti maalumu 6.

Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Wilaya, Edosi Evaristi Ndikwiki, amewataka viongozi hao wapya kutoa ushirikiano kwa wataalam na kuwa 'watatuzi wa migogoro' badala ya kuiibua.

Mwenyekiti Mollel amesema: "Naombeni ushirikiano... twendeni tukawatumikie wananchi waliotuchagua na kutatua kero zao kwa lengo la kufanikisha maendeleo."

​Kamati ya Maendeleo ya Jamii: Taiko Laizer (Diwani wa Naisinyai)
​Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira: Albert Msole (Diwani wa Ngorika)
​Wajumbe wa Kamati ya Fedha: Mwanjaa Jacob, Albert Msole, Taiko Laizer, Jackson Ole Materi, na Rehema Laizer.

​

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Arusha leo limekamilika kwa uzinduzi na uchaguzi mkuu wa Meya ulioshuhudia Bw....
04/12/2025

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Arusha leo limekamilika kwa uzinduzi na uchaguzi mkuu wa Meya ulioshuhudia Bw. Maxmilian Matle Iranqhe (Meya) na Bw. Julius W. Sekeyan (Naibu Meya) wakiibuka washindi.

​Maxmilian Matle Iranqhe ameapishwa na kuchaguliwa kuwa Meya wa Jiji la Arusha kwa kishindo cha kura 33 kati ya kura 34 zilizopigwa, huku kura moja ikimkataa.

​Baraza la madiwani lililokamilika kwa kuapishwa, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Boniface R. Semroki, lina jumla ya Madiwani 34, wakiwemo Madiwani 25 waliochaguliwa na Madiwani 9 wa Viti Maalum.

​Katika nafasi ya Naibu Meya, Bw. Julius W. Sekeyan (CCM) alichaguliwa kwa kupata kura 31, akimshinda Stanley Nathan wa NLD ambaye aliambulia kura 3, dhidi ya wapiga kura wote 34.

Nyangusi Ole Sang'ida

​

Address

P O Box 12785 Arusha
Arusha
27613-16

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Orkonerei FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category