Orkonerei FM Radio

Orkonerei FM Radio đź“» Orkonerei FM 94.3
Sauti ya Jamii – Redio ya kwanza ya kijamii 🇹🇿
Terrat – Simanjiro, Manyara

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Ndugu Gracian Makota, amejitokeza mapema leo kushiriki zoezi ...
29/10/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Ndugu Gracian Makota, amejitokeza mapema leo kushiriki zoezi la kupiga kura katika kituo cha Bomani, kilichopo kwenye Mji Mdogo wa Orkesumet.

Zoezi la upigaji kura kwa ajili ya kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani linaendelea kote nchini leo tarehe 29 Oktoba 2025.



Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Fakii Lulandala ameshiriki zoezi la upigaji kura katika kituo kilichopo Bomani Mji mdogo wa ...
29/10/2025

Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Fakii Lulandala ameshiriki zoezi la upigaji kura katika kituo kilichopo Bomani Mji mdogo wa Orkesumet Simanjiro Leo Oktoba 29,2025.

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga amewaongoza wananchi wa Mkoa wa Manyara katika zoezi la upigaji kura Leo Oktoba 29...
29/10/2025

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga amewaongoza wananchi wa Mkoa wa Manyara katika zoezi la upigaji kura Leo Oktoba 29,2025.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Gabriel Makalla ameongoza wananchi wa Arusha kupiga kura mapema leo Oktoba 29, 2025.Ames...
29/10/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Gabriel Makalla ameongoza wananchi wa Arusha kupiga kura mapema leo Oktoba 29, 2025.

Amesema hali ya usalama katika mkoa huo ni shwari na salama, na amewataka wananchi wote wenye sifa kujitokeza kwa wingi kutimiza wajibu wao wa kikatiba.

Makalla amepongeza maandalizi mazuri ya uchaguzi, akieleza kuwa vituo vya kupigia kura vipo vingi na vinatoa huduma bila foleni kubwa.

“Mimi mwenyewe nimeshapiga kura. Vituo viko wazi, hakuna msongamano — kila mmoja atumie haki yake ya kikatiba,” amesema CPA Makalla.

27/10/2025

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude akizungumza na wanahabari ofisini kwake amesema wilaya hiyo ipo tayari kwa zoezi la upigaji kura Oktoba 29 2025.

Aliyekuwa mgombea Udiwani wa Kata ya Terrat wilayani Simanjiro kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Ndg. Thomas Kiloji, amer...
24/10/2025

Aliyekuwa mgombea Udiwani wa Kata ya Terrat wilayani Simanjiro kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Ndg. Thomas Kiloji, amerejea rasmi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM).

​Ndugu Kiloji amepokelewa na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Manyara, Ndg. Peter Toima, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Komolo, Simanjiro.

23/10/2025

Akizungumza katika sherehe za uzinduzi wa kuwaingiza jando Rika la Irmegoliki katika Kata ya Lemooti Monduli alaigwanan Isack Ole Lekisongo amesema yeye ni mwanachama wa CCM na atapiga kura Tarehe 29 Oktoba 2025.

Part 5

23/10/2025

Akizungumza katika sherehe za uzinduzi wa kuwaingiza jando Rika la Irmegoliki katika Kata ya Lemooti Monduli alaigwanan Isack Ole Lekisongo amesema yeye ni mwanachama wa CCM na atapiga kura Tarehe 29 Oktoba 2025.

21/10/2025

Viongozi wakuu wa Jamii ya Kimasai (Malaigwanan) wametoa tamko rasmi wakitaka Watanzania wote kudumisha amani na kukataa wito wa maandamano siku ya Uchaguzi Mkuu, Oktoba 29, 2025.

Kupitia tamko lao lililosomwa na Katibu wao, Bw. Jeremia Laizer, kutoka Wilayani Siha, Mkoani Kilimanjaro.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Namelok Sokoine, alihudhuria mkutano huo na kuwapongeza kwa msimamo wao.

21/10/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Gabriel Makalla Jumatatu Oktoba 20, 2025, amezindua sherehe za msimu wa tohara kwa jamii ya Kimasai nchini Tanzania.

Sherehe hizo maarufu k**a Enkipaata zimezinduliwa kwenye Kijiji cha Oldonyosapu Wilaya ya Arumeru zikitarajiwa kuhusisha zaidi ya Vijana 2,000 wa kundi rika la Irmegoliki litakalodumu mpaka Oktoba 2032.

Ankara za Maji unazoletewa zinaendana na matumizi yako?
20/10/2025

Ankara za Maji unazoletewa zinaendana na matumizi yako?

Kurunzi Maalum Orkonerei FM Radio kupitia kipindi cha Kurunzi Maalumu inamulika sekta ya maji, ikizungumzia changamoto za bili (ankara) za maji katika Kata ya Terati, Wananchi wengi wanalalamika kupokea bili zinazokuja na gharama kubwa, na wakati mwingine wanaona ni kubwa…

19/10/2025

Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Jumatano, Oktoba 29, 2025, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Arusha Mjini, Shaban Ferdinand Manyamba, ametoa ufafanuzi kwa wapiga kura.

Ikiwa ​umepoteza kadi yako ya mpiga kura? Usijali! Bado unaweza kutimiza haki yako ya kidemokrasia.

​Manyamba amesema wananchi waliosajiliwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lakini wamepoteza kadi zao wataruhusiwa kupiga kura kwa kutumia kitambulisho mbadala.

​Vitambulisho vinavyokubalika ni:
​🆔 Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
​🛂 Pasi ya Kusafiria
​🚗 Leseni ya Udereva

​Sharti Kuu: Jina lililopo kwenye kitambulisho chako mbadala ni lazima lifanane na lile lililosajiliwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

​Msimamizi huyo amewahimiza wananchi wote wa Arusha Mjini wenye sifa kujitokeza kwa wingi kutimiza wajibu wao wa kikatiba kwa amani na utulivu.

​

Address

P O Box 12785 Arusha
Arusha
27613-16

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Orkonerei FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category