29/10/2025
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Ndugu Gracian Makota, amejitokeza mapema leo kushiriki zoezi la kupiga kura katika kituo cha Bomani, kilichopo kwenye Mji Mdogo wa Orkesumet.
Zoezi la upigaji kura kwa ajili ya kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani linaendelea kote nchini leo tarehe 29 Oktoba 2025.