03/06/2026
Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, ametangaza mabadiliko ya vituo vya kazi na uteuzi mpya wa watendaji katika sekta ya maji nchini. Lengo kuu la uamuzi huu ni kuimarisha utendaji, kuongeza ufanisi, na kuhakikisha huduma za maji zinaboreka na kuwafikia wananchi kwa wepesi zaidi.
βMabadiliko haya yanagusa maeneo mbalimbali muhimu ya kiutendaji, ikiwemo:
π§ Wakurugenzi Wasaidizi ngazi ya Wizara.
π§ Uhamisho na uteuzi wa Wakuu wa Maabara za Maji.
π§ Mameneja wa Mikoa wa RUWASA.
π§ Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira.