14/06/2020
JUMATANO USIKU:1
Luciana
Naitwa Lucy nimezaliwa katika familia ya bwana na bibi lameck ni mtoto wa mwisho kati ya watoto watatu wa kwanza alikua ni kaka yangu alieitwa peter na wapili Dada yangu alieitwa zawadi familia ilikua na upendo wa hali ya juu sana kila kitu kilikua nyumbani baba na mama walitupenda sana ila sana walinipenda mimi kaka yangu na Dada yangu walikua wakinita mtoto wa mama na baba nilikua nasoma chuo mwaka wa kwanza ila kaka yeye alikua anafanya kazi ila bado alikua ajaoa na Dada yeye alikua mwaka wa mwisho mana akisomea sheria alikua anasoma kwa mda wa miaka mitano mimi niliamua kusomea uandishi wa habari kwa kua nilikua napenda sana kuongea na kupeleleza badhi ya vitu"""
Nakumbuka siku moja baba alituita na kuanza kuongea na sisi "" watoto wangu wote mmekua na nimewalelea maisha ya upendo ata nikifa leo au kesho nitawaacha mkiwa na amani na upendo"" baba aliongea kwa msisitizo na hisia kali sana kaka alimwambia asijali kwani yeye yupo kwa ajili yetu Dada nae hakusita kuonesha hisia zake kwa baba""
Nakumbuka ilikua majira ya usiku nikiwa nimekaa chumbani kwangu alikuja baba na kuitaji kuzungumza na mimi sikua na pingamizi nilikuabali ""Lucy mwanangu wewe ndo mtoto wangu ninae kupenda naomba jitahidi sana kua na ujasiri na upendo pia usikate tamaa kwakila jambo"" baba alinambia hivyo nilishindwa kumwelewa anamanisha nini ila alinambia haya ni maisha ipo siku ataelewa namanisha nini sikutaka kuuliza zaidi aliondoka zake nakuniacha nikiwaza ""
Dada alimaliza mafunzo yake na mimi nikafanikiwa kuingia mwaka wa pili nilikua na mpenzi wangu nilimpenda sana nae alikua akinipenda Lucas ndo mwanaume niliekua nae alikua nae anasomea uandishi wa habari mwaka wa mwisho nikitokea kumpenda ghafla kutokana na ucheshi wake na kupenda sana kudadisi k**a mimi""
Siku moja nikiwa natoka chuoni nikiwa na Lucas tulikutana na Dada yeye alikua ametoka kufatilia kazi nilipomuona nilimsalimia na kufurahi kuniona ila alimwangalia sana Lucas....