20/02/2026
Hivi Leo Kuna habari zinazosambaa kila kona, kuhusu kadinari Pengo kufariki.
Lakini je huyu ni nani? Na kwanini ni maarufu sana Tanzania?
Polycarp Pengo alikuwa mmoja wa viongozi wakuu wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla. Alizaliwa tarehe 5 Agosti 1944 huko Mwazye, mkoani Rukwa, Tanzania. Alijiunga rasmi na utumishi wa Kanisa Katoliki na kupata Daraja Takatifu ya Upadre tarehe 20 Juni 1971 chini ya Hayati Askofu Charles Msakila.
Baada ya masomo yake ya teolojia, akajifunza pia Uthabiti wa Maadili mjini Roma, Italia ambapo alipata digrii ya uzamili (PhD) mwaka 1977. Alifundisha teolojia katika semina mbalimbali na hata kuwa Mkurugenzi wa Segerea Theological Seminary kabla ya uteuzi wake kuwa uaskofu.
1983 – Aliteuliwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Nachingwea.
1985 – Alihamishiwa kuwa Askofu wa Jimbo la Tunduru-Masasi.
1990 – Aliteuliwa kuwa Coadjutor Archbishop wa Jimbo kuu la Dar es Salaam.
1992–2019 – Alihudumu k**a Askofu Mkuu wa Jimbo kuu Katoliki la Dar es Salaam, akiwa kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki mkoani humo na nchi kwa ujumla.
Katika utumishi wake, bila kujali dini au chama, alijitahidi kujenga umoja wa kitaifa, amani, ustawi wa jamii na kutoa mchango mkubwa katika malezi ya mapadre, watawa na waumini wengi. Alikuwa kiongozi anayeheshimiwa kwa unyenyekevu, uongozi thabiti na mshik**ano wa kitaifa.
Afama Tv