Habari Maalum Fm

Habari Maalum Fm Christian radio/Habari Maalum Media

Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia SuluhuHassan ameendelea na kampeni zake za uchaguzi mkuu wa mwaka 2025...
10/09/2025

Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu
Hassan ameendelea na kampeni zake za uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa kuzungumza na wananchi wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, akiahidi kuendeleza miradi mikubwa ya kijamii na kiuchumi.
Amesema Serikali itakamilisha ujenzi wa vituo vitatu vya afya eneo la Mtoa, Mwandegembe na Irungu ili kuboresha huduma za afya.
Katika elimu, ameeleza kuwa shule mpya ya Amali na Shule ya Sekondari ya Mbelekese zimekamilika, hatua itakayoongeza nafasi za masomo kwa wanafunzi.
Samia amesema tenki kubwa la maji Kizonzo lenye ujazo wa lita 300,000
limekamilika na Serikali itaendeleza mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuhakikisha wananchi wanapata maji safi.
Pia, kupitia sekta ya madini, Serikali imeanzisha soko la dhahabu litakalowawezesha wachimbaji wadogo kupata masoko ya uhakika na kuongeza kipato chao.

09/09/2025

JUMLA ya Watahiniwa 1,172,279 wanatarajiwa kuanza Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi unaotarajiwa kuanzia kesho, Septemba 10 mpaka Septemba 11. Akizungumza na Waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa NECTA, Profesa Said Ally Mohamed, amesema kati ya watahiniwa hao, Wavulana ni 535,138 sawa na asilimia 45.65 na Wasichana ni 637,141 sawa na asilimia 54.35. Aidha amesema kuwa Mtihani huo utafanyika katika jumla ya shule 10,941 zilizoko Tanzania ambapo ameongeza kuwa maandalizi yote muhimu tayari yamekamilika, ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mitihani na nyaraka nyingine muhimu katika mikoa yote

09/09/2025

Aliyewahi kuwa mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu amesema katika Mkoa wa Singida wamepanga kutafuta kura za mgombea urais, Samia Suluhu Hassan kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kijiji kwa kijiji. Amesema hayo leo Septemba 9,2025 mkoani Singida kwenye kampeni za chama hicho na kuongeza kuwa, watasimama kwa pamoja k**a watoto wa baba mmoja. “Mimi na wenzangu wote tumepanga tutafute kura zako za urais kijiji kwa kijiji, tawi kwa tawi, nyumba kwa nyumba, wilaya kwa wilaya… tutasimama pamoja k**a watoto wa baba mmoja.” Aidha, amesema wanatakiwa kuonesha chama hicho ni chama kilichokomaa na kuwa na amani, pia ni chama kiongozi kwa kubeba maono ya Watanzania.

29/08/2025

Safu yetu ya Ushambuliaji kwa sasa inaweza kufunga hadi magoli
100 kwenye Ligi kuu"_Afisa Habari wa Simba Ahmed Ally akizungumzia ubora
kikosi kipya cha Simba Sc.

Habari picha ya matukio ya ibada ya usiku wa amani  iliyohusisha maombezi kusifu na kuabudu.. Ibada hii iliandaliwa na h...
23/08/2025

Habari picha ya matukio ya ibada ya usiku wa amani iliyohusisha maombezi kusifu na kuabudu.. Ibada hii iliandaliwa na habari maalum media na kwa hakika tuliona mkono wa Mungu ukitenda.. tunapenda kutoa shukrani kwa wasikilizaji wote waliojitokeza kwenye mkesha huu. Mungu awabariki sana

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)imewakumbusha waombaji wa mikopo na ufadhili wa Samia Scholarship kuw...
22/08/2025

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)
imewakumbusha waombaji wa mikopo na ufadhili wa Samia Scholarship kuwa
dirisha la maombi kwa mwaka wa masomo 2025/2026 litafungwa rasmi Agosti 31,
2025 bila kuongezwa muda.
HESLB imetoa kauli hiyo jana Alhamisi Agosti 21, 2025 kupitia taarifa yake kwa
vyombo vya habari, ikiwataka wanafunzi wenye sifa kuhakikisha wanakamilisha
maombi yao mapema kabla ya muda kisha.
Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Dk Bill Kiwia, akizungumza na waandishi wa habari
Agosti 11, 2025, alisisitiza kuwa dirisha la maombi lililofunguliwa Juni 15, 2025
halitaongezewa muda na litafungwa k**a lilivyopangwa.
"Zimebaki siku 10 pekee, hivyo ni vyema wanafunzi wenye sifa kuhakikisha
wanafanya maombi yao mapema ili kuepuka msongamano wa dakika za mwisho,"
imeeleza taarifa hiyo.

Kwa msaada zaidi, wanafunzi wanashauriwa kutembelea tovuti rasmi ya HESLB.

21/08/2025

Kuelekea Mchezo vwa kesho wa hatua ya Robo fainali ya CHAN, Afisa Habari wa Simba Ahmed Ally kwa kushirikiana na Afisa habari wa Yanga Ali Kamwe,
wameungana kuhamasisha watanzania kujitokeza kvwenye mchezo wa kesho.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limewak**ata madereva watano wamagari yanayosafirishwa nje ya nchi (IT) kwa makosa ya k...
21/08/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limewak**ata madereva watano wa
magari yanayosafirishwa nje ya nchi (IT) kwa makosa ya kusafirisha abiria kinyume na utaratibu katika katika operesheni maalum inayoendelea mkoani humo ambayo
imelenga kudhibiti usalama wa watumiaji wote wa barabara.
Kwa mujibu wa taarifa ya leo Agosti 31, 2025 iliyotolevwa na Kamanda wa Polisi
Mkoani humo, SACP Alex Mk**a, uk**ataji huo umefanikiwa Agosti 20, 2025 majira
ya usiku katika eneo la Mikumi Wilaya ya Kipolisi Ruhembe ambapo waliok**atwa ni
gari namba IT. 7543, Toyota Probox iliyokuwa inaendeshwa na Richard George
Kunambi (40) mkazi wa Dar es salaam.
Wengine ni Gari namba IT.3040 Mercedes Benz ikiendeshwa na Shabani Richard
Mwambuli (37) mkazi wa Mbeya; Gari namba |T. 1682, Toyota Prado ikiendeshwa na
Mustapha Said Kikombe (39) mkazi wa Dar es salaam; gari namba IT.1100 aina ya
Nissan extrail ikierndeshwa na Omary Mohammed Mwinjega (40) mkazi Dar es salaam; na gari namba IT. 5527 aina ya Toyota Sienta likiendeshwa na Ambwene Benson Kipenya (44) mkazi wa Dar es salaam.
Madereva hao watafikishwa kwenye vyombo vingine vya hakijinai ili kukamilisha
mchakato wa upatikanaji wa haki huku Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro
likiwaelekeza Madereva wanaosafirisha magari kwenda nchi za nje kuacha kubeba
abiria kwenye magari hayo ambayo kimsingi hayana usajili wa shughuli hizo na
kusisitiza kuwa watakaokaidi watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ameikabidhi timu ya taifa yasoka ya Tanzania (Taifa Stars) kiasi cha Milioni 200 z...
21/08/2025

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ameikabidhi timu ya taifa ya
soka ya Tanzania (Taifa Stars) kiasi cha Milioni 200 za Kitanzania, wakati timu hiyo
ikijiandaa kumenyana na Morocco katika mchezo wa robo fainali, utakaofanyika
Agosti 22, 2025.
Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi amesema kiasi hicho cha fedha ni k**a zawadi na hamasa kwa wachezaji hao wanapojiandaa na mchezo muhimu dhidi ya Morocco.

tarehe 21, tunakukaribisha kuungana nasi kuanzia saa 11 alfajiri hadi saa 3 asubuhi kwenye kipindi chetu kipendwa kinach...
20/08/2025

tarehe 21, tunakukaribisha kuungana nasi kuanzia saa 11 alfajiri hadi saa 3 asubuhi kwenye kipindi chetu kipendwa kinachokuletea maarifa, furaha na suluhisho la changamoto zinazokukabili kila siku.

Mada yetu ni: “Suluhisho la Tatizo la Ngozi Yako” 🌿✨
Tutazungumzia kwa kina namna ya kutunza ngozi kwa njia salama, za asili, na zenye matokeo ya kweli.

Mgeni wetu maalum ni Bi. Loveness Mgonja, ambaye ni Mkurugenzi wa MAMG ORGANIC PRODUCT – taasisi inayoongoza katika kutengeneza bidhaa bora za asili kwa afya na ngozi.

Usikose nafasi hii ya kipekee ya kujifunza, kuuliza maswali, na kupata suluhisho la changamoto za ngozi yako moja kwa moja kutoka kwa mtaalam.

Baki nasi hapa hapa Morning Shine – ambapo kila siku inaanza na nuru mpya! 🌅🎶

Klabu ya Simba Sc imetangaza kuwa itazindua jezi mpya za Msimu zaklabu hiyo Tarehe 27, 2025 katika Ukumbi wa Super Dome ...
20/08/2025

Klabu ya Simba Sc imetangaza kuwa itazindua jezi mpya za Msimu za
klabu hiyo Tarehe 27, 2025 katika Ukumbi wa Super Dome Masaki Jijini Dar es Salaam
ambapo kiingilio cha kushiriki hafla hiyo kwa mtu yeyote atakayehitaji ni Tsh. Laki
mbili na nusu kwa mtu mmoja Na yeyote atakayeshiriki kwenye uzinduzi huo atapata
jezi zote tatu za msimu pamoja na vitu vingine vitakavyopatikana siku hiyo ndani ya
ukumbi huo.
"Jezi za Simba msimu huu tutazindua kwa namna tofauti kidogo, ipo namna ambayo
tumezoea jezi huwa zinazinduliwa lakini safari hii sababu tuna mdhamini mpya wa jezi kampuni ya JayRutty akishirikiana na kampuni ya kimataifa ya Diadora tukaamua
kufanya kitu kipya chenye mvuto kwa jamii na biashara ya jezi kuwa na mvuto wa
tofauti."
"Jezi za Simba SC msimu wa 2025/26 zitazinduliwa tarehe 27|Agosti/2025, jezi
zitazinduliwa majira ya saa 1:00 usiku na shughuli itafanyika kwenye ukumbi wa Super Dome uliopo Masaki. Safari hii tumefanya kuwa tukio lenye kubwa, tukio lenye hadhi ya ushua na kulifanya kuwa tukio bora ambalo litakutanisha wadau wakubwa wa Simba Sports Club na ambao wanataka kununua jezi ya Simba baada ya
kuzinduliwa."-Ahmed Ally akizungumza na waandishi wa habari siku ya leo.

lkulu ya Marekani imezindua akaunti rasmi kwenye TikTokinayomilikiwa na Wachina ikiwa bado mwezi mmoja kuanza utekelezaj...
20/08/2025

lkulu ya Marekani imezindua akaunti rasmi kwenye TikTok
inayomilikiwa na Wachina ikiwa bado mwezi mmoja kuanza utekelezaji wa ahizo la
Rais Trump kupiga marufuku jukwaa hilo la mitandao ya kijamii kutumika nchini
Marekani.
Sheria ya Ulinzi wa Data ya Mwaka 2024 ilitaka TikTok kusitisha shughuli zake ifikapo
Januari 19 mwaka huu isipokuwa k**a ByteDance, ambayo ni kampuni mama ya
programu hiyo iwapo ingepata leseni ya uendeshaji shughuli zake Marekani.
Trump, ambaye alikuwa mtumiaji mkubwa wa TikTok wakati wa kampeni zake za
urais, aliongeza muda wa mwisho hadi mapema Aprili, kisha Juni 19 na kuwapa muda
hadi Septemba 17.
Akaunti hiyo ya WhiteHouse tayari imepata zaidi ya wafuasi 80,000 tangu
izinduliwe jana Jumanne Agosti 19, 2025 kupitia video fupi iliyomwonyesha Rais na
maandishi yaliyosomeka: "America we are Back! VWhat's up TikTok?"
Awali, Rais Trump alitahadharisha kuwa kutumia TikTok nchini humo kuwa ni hatari
kwao. Kauli hiyo alitoa aliposaini agizo la kiutendaji mwaka 2020 lililoweka vikwazo
vingi dhidi ya programu hiyo wakati wa muhula wake wa kwanza wa urais.

Address

P. O Box 7292
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari Maalum Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Habari Maalum Fm:

Share