Habari Maalum Fm

Habari Maalum Fm Christian radio/Habari Maalum Media

02/06/2025

Mwenyekiti Lissu akitoa shule ya mbele ya
Askari polisi, Askari Magereza, Mahakimu, makarani wa mahak**a na Mawakili wa Jamhuri, akiwa kizimbani Kisutu
leo.!

02/06/2025

Baadhi ya wanachama na viongozi wa chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) wamezuiliwa kuingia eneo la ndani ya
Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu inaposikilizwa kesi ya mwenyekiti wa chama hicho Tundu Antiphas Lissu.
Baadhi yao wamepiqwa marungu wakidaiwa kukaidi amri ya polisi ya
kuondoka eneo la nje ya mahak**a hiyo kwakuwa wamechelewa hivyo haiwezekani tena kuingia ndani.

30/05/2025

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeahidi kuhuisha na
kukamilisha mchakato wa Katiba mpya kabla ya mwaka 2030, ikiwa ni
sehemu ya utekelezaji wa llani yake ya uchaguzi ya mwaka 2025-2030.
Akizungumza jijini Dodoma leo ljumaa Mei 30, 2025 katika Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM, Mwenyekiti wa Kamati ya llani ya CCM, Profesa Kitila Mkumbo amesema hatua hiyo inalenga kudumisha demokrasia, utawala bora na mshik**ano wa kitaifa.
Amesema CCM inaamini kuwa misingi ya utawala wa sheria, haki za
binadamu na demokrasia ni msingi muhimu kwa maendeleo endelevu ya Taifa, na kwamba chama hicho kitaielekeza serikali kuweka mfumo wa kisheria wa kutekeleza falsafa ya uongozi ya 4R.

30/05/2025
28/05/2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametoa
wito kwa viongozi wa chama hicho kuwa wanyenyekevu na karibu na
wananchi, akisisitiza kuwa mamlaka waliyonayo ni dhamana ya muda.
Akizungumza leo Jumatano, Mei 28, 2025, jijini Dodoma, katika hafla ya
uwekaji jiwe la msingi la jengo jipya la makao makuu ya CCM, Samia
amesema viongozi hawapaswi kujiona juu ya wananchi kwa kuwa wao
ndio wamiliki halali wa chama.
"Ni muhimu wakati wote viongozi kuwa karibu na wanyenyekevu mbele ya wananchi, maana wao ndiyo wamiliki wa chama hiki. Sisi viongozi
tumekabidhiwa dhamana na dhamana hizi tunapita," amesema Rais
Samia. Ameeleza kuwa historia ya CCM inaonyesha mabadiliko ya uongozi kwa nyakati tofauti, na hivyo hakuna kiongozi anayebaki milele, bali wotewanapita na kuacha nafasi kwa wengine kuendeleza pale walipoishia. "Sisi tu wapita, tunaendesha. Kipindi kikipita wanakuja wengine kuendeleza. Kwa hiyo ni muhimu vijana na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi mkalijua hilo na wote tukakaa mguu sawa katika kukijenga chama hiki
ameongeza.

28/05/2025

Rais wa Kenya, William Ruto amewaomba msamaha
Watanzania k**a kuna jambo lolote ambalo Kenya imeikosea Tanzania.Akiongea wakati wa maombi maalum ya kuliombea Taifa la Kenya leo May 28,2025, Ruto amesema "Nimesimama hapa kuwaambia kwamba nina uhakika na kesho bora ya Kenya na sina wasiwasi najiamini kwamba Kenya ni nchi iliyobarikiwa na kesho ya Kenya haijalishi kitu gani kimetokea itakuwa nzuri "
"Majirani zetu kutoka Tanzania k**a kuna kitu tumewakosea kwa namna yoyote, mtusamehe, Rafiki zetu wa Uganda k**a kuna kitu tumefanya ambacho hakipo sawa tunaomba radhi, kwa Watoto
Wetu (ikiwemo Gen Z) k**a kuna hatua zozote mbaya mmefanyiwa
tunaomba radhi, kwa Majirani zetu k**a kuna hatua yoyote tumefanya
mtusamehe, tunataka kujenga ushirikiano ambao utaifanya nchi yetu
kuwa bora" Ruto ameomba radhi wakati huu ambapo kumekuwa na malumbano makubwa mitandaoni kati ya Wakenya na Watanzania tangu Mwanaharakati Martha Karua na wenzake waliporejeshwa nchini kwao baada ya kuwasili Tanzania kufuatilia kesi ya Tundu Lissu ambapo malumbano hayo yameshika kasi zaidi baada ya Wabunge wa Mabunge ya nchi zote mbili kutoa maoni yao tofautitofauti kuhusu kinachoendelea.

28/05/2025

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel Nchimbi amesema kuwa ujenzi wa makao makuu mapya
ya chama hicho unatarajiwa ugharimu Sh34.13 bilioni hadi kukamilika
kwake, huku kiasi cha awali cha Sh8 bilioni kikiwa tayari kimepatikana.
Akizungumza leo Jumatano, Mei 28, 2025, jijini Dodoma katika hafla ya
uwekaji wa jiwe la msingi, Dk Nchimbi alieleza kuwa fedha hizo
zimetokana na mapato halali ya kampuni zinazomilikiwa na CCM kupitia miradi ya biashara. "Nitumie nafasi hii kusema kuwa mapato haya yametokana na kampuni za CCM, zinazojitegemea - Holding na Trading. Zimechangia asilimia 100 ya fedha za kuanzia. Hii ni faraja kubwa kwa wana-CCM," amesema Dk Nchimbi. Ameongeza kuwa licha ya kuchangia kwenye ujenzi huo, kampuni hizo zimeendelea kuwa na mchango mkubwa kwa Taifa kwa kulipa kodi zaidi ya Sh25 bilioni kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika miaka miwili iliyopita.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwaamesema katika juhudi za kuzuia uhalifu wa usafirishaji haramu wabin...
26/05/2025

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa
amesema katika juhudi za kuzuia uhalifu wa usafirishaji haramu wa
binadamu, Serikali imeongeza ufanisi katika kudhibiti biashara hiyo kwa
kutunga sheria za kukabiliana na uhalifu wa aina hiyo.
Akiwasilisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya fedha 2025/2026 bungeni Jijini Dodoma leo. Bashungwa amewataja watu wanaojihusisha na biashara hiyo kuacha mara moja na kuahidi kusimamia sheria za ulinzi wa binadamu. Ndani ya Nchi kwa mwaka wa
Mei 26, 2025

26/05/2025

Mbunge wa Geita Vijjini, Joseph Musukuma, ametoa kauli kali
bungeni akilaani matusi na kejeli anazotupiwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, mtandaoni, hususan na
baadhi ya wanaharakati kutoka nchini Kenya.
Akichangia hoja ya bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa
mwaka wa fedha 2025/2026 leo bungeni jijini Dodoma, Musukuma
amesema si jambo la busara kwa wabunge kukaa kimya wakati kiongozi mkuu wa nchi anadhalilishwa.
Musukuma amesema Tanzania haina ugomvi na wananchi wa kawaida
wa Kenya, bali na wanaharakati wa taifa hilo ambao wanatumia mitandao ya kijamii kutoa lugha za matusi dhidi ya Rais Samia.
"Hatuna ugomvi na Wakenya wa kawaida, lakini tuna ugomvi na
wanaharakati wao. Tanzania hatuna cha kujifunza kutoka Kenya;
hatuwazidi siasa tu, bali hata akili. Hili suala la Kiingereza siyo kipaumbele kwetu, sisi tuna maisha yetu, amesema Musukuma
Amesisitiza kuwa Tanzania ni nchi inayojitambua na isiyokubali kuingiliwa au kuchochewa kuvuruga amani yake, akivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuendelea kuchukua hatua dhidi ya wanaoeneza chuki na matusi mtandaoni. Mbunge huyo pia amesema si sawa kwa taifa kuwa na mazingira ambayo mtu anaweza kumdharau Rais wa nchi bila kuchukuliwa hatua, k**a ambavyo imekuwa ikifanyika kwenye baadhi ya mitandao kwa kutumia video za kejeli.

26/05/2025

SITAKI CHAMA CHANGU KUINGIA KWENYE UCHAGUZI, MKOA
WA ARUSHA HAUNA STENDI NA SOKO
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. paul Christian Makonda amesema kuwa atahakikisha ujenzi wa Soko la Kilombero na Stendi kuu ya mabasi ambavyo vimetajwa kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020/2025 k**a alivyosimamia ujenzi wa stendi wakati akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam

20/05/2025

Kikosi Cha Simba kwenda visiwani Zanzibar kesho Jumatano kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa marudiano wa fainali ya Kombe la
Shirikisho Afrika

20/05/2025

RC MAKONDA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MRADI WA
MADARAJA YA KING'ORI BARABARA YA ARUSHA- MOSHI
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, leo asubuhi
amefanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa madaraja mawili ya
King'ori yanayojengwa katika barabara kuu ya Arusha - Moshi na kuridhishwa na kasi na ubora wa ujenzi wa madaraja hayo ambayo ni
kiunganishi muhimu kati ya mikoa ya Arusha na Kilimanjaro. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Makonda amesema kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za serikali katika kuboresha miundombinu ya usafiri nchini, hasa maeneo ambayo yamekuwa na changamoto kubwa wakati wa mvua ambapo serikali imechukua hatua hiyo baada ya wananchi kadhaa kupoteza maisha katika eneo hilo mwaka uliopita kutokana na changamoto za miundombinu hafifu.
"Serikali ina wajibu wa kulinda maisha ya wananchi wake, ndiyo maana tumetafuta suluhu ya kudumu kwa kujenga daraja imara badala ya makalvati yaliyokuwa yakisababisha madhara na hii ni hatua kubwa ya maendeleo katika kuhakikisha usalama wa barabara hii muhimu."
Amesema Mhe. Makonda. Aidha, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuhakikisha miundombinu ya barabara nchini inaboreshwa na kuwa salama wakati wote - iwe ni kipindi cha mvua au kiangazi pamoja na kuipongeza Wizara ya Ujenzi na taasisi
husika kwa kutekeleza kwa ufanisi maelekezo ya Mhe. Rais. Hata hivyo, mesisitiza umuhimu wa watumiaji wa barabara kufuata sheria
na taratibu za usalama baratbarani ili miundombinu hii iweze kudumu kwa muda mrefu, hasa ikizingatiwa kuwa barabara hii inapita magari
makubwa ya mizigo na pia hutumiwa na watalii wengi wanaotembelea
maeneo ya kitalii ya Kaskazini mwa Tanzania.
"Natoa wito kwa wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za Mhepp
Rais. Badala ya maneno, tuongeze bidii ya kufanya kazi na kutafuta fedha halali. Hii ndiyo njia ya kweli ya kuleta maendeleo ya kweli kwa taifa letu," ameongeza.

Address

P. O Box 7292
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari Maalum Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Habari Maalum Fm:

Share