Habari Maalum Fm

Habari Maalum Fm Christian radio/Habari Maalum Media

Leo tunasherehekea mwaka mwingine wa neema na utu uzima kwa kiongozi wetu.  Asante kwa moyo wako wa utumishi, uongozi we...
22/11/2025

Leo tunasherehekea mwaka mwingine wa neema na utu uzima kwa kiongozi wetu. Asante kwa moyo wako wa utumishi, uongozi wenye maono na kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu na maendeleo ya watu. Tunakuombea miaka mingi zaidi yenye hekima, nguvu na baraka tele. Happy Birthday, Director. Habari maalum media Tunakupenda!.

13/11/2025

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dkt. Mwigulu Nchemba, kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwigulu amethibitishwa kwa kura za Ndio 369 kati ya kura 371 zilizopigwa huku za Hapana zikiwa 0, zilizoharibika zikiwa 2.

Uthibitisho huo unafuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kumteua Waziri huyo wa zamani wa Fedha na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mkoani Singida kwenye nafasi hiyo.

13/11/2025

Tunayo habari njema kwako mtu wa lindi kilwa kuwa redio habari maalum fm tunasikika sasa huko kwa masafa ya 97.1
tumedhamiria kukuhudumia zaidi ya matarajio yako, pata ukweli.

kutana na watangazaji mahiri na wengine wengi kwa habari moto moto na za uhakika.


Tunaendelea kukiwasha Hadi ng'ambo ya pili. Tunasikika lindi Sasa kwa masafa ya 97.1
12/11/2025

Tunaendelea kukiwasha Hadi ng'ambo ya pili. Tunasikika lindi Sasa kwa masafa ya 97.1

Mhe. Musa Azzan Zungu akila kiapo kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kushinda nafasi hiyo k...
11/11/2025

Mhe. Musa Azzan Zungu akila kiapo kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kushinda nafasi hiyo kwa kupata kura 378 kati ya kura zote 383 zilizopigwa leo Bungeni wakati wa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge la Kumi na Tatu wa Bunge leo Novemba 11, 2025.

Shirika la kupambana na Ufisadi nchini Nigeria limesema kibali kimetolewa cha kuk**atwa kwa Waziri wa zamani wa Mafuta n...
11/11/2025

Shirika la kupambana na Ufisadi nchini Nigeria limesema kibali kimetolewa cha kuk**atwa kwa Waziri wa zamani wa Mafuta nchini humo Timipre Sylva kwa madai ya kula njama na kufanya Ubadhirifu wa Dola Milioni 14.86.

Fedha hizo zilikuwa sehemu ya Uwekezaji wa Bodi ya Maendeleo ya Maudhui na ufuatiliaji ya Nigeria katika Kampuni ya Atlantic International Refinery and Petrochemical Ltd kwa ajili ya mradi wa kusafishia Mafuta.

Mamlaka ilimtaka yeyote aliye na taarifa za alipo Sylva kuwasiliana na ofisi zake nchi nzima au kuripoti katika kituo cha Polisi kilicho karibu naye.

Sylva alihudumu k**a Waziri wa Mafuta kutoka 2019 hadi 2023 chini ya Rais wa zamani Muhammadu Buhari.

Wajasiriamali wa Tanzania wamepongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwaw...
10/11/2025

Wajasiriamali wa Tanzania wamepongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwawezesha kushiriki Maonesho ya 25 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), maarufu k**a Nguvu Kazi au Jua Kali, yanayoendelea jijini Nairobi, Kenya.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wajasiriamali hao wamesema Serikali imewasaidia kugharamia usafiri pamoja na mizigo yao, jambo ambalo limeongeza ari na hamasa ya kushiriki kwa wingi katika maonesho hayo.

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuwezesha kufika Nairobi. Hii ni fursa ya kipekee kwetu kukuza biashara zetu na kujifunza kutoka kwa wajasiriamali wa nchi nyingine,” amesema mmoja wa washiriki.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati katika Jumuiya ya Afrika Mashariki upande wa Tanzania (CISO–Tanzania), Josephat Rweyemamu, amesema Serikali imeendelea kuratibu ushiriki wa wajasiriamali hao ili kuwawezesha kutangaza bidhaa na huduma zao nje ya mipaka ya nchi.

Maonesho hayo ya 25 yamebeba kaulimbiu isemayo: “Miaka 25 ya Ujumuishaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki: Kuendeleza Ubunifu na Minyororo ya Thamani ya Kikanda kwa Biashara Ndogo na za Kati Shindani kuelekea Maendeleo Endelevu.”

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Ahmed Abbas,anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa mnada wa kwanza wa ...
10/11/2025

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Ahmed Abbas,anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa mnada wa kwanza wa zao la Korosho kwa msimu wa mauzo 2025/2026 chini ya usimamizi wa Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Tunduru(TAMCU LTD).

Akizungumza ofisini kwake Mjini Tunduru Meneja Mkuu wa Chama hicho Marcelino Mrope amesema,katika msimu wa 2025/2026 mnada wa kwanza utafanyika Tarehe 12 Jumatano katika Chama cha Msingi cha Ushirika Namitili(Amcos) kilichopo Kijiji cha Nakapanya Tarafa ya Nakapanya Wilayani humo.

Amesema kuwa,awali mnada huo ulitakiwa kufanyika wiki iliyopita lakini kutokana na changamoto mbalimbali zilizo nje ya uwezo wao ikiwemo kukosekana kwa mtandao unaotumika kwenye uendeshaji wa minada ya mazao yanayouzwa kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

Amesema,katika msimu 2025/2026 korosho zitauzwa kwa mfumo wa stakabadhi ghalani chini ya Usimamizi wa soko la bidhaa Tanzania(TMX) na hakuna mfanyabiashara au kampuni itakayoruhusiwa kununua korosho majumbani badala yake wafike kwenye minada.

Mrope,amewataka wakulima kuhudhuria kwa wingi katika mnada huo ili wapate kufahamu mwenendo mzima wa soko,utaratibu utakaotumika katika kuuza korosho msimu 2025/2026 na mambo mengine muhimu yanayohusu zao hilo.

Mrope amesema,katika msimu 2025/2026 wamejipanga kumaliza changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika msimu wa 2023/2024/2024/2025 ikiwemo upungufu wa magunia na vifaa vingine vinavyotumika kwenye uendeshaji wa minada ya korosho.

“Lengo ni kutaka kuhakikisha wakulima wote wanakusanya korosho zao kwa wakati na kuzifikisha kwenye maghala ya vyama vyao vya msingi vya ushirika vilivyopo kwenye maeneo yao kwa ajili ya minada,natumia nafasi hii kuwasisitiza wakulima waendelee kukusanya korosho na wazingatie ubora ili wapate bei nzuri”amesema Mrope.

Amesema hadi sasa wamefanikiwa kupata gunia 600,000 zenye uwezo wa kuhifadhi kilo 48,000,000 ambazo zimesambazwa kwenye vyama mbalimbali vya msingi vya ushirika na mahitaji ya gunia kwa wakulima ni 437,500.

Kwa mujibu wa Mrope,usambazaji wa gunia kwenda kwa vyama vya msingi vya ushirika ulifanyika kwa awamu na katika awamu ya kwanza wamesambaza gunia zaidi ya gunia 300,000 kwa Amcos zilizopo katika Mkoa wa Ruvuma na mikoa ya Njombe na Mbeya ambayo inayohudumiwa na TAMCU.

Aidha amesema,katika msimu wa mauzo 2025/ 2026 Chama Kikuu (TAMCU) kimepanga kukusanya zaidi ya tani korosho 35,000 za korosho ambazo ni sawa na kilo 35,000,000 ikiwa ni ongezeko la kilo 3,391,962 zilizokusanywa katika msimu wa 2024/2025.

Amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa viuatilifu bure pamoja na mabomba ya kupulizia dawa za korosho kwa bei ya ruzuku kwa wote wakulima wanaojihusisha na kilimo cha zao hilo ili kuwapunguzia wakulima mzigo mkubwa wa kuhudumia mikorosho yao.

Amesema,wakulima wamenufaika na utaratibu wa upatikanaji wa pembejeo hizo ambapo kilo milioni 5,962,550 za Salfa ya unga imesambazwa,viuatilifu vya maji lita 270,573 na sumu ya kudhibiti wadudu lita 110,432.

Mrope amesema,uzalishaji wa zao la korosho unaongezeka mwaka hadi mwaka kutokana na wadau wote kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya za hilo hasa upatikanaji wa huduma mbalimbali ikiwemo huduma za ugani.

Amesema, kuanzishwa na kusimamia kikamilifu mfumo wa stakabadhi ghalani umewezesha wakulima kuuza mazao yao kwa bei kubwa ambapo msimu uliopita bei wastani ilikuwa Sh.2.942.75 kwa kilo moja.

Amesema,mafanikio yaliyopatikana katika msimu 2024/2025 yametokana na maboresho ya sheria,kanuni na miongozo ya utekelezaji wa mfumo wa mauzo wa stakabadhi ghalani kwenye zao hilo chini ya usimamizi wa Soko la Bidhaa Tanzania(TMX).

Mkulima wa korosho wa Kijiji cha Malumba Abdala Kawanga,ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya kilimo kuwajali wakulima kwa kuwapatia pembejeo bure hali iliyosaidia kulima kwa tija na kuongezeka kwa uzalishaji mashambani.

Ameiomba Serikali,kuhakikisha inasimamia soko la korosho kwa kuwashawishi wanunuzi kutoa bei nzuri ili kuhamasisha wakulima waendelee na uzalishaji wa zao hilo ambalo linamchango mkubwa kiuchumi wa Wilaya ya Tunduru,Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla.

Kocha wa klabu ya Simba Selemani Matola amesema wamejiandaa vizuri kuwakabili Jkt Tanzania na wanajeuri za kushinda mche...
07/11/2025

Kocha wa klabu ya Simba Selemani Matola amesema wamejiandaa vizuri kuwakabili Jkt Tanzania na wanajeuri za kushinda mchezo wa kesho November 8 katika uwanja wa meja Isamuhyo.

Ameyasema hayo akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo huku akisisitiza kikosi chake kipo vizuri kwaajili ya mchezo huo ilhali wanakutana na mpinzani mgumu.

Mfanyabiashara Jenifer Jovin (26) maarufu Niffer na wenzake 21 amefikishwa katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu na kus...
07/11/2025

Mfanyabiashara Jenifer Jovin (26) maarufu Niffer na wenzake 21 amefikishwa katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa kesi uhaini.

Niffer na wenzake hao wamefikishwa Mahak**ani hapo leo mchana, Ijumaa Novemba 7, 2025 na kusomewa mashtaka matatu, ambayo ni kula njama ya kutenda kosa la kuharibu miundombinu na mawili ni ya uhaini.

Kosa la kwanza linalowahusu washtakiwa wote 22 ambapo ni kwamba kwa pamoja wamekula njama ya kutenda kosa au kupanga uhalifu ambao ni uhaini

Kosa la pili ambalo ni la uhaini linawahusu washtakiwa 21 isipokuwa mshtakiwa mmoja pekee ambaye ni Niffer, ambapo washtakiwa walianzisha nia ya kuzuia uchaguzi Mkuu 2025, na kutishia mamlaka na wakatekeleza nia hiyo kwa kufanya vurugu zilisababisha uharibifu wa mali za umma,

Na kosa la tatu la uhaini pia linamuhusu mshtakiwa namba moja pekee ambaye ni Niffer, ambapo alihamasisha watu kuvuruga uchaguzi Mkuu 2025 na kuhamasisha umma kununua barakoa za kuzuia mabomu ya machozi kutoka dukani kwake.

07/11/2025

Mfanyabiashara maarufu Jenifer Bilikwiza Jovin (Niffer) amefikishwa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam leo ljumaa, Novemba 7, 2025.

Niffer, anakabiliwa na makosa ya uchochezi na kuhamasisha vurugu siku ya Uchaguzi Mkuu.

Zaidi ya asilimia 81 ya watahiniwa wa darasa la saba 2025 wafaulu
06/11/2025

Zaidi ya asilimia 81 ya watahiniwa wa darasa la saba 2025 wafaulu

Address

P. O Box 7292
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari Maalum Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Habari Maalum Fm:

Share