Jiji la Arusha

Jiji la Arusha Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Jiji la Arusha, News & Media Website, Bomani Street, Arusha.

🛑ARUSHA, TANZANIARC MAKALLA ATANGAZA KAMATI 7 ZA MAANDALIZI YA AFCON 2027, ARUSHA Asema Kuundwa kwa Kamati hizo ni kuone...
04/02/2026

🛑ARUSHA, TANZANIA
RC MAKALLA ATANGAZA KAMATI 7 ZA MAANDALIZI YA AFCON 2027, ARUSHA

Asema Kuundwa kwa Kamati hizo ni kuonesha utayari wa Arusha kwa AFCON

Wananchi, wenye Mahoteli, Makampuni ya utalii na usafirishaji wahimizwa kuchangamkia fursa

Aagiza Jiji Arusha kuhimiza usafi na kupendezesha Jiji la Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumanne Februari 04, 2026 ametangazwa kuundwa kwa Kamati Saba Maalumu kwaajili ya maandalizi ya Michuano ya Mpira wa Miguu kwa Mataifa ya Afrika, AFCON 2027.

Mbele ya Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Wenyeviti wa Halmashauri, Makatibu Tawala, Waganga wakuu na Maafisa Tarafa wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Makalla amesema kuundwa kwa Kamati hizo ni kuonesha utayari wa Mkoa kuwa Mwenyeji wa michuano hiyo mikubwa zaidi barani Afrika.

Amemuelekeza Kaimu Katibu Tawala mkoa kuunda kamati hizo 7 ikiwemo Kamati ya Usalama, Kamati ya Itifaki na Mapokezi, Kamati ya Habari, Mawasiliano na Hamasa, Kamati ya Afya, Kamati ya Malazi, ya Miundombinu pamoja na kamati ya utalii na ukarimu.

Katika hotuba yake, Mhe. Makalla amewataka wananchi, wamiliki wa Mahoteli, Makampuni ya Utalii na usafirishaji kuchangamkia fursa za kiuchumi za Ujio wa michuano hiyo, akiagiza Jiji la Arusha pia kuhimiza usafi na kuongeza jitihada za kupendezesha maeneo ya Jiji hilo.

Aidha, Mhe. Makalla amemshukuru Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuichagua Arusha na kujenga uwanja wa kisasa wa 'category 4' wenye sifa za CAF na kuahidi kushirikiana na watalamu wa ngazi zote kusimamia kikamilifu maandalizi yote ili kuhakikisha Taifa linapata sifa pamoja na ushiriki wa wananchi waweze kujipatia kipato.

🛑DUBAI, UAERais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa Ma...
04/02/2026

🛑DUBAI, UAE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa Makamu wa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, mara baada ya mazungumzo kati yao, kando ya Mkutano wa Dunia (WGS2026) hapa, Dubai, tarehe 04 Februari, 2026.

04/02/2026

🛑ARUSHA, TANZANIA
SERIKALI YATOA FEDHA BILIONI 19. 513 KUPELEKA UMEME KWENYE VITONGOJI 127 ARUSHA

Rc Makalla ampongeza Rais Samia kwa kutimiza ahadi za Ilani ya CCM

_Mkandarasi aombwa kutoa ajira kwa vijana maeneo ya utekelezaji wa mradi_

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amesema Shilingi 19,513,813,347 zimetolewa ili kusambaza umeme kwenye Vitongoji 127 vya Majimbo sita ya Mkoa wa Arusha ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa Rais Samia Suluhu Hassan ya kufikisha umeme kwenye Vitongoji vyote Mkoani Arusha mara baada ya kuwa Serikali imefikisha umeme kwenye Vijiji vyote 368.

Mhe. Makalla amebainisha hayo leo Jumanne Februari 04, 2026 Ofisini kwake Jijini Arusha alipotambulishwa Mkandarasi Nakuroi Investment Company Ltd, atakayetekeza mradi wa usambazaji umeme katika Vitongoji hivyo 127 kutoka katika Wilaya zote za Arusha.

"Kikubwa kwaniaba ya Wakuu wa Wilaya niwahakikishie ushirikiano Tanesco pamoja na Mkandarasi anayetekeleza mradi huu na niagize Mradi mmoja unapokamilika, uzinduliwe wananchi waanze kufaidika. Niagize pia kutumika kwa Vijana wa maeneo husika ili wapate ajira wakati wa utekelezaji wa mradi huu wa Umeme." Amesisitiza Mhe. Makalla.

Kwa upande wake Mhandisi Erin Mhina, Mratibu wa miradi ya REA amemueleza Mhe. Makalla kuwa jumla ya wateja 4086 wataunganishwa na umeme katika mradi huu, akimshukuru Rais Samia kwa uwekezaji wake mkubwa katika miradi ya umeme Mkoani Arusha, akisema kando ya mradi huu wa sasa ipo miradi mingine 6 inayotekelezwa Mkoani hapa, yote ikigharimu Shilingi Bilioni 99.18.

03/02/2026

📍Arusha, Tanzania

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Paul Makonda ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Arusha pamoja na Serikali ya Mkoa kwa usimamizi mzuri wa mradi wa jengo la utawala lenye ghorofa 9, akieleza kuridhishwa na kasi kubwa ya utekelezaji wa mradi huo wakati wa ziara yake leo tarehe 3 Februari.

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Ndg. John L. Kayombo anawatakia Wananchi wote Heri ya Mwaka Mpya,2025.
01/01/2025

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Ndg. John L. Kayombo anawatakia Wananchi wote Heri ya Mwaka Mpya,2025.

31/12/2024

Happy New Year

Address

Bomani Street
Arusha
P.O.BOX8844

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jiji la Arusha posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jiji la Arusha:

Share