Jiji la Arusha

Jiji la Arusha Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Jiji la Arusha, News & Media Website, Bomani Street, Arusha.

08/06/2026

πŸ“ ARUSHA TANZANIA

AUWSA NA ROTARY CLUB WAKABIDHI VYOO VYA KISASA SHULE YA MSINGI LEVOLOSI

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Arusha (AUWSA) kwa kushirikiana na Rotary Club pamoja na wadau wengine wa maendeleo, wamekabidhi rasmi mradi wa vyoo vya kisasa katika Shule ya Msingi Levolosi iliyopo Kata ya Levolosi, Jiji la Arusha, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha mazingira ya elimu na afya kwa wanafunzi.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika Juni 8, 2026, Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa AUWSA, Anne Mshana, alisema mamlaka hiyo imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutekeleza miradi ya usafi wa mazingira katika shule za msingi, ambapo zaidi ya vyoo 49 vinatarajiwa kujengwa katika maeneo tofauti ya jiji.

Alieleza kuwa mradi wa Shule ya Msingi Levolosi umehusisha ujenzi wa vyoo vyenye matundu 13 kwa ajili ya wasichana na wavulana, kwa gharama inayozidi shilingi milioni 50. Mradi huo unatarajiwa kuhudumia zaidi ya wanafunzi 1,200 na kuchangia kuboresha hali ya usafi, afya pamoja na mazingira ya kujifunzia.

Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo walieleza kufurahishwa na kukamilika kwa mradi huo, wakisema miundombinu hiyo mpya itawasaidia kupata huduma bora za usafi na kuondoa changamoto zilizokuwepo awali kutokana na uchakavu wa vyoo vya zamani.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Levolosi, Abas Haji, aliipongeza AUWSA, Rotary Club na wadau wote walioshiriki kufanikisha mradi huo, akisema umeongeza thamani katika sekta ya elimu na ustawi wa wanafunzi.

Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kuhamasisha ushirikiano na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha huduma muhimu za kijamii zinaimarishwa zaidi, huku akisisitiza umuhimu wa kujenga miundombinu jumuishi inayozingatia mahitaji ya watu wote, ikiwemo wanafunzi wenye mahitaji maalum na watu wenye ulemavu.






08/06/2026

πŸ“ ARUSHA, TANZANIA

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Ndugu Kenani Kihongosi, amempongeza Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Ndg. John L. Kayombo, kwa usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Jiji la Arusha.

Akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Kilombero, Jijini Arusha, tarehe 6 Juni 2026, Ndugu Kihongosi alisema utekelezaji wa miradi hiyo unaakisi matumizi sahihi ya rasilimali za umma pamoja na dhamira ya dhati ya Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Katika hotuba yake, alimuita Mkurugenzi huyo "Mkurugenzi Chuma", akieleza kuwa utendaji kazi wake umechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Jiji la Arusha.

Aidha, alibainisha kuwa Ndg. Kayombo ni miongoni mwa viongozi wanaoacha alama katika halmashauri wanazozitumikia, jambo linalodhihirisha rekodi nzuri ya utendaji na utumishi wa kujituma kwa maslahi ya wananchi.

Kauli hiyo ilitolewa ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa ziara za Katibu huyo wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa zinazofanyika katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuzungumza na wananchi, kusikiliza kero zao na kukagua utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

06/06/2026

πŸ“ ARUSHA, TANZANIA

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imepongeza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha ukiongozwa na Mkurugenzi wa Jiji, Ndugu John L. Kayombo, pamoja na Timu ya Menejimenti kwa usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo na ushirikishwaji mzuri wa wananchi katika utekelezaji wake.

Pongezi hizo zimetolewa leo, Juni 6, 2026, wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Soko la Mrombo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ndani ya Jiji la Arusha.

Kamati hiyo imeeleza kuridhishwa na hatua za utekelezaji wa mradi huo pamoja na namna Halmashauri ilivyozingatia uwazi, usimamizi wa rasilimali za umma na ushirikishwaji wa wananchi, mambo ambayo yameendelea kuimarisha thamani na tija ya miradi ya maendeleo kwa jamii.

Aidha, wananchi waliofika katika eneo la mradi wakati wa ziara hiyo walitoa shukrani zao kwa Serikali kwa kutekeleza mradi huo mkubwa, wakieleza kuwa utakuwa chachu ya kukuza shughuli za biashara na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Jiji la Arusha na maeneo jirani.

Pamoja na pongezi hizo, wananchi hao waliomba kuboreshwa kwa miundombinu ya barabara zinazozunguka soko hilo mara baada ya kukamilika kwake. Akijibu ombi hilo, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Ndugu John L. Kayombo, aliwahakikishia kuwa eneo lote linalozunguka Soko la Mrombo litaboreshwa kwa kujengwa barabara za lami ili kurahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa.

Ziara ya Kamati ya LAAC ni sehemu ya jukumu lake la kusimamia matumizi sahihi ya fedha za umma na kuhakikisha miradi ya maendeleo inayotekelezwa inakidhi malengo yaliyokusudiwa na kutoa manufaa kwa wananchi.







tanzania

06/06/2026

πŸ“ ARUSHA, TANZANIA

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Mhe. Ado Shaibu, amesisitiza kuwa miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika Jiji la Arusha inapaswa kukamilika kwa wakati na kwa kuzingatia thamani ya fedha, ili iweze kutoa huduma bora kwa wananchi na kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Mhe. Shaibu ametoa maelekezo hayo leo, Juni 6, 2026, mara baada ya Kamati hiyo kufanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Jiji la Arusha.

Katika ziara hiyo, Kamati ya LAAC ilikagua miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Arusha, ikiwemo Ujenzi wa Mradi wa Soko la Kilombero, Mradi wa Ujenzi wa Soko la Mrombo, ujenzi wa Mradi wa Stendi Kuu ya Mabasi ya Mkoa wa Arusha, pamoja na ujenzi wa Mradi wa Bustani ya Mapumziko ya Themi Living Garden.

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mhe. Shaibu amesema Kamati imeridhishwa na maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo, huku akitaka kasi ya utekelezaji iendelee ili miradi hiyo ikamilike ndani ya muda uliopangwa na kwa ubora unaozingatia matumizi sahihi ya fedha za umma.

Amebainisha kuwa kukamilika kwa miradi hiyo kutaimarisha utoaji wa huduma za kijamii na kiuchumi, kuongeza fursa za ajira na biashara, pamoja na kuchochea maendeleo endelevu ya Jiji la Arusha na wananchi wake.







πŸ“ ARUSHA, TANZANIA Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imepongeza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Ar...
06/06/2026

πŸ“ ARUSHA, TANZANIA

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imepongeza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha ukiongozwa na Mkurugenzi wa Jiji, Ndugu John L. Kayombo, pamoja na Timu ya Menejimenti kwa usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo na ushirikishwaji mzuri wa wananchi katika utekelezaji wake.

Pongezi hizo zimetolewa leo, Juni 6, 2026, wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Soko la Mrombo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ndani ya Jiji la Arusha.

Kamati hiyo imeeleza kuridhishwa na hatua za utekelezaji wa mradi huo pamoja na namna Halmashauri ilivyozingatia uwazi, usimamizi wa rasilimali za umma na ushirikishwaji wa wananchi, mambo ambayo yameendelea kuimarisha thamani na tija ya miradi ya maendeleo kwa jamii.

Aidha, wananchi waliofika katika eneo la mradi wakati wa ziara hiyo walitoa shukrani zao kwa Serikali kwa kutekeleza mradi huo mkubwa, wakieleza kuwa utakuwa chachu ya kukuza shughuli za biashara na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Jiji la Arusha na maeneo jirani.

Pamoja na pongezi hizo, wananchi hao waliomba kuboreshwa kwa miundombinu ya barabara zinazozunguka soko hilo mara baada ya kukamilika kwake. Akijibu ombi hilo, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Ndugu John L. Kayombo, aliwahakikishia kuwa eneo lote linalozunguka Soko la Mrombo litaboreshwa kwa kujengwa barabara za lami ili kurahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa.

Ziara ya Kamati ya LAAC ni sehemu ya jukumu lake la kusimamia matumizi sahihi ya fedha za umma na kuhakikisha miradi ya maendeleo inayotekelezwa inakidhi malengo yaliyokusudiwa na kutoa manufaa kwa wananchi.







06/06/2026
06/06/2026

Dar es Salaam,Tanzania

06/06/2026

πŸ“MOSCOW,RUSSIA
Hatimaye Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ahitimisha ziara yake na kurejea nyumbani leo.

06/06/2026

πŸ“ ARUSHA, TANZANIA

Halmashauri ya Jiji la Arusha imetoa hundi ya mfano yenye thamani ya shilingi bilioni 1.2 kwa vikundi 101 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vilivyonufaika na mikopo ya asilimia 10, hatua inayolenga kuendelea kuyawezesha makundi hayo kiuchumi na kuboresha maisha yao.

Hafla ya kukabidhi hundi hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Shule ya Msingi Arusha na kuhudhuriwa na maafisa maendeleo ya jamii, wanufaika wa mikopo pamoja na watumishi mbalimbali kutoka Wilaya ya Arusha.

Akisoma taarifa ya utoaji wa mikopo hiyo mbele ya mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Arusha, Shaban Manyama, amesema jumla ya vikundi 155 viliwasilisha maombi ya mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8.

Amesema vikundi vyote vilitembelewa na kukaguliwa na Kamati ya Mikopo ya Halmashauri ili kujiridhisha kuhusu uhalali na uendelevu wa miradi yao, ambapo vikundi 101 pekee vilifanikiwa kukidhi vigezo na masharti yaliyowekwa kwa ajili ya kunufaika na mikopo hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, vikundi 74 vya wanawake vimenufaika na mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 781.6, huku vikundi 19 vya vijana vikitengewa shilingi milioni 354.3. Aidha, vikundi 8 vya watu wenye ulemavu vimepatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 75.4.

Manyama amesema kabla ya kupatiwa mikopo hiyo, wanachama wa vikundi husika walipatiwa mafunzo kwa muda wa wiki sita yaliyolenga kuwaimarisha katika usimamizi wa shughuli zao za kiuchumi na matumizi sahihi ya fedha za mikopo.

Mafunzo hayo yalihusisha mada mbalimbali ikiwemo umuhimu wa kuweka akiba, faida za kufanya kazi kupitia vikundi, hatua za utambuzi wa vikundi, sifa zinazotakiwa kwa vikundi vinavyoomba mikopo, namna ya kuandaa andiko rahisi la mradi pamoja na utaratibu wa kuwasilisha maombi kupitia mfumo wa Wezesha Portal.

Utoaji wa mikopo hiyo unaendelea kudhihirisha dhamira ya Serikali ya kuwawezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali, kuongeza kipato cha kaya na kuchochea maendeleo ya uchumi wa Jiji la Arusha na taifa kwa ujumla.





05/06/2026

πŸ“ ARUSHA, TANZANIA

Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe.Joseph Mkude, amewataka wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kuweka akiba kwa uaminifu na nidhamu ili kuwawezesha kurejesha mikopo yao kwa wakati na kujiwekea msingi imara wa kukuza biashara zao.

Mhe. Mkude ametoa rai hiyo leo wakati wa hafla ya kukabidhi hundi ya mfano kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vilivyonufaika na mikopo hiyo katika hafla iliyoandaliwa na Halmashauri ya Jiji la Arusha k**a sehemu ya muendelezo wa utekelezaji wa mpango wa uwezeshaji wa makundi maalum kiuchumi.

Amesema kuwa mikopo ya asilimia 10 ni fursa muhimu inayolenga kuinua hali za maisha ya wananchi, hivyo ni wajibu wa wanufaika kuitumia kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuleta tija kwao binafsi, familia zao na jamii kwa ujumla.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa wanufaika kuwa waaminifu katika usimamizi wa fedha wanazopatiwa kwa kuhakikisha wanaweka akiba, wanatunza kumbukumbu za biashara zao na kurejesha mikopo kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa.

Mhe. Mkude amebainisha kuwa urejeshaji mzuri wa mikopo utaziwezesha halmashauri kuendelea kuwafikia wananchi wengi zaidi wanaohitaji mtaji wa kuanzisha au kupanua shughuli zao za kiuchumi.

Halmashauri ya Jiji la Arusha imeendelea kutekeleza kwa vitendo mpango wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu k**a sehemu ya juhudi za Serikali za kukuza uchumi jumuishi na kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.






Address

Bomani Street
Arusha
P.O.BOX8844

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jiji la Arusha posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jiji la Arusha:

Shortcuts

Share