Habari za Zanzibar

Habari za Zanzibar Ukurasa utakaokupa habari mbalimbali kutoka Zanzibar na Ulimwenguni kote.

27/07/2025

Fix za Gwaji: Askofu Anamzidi Shetani Kwa Uongo

26/07/2025

Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), Mbunge wa Makete, na Waziri wa Nchi - Ofisi ya Rais (Usalama wa Taifa), Dkt. Hassy Kitine, lilivyowasili katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam kwa ajili ya taratibu za Mazishi.

📽 Global Publishers

26/07/2025

Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), Mbunge wa Makete, na Waziri wa Nchi - Ofisi ya Rais (Usalama wa Taifa), Dkt. Hassy Kitine, lilivyowasili nyumbani kwake Osterbay, mtaa wa Laibon, Dar es Salaam.

Mazishi yanatarajiwa kufanyika leo Julai 26, 2025 katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam.

📽 Global Publishers

26/07/2025

Nipe maoni yako kwenye pambano la leo kati ya Mfaume Mfaume na Banda kutoka Malawi

Tanzania na Rwanda Zaimarisha Ushirikiano kwa Kusaini Hati Mbili za MakubalianoMkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja...
26/07/2025

Tanzania na Rwanda Zaimarisha Ushirikiano kwa Kusaini Hati Mbili za Makubaliano

Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Rwanda umefungwa rasmi jijini Kigali leo tarehe 26 Julai 2025, baada ya mawaziri wa pande zote mbili kusaini hati mbili za makubaliano ya ushirikiano ikiwemo ya kilimo na uanzishwaji wa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) jijini Kigali, k**a sehemu ya hatua za kuimarisha uhusiano wa karibu na kukuza maendeleo ya pamoja baina ya nchi hizo mbili.

Hati hizo zimesainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Olivier Nduhungirehe ikilenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya Tanzania na Rwanda kwa manufaa ya wananchi wa mataifa haya mawili. Kupitia makubaliano ya sekta ya kilimo, pande zote zimekusudia kubadilishana uzoefu, teknolojia, utaalamu na taarifa muhimu ili kuongeza uzalishaji, usalama wa chakula na fursa za biashara ya mazao ya kilimo.

Aidha, uanzishwaji wa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) jijini Kigali unalenga Kurahisisha upatikanaji wa huduma za Bandari nchini Rwanda, kupunguza gharama za bidhaa, kuimarisha na kuongeza matumizi ya Bandari za Tanzania k**a lango kuu ka kupitisha mizigo na shehena za Rwanda

Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mkutano, Waziri Kombo amesisitiza umuhimu wa utekelezaji wa makubaliano yote yaliyoafikiwa katika mkutano huo na kuwataka wataalamu na viongozi wa serikali kuhakikisha kuwa mipango na maazimio ya JPC yanatekelezwa kwa wakati.

Kwa upande wake, Waziri Nduhungirehe ameipongeza Tanzania kwa ushirikiano mzuri na kusisitiza kuwa Rwanda itaendelea kushirikiana kwa karibu na nchi jirani ili kuhakikisha maridhiano ya kweli yanapatikana kupitia utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa. Ameeleza kuwa makubaliano k**a hayo ni nyenzo muhimu ya kukuza uchumi, kuboresha usalama wa chakula, na kuimarisha mshik**ano wa kidiplomasia na kijamii kati ya mataifa hayo mawili.

Mkutano wa 16 wa JPC umejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo biashara, ulinzi na usalama, miundombinu, afya, elimu, nishati, na kilimo. Mazungumzo hayo yamekuwa na tija kubwa na kufanikisha hatua za pamoja za kuendeleza mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi baina ya Tanzania na Rwanda.

WAZIRI KOMBO AFUNGUA MILANGO MIPYA YA USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA RWANDA KUPITIA MKUTANO WA JPC KIGALIWaziri wa Mamb...
26/07/2025

WAZIRI KOMBO AFUNGUA MILANGO MIPYA YA USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA RWANDA KUPITIA MKUTANO WA JPC KIGALI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amefungua rasmi Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Rwanda, uliofanyika tarehe 26 Julai 2025 jijini Kigali, Rwanda.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Waziri Kombo ametoa salamu za kindugu kutoka kwa Serikali na Wananchi wa Tanzania kwa Serikali ya Jamhuri ya Rwanda, huku akitoa shukrani za dhati kwa mapokezi ya ukarimu na mazingira mazuri ya mkutano huo.

Waziri Kombo amebainisha kuwa miradi ya pamoja ya kimkakati inayotekelezwa na nchi hizo mbili, ikiwemo Mradi wa Umeme wa Rusumo, kituo cha pamoja cha forodha cha Rusumo (OSBP), pamoja na reli ya kisasa (Standard Gauge Railway – SGR), kuwa ni vielelezo vya mafanikio ya ushirikiano wa muda mrefu.

Licha ya mafanikio hayo, Mhe. Kombo amesisitiza kuwa bado kuna nafasi kubwa ya kuendeleza ushirikiano huo, hasa katika maeneo ya biashara, uwekezaji, kilimo, afya, teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), nishati, utalii na miundombinu.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Rwanda, Mhe. Balozi Olivier Nduhungirehe, ameeleza kuwa uhusiano kati ya Rwanda na Tanzania una historia ya kina inayojengwa juu ya maadili ya pamoja, undugu wa karibu, na maono ya maendeleo ya pamoja.

Waziri Nduhungirehe pia amesisitiza mchango mkubwa wa Tanzania k**a mshirika wa kimkakati wa biashara na maendeleo ya Rwanda, akieleza kuwa zaidi ya asilimia 70 ya mizigo ya Rwanda husafirishwa kupitia Bandari ya Dar es Salaam. Aidha, amepongeza hatua ya kufunguliwa kwa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) mjini Kigali.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Mku...
26/07/2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Taifa kwa njia ya kidijitali ambapo ameongea na Wajumbe wa Mkutano huo nchi nzima kwa njia ya mtanadao tarehe 26 Julai, 2025 katika ukumbi wa mkutano wa NEC (White House) Makao Makuu ya CCM, Jijini Dodoma.

𝗦𝗜𝗞𝗨 𝗬𝗔 𝗠𝗔𝗦𝗛𝗨𝗝𝗔𝗔 𝗦𝗜𝗢 𝗝𝗨𝗞𝗪𝗔𝗔 𝗟𝗔 𝗞𝗜𝗦𝗜𝗔𝗦𝗔,𝗪𝗔𝗡𝗔𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗧𝗨𝗦𝗜𝗣𝗢𝗧𝗢𝗦𝗛𝗪𝗘!Siku ya Mashujaa Tanzania ni siku muhimu ya kumbukumbu amba...
26/07/2025

𝗦𝗜𝗞𝗨 𝗬𝗔 𝗠𝗔𝗦𝗛𝗨𝗝𝗔𝗔 𝗦𝗜𝗢 𝗝𝗨𝗞𝗪𝗔𝗔 𝗟𝗔 𝗞𝗜𝗦𝗜𝗔𝗦𝗔,𝗪𝗔𝗡𝗔𝗡𝗖𝗛𝗜 𝗧𝗨𝗦𝗜𝗣𝗢𝗧𝗢𝗦𝗛𝗪𝗘!

Siku ya Mashujaa Tanzania ni siku muhimu ya kumbukumbu ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Julai kwa heshima ya mashujaa wa Taifa letu waliojitolea kwa ajili ya uhuru, umoja, na maendeleo ya Tanzania. Kwa miaka mingi, siku hii imekuwa na desturi maalum ya 𝐤𝐮𝐭𝐨𝐤𝐮𝐞𝐩𝐨 𝐤𝐰𝐚 𝐡𝐨𝐭𝐮𝐛𝐚 𝐫𝐚𝐬𝐦𝐢 𝐲𝐚 𝐑𝐚𝐢𝐬 𝐰𝐚𝐤𝐚𝐭𝐢 𝐰𝐚 𝐬𝐡𝐞𝐫𝐞𝐡𝐞 𝐡𝐢𝐳𝐨, tofauti na siku nyingine za maadhimisho ya kitaifa k**a Siku ya Uhuru (9 Desemba) au Siku ya Muungano (26 Aprili).

𝙆𝙬𝙖 𝙉𝙞𝙣𝙞 𝙍𝙖𝙞𝙨 𝙃𝙖𝙩𝙤𝙞 𝙎𝙞𝙠𝙪 𝙮𝙖 𝙈𝙖𝙨𝙝𝙪𝙟𝙖𝙖?

1. 𝙈𝙖𝙙𝙖 𝙮𝙖 𝙎𝙞𝙠𝙪 𝙃𝙞𝙮𝙤 𝙣𝙞 𝙆𝙪𝙢𝙗𝙪𝙠𝙪𝙢𝙗𝙪, 𝙎𝙞𝙤 𝙎𝙞𝙖𝙨𝙖.

Siku ya Mashujaa imekuwa ikilenga zaidi kutukuza na kuwakumbuka mashujaa wa historia (k**a vile Julius Nyerere, Abeid Amani Karume, na wengine) badala ya kufanyika k**a tukio la kisiasa. Hivyo, haihitaji hotuba ya kisiasa au ya serikali, bali ni siku ya heshima na shukrani.

2. 𝘿𝙚𝙨𝙩𝙪𝙧𝙞 𝙮𝙖 𝙆𝙞𝙝𝙞𝙨𝙩𝙤𝙧𝙞𝙖

Tangu zamani, sherehe za Siku ya Mashujaa zimekuwa na mfumo wa matoleo ya heshima, maua, na kusimama kwa muda wa dakika moja kwa kuwakumbuka mashujaa. Rais hushiriki kwa kutoa heshima kimya kimya na kuweka Ngao na Mkuki badala ya kuzungumza. Hii ni tofauti na siku nyingine ambazo Rais ana nafasi ya kutoa hotuba kwa Taifa.

3. 𝙆𝙪𝙚𝙥𝙪𝙠𝙖 𝙠𝙪𝙥𝙤𝙩𝙚𝙯𝙖 𝙢𝙖𝙖𝙣𝙖 𝙮𝙖 𝙨𝙞𝙠𝙪 𝙝𝙞𝙞 𝙢𝙪𝙝𝙞𝙢𝙪

K**a nilivyosema, baadhi ya wanaharakati au watu wenye nia mbaya wanaweza kujaribu kupotosha maana ya siku hii kwa kuiunganisha na mambo ya kisiasa au matakwa ya kisasa. Lakini wananchi wanapaswa kujua kwamba kwamba siku hii ni ya kihistoria na ya utambulisho wa taifa sio ya mijadala ya kisiasa.

Jamba hili sio kwa Tanzania tu hata nchi nyingine zinazoadhimisha siku za mashujaa (k**a Kenya au Afrika Kusini) pia huwa hazina hotuba za marais kwa siku hiyo maalum. Badala yake, huwa na matoleo ya heshima, shughuli za kijamii, na kukumbuka kwa kimya.

Ukweli ni kwamba Tanzania haijawahi kuwa na hotuba ya Rais wakati wa Siku ya Mashujaa, na hii ni desturi thabiti iliyotunzwa kwa miaka mingi. Ikiwa kuna mtu anayesema vinginevyo au kujaribu kuifanya siku hii kuwa platform ya kisiasa basi anapotosha historia na maadili ya taifa.

Mwisho.

WAZIRI KOMBO APONGEZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA JPC RWANDA, AHIMIZA KUCHANGAMKIA FURSA ZA USHIRIKIANOWaziri w...
25/07/2025

WAZIRI KOMBO APONGEZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA JPC RWANDA, AHIMIZA KUCHANGAMKIA FURSA ZA USHIRIKIANO

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amewapongeza wajumbe wa Tanzania waliowasili jijini Kigali, Rwanda kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Rwanda.

Akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Ubalozi wa Tanzania jijini Kigali, Waziri Kombo ameeleza kuridhishwa na ushiriki wa ujumbe huo, akisema hatua yao ya kuwasili mapema ni uthibitisho wa uzalendo, uwajibikaji na dhamira ya dhati ya kulitumikia taifa.

Aidha, Waziri Kombo ameeleza kuwa hatua hiyo imewezesha wajumbe kufanya maandalizi ya kina kwa ajili ya majadiliano yenye tija, kwa kuzingatia masuala muhimu ya kipaumbele yatakayowasilishwa katika mkutano huo.

Katika hotuba yake, Waziri Kombo amesisitiza umuhimu wa kutumia kikamilifu fursa zinazojitokeza kupitia ushirikiano kati ya Tanzania na Rwanda. Ametoa wito kwa wajumbe kuwa na mikakati madhubuti ya kuzitumia ipasavyo fursa hizo kwa ajili ya maendeleo ya nchi na ustawi wa wananchi.

Vilevile, amewahimiza wajumbe kuendelea kusimamia maslahi ya taifa katika majadiliano yote, akisisitiza kuwa wao ni wawakilishi wa Watanzania na wanapaswa kuhakikisha kuwa Tanzania inanufaika kikamilifu na makubaliano yatakayofikiwa.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib M***a, ameeleza kuwa mkutano huo una ajenda mahsusi zilizoandaliwa na wataalamu kutoka pande zote mbili, zikilenga kuimarisha ushirikiano katika nyanja za uchumi, biashara, miundombinu, afya, elimu na usalama wa mipaka.

Mkutano wa 16 wa JPC unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 26 Julai 2025 kwa ngazi ya Mawaziri, ambapo viongozi hao watapitisha maazimio ya pamoja na kuweka mikakati ya utekelezaji, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uhusiano wa kidugu kati ya Tanzania na Rwanda na kufungua kurasa mpya za ushirikiano wa kimkakati.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amewasili jijini Kiga...
25/07/2025

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amewasili jijini Kigali, Rwanda, kushiriki Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Rwanda.

Mhe. Kombo amepokelewa na Mshauri wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Bi. Isabelle Umugwaneza, pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Dkt. Habib Kambanga, na maafisa wengine waandamizi kutoka pande zote mbili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki maadhimisho ya Sik...
25/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki maadhimisho ya Siku ya Mashujaa katika uwanja wa Mashujaa, Mtumba Jijini Dodoma leo, tarehe 25 Julai, 2025.

Yarrabi Mjalie Rais Wetu Subra na Uvumilivu, Ijalie Nchi yetu Amani na Utulivu, Jummah Mubarak
25/07/2025

Yarrabi Mjalie Rais Wetu Subra na Uvumilivu, Ijalie Nchi yetu Amani na Utulivu, Jummah Mubarak

Address

Bagamoyo

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari za Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share