Habari za Zanzibar

Habari za Zanzibar Ukurasa utakaokupa habari mbalimbali kutoka Zanzibar na Ulimwenguni kote.

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt....
25/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia wananchi wa Lindi mjini katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi kwa CCM, mkoani Lindi tarehe 25 Septemba, 2025.

Asante Lindi29
25/09/2025

Asante Lindi

29

SALAMU ZA POLE
25/09/2025

SALAMU ZA POLE

Waziri Kombo amwakilisha Rais Samia katika kikao cha Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika.Waziri wa Mambo ya Nj...
25/09/2025

Waziri Kombo amwakilisha Rais Samia katika kikao cha Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabiti Kombo, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa 1303 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, uliofanyika tarehe 24 Septemba, 2025 jijini New York, Marekani.

Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Waziri Kombo amesema Tanzania inaendelea kutekeleza azma yake ya kushirikiana na wadau wa maendeleo katika kulinda amani na kutatua migogoro kwa kuzingatia misingi ya diplomasia.

Ameongeza kuwa Viongozi wengi Barani Afrika wanatambua mafanikio yaliyopatikana katika kuimarisha miundombinu ya amani na usalama kupitia utekelezaji wa Miundombinu ya Amani na Usalama ya Afrika, pamoja na Miundombinu ya Utawala Bora.

“Hatua hii imewezesha kuanzishwa kwa majukwaa ya kubadilishana maarifa kati ya Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika, na hivyo kuimarisha mshik**ano pamoja na dhamira ya pamoja ya kuiwezesha Afrika kufikia amani ya kudumu katika siku zijazo,” alifafanua Mhe. Waziri Kombo.

Amesema mwaka 2013 wakati wa maadhimisho ya Miaka 50 ya Umoja wa Afrika, bara la Afrika liliweka lengo la kumaliza vita ifikapo mwaka 2020 kupitia mpango wa Kukomesha Silaha (Silencing Guns).

Aliongeza kuwa muda utekelezaji wa azimio hilo uliongezwa hadi mwaka 2030, ili kuiwezesha Afrika kufikia dhamira ya pamoja ya kuleta amani ya kudumu katika eneo lake.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, Rais João Lourenço wa Angola, amezisihi nchi wanachama kuendelea kuimarisha juhudi za kuzuia na kutatua migogoro barani Afrika ili kuimarisha usalama wa Waafrika na maendeleo yao.

“Ikiwa hatua madhubuti hazitachukuliwa sasa, migogoro hii itaendelea kuhatarisha amani na utulivu wa bara, na pia kuzuia utekelezaji wa maazimio na mikataba ya Umoja wa Afrika chini ya Ajenda 2063 pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa,” alisisitiza Rais Lourenço.

Alisema Ajenda 2063 ni mpango wa muda mrefu wa maendeleo wa Umoja wa Afrika (AU) uliobuniwa mwaka 2013 wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa kwa AU, ili kuimarisha ustawi, amani, umoja, na maendeleo jumuishi ya Bara la Afrika ifikapo mwaka 2063.

Rais Lourenço pia alisisitiza umuhimu wa kuongeza michango ya kifedha katika Mfuko wa Amani wa Umoja wa Afrika uliohuishwa, na kushirikiana na Umoja wa Mataifa katika kutekeleza Azimio la Baraza la Usalama la UN namba 2719, ili kuweka misingi imara ya rasilimali zitakazosaidia jitihada za kuleta amani barani Afrika.

Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika lilianzishwa mwaka 2004 k**a sehemu ya taasisi za Umoja wa Afrika iliyolenga kudumisha amani, usalama, na utulivu barani Afrika.

Baraza hili pia linawajibika kuzuia migogoro kabla haijatokea, kushughulikia migogoro inayojitokeza, na kutafuta suluhisho la kudumu kwa migogoro iliyopo ili kuleta maendeleo endelevu na ustawi wa Bara la Afrika.

Mkutano huu ulihudhuriwa na nchi zote Wanachama wa Baraza la Amani na Usalama, Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa.

Mkutano huo umefanyika pembezoni mwa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umebeba kaulimbiu isemayo: 'Kuchochea Upya Juhudi za Kuzuia na Kutatua Migogoro Barani Afrika.

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, I convey my heartfelt congratulations to ...
25/09/2025

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, I convey my heartfelt congratulations to His Excellency Professor Arthur Peter Mutharika, President-elect of the Republic of Malawi, on his victory in the 2025 Malawian general election. I look forward to working together to further strengthen our historic ties.

I commend His Excellency President Dr. Lazarus Chakwera, the Malawi Congress Party (MCP) and the people of Malawi, for a peaceful election and a smooth transition.

God bless Africa.
God bless Malawi.

Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan
President of the United Republic of Tanzania

Leo ni zamu ya Mchinga na Lindi Mjini 📆 25.09.2025
25/09/2025

Leo ni zamu ya Mchinga na Lindi Mjini

📆 25.09.2025

Katika mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ( ), Afisa Mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani anaye...
24/09/2025

Katika mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ( ), Afisa Mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika, Jonathan Pratt, alifanya kikao na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabit Kombo. Walijadili umuhimu wa diplomasia ya kibiashara, ikiwemo kufungua fursa kubwa zaidi za kiuchumi kupitia kuboresha mazingira ya biashara.

On the margins of UNGA 80, 🇺🇸 Senior Bureau Official for Africa, Jonathan Pratt, had a productive meeting with 🇹🇿 Foreign Minister Embassodor Mahmoud Thabit Kombo. They discussed the importance of commercial diplomacy, potentially unlocking greater economic potential through an improved business environment.

Ahsanteni sana Ruvuma. Mmetukirimu, mmetusikiliza na kutupa heshima na ahadi kubwa ifikapo Oktoba 29. Tutaendelea kufany...
23/09/2025

Ahsanteni sana Ruvuma.

Mmetukirimu, mmetusikiliza na kutupa heshima na ahadi kubwa ifikapo Oktoba 29. Tutaendelea kufanya kazi vyema na kwa mafanikio zaidi ili tuzidi kusonga mbele.

Nakapanya mmehitimisha kwa kishindo kampeni za Chama cha Mapinduzi (CCM) ngazi ya Urais kwa Mkoa wa Ruvuma. Ninawashukuru sana kwa sala, dua na baraka zenu tunapoelekea mkoani Mtwara na mikoa mingine kuzungumza na wananchi.

Mgombea Urais Kupitia Chama Cha Mapinduzi.
Ndg. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Sehemu ya wananchi wa Nakapanya waliohudhuria mkutano wa hadhara wa Kampeni za Uchaguzi kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tu...
23/09/2025

Sehemu ya wananchi wa Nakapanya waliohudhuria mkutano wa hadhara wa Kampeni za Uchaguzi kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tunduru mkoani Ruvuma tarehe 23 Septemba, 2025.

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt....
23/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Nakapanya katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi kwa CCM, Tunduru mkoani Ruvuma tarehe 23 Septemba, 2025.

Address

Bagamoyo
61305

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari za Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share