Habari za Zanzibar

Habari za Zanzibar Ukurasa utakaokupa habari mbalimbali kutoka Zanzibar na Ulimwenguni kote.

03/01/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, akiwatembelea Rais Wastaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein na Mhe. Amani Abeid Karume, leo tarehe 03 Januari, 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amtembelea na kumjulia hali, Rais M...
03/01/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amtembelea na kumjulia hali, Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Amani Abeid Karume katika makazi yake Unguja, Zanzibar leo tarehe 03 Januari 2026.

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso (kulia kwake) na Waziri wa Fedha, Balozi, K...
03/01/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso (kulia kwake) na Waziri wa Fedha, Balozi, Khamis Omar (kushoto) katika kikao cha kazi kilichofanyika ofisini kwa Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Januari 3, 2026. Kikao hicho pia kiliwahusisha viongozi na watendaji kutoka TAMISEMI, Wizara ya Fedha na Wizara ya Maji.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amtembelea na kumjulia hali, Rais M...
03/01/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amtembelea na kumjulia hali, Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein katika makazi yake Unguja, Zanzibar, leo tarehe 03 Januari, 2026.

Circa, 2014Aliyekuwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimtambulisha mgombea wa nafasi ya uwakilishi wa Jimbo...
03/01/2026

Circa, 2014

Aliyekuwa Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimtambulisha mgombea wa nafasi ya uwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki Ndugu Mahmoud Thabit Kombo mara baada ya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kumteua kuwa mgombea wa nafasi uwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki kwa tiketi ya CCM.

Mahmoud sasa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Ndugu Nape ni Mbunge wa Jimbo la Mtama.

𝗖𝗛𝗨𝗒 𝗖𝗛𝗔 𝗨𝗧𝗔π—ͺπ—”π—Ÿπ—” π—ͺ𝗔 𝗨𝗠𝗠𝗔 (π—œπ—£π—”)𝗨π—ͺπ—˜π—žπ—”π—π—œ π—π—œπ—ͺπ—˜ π—Ÿπ—” π— π—¦π—œπ—‘π—šπ—œ π—žπ—”π—§π—œπ—žπ—” π—π—˜π—‘π—šπ—’ π—Ÿπ—” 𝗠𝗔𝗙𝗨𝗑𝗭𝗒 π—žπ—ͺ𝗔 π—ͺπ—”π—§π—¨π— π—œπ—¦π—›π—œMgeni rasmi: Mhe. Balozi Mahmo...
03/01/2026

𝗖𝗛𝗨𝗒 𝗖𝗛𝗔 𝗨𝗧𝗔π—ͺπ—”π—Ÿπ—” π—ͺ𝗔 𝗨𝗠𝗠𝗔 (π—œπ—£π—”)

𝗨π—ͺπ—˜π—žπ—”π—π—œ π—π—œπ—ͺπ—˜ π—Ÿπ—” π— π—¦π—œπ—‘π—šπ—œ π—žπ—”π—§π—œπ—žπ—” π—π—˜π—‘π—šπ—’ π—Ÿπ—” 𝗠𝗔𝗙𝗨𝗑𝗭𝗒 π—žπ—ͺ𝗔 π—ͺπ—”π—§π—¨π— π—œπ—¦π—›π—œ

Mgeni rasmi: Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

πŸ“† 04 Januari, 2026.
πŸ•°οΈ 02:00 Asubuhi.
πŸ“ Tunguu, Zanzibar.

03/01/2026

π—¦π—˜π—₯π—œπ—žπ—”π—Ÿπ—œ π—žπ—¨π—π—˜π—‘π—šπ—” 𝗠𝗔𝗕π—ͺ𝗔π—ͺ𝗔 𝗬𝗔 π—žπ—¨π—›π—œπ—™π—”π——π—›π—œ π— π—”π—π—œ 𝗬𝗔 𝗠𝗩𝗨𝗔.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imeanza mikakati ya ujenzi wa mabwawa
ya kuhifadhi maji ya katika mikoa ya Morogoro na Dodoma ambayo yatasaidia kukabiliana na changamoto ya mafuriko yanayotokana mvua.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa hayo imeshafanyika na ujenzi utaanza pindi kazi ya upembuzi yakinifu itakapokamilika.

Ametoa kauli hiyo Januari 02, 2026 wakati alipokagua athari zilizotokana na mvua katika mikoa ya Morogoro na Dodoma.

π——π—žπ—§. 𝗠π—ͺπ—œπ—šπ—¨π—Ÿπ—¨ π—”π—žπ—”π—šπ—¨π—” π— π—”π—˜π—‘π——π—˜π—Ÿπ—˜π—’ 𝗠π—₯π—”π——π—œ π—ͺ𝗔 𝗕π—ͺ𝗔π—ͺ𝗔 π—Ÿπ—” π— π—”π—π—œ π—žπ—œπ——π—¨π—‘π——π—”Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagu...
02/01/2026

π——π—žπ—§. 𝗠π—ͺπ—œπ—šπ—¨π—Ÿπ—¨ π—”π—žπ—”π—šπ—¨π—” π— π—”π—˜π—‘π——π—˜π—Ÿπ—˜π—’ 𝗠π—₯π—”π——π—œ π—ͺ𝗔 𝗕π—ͺ𝗔π—ͺ𝗔 π—Ÿπ—” π— π—”π—π—œ π—žπ—œπ——π—¨π—‘π——π—”

Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Bwawa la Maji Kidunda lililopo Mkoani Morogoro.

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Dkt. Mwigulu amesema kuwa mradi huo unaakisi maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha nchi inakabiliana na changamoto ya upungufu wa maji hasa kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

Pia, ameiagiza Wizara ya Maji kuhakikisha mradi huo hausimami na unakamilika kwa wakati ili uanze kutoa huduma ya maji kwa wananchi.

π——π—žπ—§. 𝗠π—ͺπ—œπ—šπ—¨π—Ÿπ—¨ π—”π—­π—¨π—‘π—šπ—¨π— π—­π—” 𝗑𝗔 π—ͺπ—”π—‘π—”π—‘π—–π—›π—œ π—ͺπ—”π—Ÿπ—œπ—’π—”π—§π—›π—œπ—₯π—œπ—ͺ𝗔 𝗑𝗔 𝗠𝗩𝗨𝗔 π—žπ—œπ—Ÿπ—’π—¦π—”- Autaja mradi wa ujenzi wa mabwawa ya kuhifadhi maji ya ...
02/01/2026

π——π—žπ—§. 𝗠π—ͺπ—œπ—šπ—¨π—Ÿπ—¨ π—”π—­π—¨π—‘π—šπ—¨π— π—­π—” 𝗑𝗔 π—ͺπ—”π—‘π—”π—‘π—–π—›π—œ π—ͺπ—”π—Ÿπ—œπ—’π—”π—§π—›π—œπ—₯π—œπ—ͺ𝗔 𝗑𝗔 𝗠𝗩𝗨𝗔 π—žπ—œπ—Ÿπ—’π—¦π—”

- Autaja mradi wa ujenzi wa mabwawa ya kuhifadhi maji ya Mvua eneo la Kidete.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amezungumza na wakazi wa Tindiga wilaya ya kilosa mkoani Morogoro ambao wameathirika na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewaeleza wakazi hao kuwa Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ilishaanza mikakati ya kukabiliana na athari za mvua katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa morogoro kwa kutekeleza mradi wa ujenzi wa Mabwawa eneo la Kidete.

Amesema kuwa ujenzi wa mabwawa hayo ya maji yatakuwa ni suluhisho la kudumu ya mafuriko katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Morogoro.

Ameongeza kuwa kwa sasa mpango huo upo katika hatua za kitalaam ikiwemo kumpata mkandarasi. ”Fedha imepatikana kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa kwa sasa tunaendelea na taratibu za kitaalam, Wizara zinazohusika hakikisheni mnakamilisha taratibu hizo ili ujenzi uanze”

π——π—žπ—§. 𝗠π—ͺπ—œπ—šπ—¨π—Ÿπ—¨ π—”π—žπ—”π—šπ—¨π—” 𝗔𝗧𝗛𝗔π—₯π—œ 𝗭𝗔 𝗠𝗩𝗨𝗔, π—žπ—œπ——π—˜π—§π—˜Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua hali ya athari ...
02/01/2026

π——π—žπ—§. 𝗠π—ͺπ—œπ—šπ—¨π—Ÿπ—¨ π—”π—žπ—”π—šπ—¨π—” 𝗔𝗧𝗛𝗔π—₯π—œ 𝗭𝗔 𝗠𝗩𝗨𝗔, π—žπ—œπ——π—˜π—§π—˜

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua hali ya athari iliyosababishwa na mvua katika eneo la kidete, Kilosa mkoani Morogoro.

Akiwa eneo hilo Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewahakikishia wakazi wa eneo hilo kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ilishachukua hatua za kukabiliana na mvua kwa kuamua kujenga mabwawa katika eneo hilo.

Salamu za Pole | 02 Januari, 2026
02/01/2026

Salamu za Pole | 02 Januari, 2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amtembelea na kumjulia hali, Makamu...
02/01/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amtembelea na kumjulia hali, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal, katika makazi yake Masaki Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Januari 2026.

Address

Bagamoyo
61305

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari za Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share