Habari za Zanzibar

Habari za Zanzibar Ukurasa utakaokupa habari mbalimbali kutoka Zanzibar na Ulimwenguni kote.

Rais wa Taasisi ya Kupambana na Rushwa nchini Comoro (Chambre anti-corruption) Bi Fahamoue Youssouf akiambatana na maafi...
16/11/2025

Rais wa Taasisi ya Kupambana na Rushwa nchini Comoro (Chambre anti-corruption) Bi Fahamoue Youssouf akiambatana na maafisa wake amewasili Dar es salaam kwa ziara ya kikazi kwa mwaliko wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) Ndugu Crispin Chalamila.

Ziara hiyo imeratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro ambapo Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Balozi Saidi Yakubu aliwakaribisha Tanzania na kuwaeleza namna ziara hiyo itakavyokuza ushirikiano katika eneo la utawala bora.

Wakiwa nchini, Bi. Fahamoue Youssouf anatarajiwa kufanya mazungumzo na mwenyeji wake, Ndugu Chalamila na kujifunza namna TAKUKURU wanavyofanya kazi na pia kuainisha maeneo ya ushirikiano wa Comoro na Tanzania katika vita dhidi ya Rushwa.

Officials on Notice to Prioritize People-first Leadership_________________• Tanzania’s president Samia Suluhu Hassan has...
16/11/2025

Officials on Notice to Prioritize People-first Leadership
_________________

• Tanzania’s president Samia Suluhu Hassan has vowed to form a government that is fully accountable to citizens and to carry forward bold policy reforms benefiting everyday Tanzanians.

• ⁠She directed leaders at all levels stay close to the people, accelerate problem-solvings and meet public expectations.

• ⁠With promises vast and time short, the president stressed urgency in delivering results, warning that if officials do not adapt to serve the people, they will be replaced.



Mother’s Appeal to Youth as Nation Builders________________• Speaking as “Mother of the Nation,” Tanzania’s president Sa...
16/11/2025

Mother’s Appeal to Youth as Nation Builders
________________

• Speaking as “Mother of the Nation,” Tanzania’s president Samia Suluhu Hassan reached out to the youth with both compassion and conviction.

• ⁠She acknowledged that many young people caught up in the recent unrest “did not know what they were doing” and directed authorities to drop charges against those misled into offenses.

• ⁠Citing forgiveness, she implored Tanzania’s young generation never to destroy their own country, urging them instead to safeguard peace.

• ⁠“This nation is yours,” she reminded, calling on youth to be guardians and builders of the nation, not destroyers



16/11/2025

VIDEO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, akishiriki katika Mkutano wa Tisa wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR), uliyofanyika, Jijini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

𝗞𝘂𝗹𝗶𝗻𝗴𝗮𝗻𝗮 𝗻𝗮  𝗪𝗮𝗿𝗮𝗸𝗮 𝘄𝗮 𝗕𝗮𝗿𝗮𝘇𝗮 𝗹𝗮 𝗠𝗮𝗮𝘀𝗸𝗼𝗳𝘂 𝗞𝗮𝘁𝗼𝗹𝗶𝗸𝗶 𝗧𝗮𝗻𝘇𝗮𝗻𝗶𝗮, 𝘇𝗶𝗳𝘂𝗮𝘁𝗮𝘇𝗼 𝗻𝗶 𝗵𝗲𝗸𝗶𝗺𝗮 𝗮𝗺𝗯𝗮𝘇𝗼 𝘇𝗶𝗻𝗴𝗲𝘄𝗲𝘇𝗮 𝗸𝘂𝘁𝘂𝗺𝗶𝗸𝗮 Moja,  K**a ...
16/11/2025

𝗞𝘂𝗹𝗶𝗻𝗴𝗮𝗻𝗮 𝗻𝗮 𝗪𝗮𝗿𝗮𝗸𝗮 𝘄𝗮 𝗕𝗮𝗿𝗮𝘇𝗮 𝗹𝗮 𝗠𝗮𝗮𝘀𝗸𝗼𝗳𝘂 𝗞𝗮𝘁𝗼𝗹𝗶𝗸𝗶 𝗧𝗮𝗻𝘇𝗮𝗻𝗶𝗮, 𝘇𝗶𝗳𝘂𝗮𝘁𝗮𝘇𝗼 𝗻𝗶 𝗵𝗲𝗸𝗶𝗺𝗮 𝗮𝗺𝗯𝗮𝘇𝗼 𝘇𝗶𝗻𝗴𝗲𝘄𝗲𝘇𝗮 𝗸𝘂𝘁𝘂𝗺𝗶𝗸𝗮

Moja, K**a ilivyoandikwa kwenye kitabu cha Mathayo 5:9

Mt 5:9 SUV
Neno la Mungu linasema.. [9] Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

K**a Kanisa ni muhimu kujua nafasi yake kwenye jamii kwa kusimama kuwa wapatanishi wa Serikali na Wananchi, kuliko kusimama upande wa wananchi peke yake k**a waraka wao ulivyosema. Kwa sababu nafasi ya Kanisa kwenye jamii sio kuwasemea wananchi au kuisemea Serikali bali kufanyika daraja kati ya pande zote mbili.

Vile vile, Kanisa huchangia kuwa na Jamii bora kwa kusaidia kutii sheria, uadilifu, kufanya kazi kwa bidii, na kuwa raia waaminifu.


Pili, TEC walitakiwa kuomba nafasi ya kukutana na Serikali na kutoa mapendekezo yao.

Katika Kitabu cha Yakobo 3:17-18
Yak 3:17-18 SUV
Neno la Mungu linasema..

[17] Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, TAYARI KUSIKILIZA MANENO YA WATU, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki. Na tunda la haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.

K**a Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania wakiwa ni wawakilishi wa Kanisa Katoliki, wangeomba nafasi ya kukaa pamoja na Serikali ili watoe mapendekezo yao kufuatia kilichotokea ili kuweza kuijenga Nchi kwa pamoja. Hakuna njia nyingine ambayo Kanisa imepewa kwenye maandiko ya kuhusiana na tawala na uongozi mbalimbali isipokuwa kwa NJIA YA HEKIMA.

Na hii ndio njia ya hekima ambayo tunaisoma katika Maandiko matakatifu ya Mungu, Kitabu cha Waefeso 3:10 – yanayosema..

Efe 3:10 SUV
[10] ili sasa, KWA NJIA YA KANISA, HEKIMA YA MUNGU iliyo ya namna nyingi IJULIKANE NA FALME NA MAMLAKA katika ulimwengu wa roho.

Tatu, Uponyaji wa kweli unaanzia kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.

Katika Kitabu cha 2 Wakorintho 5:19 - Neno la Mungu linasema..

[19] yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.

Watu wote walioumiza na walioumizwa ni Watu wa Mungu. Wote wanahitaji msaada wa Mungu ili kuwafanya wawe bora. Ianzie Kanisani kwenye kuwasaidia watu kupona majeraha ya ndani kuliko kuchochea chuki dhidi ya Taifa lao. Tanzania itajengwa na watanzania wenye mioyo iliyo na matumaini makubwa kwa Mungu juu ya maendeleo ya nchi yao.

Nne, Mamlaka zote zinatoka kwa Mungu, hivyo ni tendo la Imani pia kuiachia Serikali mpya ya Awamu ya 6 kushughulika na yote ambayo Mheshimiwa Rais aliyasema kwenye Hotuba yake alipokuwa akifungua Bunge ikiwa ni jitihada zao katika kuliunganisha Taifa letu na kuijenga Tanzania moja.

K**a ambavyo tumekuwa tukiwaeleza tangu awali, Serikali hii ya Awamu ya 6 ni Serikali sikivu na Serikali inayojali, hasa kwa wakati huu tunapotafuta kujenga na kuponya majeraha tuliyopata k**a ambavyo Mheshimiwa Rais alivyosema kwenye hotuba yake alipokuwa akifungua Bunge.

Mtu yoyote akisikiliza kwa umakini Hotuba ya Mheshimiwa Raisi atagundua nia yake ya dhati kwenye kuikumbatia nchi nzima k**a mama na makundi yake yote, yakiwemo makundi yaliyoathiriwa na changamoto zilizotokea wakati wa uchaguzi.

Hakuna ambaye angependa kuongoza Taifa ambalo limegawanyika au linamaumivu, na ndio maana Mheshimiwa Rais aliweka wazi kuwa ameamua kuunda TUME MAALUMU itakayochunguza yote yaliyotokea kwenye uchaguzi na KILA ALIYEHUSIKA ATAWAJIBISHWA NA KUWAJIBIKA KATIKA NGAZI ZOTE.

Tumeuona Waraka wa Viongozi wa dini wa Kanisa Katoliki Wahashamu na Ma-Baba Askofu ambao sisi tunawaheshimu mnoo, na tunaamini yote waliyoyaandika ni kwasababu wameisikiliza Hotuba ya Mheshimiwa Rais na ndio maana yote ambayo wameyaeleza kwenye waraka huo, asilimia 70-90 Mheshimiwa Rais aliyazungumzia kwenye hotuba yake alipokuwa anafungua Bunge la 13, hivyo KANISA NA WANANCHI WOTE KWA UJUMLA waiamini Serikali yao kuwa inajali na inasikiliza na k**a ambavyo Mheshimiwa Rais alivyosema kwenye Hotuba yake tuone Rais na Serikali yake watakalolifanya baada ya kusikiliza Ripoti ya Tume itayoundwa na kuleta majibu ya kiuwajibikaji.

Bado nipo kwenye maumivu ya moyo juu ya kinachoendelea kwenye Kanisa langu KATOLIKI.

Kila siku zinavyokwenda naona tunalizamisha Kanisa letu na kuendelea kuwagawa Waumini na kanisa kiujumla na kupelekea udini ndani ya nchi yetu.

Hili si Kanisa ninalolijua, lililotupa mafunzo ya unyenyekevu na utii kwa Mamlaka za Nchi.

Hili si Kanisa langu ninalolipenda kwa miaka yote 47 ya umri wangu.

Kanisa letu linatoka kwenye mstari kila kukicha na linatoka kwenye kazi ya kutibu roho zetu na linaenda kuumiza na kizichana roho zetu.

Kanisa letu limetoka kuwa Kanisa la Mungu na Mkakati wa kuwapika, kuwajenga Vijana kuwa Viongozi bora kabisa Nchini k**a lilivyofanya kwa Viongozi wetu na Wazee wetu k**a Mwalimu Nyerere, Mzee Mkapa, Wazee wetu kina Simbakalia, Profesa Mahalu, Bernard Membe na wengine wengi sana ambao kanisa liliwalea, kuwafunza na kuwajenga kuwa Viongozi waliotukuka kwenye Taifa leo.

Namuonea huruma sana Kaka yangu Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, Makamu wa Rais wa sasa ambaye ni Mkatoliki safi kwa namna anavyopitia haya yanayotoka kwenye Kanisa letu tunalolipenda.

Kanisa lina Makamu wa Rais ambaye wamemlea na kumkuza wenyewe. Kwa njia zingine tunasema wana Direct contact ndani ya Viongozi wakuu kwenye Nchi akiwa ni namba mbili. Najua na nakupa pole sana Daktari Emanuel Nchimbi maana haya yanayofanywa na Kanisa letu yanakuumiza na kukukwaza mno ila kwa kuwa Kanisa letu limetoka kuwa Kanisa la KIMKAKATI wa kuwafunda na Kuwajenga VIONGOZI na kugeuka kuwa Kanisa la UWANAHARAKATI la kuwabomoa Viongozi wa Serikali na kuwagawa Waumini wao na Wananchi kwa Ujumla. Yani limegeuka Kanisa la kupingana na Serikali. HILI LINALITIA AIBU KANISA LETU.

Kanisa hili ni letu na siyo la Maaskofu peke yao. Haya yanayoendelea kwenye Kanisa letu k**a itafanyika takwimu za haki na ukweli basi nina uhakika Kanisa hili limepoteza na litapoteza Waumini wengi mno kuliko kipindi chochote kilichowahi kutokea Nchini kwetu. Na haya yamewahi kutokea Nchini Kenya, Uganda, DRC, Burundi, Rwanda na kwengineko ambapo leo hii kwenye Nchi zote hizo nilizozitaja Kanisa limepoteza nguvu yake kwasababu ya kujiingiza kwenye Siasa na tena siasa za Kiuwana-harakati. Hili linapaswa kulindwa ndani ya kanisa letu Katoliki lisitokee hapa TANZANIA. Heshima ya Kanisa hili ni kubwa sana tusikubali kupelekwa tunakopelekwa.

WAPI VIONGOZI WETU WA KIROHO MNATUPELEKA?

Haya ndiyo yale mafunzo ya hili KANISA?

WAKATOLIKI TUAMKE NA TUZINDUKE KULINDA HESHIMA YA KANISA LETU NA KURUDI KWENYE MSTARI WETU WA KULILEA TAIFA HILI.

𝗕𝗔𝗥𝗔𝗭𝗔 𝗟𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗦𝗞𝗢𝗙𝗨 (𝗧𝗘𝗖) 𝗠𝗡𝗔𝗧𝗨𝗞𝗢𝗦𝗘𝗔 𝗦𝗔𝗡𝗔 𝗪𝗔𝗞𝗔𝗧𝗢𝗟𝗜𝗞𝗜.Tumsifu Yesu Kristo.Jina langu ni Joseph Simon Mapunda, Muumini wa K...
16/11/2025

𝗕𝗔𝗥𝗔𝗭𝗔 𝗟𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗦𝗞𝗢𝗙𝗨 (𝗧𝗘𝗖) 𝗠𝗡𝗔𝗧𝗨𝗞𝗢𝗦𝗘𝗔 𝗦𝗔𝗡𝗔 𝗪𝗔𝗞𝗔𝗧𝗢𝗟𝗜𝗞𝗜.

Tumsifu Yesu Kristo.

Jina langu ni Joseph Simon Mapunda, Muumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga Mkoani Ruvuma ambaye kwa mapenzi ya Mungu mwaka jana 2024 nilikuja Dar es Salaam kikazi na naishi Tegeta.

Leo tarehe 15 Novemba, 2025 nimesoma andiko la Baraza la Maaskofu lililoitwa “Tafakari ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Juu ya Yaliyotokea Siku na Baada ya Uchaguzi-2025”

Awali ya yote kabisa naomba kuchukua nafasi hii kutoa pole za dhati kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wote waliopoteza ndugu zao katika vurugu zilizotokea tarehe 25 Oktoba, 2025 na siku zilizofuata wakati ambapo nchi yetu Tanzania ilijikuta katika matukio ambayo hayajawahi kutokea na hayafanani kabisa na utamaduni wa Watanzania. Matukio mageni haswa.

Naungana na Watanzania wote kuwaombea Marehemu wote wapumzike mahali pema peponi na majeruhi wote wapone haraka.

Napenda pia kuwapa pole wote waliopoteza mali zao, walipoteza biashara zao, walipoteza ajira zao na ambao wanapitia kipindi kigumu cha giza nene kutokana na kupoteza kipato ambacho kiliendesha maisha yao na familia zao ama wapendwa wao.

Kwa wale ambao wamehusika na uhuni huu ama kwa kuchochea ama kwa kutekeleza matukio ya uharibifu wa miundombinu ya umma, wizi wa mali za watu binafsi na umma, uchomaji moto wa majengo, magari na biashara za watu mbalimbali, Mwenyezi Mungu mwenye kutoa haki awape wanachostahili.

Naomba nirudi kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), bila kupepesa macho naomba kusema wazi nasikitishwa sana na mwenendo wa TEC kutoa matamko na maandiko ambayo badala ya kuponya Taifa yanachochea mgawanyiko, uhasama na kuligombanisha Kanisa na Serikali. Ni kweli Maaskofu ndio viongozi wakuu wa majimbo ya Kanisa Katoliki lakini ni muhimu Mababa Askofu mkaheshimu demokrasia na haki ya waumini wa Kanisa Katoliki kwa kutofanya mambo ambayo yanatokana na matakwa yenu, hayana baraka za waumini na yanawaharibia waumini wa Kanisa hili lenye heshima kubwa hapa Tanzania na ambalo limejengwa kwa jasho jingi la Watanzania vizazi na vizazi.

Nimeona mara kadhaa mnavyotoa matamko yenye vinasaba vya Kisiasa ambayo hakuna asiyejua kuwa yana mwelekeo wa siasa za upinzani na yanalenga kuishambulia Serikali. Sina tatizo na hoja mnazojenga lakini muhimu hapa kwa nini mnatumia Kanisa kufanya minyukano ya Kisiasa? Sisi Wakatoliki tumejenga Kanisa hili ili litupe huduma za kiroho, lihubiri Injili, lituweke pamoja na lidumishe amani na upendo kwa mwanadamu. Mnayoyafanya mnakiuka misingi hii.

Matukio yaliyotokea tarehe 29 Oktoba, 2025 na siku kadhaa za mbele hakuna yaliyemfurahisha, kwa nini nyie TEC mnaibuka na andiko la namna hii tena siku moja baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kutoa hotuba ya kuwaunganisha Watanzania, ya kuhimiza amani na utulivu, ya kujibu hoja za vijana na ya kuendeleza mkono wa maridhiano? Kwa nini Kanisa langu mnafanya mambo haya?

Tuseme Waumini wa Kanisa Katoliki na wanaopendezwa na mambo yanayoendelea nchini watawashangilia na kwa kuwa kuna kampeni ya mitandaoni ya kuitisha maandamano tarehe 9 Desemba, 2025 ili wajitokeze tena kupambana na vyombo vya dola k**a ilivyokuwa tarehe 29 Oktoba, 2025, mnataka watu wengine wauawe? hata wale ambao hawahusiki na uchochezi huu? Mnataka watu wengine waingie kwenye umasikini kwa biashara zao kuvamiwa, kuibiwa, kuharibiwa na kuchomewa moto? Au tuseme mnataka nchi iingie katika mapinduzi? Hamzijui gharama za mapinduzi?

Nimesoma andiko lenu mstari kwa mstari. Nataka niwaulize hoja chache kabisa na nyie mtafakari huku mkiongozwa na Roho Mtakatifu na roho wa haki;

1. Hivi Mababa Askofu kwenye andiko lenu mnasema tarehe 29 Oktoba, 2025 waandamaji walishambuliwa na kuuawa. Naomba kuuliza wale walikuwa waandamanaji au waleta vurugu, wezi na waharibifu wa mali za umma? Nyie mmetembea nchini nyingi Duniani, watu wanaoandamana huwa wanafanya vitendo ambavyo vilifanyika siku ile? Waandamaji wanakwenda kuwatia umasikini binadamu wenzao na kutishia maisha yao au wanakwenda kudai haki zao kwa watawala? Mababa Askofu mnafahamu kuwa hao mnaowaita waandamanaji walikuwa na silaha za moto na wameua askari polisi ambao walikuwa wanakabiliana nao walipokuwa wanakwenda kuvamia mali za watu kuvunja na kuiba? Mnafahamu hao watu wameua watu wasio na hatia wakijiita ni Askari?

2. ⁠Mababa Askofu mnajua kuwa hao mnaowaita waandamanaji walivamia vituo vya polisi ili kuchukua silaha na walipozikosa walivichoma moto vituo vya polisi vingi? mababa Askofu ina maana hamjuia madhara ya makundi ya wahuni kuchukua silaha na kuvamia watu na biashara zao? Mlitaka Askari wafanyeje? Nyie wenyewe nyumba zenu mmeweka Askari wenye silaha, leo watu waje kuvamia nyumba ya Askofu wachome moto na kisha waanze kutaka kuingia ndani hao Askari wenu watawaacha?

3. ⁠Mababa Askofu mnafahamu kuwa hao mnaowaita Waandamanaji walikwenda kuchoma moto jengo la Mawasiliano ambalo sio tu lingesababisha kuzimwa kwa mawasiliano yote bali nchi ingekosa mawasiliano kwa asilimia 100 kwa muda usiojulikana. Mnajua kuwa watu hao walishachoma eneo la mapokezi na jengo hilo liliokolewa na Askari Zimamoto waliowahi kabla ya moto kusambaa. Mnajua madhara ambayo yangetokea kwa nchi kukosa mawasiliano kabisa? Madhara kwa huduma za kifedha, mapato ya Serikali, huduma za matibabu hospitali, elimu na biashara zao watu.

4. ⁠Mababa Askofu mnafahamu kuwa hao mliowaita waandamanaji wamechoma moto vituo vya mafuta. Hamjui madhara ya kituo cha mafuta kikiungua hadi kufika hatua ya kulipuka?

5. ⁠Mababa Askofu mnahamu kuwa uharibifu wa miundombinu ya mwendokasi umesababisha huduma hiyo kusitishwa? Mnajua madhara yake? Kwa sababu nyie hamsafirii usafiri wa umma, mnatumia magari binafsi ambayo sisi waumini tumewanunulia.

6. ⁠Mababa Askofu mnafahamu kuwa vijana waliokuwa wanapambana kutafuta kipato wamefirisika na hivi sasa wanakosa mpaka pesa ya kununua chakula cha watoto wao majumbani kwa sababu hao mnaowaita waandamanaji wamewaibia na kuharibu kabisa biashara zao?

7. ⁠Mababa Askofu mnafahamu madhara mengine mengi ambayo k**a Nchi tunayapitia kutokana na vurugu zile?

Mababa Askofu hamuoni kuwa sio sawa kwa chombo hiki cha Dini, cha Kanisa Katoliki kubeba ajenda za chama cha upinzani ambacho kimeamua kutoshiriki uchaguzi ambao ni takwa la kikatiba ili kihamasishe watu kuleta vurugu ndani ya nchi? Kwani mkitoa tamko la kujenga imani za watu, watu kumrudia Mungu, kutubu na kujisahihisha pamoja kuhamasisha amani, upendo na utulivu mtapungukiwa nini?

Sawa, sasa mnatwambiaje Wakatoliki tujiandae kwa majambia, visu shoka, mawe na manati ili tukapambane na Polisi wenye silaha na JWTZ tarehe 9 Desemba, 2025 ili mje muandike tafakari nyingine ya TEC au mtatuletea bunduki, mabomu na mizinga ya kukabiliana na dola inayosimamia utawala wa Sheria?

Rais kaunda tume ya kuchunguza chanzo cha vurugu na kutoa mapendekezo ya namna ya kushughulikia mambo yaliyojitokeza tarehe 29 Oktoba, 2025 na nyie mmetoa tamko siku inayofuata, kwa hiyo mnataka sisi Wakatoliki tumsikilize Rais au tuwasikilize nyinyi TEC? Kwa nini mnataka kushindana na Rais? Hii nchi inaongozwa na TEC au inaongozwa na Serikali ambayo imewekwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi?

K**a na nyie TEC mnataka kuwa viongozi wa kisiasa kwa nini msiwe mnagombea nafasi za kisiasa k**a wanavyofanya viongozi wa madhehebu mengine ya Kikristo? Ili nanyi muwe na haki na mamlaka ya kiuwakilishi. Maana hivi mnavyofanya mnapaswa kuulizwa ni wananchi wanawatuma au mnajituma wenyewe?

Hamkuanza tabia hizi leo, mlifanya sana wakati wa tawala zilizopita. Hivi mmewahi kuwaza viongozi wa Serikali ambao ni Wakatoliki tena wengine ni wasaidizi wa karibu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mnawaweka katika mazingira gani? Hebu vaeni viatu vya Makamu wa Rais Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye ni Mkatoliki, Wasaidizi katika Ofisi Binafsi ya Rais ambao ni Wakatoliki na wanakuja kusali kwenye Ibada ambazo nyie mnaacha kuhubiri Injili na mnaanza kuhubiri hoja za Vyama vya Siasa, wanajisikiaje hawa?

Naomba kuwauliza TEC, kwa nini hamkusubiri Tume ya Uchunguzi ifanye kazi kisha ilete majibu? Mnajua tume itakuja na majibu gani? Hivi ikija na majibu ya sababu za msingi za namna vyombo vilivyokabiliana na matukio yale, mtabadilisha andiko na tamko lenu?

Mababa Askofu ina maana hamjui kuwa kinachoendelea ni ushawishi mkubwa wa watu wasioitakia mema Tanzania?

Mababa Askofu hamsikii hoja za kwamba mnaipiga vita Serikali hii kwa sababu Rais sio Mkatoliki? Kwamba mmeshaona Kanisa Katoliki ndio pekee lenye haki ya kuweka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Labda niulize Rais Samia amefanya mangapi ambayo huko nyuma Kanisa Katoliki lilinyimwa? Hivi mnadhani Serikali ikikunjua makucha Kanisa litabaki salama? Mmesahau jinsi Hayati Rais Magufuli alivyowashughulikia? Mmesahau jinsi Rais Samia alivyowasaidia? Kwa nini mnafanya mipango ya kumkwamisha huyu Mama Rais Samia. Amekosa nini?

Hayo madai ya wanasiasa ambayo na nyinyi mmefanya ajenda yenu hamjui majibu yake?

Hamjui k**a Rais Samia ameahidi katika kipindi cha miaka mitano tutapata Katiba mpya? Hamjasikia ahadi ya maridhiano? Hamjasikia mipango ya mageuzi ya kiuchumi? Hamna ufahamu na falsafa ya R nne na namna ambavyo Rais Samia ameanza kuzitekeleza?

Mababa Askofu hamjui namna ambavyo Serikali ya Awamu ya Sita imechukua hatua madhubuti za kujenga uchumi na kukuza kipato cha Watanzania? Hamjui namna ambavyo Rais Samia ameongeza fursa za ukuaji wa demokrasia, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kisiasa na uhuru wa masuala mengine mengi? Mmesahau jinsi mambo haya yalivyobanwa wakati wa utawala wa Mkatoliki mwenzetu Hayati Dkt. John Pombe Magufuli?

Naomba kuwasihi, msitukwaze Wakatoliki, msiwagombanishe Watanzania na Serikali yao, msiwe chanzo cha machafuko ya nchi. Nawasihi kwa unyenyekevu, fanyeni jitihada za kuliunganisha Taifa, na k**a haiwezekani basi kaeni kimya muache Wadau wengine waunganishe Taifa.

Mwacheni Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aongoze Tanzania, acheni Tanzania idumishe amani na waacheni Watanzania waamue wanataka nchi iendaje.

Naiomba Serikali isisite kuchukua hatua kali dhidi ya viongozi wa Kanisa Katoliki ambao wanatupeleka katika mwelekeo huu. Mimi ni Mkatoliki, najua sio viongozi wote wa Kanisa hili wanafurahishwa na mwenendo huu, najua najua ubabe na utamaduni usio wa kidiplomasia ndani ya Kanisa unaficha sauti za Wakatoliki ambao wanatofautiana na msimamo wa NEC. Acheni kufanya hivyo viongozi wangu, mnatukwaza waumini.

Kaeni mbali na siasa na pambaneni na kueneza Injili na kuunganisha watu wa Mungu. Sambazeni upendo na usuluhishi, tangazeni amani na upendo na muwe na furaha pale nchi inapokuwa na amani.

Tumsifu Yesu Kristo.

15/11/2025

Tamko la Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mhe. Felix Tshisekedi, akimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ushindi alioupata katika uchaguzi uliyofanyika mwezi Oktoba 2025.

Pongezi hizo zimetolewa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tisa wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) uliyofanyika Jijini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Leo tarehe 14 Novemba 2025.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazotarajia kunufaika na fedha kiasi cha hadi dola milioni 20 kwa ajili ya utekelezaji w...
15/11/2025

Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazotarajia kunufaika na fedha kiasi cha hadi dola milioni 20 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kupitia Mfuko wa Kukabiliana na Hasara na Uharibifu.

Hayo yamesemwa na Mshauri wa Rais katika masuala ya Mazingira na Mwenyekiti wa Kundi la Majadiliano la Afrika kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (AGN) Dkt. Richard Muyungi alipokutana na Watanzania wanaoshiriki Mkutano wa Mkutano wa 30 wa Umoja wa Mataifa wa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP 30) unaoendelea katika Jiji la Belem nchini Brazil.

Dkt. Muyungi amesema kuwa katika utekelezaji huo tayari zimetengwa fedha kiasi cha dola milioni 250 kwa mwaka ujao kwa kwa ajili ya kufadhili miradi hiyo ambayo Tanzania ni nchi mnufaika.

“Nasisitiza huu sio mkopo bali ni ufadhili na hadi sasa tuna mambo ya kufuatilia na sisi k**a nchi tumepewa kipaumebele hivyo tunaweza kuwa na miradi hata miwili ambayo inaweza kuwa na manufaa makubwa, naomba Ofisi ya Makamu wa Rais tuteua mtu mmoja yaani focal person kwa ajili ya Mfuko wa Kukabiliana na Hasara na Uharibifu,” amesema.

Kubwa zaidi amebainisha kuwa mwaka 2025 Tanzania imeteuliwa kuwa Kituo cha Santiago ambacho kitakuwa kinaratibu msaada wa kiufundi kwa nchi zinazoathiriwa na hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi.

Aidha, Dkt. Muyungi ameomba Watanzania kutoka serikalini na sekta binafsi wanaoshiriki mkutano huo wenye takriban washriki 60,000 kusimama k**a nchi na kujenga mitandao ya kuchangamkia fursa ili kuendelea kuinufaisha nchi.

“K**a tunavyoona hapa COP 30 yapo mabanda mengi yenye wingi wa washiriki nawaomba tutumie fursa hii kutengeneza network, tuna timu ya negotiation tufuatilie fursa za benki , NGOs na Serikali ili tukitoka hapa tutoke na faida,” amesisitiza.

Vilevile, Dkt. Muyungi alitumia nafasi hiyo kuwaeleza washiriki hao kuwa wana jukumu la kuitangaza Dira ya Maendeleo 2025 na Serikali ya Tanzania imetekeleza mambo gani ya msingi kwa wananchi na hivyo kuchagiza upatikanaji wa fursa zaidi kwa maendeleo endelevu

Makamu wa Rais

15/11/2025

Maagizo ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba kwa hospital zote nchini, baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kwenye Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma leo Novemba 15, 2025.

𝗪𝗔𝗭𝗜𝗥𝗜 𝗠𝗞𝗨𝗨 𝗔𝗙𝗔𝗡𝗬𝗔 𝗭𝗜𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗦𝗛𝗧𝗨𝗞𝗜𝗭𝗔 𝗛𝗢𝗦𝗣𝗜𝗧𝗔𝗟𝗜 𝗬𝗔 𝗠𝗞𝗢𝗔 𝗪𝗔 𝗗𝗢𝗗𝗢𝗠𝗔▪️𝗔𝘁𝗼𝗮 𝗺𝗮𝗮𝗴𝗶𝘇𝗼 𝗸𝘄𝗮 𝗪𝗶𝘇𝗮𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝗔𝗳𝘆𝗮, 𝗠𝗦𝗗 𝗻𝗮 𝗵𝗼𝘀𝗽𝗶𝘁𝗮𝗹𝗶 𝘇𝗼...
15/11/2025

𝗪𝗔𝗭𝗜𝗥𝗜 𝗠𝗞𝗨𝗨 𝗔𝗙𝗔𝗡𝗬𝗔 𝗭𝗜𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗦𝗛𝗧𝗨𝗞𝗜𝗭𝗔 𝗛𝗢𝗦𝗣𝗜𝗧𝗔𝗟𝗜 𝗬𝗔 𝗠𝗞𝗢𝗔 𝗪𝗔 𝗗𝗢𝗗𝗢𝗠𝗔

▪️𝗔𝘁𝗼𝗮 𝗺𝗮𝗮𝗴𝗶𝘇𝗼 𝗸𝘄𝗮 𝗪𝗶𝘇𝗮𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝗔𝗳𝘆𝗮, 𝗠𝗦𝗗 𝗻𝗮 𝗵𝗼𝘀𝗽𝗶𝘁𝗮𝗹𝗶 𝘇𝗼𝘁𝗲 𝗻𝗰𝗵𝗶𝗻𝗶.

▪️𝗪𝗮𝗴𝗼𝗻𝗷𝘄𝗮 𝘄𝗮𝗶𝗽𝗼𝗻𝗴𝗲𝘇𝗮 𝗦𝗲𝗿𝗶𝗸𝗮𝗹𝗶 𝗸𝘄𝗮 𝗸𝘂𝗯𝗼𝗿𝗲𝘀𝗵𝗮 𝗵𝘂𝗱𝘂𝗺𝗮 𝘇𝗮 𝗮𝗳𝘆𝗮

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 15, 2025 amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kuziagiza hospitali zote nchini zihakikishe wajawazito wanapofika hospitali wahudumiwe kwa haraka ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizaya ya Afya, Bohari ya Dawa (MSD) na Hospitali zote nchini ziweke vipaumbele vya kuwa na dawa kulingana na mahitaji ya eneo husika. “ Haipendezi mwananchi kufika hospitali na kupatiwa vipimo vyote kisha anaambiwa dawa akanunue kwingine, k**a duka binafsi linaweza kupata dawa hizo, inawezekanaje hospitali za serikali hapati? Naagiza Hospitali zote ziwe na dawa.”

Ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi nje ya hospitali hiyo baada ya kutembelea wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma mbalimbali za kitabibu ambapo amesisitiza wananchi waendelee kuhudumiwa vizuri kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini vikiwemo vifaa tiba na dawa.

Kadhalika Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe zinakuwa na vifaa vya usafi binafsi vya dharura vikiwemo ndoo na beseni katika wodi za wazazi ili viwasaidie akinamama wasiokuwa na vifaa hivyo. “Ujauzito sio suala la dharura vifaa k**a ndoo tunapaswa kuwa navyo katika hospitali zetu za serikali.”

Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika uboreshaji wa huduma za afya nchini. Waziri Mkuu akiwa hospitalini hapo, wananchi walimueleza kuwa wanahudumiwa vizuri na kwa uangalizi wa karibu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zizingatie maelekezo ya kutumia mifumo sahihi ya malipo katika taratibu za kutoa huduma ili kuwezesha Serikali kuendelea kuhudumia wananchi.

Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo kufuatia kuwepo kwa hospitali ambazo baadhi ya huduma wanapokea malipo kwa njia ya mtandao na nyingine malipo yanapokelewa malipo kwa njia zisizo rasmi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wagonjwa na wananchi wanaoguza ndugu zao wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za afya.

“Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa tunapatiwa huduma nzuri k**a tupo hospitali za private (binafsi).” Kauli hiyo imetolewa na Dinna Enock, mkazi wa Makulu jijini Dodoma ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi.

15/11/2025

Tutaongeza kasi ya utekelezaji mipango ya serikali ili kufikia malengo tuliyojiwekea — Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan









15/11/2025

Serikali kuwezesha huduma za kibingwa za afya hospitali za rufaa za mikoa na kanda

Address

Bagamoyo
61305

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari za Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share