Radio Rumuli Fm 98.5 Bukoba

Radio Rumuli Fm 98.5 Bukoba A Christian Radio in Bukoba that intends to send God's word in the region.

09/12/2025

Jeshi la Polisi Tanzania limesema hali ya usalama nchini imeendelea kuwa shwari hadi kufikia mchana wa Desemba 9, 2025, siku ambayo baadhi ya watu wamepanga kufanya maandamano yanayodaiwa kuwa ya amani, huku Serikali na vyombo vya ulinzi na usalama vikisema maandamano hayo si halali.

Kwa mujibu wa taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime, vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kuimarisha hali ya usalama na kulinda maisha na mali za wananchi kote nchini.

Polisi imewataka wananchi kupuuza picha mnato na picha mjongeo zinazoenezwa mitandaoni zikidai kuwa maandamano yameanza sehemu mbalimbali za nchi, ikibainisha kuwa picha hizo ni za matukio ya zamani zikiwemo zile za Oktoba 29, 30 na 31, 2025.

 : Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ametangaza kujiuzulu wadhifa huo kupitia chapisho aliloliweka kwen...
13/07/2025

: Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ametangaza kujiuzulu wadhifa huo kupitia chapisho aliloliweka kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram.

Katika taarifa ya Polepole pamoja na mambo mengine amesema imekuwepo kauli maarufu ya CCM isemayo "Chama kwanza mtu baadaye", mwanzoni mwa mwaka huu, nilipoona kauli hii inafanyika vinginevyo, nimejiuliza mara kadhaa ni maslahi ya nani yanapiganiwa wakati huu, mtu, kikundi au Chama Taasisi?.

Amesema kuwa "kuwa siwezi kuendelea kuwa sehemu ya uongozi usiohamasika na utii wa misingi ya katiba ya nchi na chama, haki, maadili, utu na uwajibikaji kwa wananchi, nimeamua kwa hiari yangu kujiuzulu nafasi yangu ya uongozi na utendaji serikalini, nitaendelea kuwa mwana CCM wa kawaida, mzalendo na raia mwaminifu kwa Taifa na nchi yetu"Amesema Polepole.

Ameongeza kuwa "Ninamwamini Mungu wa Mbinguni na ninahamasika na tumaini kuu kwamba siku moja nchi yetu itaongozwa kwa misingi ya haki, maadili, usimamizi thabiti wa miiko na nidhamu ya uongozi, dhamira njema, siasa safi, uongozi bora na hofu ya Mungu"

Baraza la Mitihani la Tanzania leo tarehe 7/7/2025 limetangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita (ACSEE) na Mitihani...
07/07/2025

Baraza la Mitihani la Tanzania leo tarehe 7/7/2025 limetangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita (ACSEE) na Mitihani ya Ualimu iliyofanyika Mwezi Mei, 2025. Matokeo hayo yanapatikana kwenye tovuti ya NECTA: www.necta.go.tz

 : Baadhi ya Wakulima na Wafugaji, waliohudhuria Warsha ya Kilimo, iliyoandaliwa na wauzaji wa Pembejeo "Kilimo Kwanza",...
26/02/2025

: Baadhi ya Wakulima na Wafugaji, waliohudhuria Warsha ya Kilimo, iliyoandaliwa na wauzaji wa Pembejeo "Kilimo Kwanza", katika ukumbi wa St. Theresa, uliopo Manispaa ya Bukoba, mkoani Kagera, Februari 26, 2025.



10/11/2024

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasihi Viongozi wa Vyama vya Siasa vitakavyoshiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kuwa vinara katika kulinda amani na kukemea viashiria vyote vya uvunjifu wa amani.

Waziri Mkuu Majaliwa, ametoa wito huo Novemba 10, 2024, wakati alipomwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano Mkuu na Kongamano la Umuhimu wa Amani kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, jijini Dar es Salaam.

“Mheshimiwa Rais Dkt. Samia amewasihi Watanzania na viongozi wa dini kuendelea kuitangaza amani ndani na nje.”
“Hamasisheni wanachama wenu kushiriki katika uchaguzi huo huku wakizingatia kudumisha amani iliyopo. Wananchi wote waliojiandikisha katika orodha ya wapigakura wa Uchaguzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wajitokeze kwa wingi kupiga kura katika vituo vyao siku ya Jumatano tarehe 27 Novemba, 2024. Siku hiyo itakuwa ya mapumziko maalum kwa ajili ya uchaguzi huo.”

DONDOOHotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuhitimisha shughuli za Mkutano wa 17 wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muunga...
08/11/2024

DONDOO

Hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuhitimisha shughuli za Mkutano wa 17 wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

   MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Daktari JESCA LEBBA, amesema uelewa mzuri wa jamii kuhusu matumizi sahihi ya mfumo wa ...
08/11/2024


MGANGA Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Daktari JESCA LEBBA, amesema uelewa mzuri wa jamii kuhusu matumizi sahihi ya mfumo wa M-Mama, utasaidia kuokoa maisha ya Mama na mtoto kwenye maeneo yote nchini, hivyo kuwataka wadau mbalimbali wa Afya wakiwamo wanahabari, kuendelea kutoa elimu kwa jamii, ili kuisaidia jamii kuondokana na athari zinazotokana na masuala ya uzazi.

   : MKUU wa Mkoa wa Kagera, FATUMA MWASA, amewataadharisha watu wasiokuwa Raia wa Tanzania ambao wanaishi kwenye maeneo...
10/10/2024


: MKUU wa Mkoa wa Kagera, FATUMA MWASA, amewataadharisha watu wasiokuwa Raia wa Tanzania ambao wanaishi kwenye maeneo tofauti ua Mkoa huo, kutoshawishika kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za Uongozi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, utakaofanyika Novemba 27, mwaka huu, kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria, pia ni kuhatarisha amani ya Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake, Mkuu wa Mkoa MWASSA, amesema Uchaguzi huo ni kwa ajiri ya Watanzania pekee na hauwahusu raia wa kigeni, hivyo watu wote wasio na sifa za kushiriki Uchaguzi huo wasijaribiwe kushiriki katika zoezi hilo muhimu, kwani kufanya hivyo ni kusababisha taharuki na hatari ndani ya Mkoa na Taifa kwa ujumla, kwani atakayebainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha Mkuu wa Mkoa MWASA, ameeleza kuwa, Mkoa wa Kagera, unakadiriwa kuwa na watu zaidi ya milioni 1 waliofikisha umri wa miaka 18, hivyo ni shauku yake kuona idadi hiyo inashiriki kikamilifu katika Uchaguzi huo kwani mpaka sasa jumla ya vituo 3,833 mkoani humo, vimeandaliwa kwa ajiri ya zoezi hilo bila kusahau kujiandikisha katika daftari la wapiga kura, litakaloanza October 11, hadi 20, mwaka huu, ili kuwachagua viongozi watakaowaletea maendeleo kwenye maeneo yao.

https://podcasters.spotify.com/pod/show/rumuliJe, umepitwa na kipindi chochote bila kukisikiliza? Unaweza kusikiliza vip...
20/08/2024

https://podcasters.spotify.com/pod/show/rumuli

Je, umepitwa na kipindi chochote bila kukisikiliza? Unaweza kusikiliza vipindi vyetu kupitia podcast yetu ya Redio Rumuli Podcast na ukapata nafasi ya kuwashirikisha wengine.

DODOMA: WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa leo Julai 19, 2024 ni mgeni rasmi katika kilele cha Mkutano wa Baraza la Maaskofu wa...
19/07/2024

DODOMA: WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa leo Julai 19, 2024 ni mgeni rasmi katika kilele cha Mkutano wa Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Pentekoste Tanzania, unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa TAG, Miyuji jijini Dodoma. (Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu)

28/05/2024

:Uongozi wa Redio Rumuli 98.5 Fm Bukoba, unaomba radhi kwako msikilizaji wetu unayetusikiliza kwa njia ya Internet, kutokana na changamoto ya upatikanaji wa matangazo yetu na ubora wa sauti ya matangazo yetu kwa siku mbili zilizopita, kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu. Tunayo furaha kukujulisha kwamba sasa matangazo yetu yamerejea katika ubora wake, tafadhali endelea kuhudumiwa kupitia matangazo yetu na Mungu akubariki.

Unaweza kusikiliza matangazo yetu kupitia link yetu ya http://uk3-vn.mixstream.net:8098/listen.mp3 au tovuti yetu ya www.rumuliradio.or.tz ama unaweza kupakua application ya Radio Rumuli 98.5 Fm Bukoba kupitia soko la Play Store

Address

P . O. Box 1191 Bukoba
Bukoba

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Rumuli Fm 98.5 Bukoba posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category