06/08/2022
FAIDA ZA UJIO WA MOSIMANE SIKU YA MWANANCHI
Kwasasa barani Afrika, Kocha Bora ni tena akiwa na rekodi ya kipekee ya kuwa kocha wa kwanza mzawa wa Africa kushinda CAFCL mara 3.
Alishinda na 2016 na mara mbili, 2020 na 2021 lakini alicheza fainali 2022 akafungwa na so ni Kocha Mkubwa sana Afrika kwasasa. Faida ya kwanza wanayoipata ni kupata coverage kubwa barani Africa na kwengineko kwasababu ya uwepo wa Kocha Nguli kwenye siku ya Mwananchi. Media kibao na wanahabari kupitia akaunti zao binafsi wamesha trendisha siku ya Mwananchi, pitia Pan Africa Football, Africa Soccer Updates na kwengineko utaona. Hii Coverage isingekuwa rahisi bila Pitso kuwepo Tanzania kwa jambo hilo.
Faida hii itaifanya Yanga ijulikane zaidi ambapo haijulikani au ianze kutazamwa kwa utofauti.
Faida ya pili, Ni Yanga SC kuongeza mtaji wa watu kwenye Social Media Accounts zao. Kule Twitter Pitso ana watu Milioni 1, IG anao 630k+ wengi wao wataifollow Yanga SC.
Atawaongezea wafuasi ambao wengi wao ni nje ya Jeografia ya Tanzania. Mileage itazidi. Watafuatiliwa zaidi. Hata hizo media pia zitawaongezea wafuasi Wananchi. Faida ya tatu, Pitso amewapa Yanga SC mipango ya kuitumia ili wawe wanafuzu hatua za mtoano za michuano ya CAFCL au CAFCC.
Amewaambia washinde nyumbani. Hapa Yanga watakuwa wamepata msisitizo wa kuwafanya waone kucheza kwa Mkapa kimataifa ni jambo nyeti zaidi k**a wafanyavyo Simba. Wabakishe alama 9, sare ugenini. Faida ya nne, Pitso amezidi kuwafumbua macho Wananchi.
Kawaambia watumie mitaala ya Ulaya pia kuwafundishia watoto ili wazoee mapema. Ujanja huu. Faida ya tano, Yanga SC imejirahisishia kwenye kualika wageni wakubwa kutoka Africa. K**a wapo na Pitso Samuel Eto'o atashindwa kuja? Ahmad Ahmad Je? Faida ya sita, Inazidi kusimika ule Ukubwa wa klabu ambao wanauongelea kila siku. Kwa Yanga SC ni fahari, heshima kubwa na Upekee kujumuika na Pitso. Anaipandisha hadhi. Faida zipo nyingi sana, pia atakuwa amepiga stori na Viongozi wa Yanga baadhi kuwapa picha ya Ukubwa katika mabadiliko ya Uendeshwaji wa vilabu barani Africa.