Tija Cast Media

Tija Cast Media Tija Cast Media ni online TV inayosambaza maudhui yenye tija, mafanikio na matokeo chanya kwa jamii

11/04/2026

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Bulaya, ameonyesha masikitiko yake kuhusu kusuasua kwa utekelezaji wa Mradi wa TACTIC katika mji wa Bunda.

Akiwasilisha hoja yake, alieleza kuwa wananchi walikuwa na matarajio makubwa kupitia mradi huo, lakini hadi sasa bado hawajaona matokeo yaliyokusudiwa, hali inayozua maswali na malalamiko miongoni mwa wakazi wa eneo hilo.

11/04/2026

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemjibu Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, kufuatia mjadala unaoendelea kuhusu sakata la viongozi kudaiwa kula fedha za mafuta.

Katika kauli yake, Chalamila amesisitiza umuhimu wa viongozi na wananchi kuwa na taarifa sahihi kabla ya kutoa hoja hadharani, akieleza kuwa “ukiwa huna data, ni vyema ukanyamaza.”

Amesema mijadala mingi inayoendelea mitandaoni kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta imejaa hoja zinazokinzana na zisizo na ushahidi wa kutosha.

Hivyo, amewataka wadau wote kujikita katika uchambuzi wenye takwimu sahihi ili kuepusha upotoshaji wa umma.

Kauli hiyo imekuja wakati ambapo suala la bei ya mafuta linaendelea kuzua mjadala mpana, huku wananchi wakieleza kuathirika na gharama kubwa za maisha.

11/04/2026

Mbunge wa Jimbo la Bunda, Boniphace Mwita Getere alishauri Serikali kutafuta mbinu madhubuti za kupunguza bei ya mafuta ili kupunguza mzigo unaowakabili wananchi.

Alieleza kuwa hatua k**a kupunguza baadhi ya tozo na kodi, pamoja na kuimarisha usimamizi wa sekta ya nishati, zinaweza kusaidia kushusha bei na hivyo kurahisisha gharama za maisha.

Aliongeza kuwa kupungua kwa bei ya mafuta kutachochea pia ukuaji wa shughuli za kiuchumi kwa kupunguza gharama za uzalishaji na usafirishaji.

11/04/2026

Ukarabati wa majengo ya umma una nafasi kubwa katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi, hasa katika sekta muhimu k**a elimu, afya na utawala.

Majengo yaliyo katika hali nzuri huongeza ufanisi wa watumishi, huimarisha usalama wa watumiaji, na huchangia mazingira bora ya kazi na kujifunzia.

Aidha, ukarabati husaidia kuhifadhi rasilimali zilizopo badala ya kujenga upya, hivyo kupunguza gharama za muda mrefu na kuongeza thamani ya miundombinu ya umma.

Akichangia hotuba ya Waziri Mkuu bungeni jana tarehe 10 Aprili, Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Bulaya, alisisitiza umuhimu wa Serikali kuwekeza zaidi katika ukarabati wa majengo ya umma ili kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa ufanisi.

09/04/2026

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mheshimiwa Ester Bulaya, leo ameuliza swali bungeni akiitaka Serikali kueleza ni lini itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa stendi mpya ya kisasa katika Halmashauri ya Mji wa Bunda.

08/04/2026

Mbunge Mwibara (CCM), Kangi Lugola ameelezea jinsi baadhi ya watumishi wanavyotumia vibaya fedha za wananchi na zinazoweza kutumika kwenye majimbo ya wabunge endapo zisingechotwa ikiwemo kila Mtanzania angeweza kupewa Sh10,000.

Lugola aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, amebainisha hayo akirelejea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2026/27 ya Sh12.5 trilioni bungeni jijini Dodoma, leo Jumatano, Aprili 8, 2026.

Mbunge huyo ameshangazwa na Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba kasi yake kupungua tofauti na alivyoahidi bungeni kuwafyeka wabadhirifu.

08/04/2026

Wadau wa usafirishaji nchini Tanzania leo Aprili 08, 2026 wamekutana na LATRA jijini Dar Es Salaam kujadili juu mustakabali wa usafirishaji baada ya bei ya mafuta kupanda kwa kiasi kikubwa duniani, wadau hao wameitaka serikali kuacha kuwapangia nauli wasafirishaji badala yake wajitegemee ili kuondoa migogoro iliyopo.

Aidha, wameitaka serikali bei ya nauli ipande ili kuwasaidia wasafirishaji kuendelea kutoa huduma hiyo kwani gharama za mafuta zimepanda kwa kiwango kikubwa.

02/04/2026

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini imefanya hafla fupi kwa ajili ya kushukuru ushirikiano wa wataalamu wa REA kutoka makao makuu Dodoma, ambao leo wamehitimisha ziara maalum katika jimbo hilo ya kukagua maeneo yenye changamoto ya umeme.

Katika ziara hiyo, wataalamu wa REA walifanikiwa kupitia zaidi ya mitaa 39, wakifanya tathmini ya kina ili kubaini maeneo yenye uhitaji wa huduma ya umeme, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo muhimu.

Ziara hii imekuja kufuatia swali lililoulizwa Bungeni na Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Amos Bulaya, kuhusu mitaa inayokabiliwa na changamoto ya umeme.

Hafla hiyo, iliyofanyika katika eneo la Heriath mjini Bunda, iliambatana na chakula cha mchana na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, chama, viongozi wa dini pamoja na wananchi.

Baadhi ya viongozi walipata nafasi ya kuzungumza.

02/04/2026

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini imefanya hafla fupi leo kwa ajili ya kushukuru ushirikiano wa wataalamu wa REA kutoka makao makuu Dodoma, ambao leo wamehitimisha ziara maalum katika jimbo hilo ya kukagua maeneo yenye changamoto ya umeme.

Katika ziara hiyo, wataalamu wa REA walifanikiwa kupitia zaidi ya mitaa 39, wakifanya tathmini ya kina ili kubaini maeneo yenye uhitaji wa huduma ya umeme, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo muhimu.

Ziara hii imekuja kufuatia swali lililoulizwa Bungeni na Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Amos Bulaya, kuhusu mitaa inayokabiliwa na changamoto ya umeme.

Hafla hiyo, iliyofanyika katika eneo la Heriath mjini Bunda, iliambatana na chakula cha mchana na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, chama, viongozi wa dini pamoja na wananchi.

01/04/2026

Majirani (wapangaji wenzake) wamesema mara ya mwisho waliona pilikapilika za kuwepo mtu kwenye chumba hicho tangu siku ya ijumaa ambapo wanataja walimuona mke wa kijana huyo Amos Chacha, 22 akifungasha mizigo yake na kisha kuondoka huku kwenye chumba hicho akibaki kijana huyo akiwa anasikiliza mziki hadi majira ya jioni ambapo radio ilizimwa na tangu hapo hawakuona mtu tena.

01/04/2026

Mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kabarimu, Wilaya ya Bunda amesema kuwa kijana Amos Chacha, 22, amepatikana amejinyonga kwenye chumba chake.

Chanzo kinachodaiwa ni wivu wa kimapenzi.

Mjumbe wa mtaa ameomba jamii ishirikiane na mamlaka kuhakikisha tukio k**a hili halitokei tena.

01/04/2026

Imeelezwa kuwa , kijana Amos Chacha, 22, mkazi wa Mtaa wa Kabarimu wilaya ya Bunda ameonekana amejinyonga kwenye chumba chake, chanzo kinachodaiwa ni wivu wa kimapenzi.

Majirani wanasema alionekana mara ya mwisho Ijumaa wakati wake mke akifunga mizigo na kuondoka.

Alibaki akisikiliza mziki hadi jioni, kisha hakuwahi kuonekana tena.

Jana asubuhi, harufu mbaya ikatoka chumbani na nzi wengi, majirani wakiita mmiliki wa nyumba na viongozi wa mtaa.

Mama mzazi wa Amos amesimulia.

Address

Post
Bunda

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tija Cast Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share