Tija Cast Media

Tija Cast Media Tija Cast Media ni online TV inayosambaza maudhui yenye tija, mafanikio na matokeo chanya kwa jamii

29/04/2026

Aprili 27, 2026 — Katika Kikao cha 17 cha Bunge, Mbunge wa Jimbo la Butiama, Dkt. Wilson Mahera, aliuliza swali kuhusu usambazaji wa maji katika mradi wa Mugango–Kiabakari–Butiama kwa wananchi wa jimbo hilo.

Dkt. Mahera alisema kipaumbele kilipaswa kutolewa kwa vijiji 10 ambavyo ni Kisamwene, Busirime, Masurura, Kitasakwa, Ryamisanga, Kamugendi, Kyankoma, Kwisaro, Isaba na Nyanza ili wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

29/04/2026

Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara, Mwalimu Chacha Heche, amewataka wanachama wa chama hicho kutofuata mkumbo wa aina yoyote, bali watumie taaluma na uwezo walionao kuwahudumia wananchi kwa manufaa ya jamii.

Aidha, amesema taifa kwa sasa halihitaji watu waongee sana, bali hata kwa kukaa kimya, kusali na kuombea amani na mshikamano wa nchi, mtu atakuwa ametoa mchango mkubwa katika kulijenga taifa.

Mwalimu Heche amesisitiza kuwa si kila mtu anatakiwa kuzungumza kila wakati, kwani wakati mwingine kauli nyingi zinaweza kuwachanganya na kuwavuruga wananchi badala ya kujenga umoja na maendeleo ya jamii.

27/04/2026

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe Ester Amos Bulaya ameuliza swali bungeni akitaka kujua ni mkakati gani serikali imeandaa ili kupunguza changamoto za miundombinu katika sekta ya Elimu Nchini.

25/04/2026

Ujumbe wa wakili Alex Masaba nje ya viunga vya mahakama ya Wilaya ya Bunda juu ya kesi ya akina Kaunya

24/04/2026

Wakili Aloyce ni miongoni wa mawakili upande wa utetezi sikiliza ujumbe wake.

24/04/2026

Alphoce Machira Mwenyekiti BAVICHA Mkoa wa Mara ameendelea kuwashukuru mawakili kwa kazi wanayoifanya katika upande wa utetezi.

24/04/2026

Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Bunda atoa neno kesi ya Kaunya.

24/04/2026

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe Ester Amos Bulaya ameuliza swali bungeni akitaka kujua ni lini serikali itapeleka wataalamu wa afya ili kwenda kupunguza changamoto ya upungufu wa watoa huduma katika hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati za halmashauri ya Mji wa Bunda.

24/04/2026

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Bavicha Taifa, Yohana Kaunya, ameachiwa huru kwa dhamana baada ya kusota rumande kwa kipindi cha miezi sita huku washtakiwa wengine watatu wakiendelea na taratibu za kukamilisha masharti hayo.

Ikumbukwe kuwa Kaunya alikamatwa na awali kushtakiwa kwa kosa la uhaini, kabla ya shtaka hilo kubadilishwa na kuwa la unyang’anyi wa kutumia silaha, ambalo halikuwa na dhamana.

Shauri hili linatarajiwa kuendelea kusikilizwa tarehe 06–07/05/2026.

Wakili Gaston Garubindi ambaye pia ni mkurugenzi wa Sheria CHADEMA ameelezea kilichojiri mahakamani.

24/04/2026

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Bavicha Taifa, Yohana Kaunya, amezungumza kwa mara ya kwanza baada ya kuachiwa kwa dhamana, akitoa shukrani zake za dhati kwa mawakili wake waliomsimamia katika kipindi chote cha kesi hiyo.

Kaunya amesema juhudi, weledi na kujituma kwa mawakili hao ndizo zilizochangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha hatua hiyo ya yeye kupata dhamana.

Aidha, Kaunya ameongeza kuwa anaendelea kuwa na imani na mchakato wa sheria na haki, huku akisisitiza kuwa ukweli utawekwa wazi kadri kesi inavyoendelea kusikilizwa mahakamani.

Address

Post
Bunda

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tija Cast Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share