Mazingira Fm

Mazingira Fm 91.7Mhz SAUTI YA JAMII KARIBU KWENYE UKURASA WA MAZINGIRA Fm "SAUTI YA JAMII" (Disclaimer maoni ya wachangiaji haya husiani na mtazamo wa Radio)

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb)...
06/08/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb) anasikitika kutangaza kifo cha Spika Mstaafu na aliyekuwa Mbunge wa Kongwa Mheshimiwa Job Yustino Ndugai, kilichotokea leo tarehe 06 Agosti, 2025 Jijini Dodoma.

‎“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika Mstaafu wa Bunge Mheshimiwa Job Yustino Ndugai kilichotokea leo jijini Dodoma. Natoa pole kwa familia ya Marehemu, ndugu, jamaa na Wananchi wa Jimbo la Kongwa, Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu,” amesema Mheshimiwa Spika.

06/08/2025

Haya hapa matokeo ya kura za maoni Ubunge Jimbo la Bunda
Boniphace Mwita Getere awabwaga wapinzani wake

06/08/2025

Ndg Kangi Lugola ameibuka mshindi wa kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Mwibara kwa jumla ya kula 2317
‎huku akimzidi aliyekuwa Mbunge wa Jimbo Hilo ndugu Charles Kajege aliyepata kura 2091

‎Akitangaza matokeo hayo Katibu wa CCM Wilaya ya Bunda Michael Chonya

Vp Mwanamichezo Tunaondoka na A au B
05/08/2025

Vp Mwanamichezo Tunaondoka na A au B

Kiungo Mshambuliaji  wa Klabu ya Simba, Elie Mpanzu amewasili kwenye kambi ya Simba iliyopo Misri tayari kwa Pre Season....
05/08/2025

Kiungo Mshambuliaji wa Klabu ya Simba, Elie Mpanzu amewasili kwenye kambi ya Simba iliyopo Misri tayari kwa Pre Season.

‎Umeipokeaje taarifa hii

Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Ally Samatta ametambulishwa katika klabu ya Le Havre inayoshiriki ligi kuu y...
05/08/2025

Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Ally Samatta ametambulishwa katika klabu ya Le Havre inayoshiriki ligi kuu ya nchini Ufaransa (Ligue 1) akitokea Paok ya Ugiriki

‎“Nimefurahi kujiunga na Le Harve nimejifunza mengi kuhusu klabu hii ya kihistoria na ninaamini katika project yake, na niwashukuru kwa kuniamini na ninatarajia kujitoa kwa aslimia 100 katika Ligue 1 msimu ujao” - Samatta

‎Samatta anazidi kuipeperusha vyema bendera ya Taifa Barani Ulaya, mpaka sasa akishiriki katika ligi ya Nchini Uturuki, Ubelgiji, Uingereza na sasa anaenda kukipiga katika ligi kuu ya Nchini Ufaransa na kuungana na mastaa wakubwa katika ligi hiyo k**a Ousmane Dembele, Achraf Hakimi na Vitinha

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kisesa mkoani Simiyu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Luhaga Mpina ametambulishwa rasmi na...
05/08/2025

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kisesa mkoani Simiyu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Luhaga Mpina ametambulishwa rasmi na Chama cha ACT Wazalendo.

‎Mpina ambaye ameenguliwa na CCM katika kinyang'anyiro cha kuwania kuteuliwa kugombea Ubunge anatajwa kuwa na nia ya kuwa mgombea wa Urais kupitia ACT.

‎ACT Wazalendo inatarajiwa kufanya mkutano wake mkuu tarehe 6 Agosti 2025 kwa ajili ya kumpitisha mwanachama atakayepeperusha bendera ya chama hicho katika nafasi ya Urais mwaka huu.

05/08/2025

Robert Chacha Maboto ameibuka mshindi wa kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Bunda Mjini, baada ya kuwashinda wapinzani wake wakuu Kambarage Wasira na Ester Amos Bulaya.

Akitangaza matokeo hayo usiku huu, Katibu wa CCM Wilaya ya Bunda amesema kuwa Maboto amepata jumla ya kura 2,545, akifuatiwa na Kambarage Wasira aliyepata kura 2,032, huku Ester Bulaya akishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 625.

Wagombea wengine waliokuwa wakichuana katika kinyang'anyiro hicho ni Exavery Lugina aliyepata kura 222 na Joseph Buluba aliyepata kura 159.

04/08/2025

*Maboto awashinda Ester Bulaya na Kambarage Wasira kura za maoni Bunda Mjini*

Robert Chacha Maboto ameibuka mshindi wa kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Bunda Mjini, baada ya kuwashinda wapinzani wake wakuu Kambarage Wasira na Ester Amos Bulaya.

Akitangaza matokeo hayo usiku huu, Katibu wa CCM Wilaya ya Bunda amesema kuwa Maboto amepata jumla ya kura 2,545, akifuatiwa na Kambarage Wasira aliyepata kura 2,032, huku Ester Bulaya akishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 625.

Wagombea wengine waliokuwa wakichuana katika kinyang'anyiro hicho ni Exavery Lugina aliyepata kura 222 na Joseph Buluba aliyepata kura 159.

‎Thomas Masalu na Catherine Msafiri ambao ni wafanyakazi ndani ya redio Mazingirafm wamefunga pingu za Maisha August 2 m...
04/08/2025

‎Thomas Masalu na Catherine Msafiri ambao ni wafanyakazi ndani ya redio Mazingirafm wamefunga pingu za Maisha August 2 mwaka huu.

‎Ungana na wanafamilia wa Mazingirafm kuwatakia heri katika safari yao ya maisha ya ndoa.

30/07/2025
Wajumbe tuwekane wazi hapa
30/07/2025

Wajumbe tuwekane wazi hapa

Address

Nmb Street
Bunda
31530-51BUNDA

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mazingira Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mazingira Fm:

Share

Category