Mazingira Fm

Mazingira Fm 91.7Mhz SAUTI YA JAMII KARIBU KWENYE UKURASA WA MAZINGIRA Fm "SAUTI YA JAMII" (Disclaimer maoni ya wachangiaji haya husiani na mtazamo wa Radio)

‎Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya na mwanasiasa mashuhuri wa upinzani nchini humo Raila Odinga, amefariki  dunia leo Oktoba ...
15/10/2025

‎Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya na mwanasiasa mashuhuri wa upinzani nchini humo Raila Odinga, amefariki dunia leo Oktoba 15, 2025, akiwa na umri wa miaka 80.

‎Taarifa za awali zinaeleza kuwa Odinga amefariki dunia kutokana na shambulio la moyo akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali moja nchini India.

‎Odinga alihudumu k**a Waziri Mkuu wa Kenya katika kipindi cha kati ya mwaka 2008 hadi 2013.

‎Aidha, aliwahi kuwania nafasi ya Urais nchini Kenya mara tano, katika miaka ya 1997, 2007, 2013, 2017, na 2022.

Mtoto Josiah Mwambene, aliyemaliza darasa la saba katika Kijiji cha Majengo, wilayani Mbozi, mkoani Songwe, amefariki du...
14/10/2025

Mtoto Josiah Mwambene, aliyemaliza darasa la saba katika Kijiji cha Majengo, wilayani Mbozi, mkoani Songwe, amefariki dunia katika mazingira ya kushangaza baada ya kudonolewa na kuku tetea kwenye paji la uso.

‎Tukio hilo limezua simanzi na taharuki kubwa miongoni mwa wakazi wa eneo hilo, huku baadhi wakihusisha kifo hicho na imani za kishirikina kutokana na mazingira ya tukio hilo.

‎Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu, Raphael Mtafya, marehemu Josiah alikuwa mwanafunzi mwenye uwezo mkubwa kitaaluma na katika mahafali ya shule yao alitambuliwa rasmi kwa kupokea zawadi maalum kutokana na ufaulu wake.

‎“Usiku wa siku hiyo, akiwa amelala, ghafla aliamka akipiga kelele akidai kuvamiwa na kuku tetea aliyemdonoa usoni. Tuliona jeraha dogo tu, tukadhani si tatizo kubwa,” alisema Mtafya.

‎Hata hivyo, siku chache baadaye Josiah alianza kulalamika maumivu ya kichwa, jicho kuvimba, na baadaye akaanza kuharisha. Alipofikishwa hospitalini, madaktari walieleza kuwa hakukuwa na ugonjwa ulioonekana wazi, jambo lililowafanya wazazi wake kumpeleka kanisani kwa maombi. Licha ya jitihada hizo, hali yake iliendelea kuwa mbaya hadi alipofariki dunia.

‎Wakati baadhi ya wananchi wakihusisha tukio hilo na imani za kishirikina, wataalam wa afya wamesema huenda kifo hicho kimetokana na maambukizi ya bakteria hatari yaliyosababishwa na jeraha alilopata baada ya kudonolewa na kuku huyo.

‎Leo, Oktoba 14, 2025, ni siku ya kukumbuka miaka 26 tangu kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.‎‎Mw...
14/10/2025

‎Leo, Oktoba 14, 2025, ni siku ya kukumbuka miaka 26 tangu kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

‎Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alifariki dunia Oktoba 14, 1999, katika Jiji la London, Uingereza, ambapo alikuwa akipatiwa matibabu.

Leo kwenye kipindi cha Ngome ya Burudani atasikika msanii  ‎‎Akizungumza kwa kina kuhusu safari yake ya muziki ‎‎Tufuati...
07/10/2025

Leo kwenye kipindi cha Ngome ya Burudani atasikika msanii

‎Akizungumza kwa kina kuhusu safari yake ya muziki

‎Tufuatilie kupitia mitandao ya kijamii

04/10/2025

‎Shirika la Mazingira community development forum limezindua mradi wa chumba maalumu cha tehama shule ya secondary esperanto uliogharimu shilingi milioni 35 kwaajili ya kuwawezesha wanafunzi kujifunza masomo ya tehama .

‎Akisoma risala ya shirika mbele ya mgeni rasmi mratibu wa miradi Simba Mramba ameeleza baadhi ya mambo waliyofanya k**a shirika katika shule hiyo huku akitaja kuwa chumba hicho kimewekewa viti 31 na meza 31 na computer 30.

‎Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wameishukuru shirika la Mazingira kwa kuwaletea vifaa na kujenga jengo kwaajiri ya masomo ya tehama


‎Mradi huo umefanywa na ushirikiano wa Shirika la Mazingira na STICHTING MAZINGIRA NEDERLAND na WILDE GANZEN FOUNDATION

04/10/2025

Shirika la Mazingira community development forum limezindua mradi wa chumba maalumu cha tehama shule ya secondary esperanto uliogharimu shilingi milioni 35 kwaajili ya kuwawezesha wanafunzi kujifunza masomo ya tehama .

‎Akisoma risala ya shirika mbele ya mgeni rasmi mratibu wa miradi Simba Mramba ameeleza baadhi ya mambo waliyofanya k**a shirika katika shule hiyo huku akitaja kuwa chumba hicho kimewekewa viti 31 na meza 31 na computer 30.

‎Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wameishukuru shirika la Mazingira kwa kuwaletea vifaa na kujenga jengo kwaajiri ya masomo ya tehama


‎Mradi huo umefanywa na ushirikiano wa Shirika la Mazingira na STICHTING MAZINGIRA NEDERLAND na WILDE GANZEN FOUNDATION

‎Leo Septemba 27, 2025 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa clube ya Yanga wanashuka dimbani katika mchezo wa marudiano dhidi...
27/09/2025

‎Leo Septemba 27, 2025 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa clube ya Yanga wanashuka dimbani katika mchezo wa marudiano dhidi ya Wiliete Sports Clube ya Angola katika hatua za awali za kuisaka hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.
‎Yanga walifanikiwa kupata ushindi ugenini wa golo 3-0

‎Vp Yanga wataendeleza ubabe wao?

Katibu wa NEC wa Uchumi na Fedha wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Ndg Joshua Chacha Mirumbe, leo ameongoza matembezi ...
24/09/2025

Katibu wa NEC wa Uchumi na Fedha wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Ndg Joshua Chacha Mirumbe, leo ameongoza matembezi ya kampeni katika Jimbo la Tarime Mjini, ikiwa ni sehemu ya kumnadi Mgombea wa Ubunge wa jimbo hilo, Ester Matiko.

Matembezi hayo yaliyojumuisha wanachama wa CCM na wananchi wa Tarime.

Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Pamba Jiji.‎‎Leo Jumatano Septemba 24, 2025, mabingwa hao watetezi, Yanga SC wanaanza...
24/09/2025

Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Pamba Jiji.

‎Leo Jumatano Septemba 24, 2025, mabingwa hao watetezi, Yanga SC wanaanza msimu wa 2025/2026 kwa kuwakaribisha Pamba Jiji katika Dimba la Benjamin Mkapa.

‎Mechi hii itapigwa kuanzia saa 1:00 usiku.

‎Kampuni ya Mtandao wa Yas imeendelea kuwafikia karibu wateja wao kote nchini huku wakiendelea kutoa huduma k**a vile ya...
17/09/2025

‎Kampuni ya Mtandao wa Yas imeendelea kuwafikia karibu wateja wao kote nchini huku wakiendelea kutoa huduma k**a vile ya lipa kwa simu, huduma ya simu za mikopo pamoja na usajili wa lain mpya

‎Yas, anzia ulipo, Kila hatuamix

Yanga Bingwa wa Ngap ya jamiiYanga 1 - 0 SimbaPakome
16/09/2025

Yanga Bingwa wa Ngap ya jamii
Yanga 1 - 0 Simba
Pakome

Address

Nmb Street
Bunda
31530-51BUNDA

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mazingira Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mazingira Fm:

Share

Category