Mazingira Fm

Mazingira Fm 91.7Mhz SAUTI YA JAMII KARIBU KWENYE UKURASA WA MAZINGIRA Fm "SAUTI YA JAMII" (Disclaimer maoni ya wachangiaji haya husiani na mtazamo wa Radio)

07/06/2026

KATIBU TAWALA BUNDA AZITAKA TAASISI ZA SERIKALI NA HALMASHAURI ZA WILAYA YA BUNDA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAAGA WATUMISHI WAO WALIOSTAAFU.

Akizungumza katika hafla ya kumuaga Bi Anna Mathew Ouma aliyekuwa mthibiti ubora elimu halmashauri ya wilaya ya Bunda, katibu tawala wilaya ya Bunda Salumu Mtelela amesema hali hiyo humfanya mtumishi ajue alikuwa muhimu katika nafasi ya utumishi wake

Hafla hii imefanyika june 6, 2026.

TFF U17 CLUBS PREMIER LEAGUE | FT'Yanga SC 1-1 Simba SC
06/06/2026

TFF U17 CLUBS PREMIER LEAGUE | FT'

Yanga SC 1-1 Simba SC

06/06/2026

Huyu hapa mzee aliyekodisha Gari na kudhurumiwa moja kwa moja akilalamika mbele ya Waziri mkuu DKT,Mwigulu Lameck Nchemba

05/06/2026

Haki siyo hisani. Tunataka anayestahili haki apewe haki yake. Serikali haitavumilia vitendo vya kupora au kuchelewesha haki za wananchi kwa sababu yoyote ile-Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba


Amesema hayo wakati alipozungumza katika mkutano wa hadhara na wakazi wa Isimani, Mkoani Iringa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amebainisha mambo sita makubwa ambayo Ta...
05/06/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amebainisha mambo sita makubwa ambayo Tanzania imeendelea kuyatekeleza katika kuimarisha sekta ya kazi, ajira na ustawi wa wafanyakazi, hatua zinazoiwezesha nchi kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia duniani.

Mhe.Sangu ameyasema hayo Juni 5, 2026 Mjini Geneva, Uswisi katika Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unashirikisha wawakilishi wa Serikali, Waajiri na Wafanyakazi kutoka nchi wanachama 187.

Waziri Sangu ametaja mambo hayo ni pamoja na dhamira ya Tanzania chini ya uongozi wa Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha mabadiliko ya kiteknolojia yanakuza kazi zenye staha, tija, ubunifu na haki ya kijamii kupitia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Ameeleza kuwa mageuzi hayo yameongeza ushiriki wa wanawake, vijana na wananchi wa vijijini katika huduma za kifedha na shughuli za kiuchumi huku Serikali Mtandao ikiimarisha uwazi, uwajibikaji na ufanisi wa utoaji huduma.

Pia amesema Tanzania imeendelea kulinda haki za wafanyakazi katika mazingira ya kidijitali kupitia uzinduzi wa Mpango wa Taifa wa Kazi Zenye Staha (NDWCP III), pamoja na kuimarisha usalama na afya mahali pa kazi kwa kutekeleza mpango wa Vision Zero na mifumo mingine ya ulinzi wa kazi.

Sangu ametaja jambo la tatu kuwa ni kuimarishwa kwa mifumo ya hifadhi ya jamii kupitia Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2023, ambapo zaidi ya wanachama 560,000 wa sekta isiyo rasmi na wanaojiajiri wamefikiwa kupitia usajili wa kidijitali kufikia Machi 2026.

Aidha, jambo la sita ni kuendelea kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Shirika la Kazi Duniani (ILO) katika kuhakikisha matumizi ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI) yanachochea maendeleo endelevu, ujumuishi, haki ya kijamii na ukuaji wa uchumi unaowanufaisha wananchi wote.

Mhe. Sangu amesisitiza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na wadau wa kazi wa ndani na wa kimataifa ili kuhakikisha maendeleo ya teknolojia yanatumika kuboresha mazingira ya kazi, kuongeza tija na kuimarisha ustawi wa wafanyakazi nchini.

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inafanyia kazi mapitio ya sheria inayosimamia uchaguzi wa Naibu Meya n...
04/06/2026

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inafanyia kazi mapitio ya sheria inayosimamia uchaguzi wa Naibu Meya na Makamu Wenyeviti wa Halmashauri kwa lengo la kuondoa migogoro na kuongeza ufanisi katika utendaji wa halmashauri nchini.

Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi, Juni 4, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la papo kwa papo la Mbunge wa Segerea, Mhe. Agenesta Lambert Kaiza, ambaye alitaka kujua k**a Serikali ina mpango wa kurekebisha utaratibu wa uchaguzi wa Naibu Meya na Makamu Wenyeviti wa Halmashauri unaofanyika kila mwaka na kusababisha migawanyiko pamoja na kuathiri utendaji wa halmashauri.

Amesema tayari amemuelekeza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kulifanyia kazi suala hilo ili kuandaa mapendekezo ya marekebisho ya sheria yatakayowasilishwa Bungeni kwa hatua zaidi.

Aidha, Waziri Mkuu amewataka viongozi wa halmashauri kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maslahi ya wananchi badala ya kujikita katika kampeni za uchaguzi wa ndani ya halmashauri.

Katika swali jingine, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa wawekezaji wa ndani na nje huku ikiweka mkazo katika kujenga uwezo wa sekta binafsi inayomilikiwa na Watanzania.

Kauli hiyo ameitoa wakati akijibu swali la papo kwa papo la Mbunge wa Kikwajuni, Mhe. Ally Hassan Omary King, ambaye alitaka kujua mkakati wa Serikali wa kuwawezesha wawekezaji wa ndani bila kuweka vikwazo kwa wawekezaji wa nje, kwa kuzingatia mchango wa uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje katika kukuza uchumi wa Taifa.

Amesema Serikali imeendelea kutoa vivutio mbalimbali kwa wawekezaji wa nje sambamba na kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani ili washiriki kikamilifu katika shughuli za uwekezaji na uzalishaji.

Aidha, amesema Serikali imeanzisha dirisha maalum kwa wawekezaji wa ndani na kushusha kiwango cha chini cha mtaji kinachohitajika kwa wawekezaji hao ili kuongeza ushiriki wa Watanzania katika shughuli za uwekezaji.

Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tanzania bado ni salama dhidi ya ugonjwa wa Ebola huku Serikal...
04/06/2026

Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tanzania bado ni salama dhidi ya ugonjwa wa Ebola huku Serikali ikiendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari, ufuatiliaji na utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu magonjwa ya mlipuko.

Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi, Juni 4, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la papo kwa papo la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Asha Salum Moto, ambaye alitaka kujua namna Serikali ilivyojipanga kukabiliana na ugonjwa wa Ebola unaoripotiwa katika baadhi ya nchi jirani.

Amesema Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kujikinga na magonjwa ya mlipuko, kuimarisha ufuatiliaji mipakani pamoja na kuhimiza utoaji wa taarifa mapema pale dalili za magonjwa hayo zinapojitokeza.

Katika swali jingine, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya reli na miundombinu mingine ya usafiri ili kukabiliana na changamoto zinazotokana na ukuaji wa miji na kuongeza ufanisi wa shughuli za kiuchumi.

Kauli hiyo ameitoa alipokuwa akijibu swali la papo kwa papo la Mbunge wa Kigamboni, Mhe. Haran Sanga, ambaye alitaka kujua mpango wa Serikali wa kuimarisha miundombinu ya reli katika majiji yanayokuwa kwa kasi nchini.

Aidha, akijibu swali la Mbunge wa Mvomero, Mhe. Sarah Msafiri, ambaye alitaka kujua mpango wa Serikali wa kuwekeza kikamilifu katika kilimo cha umwagiliaji ili kuongeza uzalishaji, kuchochea ukuaji wa uchumi na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Waziri Mkuu amesema Serikali imeongeza uwekezaji katika sekta hiyo na kuendelea kufufua miradi mbalimbali ya umwagiliaji nchini.

Kadhalika, akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini, Mhe. Dickson Nathan Lutevele, ambaye alitaka kujua hatua zinazochukuliwa na Serikali kuhakikisha wakulima wa mazao ya biashara wanalipwa kwa wakati ili waendelee kuimarisha uzalishaji, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua za kuboresha masoko ya mazao, kuongeza uwezo wa uchakataji ndani ya nchi na kuimarisha ushirikiano na wadau wa sekta hiyo.

Amesema Serikali itaendelea kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya uchakataji wa mazao ya kilimo ili kuongeza thamani ya mazao, kupanua masoko na kuongeza mapato kwa wakulima.

Shirikisho la Urusi limesema litaendelea kufungua fursa mbalimbali za uwekezaji na ushirikiano kwa Tanzania kwa manufaa ...
03/06/2026

Shirikisho la Urusi limesema litaendelea kufungua fursa mbalimbali za uwekezaji na ushirikiano kwa Tanzania kwa manufaa ya mataifa yote mawili, huku likiahidi kutangaza fursa hizo katika Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi unaotarajiwa kufanyika kesho kutwa nchini humo.

Hayo yameelezwa na Rais wa Shirikisho la Urusi, Vladimir Putin, baada ya kufanya mazungumzo rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, jijini Moscow.

Rais Putin amesema Urusi imekuwa ikifuatilia kwa karibu mageuzi ya kiuchumi na kijamii yanayofanyika Tanzania na kuridhishwa na kasi ya maendeleo inayopatikana nchini.

Amesema mazungumzo yake na Rais Samia yamekuwa na manufaa makubwa kwa pande zote mbili na yamefungua ukurasa mpya wa kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Urusi kwa sasa ina miradi takribani 70 nchini Tanzania yenye thamani ya dola za Marekani milioni 434.22, ambayo imechangia kutoa ajira zaidi ya 3,000 kwa Watanzania.

Kwa upande wake, Rais Samia amesema ziara yake nchini Urusi ni ya kihistoria kwa kuwa ni mara ya kwanza kwa kiongozi wa Tanzania kufanya ziara ya kiserikali nchini humo baada ya kupita zaidi ya nusu karne.

Aidha, Rais Samia alimshukuru Rais Putin na Serikali ya Urusi kwa mwaliko huo na ukarimu waliompatia wakati wa ziara yake nchini humo.

Katika mazungumzo hayo, Rais Samia pia alikumbusha mchango mkubwa wa Urusi katika harakati za Tanzania za kupigania uhuru na kumpongeza Rais Putin kwa maadhimisho ya miaka 81 ya Ushindi katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia yaliyofanyika Mei 9 mwaka huu.

Rais Samia aliwasili Moscow kwa ziara yake ya kwanza nchini Urusi, ambayo pia ni ziara ya kwanza ya kiongozi wa Tanzania nchini humo katika kipindi cha zaidi ya miaka 50.

Kwa mujibu wa viongozi hao, mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha zaidi uhusiano wa kirafiki na ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Urusi, pamoja na kubadilishana mawazo kuhusu masuala muhimu ya kikanda na kimataifa yanayoendelea duniani.

Ziara hiyo inatarajiwa kufungua fursa mpya za uwekezaji, biashara, elimu, teknolojia na ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Shirikisho la Urusi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemteua Bi. Ummy Ally Mwalimu kuwa Mshauri wa R...
03/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemteua Bi. Ummy Ally Mwalimu kuwa Mshauri wa Rais anayeshughulikia Masuala ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo umetangazwa leo Juni 2, 2026 kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Bi. Ummy Mwalimu ni mmoja wa viongozi wenye uzoefu mkubwa katika utumishi wa umma nchini, akiwa amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uwaziri katika Serikali ya Tanzania. Katika kipindi cha uongozi wake, amewahi kuhudumu katika sekta za afya, mazingira, Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Kwa upande wa dizeli, watumiaji wanakabiliwa na ongezeko dogo la bei, ambapo kwa Dar es Salaam bei kikomo imefikia Shili...
03/06/2026

Kwa upande wa dizeli, watumiaji wanakabiliwa na ongezeko dogo la bei, ambapo kwa Dar es Salaam bei kikomo imefikia Shilingi 4,333 kwa lita. Ongezeko hilo limechangiwa na kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la dunia pamoja na kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa bidhaa hiyo.

Licha ya changamoto hizo za kimataifa, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kulinda uchumi na wananchi kwa kuweka ruzuku ya Shilingi 534.91 kwa kila lita ya dizeli. Hatua hiyo imelenga kupunguza athari za ongezeko la bei kwa sekta muhimu k**a usafirishaji, viwanda na huduma za kijamii.

Mabadiliko haya yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati, vinavyohusisha Marekani, Israeli na Irani. Mgogoro huo umeathiri uzalishaji, uhifadhi na usafirishaji wa mafuta duniani, huku kufungwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz kukiongeza gharama za usafirishaji na bima za meli za mafuta.

Address

Nmb Street
Bunda
31530-51BUNDA

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mazingira Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mazingira Fm:

Share

Category