Mazingira Fm

Mazingira Fm 91.7Mhz SAUTI YA JAMII KARIBU KWENYE UKURASA WA MAZINGIRA Fm "SAUTI YA JAMII" (Disclaimer maoni ya wachangiaji haya husiani na mtazamo wa Radio)

09/08/2026

Mashabiki na wanachama wa Yanga SC Shina la Ruselu wilayani Bunda wameadhimisha Yanga Day kwa kuzindua mnara wa timu hiyo, uliogharimu shilingi milioni 3.4.

Katika risala iliyosomwa wakati wa uzinduzi mbele ya mgeni rasmi, Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Amos Bulaya, aliyewakilishwa na Diwani wa Kata ya Sazira, Michael Thomas Kweka, tawi hilo limeeleza kuwa lilianzishwa rasmi Septemba 21, 2024, likiwa na wanachama 92.

Hata hivyo, hadi wakati wa uzinduzi huo, idadi ya wanachama hai imefikia 56.

Kwa kuunga mkono juhudi za mashabiki na wanachama wa Yanga Tawi la Ruselu, Mbunge Ester Bulaya ametoa mchango wa shilingi 300,000.

09/08/2026

Mshik**ano katika ndoa husaidia wanawake kiuchumi

Ushirikiano, uaminifu na kusaidiana kati ya wanandoa umetajwa kuwa miongoni mwa misingi inayoweza kumsaidia mwanamke kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya familia, huku pia ukisaidia kupunguza migogoro ndani ya familia.

Hayo yameelezwa na Rebecca Shilinde, mwalimu mstaafu na mjasiriamali wa mapambo na bidhaa za urembo, mkazi wa Nyashimo mkoani Simiyu, wakati wa mahojiano yaliyofanyika katika viwanja vya maonesho ya Nanenane Nyakabindi mkoani Simiyu, ambako alikuwa akionesha na kutangaza bidhaa zake.

Rebecca, ambaye aliamua kutumia kwa vitendo ujuzi wa stadi za kazi aliokuwa akifundisha shuleni baada ya kustaafu, anasema safari yake ya ujasiriamali imekuwa na mchango mkubwa kutoka kwa mume wake, ambaye amekuwa akimpa taarifa za fursa, kumsaidia katika mahitaji ya biashara na kumpa nafasi ya kushiriki katika maonesho na maeneo mbalimbali ya kutafuta fursa.

08/08/2026

VIJANA 600+ WAUDHURIA KONGAMANO LA VIJANA PLATFORM BUNDA DC

Kolman, Afisa Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambaye pia ni Mratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa Halmashauri hiyo, amesema kongamano hilo linalenga kuwajengea vijana uelewa kuhusu uzalendo na kuwaunganisha na fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo katika maeneo yao.

Amesema fursa hizo zinapatikana katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, mifugo, uvuvi, biashara, ujasiriamali na ubunifu, huku akieleza kuwa kongamano hilo ni sehemu ya utekelezaji wa kampeni za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2026.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Mhe. Aswege Enock Kaminyoge, amewataka vijana kutumia fursa za mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri pamoja na mfuko wa kuwawezesha vijana kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, ili kujikwamua kiuchumi na kuondokana na utegemezi.

08/08/2026

KAMBARAGE WASIRA MBUNGE WA AFRIKA MASHARIKI ATOA KOMPYUTA 10 BUNDA,

Elly Mwabe, akizungumza kwa niaba ya Mhe. Kambarage Wasira, amesema kompyuta hizo zimetolewa kwa lengo la kusaidia kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule za msingi na sekondari.

Mwabe amesema Mhe. Kambarage amedhamiria kuendelea na zoezi hilo la kutoa vifaa vya kielimu, ili kufikia halmashauri zote za Mkoa wa Mara na kusaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Mhe. Aswege Enock Kaminyoge, amemshukuru Mhe. Kambarage kwa msaada huo, huku akiitaka Halmashauri kuhakikisha kompyuta hizo zinagawanywa kwa shule kwa kuzingatia mahitaji halisi, bila upendeleo.

05/08/2026

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Amos Bulaya, amesema kuwa msingi wa kupata viongozi bora ni kuwekeza katika elimu, akieleza kuwa kiongozi bora ni yule anayeacha alama ya utendaji na maendeleo yenye manufaa kwa wananchi wake.

Bulaya ametoa kauli hiyo leo, Agosti 5, 2026, wakati akiendelea na ziara yake ndani ya jimbo hilo, ya kukabidhi mashine 10 za kunakili nyaraka (photocopy) kwa shule 10 za msingi na sekondari zilizopo katika kata 10 za Jimbo la Bunda Mjini. Amesema lengo la msaada huo ni kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia kwa wanafunzi pamoja na walimu.

Aidha, Mbunge Bulaya amesema ataendelea kuboresha miundombinu ya huduma za jamii katika jimbo lake, ikiwemo barabara, upatikanaji wa maji safi na salama, pamoja na kuhakikisha wananchi wanaoishi katika mitaa ya pembezoni mwa mji wanaunganishiwa huduma ya umeme kwa gharama ya shilingi 27,000.

Amesema pamoja na Serikali kujenga shule nyingi nchini, bado changamoto kubwa ipo katika ukarabati wa miundombinu ya elimu kutokana na kutotengwa kwa fedha za kutosha kwa ajili ya matengenezo. Amefafanua kuwa bajeti ya Taifa ni takribani shilingi trilioni 3.5, huku Jimbo la Bunda Mjini likihitaji zaidi ya shilingi bilioni 2.4 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya shule.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania Wilaya ya Bunda mwalimu dotto luhende amesema kupatikana kwa mashine hizo za kunakili nyaraka kutarahisisha shughuli za ufundishaji na ujifunzaji, na kwamba anaamini hatua hiyo itachangia kuimarika kwa kiwango cha ufaulu wa wanafunzi katika halmashauri hiyo.

Nao madiwani wa Kata za Guta, Bunda Stoo na Nyasura wamemshukuru Mbunge Ester Bulaya kwa kutatua changamoto ya muda mrefu ya ukosefu wa mashine za kunakili nyaraka, wakisema msaada huo utaboresha utoaji wa huduma za elimu katika shule zilizopo kwenye kata zao.

Hadi kufikia sasa, jumla ya shule sita kutoka kata sita zimepokea mashine hizo za kunakili nyaraka (photocopy). Kata zilizonufaika katika awamu hiyo ni Sazira, Manyamanya, Kabasa, Guta, Bunda Stoo na Nyasura.

31/07/2026

Kampuni ya mawasiliano ya Yas yakabidhi milioni moja kwa mshindi wa kampeni ya "Ikiingia Tu Goli"

Katika kuendelea kudhihirisha ubora wa huduma zake na kuwazawadia wateja wake, kampuni ya mawasiliano ya Yas Kanda ya Mara Kusini imekabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja kwa mshindi wa kampeni ya "Ikiingia Tu Goli", kampeni maalumu iliyoendeshwa wakati wa michuano ya Kombe la Dunia.

Meneja wa Yas Kanda ya Mara Kusini, Halid Omary, amesema kampeni ya "Ikiingia Tu Goli" ilihitimishwa Julai 30 kwa kuwa ilikuwa maalumu kwa kipindi cha michuano ya Kombe la Dunia. Amesema wanafurahia kumpata mshindi kutoka Wilaya ya Serengeti ambaye amejishindia shilingi milioni moja k**a zawadi ya droo ya kila siku ya kampeni hiyo.

Mshindi wa zawadi hiyo, Lightness Mushi, mkazi wa Wilaya ya Serengeti, amesema hakutarajia kuwa mshindi wa kampeni hiyo. Amesema alipigiwa simu kutoka namba 100, lakini mwanzoni hakupokea akidhani ni simu ya kawaida. Baada ya kupigiwa kwa mara ya pili ndipo alipokea na kupewa taarifa kuwa amejishindia shilingi milioni moja.

27/07/2026

Esther Bulaya Aunga Mkono Ujenzi wa Kanisa la KKKT Mugaja kwa Msaada wa Mabati

Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mariam Amosi, kwa niaba ya Mbunge Esther Bulaya, leo Julai 27, 2026, amekabidhi mabati bando mbili zenye thamani ya shilingi 700,000 kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Mugaja Manyamanyama.

Msaada huo umetolewa kufuatia ombi lililowasilishwa na uongozi wa kanisa hilo, uliolenga kuomba mchango wa kusaidia ujenzi wa nyumba ya ibada.

24/07/2026

UWEPO WA MNARA NYAMOKO KUIBUA FURSA KWA VIJANA

Diwani wa kata ya Nyamoko iliyopo wilayani Serengeti mkoani Mara Mhe Emmanuel Gabriel Saina ameupongeza mtandao wa simu wa YAS kwa kuzindua mnara ambao utasaidia kutatua changamoto ya mawasiliano kwenye kata hiyo na vijiji Jirani.

Akiwa mgeni rasmi Mhe Saina ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa mnara wa YAS uliopo Kijiji cha Itununu wilayani Serengeti ambapo amesema mwanzoni ilikuwa changamoto katika vijiji vya kata hiyo kwenye suala la mawasiliano hali iliyokuwa inapelekea Kwenda mbali kutafuta mawasiliano

24/07/2026

YAS YAZINDUA MNARA KATA YA NYAMOKO KIJIJI CHA ITUNUNU SERENGETI

Meneja wa YAS Mara ya kusini Ndugu Kharid Omary Mtwange amesema baada ya kupokea maombi kutoka kwa wakazi wa maeneo hayo na wao k**a mtandao walifanya utafiti leo wamezindua mnara huo ambao anaamini utawasaidia wananchi ambao wamekuwa wakipata changamoto ya mawasiliano na yas wamekuwa wakifanya hivyo kwa maeneo yote nchini ili kuahkikisha hakuna mwananchi anakosa mawasiliano.

Msanii Zola atasikika kupitia Ngome ya Burudani ndani ya Mazingira FM Redio!  Stay Tuned!
24/07/2026

Msanii Zola atasikika kupitia Ngome ya Burudani ndani ya Mazingira FM Redio!

Stay Tuned!

Address

Nmb Street
Bunda
31530-51BUNDA

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mazingira Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mazingira Fm:

Share

Category