Mazingira Fm

Mazingira Fm 91.7Mhz SAUTI YA JAMII KARIBU KWENYE UKURASA WA MAZINGIRA Fm "SAUTI YA JAMII" (Disclaimer maoni ya wachangiaji haya husiani na mtazamo wa Radio)

17/12/2025

Mvulana mwenye umri wa miaka 15, mkazi wa Kijiji cha Marambeka, Kata ya Ketare wilayani Bunda, Festo Mramba amejeruhiwa na kitu chenye ncha kali mguuni eneo la kisigino chanzo kikielezwa ni baada ya ng'ombe kuruka uzio na kuingia kwenye eneo la mtu mwingine wakati akiwa anachunga mifugo katika eneo lao.

Katika tukio hilo lililotokea tarehe 13 Desemba, 2025, majira ya saa 10 jioni, Festo amesema aliporuka uzio kwa lengo la kumrudisha ng’ombe huyo, k**a alivyoelekezwa na mmiliki wa eneo hilo Yona Katani, ambaye anatajwa kuwa mtuhumiwa wa tukio hilo, ghafla alirushiwa jiwe na alipogeuka kukimbia, mtuhumiwa alimrushia panga lililomjeruhi mguu wa kulia eneo la kisigino.

Mazingira Fm imemfikia mtoto huyo kujua kilichotokea na kufika kwa uongozi wa serikali ya kijiji ambao umethibitisha kupokea taarifa za tukio hilo na kueleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa kuzuia migogoro hiyo kwa wananchi

Yas na zawadi za December Halid Omary Meneja wa YAS Mara Kusini  💛💙
17/12/2025

Yas na zawadi za December
Halid Omary Meneja wa YAS Mara Kusini
💛💙

17/12/2025

Unakosaje kuwa bilionea 2025?
Kupitia magift ya Mixx Pesa kutoka Yas utaweza kujishindia milioni 1 kila siku au milioni 5 kila wiki au milioni 10 kila mwezi au kuibuka mshindi wa milioni 50 kwenye droo ya mwisho kabisa

Unachotakiwa fanya miamala mingi kadri uwezavyo kutumia Yas tuma pesa, pokea pesa, nunuua muda wa maongezi kupitia Mixx by Yas au tumia Mixx by Yas super app uingie kwenye droo ya kuwa bilionea

Vigezo na masharti kuzingatiwa
💛💙

16/12/2025

Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mhe. Thecla Mkuchika ameiagiza Mamlaka ya Maji Mugango-Kiabakari kupeleka huduma ya maji katika hospitali mpya ya wilaya hiyo, Kizurira Nyerere

Maagizo hayo yametolewa Jumamosi ya tarehe 13 Desemba 2025 katika kikao cha kawaida cha k**ati ya ushauri wa wilaya kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na kuhudhuriwa na Wakuu wa Idara, viongozi wa dini na wadau wa maendeleo, viongozi wa vyama vya kisiasa, watendaji wa kata na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo na Mbunge wa jimbo la Butiama

12/12/2025

Wananchi wa Kijiji cha Kirumi, kata ya Bukabwa wilayani Butiama, mkoani Mara, kwa kushirikiana na Serikali ya kijiji, wameadhimisha Siku ya Lishe na Afya ya Kijiji kwa shamrashamra na uhamasishaji mkubwa.

Maadhimisho haya yamefanyika tarehe 11 Desemba 2025 na kuhudhuriwa na viongozi na wataalam mbalimbali akiwemo Diwani wa Kata ya Bukabwa, Afisa Lishe kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Afisa Mtendaji wa Kata ya Bukabwa, Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kirumi, Wahudumu wa Afya kutoka Kituo cha Afya Kirumi, pamoja na wananchi wa kijiji hicho.

Katika maadhimisho hayo, wananchi walipata fursa ya kushiriki na kunufaika na shughuli mbalimbali za kitaalam zikiwemo, Elimu ya maandalizi sahihi ya uji wa lishe unaozingatia makundi muhimu ya chakula, Elimu juu ya umuhimu wa chanjo kwa watoto na wajawazito, Upimaji wa hali ya lishe kwa watoto, Utoaji wa chanjo kwa watoto waliostahili, Uhamasishaji wa uchangiaji wa chakula shuleni kwa ajili ya lishe bora kwa wanafunzi.

Maadhimisho haya yamelenga kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora, kuimarisha afya ya mama na mtoto, na kuboresha ushirikishwaji wa jamii katika masuala ya afya na malezi bora kwa watoto.

Rais samia Suluhu Hassan amesema amesikitishwa na taarifa ya kifo Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim...
11/12/2025

Rais samia Suluhu Hassan amesema amesikitishwa na taarifa ya kifo Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo Disemba 11, 2025 jijini Dodoma.

Kupitia mitandao yake ya kijamii, Rais Samia ameandika “Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama. Ninatoa pole kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa M***a Azzan Zungu, wananchi wa Jimbo la Peramiho, familia, ndugu, jamaa na marafiki.

Kwa miaka 38, Mheshimiwa Mhagama amekuwa mwanachama mahiri wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kiongozi wa vijana, kiongozi wa wanawake, waziri katika awamu mbalimbali na mnasihi wa wengi katika siasa na maisha.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi Amen"

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu ameatangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Jenista Mh...
11/12/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu ameatangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama kilichotokea leo Desemba 11, 2025 jijini Dodoma.

Mazingira FM inakutakia heri ya maadhimisho ya miaka 64 ya uhuru .
09/12/2025

Mazingira FM inakutakia heri ya maadhimisho ya miaka 64 ya uhuru .

Yanga Yasubiri zaidi ya dakika 85 kuifunga Coastal Union Nii Dube tena je ndo gari lake limewaka au tumpe muda FT Coasta...
07/12/2025

Yanga Yasubiri zaidi ya dakika 85 kuifunga Coastal Union
Nii Dube tena je ndo gari lake limewaka au tumpe muda

FT Coastal Union 0 - 1 Yanga

Unadhani Simba wamekosea wapi?  au ndiyo ubora wa Azam?FT Simba 0 - 2 AzamKitambala Bola.  82Iddi Nado.  87
07/12/2025

Unadhani Simba wamekosea wapi? au ndiyo ubora wa Azam?
FT Simba 0 - 2 Azam

Kitambala Bola. 82
Iddi Nado. 87

Renatus Mujungu Mujungu achaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Bunda Katika kikao hicho cha kwanza cha b...
07/12/2025

Renatus Mujungu Mujungu achaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Bunda

Katika kikao hicho cha kwanza cha baraza la madiwani mkuu wa wilaya ya Bunda mhe Aswege Enock Kaminyoge ameelekeza madiwani kupata mafunzo ili wajue wajibu wao.

06/12/2025

Camera za Redio Mazingira FM zimerekodi wananchi wa Wilaya ya Bunda, mkoani Mara, wanaoishi pembezoni mwa Ziwa Victoria wakiendelea na shughuli zao za kila siku katika maeneo ya ziwa hilo.

Hii ni pamoja na matumizi ya vizimba vilivyojengwa na serikali kwa ajili ya kuwalinda dhidi ya hatari ya kushambuliwa na mamba.

Vizimba hivyo vimekuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa maeneo hayo, hasa kwa wale wanaoosha, kuchota maji au kufanya shughuli nyingine karibu na ziwa, kwani sasa wanafanya shughuli hizo wakiwa katika mazingira salama zaidi.

Address

Nmb Street
Bunda
31530-51BUNDA

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mazingira Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mazingira Fm:

Share

Category