17/12/2025
Mvulana mwenye umri wa miaka 15, mkazi wa Kijiji cha Marambeka, Kata ya Ketare wilayani Bunda, Festo Mramba amejeruhiwa na kitu chenye ncha kali mguuni eneo la kisigino chanzo kikielezwa ni baada ya ng'ombe kuruka uzio na kuingia kwenye eneo la mtu mwingine wakati akiwa anachunga mifugo katika eneo lao.
Katika tukio hilo lililotokea tarehe 13 Desemba, 2025, majira ya saa 10 jioni, Festo amesema aliporuka uzio kwa lengo la kumrudisha ng’ombe huyo, k**a alivyoelekezwa na mmiliki wa eneo hilo Yona Katani, ambaye anatajwa kuwa mtuhumiwa wa tukio hilo, ghafla alirushiwa jiwe na alipogeuka kukimbia, mtuhumiwa alimrushia panga lililomjeruhi mguu wa kulia eneo la kisigino.
Mazingira Fm imemfikia mtoto huyo kujua kilichotokea na kufika kwa uongozi wa serikali ya kijiji ambao umethibitisha kupokea taarifa za tukio hilo na kueleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa kuzuia migogoro hiyo kwa wananchi