Veriafya

Veriafya Chanzo namba moja cha Taarifa, Elimu na Dondoo za Afya kwa Kiswahili

Kwa mtazamo wa Kisayansi na Kiafya, gari lolote lililoegeshwa, iwe limezimwa au bado limewaka lakini halina mfumo wa Uba...
14/02/2025

Kwa mtazamo wa Kisayansi na Kiafya, gari lolote lililoegeshwa, iwe limezimwa au bado limewaka lakini halina mfumo wa Ubaridi (AC) unaofanya kazi ipasavyo, linaweza kuwa hatari kwa mtoto aliyeko ndani. Joto la gari iliyofungwa linaweza kupanda kwa zaidi ya nyuzi 10–15°C ndani ya dakika 10 za kwanza, na linaweza kufikia kiwango cha hatari cha zaidi ya 50°C ikiwa litaachwa kwa muda mrefu

Katika hali k**a hizi, Mtoto mwenye Umri chini ya Miaka 6 anaweza kupata Kiharusi cha Joto kali (Heat Stroke), hali inayoweza kusababisha Homa kali, Kuweweseka, Kuchanganyikiwa, Kuzimia, Kushindwa kufanya kazi kwa viungo Muhimu vya Mwili k**a Figo na hatimaye Kifo ikiwa haitadhibitiwa haraka.

Kwa kuzingatia haya, ni muhimu kuhakikisha kuwa mtoto haachwi ndani ya gari, iwe limezimwa au linawaka bila mfumo mzuri wa kuhifadhi Ubaridi na Kuruhusu kuingia na Kutoka kwa Hewa.

Kwa Tanzania, baadhi ya Mifano ya Vifo vya aina hii ni vile vilivyohusisha Watoto 2 Dar es Salaam (2007), Watoto 4 Zanzibar (2017) na Watoto wengine 2 Mkoani Shinyanga (2023)

Idadi ya Wanaume wanaougua ‘Fat Wallet Syndrome’ au ‘Wallet Neuritis’ imeongezeka kwa miaka ya hivi karibuni. Hili ni ta...
13/02/2025

Idadi ya Wanaume wanaougua ‘Fat Wallet Syndrome’ au ‘Wallet Neuritis’ imeongezeka kwa miaka ya hivi karibuni. Hili ni tatizo linalosababishwa na kuweka Wallet kubwa kwenye Mifuko ya Nyuma ya Suruali* ambazo hugandamiza Mishipa ya Fahamu, huondoa usawa wa Mwili na kupindisha Uti wa Mgongo wanapokaa, na kusababisha Maumivu ya Mgongo na Kiuno.

Ili kuepuka hali hii, Wanaume wanashauriwa kutojaza wallet zao na vitu vingi k**a Pesa, Kadi na Vitambulisho. Pia, inashauriwa kuweka Wallet kwenye mifuko ya mbele wanapokaa ili kupunguza athari hizi zinazoonekana baada ya muda mrefu.

Mtag Mwanaume anayebeba Wallet kubwa ili ajifunze kwani Kinga ni bora kuliko tiba.

Kujilinganisha na wengine, hasa kupitia Mitandao ya kijamii, kunahusishwa na kuongezeka kwa Msongo wa Mawazo miongoni mw...
13/02/2025

Kujilinganisha na wengine, hasa kupitia Mitandao ya kijamii, kunahusishwa na kuongezeka kwa Msongo wa Mawazo miongoni mwa vijana. Utafiti wa *Twindi & Joiner (2017)* ulibaini kuwa vijana wanaojilinganisha mara kwa mara na wenzao kwenye Mitandao ya kijamii wanakabiliwa na viwango vya juu vya Wasiwasi, Huzuni na Msongo wa Mawazo. Hii ni kwa sababu wanapolinganisha maisha yao na yale wanayoona kwa wengine, ambayo mara nyingi huwasilishwa kwa njia chanya kupita kiasi huhisi kuwa maisha yao hayana Thamani au Mafanikio ya kutosha.

Tafiti zingine za sasa pia zinaonesha kuwa tabia hii inaweza kusababisha kujiona duni na hata kupatwa na Changamoto za Afya ya Akili.

Kwa hivyo, ni muhimu kwa vijana kuelewa kuwa kile wanachokiona Mtandaoni si taswira halisi ya maisha ya watu wengine, bali ni sehemu zilizochaguliwa kwa makusudi ili kuonekana kamilifu.

“Ule wekundu wa Nyama tunaouona kwenye Nyama zetu tunazokula ni sababu ya Madini ya Myoglobin ambayo ukila kwa wingi hiy...
13/02/2025

“Ule wekundu wa Nyama tunaouona kwenye Nyama zetu tunazokula ni sababu ya Madini ya Myoglobin ambayo ukila kwa wingi hiyo Protini inaweza kuathiri Figo. Ulaji wa Nyama wa kupitiliza na wote tunajua, na ndo maana mnasikia saa zingine tunashauri baadhi ya Wagonjwa wanatakiwa kupunguza Nyama nyekundu sababu ile Myoglobin nyingi hufanya damu iwe kwenye hali ya Tindikali (Acidity) ambayo kuiondoa kwenye damu inakuwa shida na Pale ndipo Figo zinapoathirika”

Prof. Mohamed Janabi, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili na Mshauri wa Rais kuhusu Masuala ya Afya alisema haya Aprili 7, 2024 kupitia Afya Podcast ya Muhimbili TV alipokuwa akifafanua tabia Mbaya 10 zinazohatarisha afya ya Figo.

Pia, alitaja mambo k**a Unywaji wa Pombe nyingi, Uvutaji wa Sigara, Kutokunywa maji mengi na Matumizi Makubwa ya Chumvi na Sukari kuwa miongoni mwa Sababu zingine zinazochangia Kuharibika kwa Figo

Wazazi wanapaswa kuanza kuzingatia Faragha mbele ya Mtoto anapofikia Umri wa Miaka 2 na kuendelea. Katika hatua hii, Wat...
12/02/2025

Wazazi wanapaswa kuanza kuzingatia Faragha mbele ya Mtoto anapofikia Umri wa Miaka 2 na kuendelea. Katika hatua hii, Watoto huanza kuelewa na kuiga tabia za watu wanaowazunguka, hivyo ni muhimu kuwafundisha kuhusu mipaka ya Mwili. Kujenga utaratibu wa kutovua nguo mbele yao husaidia kuwaandaa kuelewa maana ya Faragha na heshima ya mwili.

Kadri watoto wanavyokua, wanapaswa kuelewa Thamani ya faragha na mipaka ya mwili ili kuwasaidia kujenga heshima kwao wenyewe na kwa wengine. Pia, hii huwapa Msingi wa kujilinda na kuelewa mabadiliko ya miili yao kwa njia sahihi.

Kuendelea kuvua nguo mbele yao kunaweza kuwachanganya, hivyo ni muhimu kuwapa mwongozo unaowasaidia kuelewa maadili na utu wao bila mkanganyiko wa Kisaikolojia.

Baadhi ya Mihogo, hasa ile yenye ladha ya Uchungu, ina Kemikali zinazoweza kubadilika na kuwa Sumu Mwilini. Kemikali hiz...
12/02/2025

Baadhi ya Mihogo, hasa ile yenye ladha ya Uchungu, ina Kemikali zinazoweza kubadilika na kuwa Sumu Mwilini. Kemikali hizi (Cyanide), zinapovunjwa ndani ya mwili, hutengeneza sumu inayoweza kuzuia mwili kutumia Oksijeni vizuri, jambo linaloweza kusababisha Madhara k**a Kichefuchefu, Maumivu ya tumbo, Kizunguzungu, Kifafa na hata Kifo.

Ili kuzuia Sumu hii, Mihogo Michungu inapaswa kuandaliwa kwa uangalifu. Njia salama ni k**a kuiloweka kwenye maji kwa muda mrefu, Kuchemsha, Kukaanga, au Kuikausha kabla ya kula. Njia hizi husaidia kuondoa sumu na kuifanya mihogo iwe salama kwa chakula. Ikiwa haitachakatwa vizuri, ulaji wake unaweza kuwa hatari kwa afya.

Kwa Tanzania, vipo visa kadhaa vilivyowahi kuripotiwa kuhusu suala hili ikiwemo vifo vya Watoto 3 wa familia moja mwaka 2016 na vifo vingine vya Watoto 4 wa familia moja mwaka 2019.

Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Magonjwa ya Ngono na Homa ya Ini (NASHCoP), Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAI...
12/02/2025

Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Magonjwa ya Ngono na Homa ya Ini (NASHCoP), Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Shirika la Aids Healthcare Foundation (AHF) kwa pamoja wataadhimisha siku ya Kondomu Duniani kwa mara ya kwanza nchini Februari 13 Februari, 2025.

Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Magonjwa ya Ngono na Homa ya Ini (NASHCoP), Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Shirika la Aids Healthcare Foundation (AHF) kwa pamoja wataadhimisha siku ya Kondomu Duniani kwa mara ya kwanza nchini siku hiyo.

Kufanya tendo la Ndoa asubuhi kuna faida mbalimbali za kiafya kulingana na Tafiti za Kisayansi. Kwanza, huongeza kiwango...
10/02/2025

Kufanya tendo la Ndoa asubuhi kuna faida mbalimbali za kiafya kulingana na Tafiti za Kisayansi.

Kwanza, huongeza kiwango cha Homoni za furaha (Endorphins) na Oxytocin, homoni zinazoboresha hisia na kupunguza Msongo wa Mawazo.

Pili, huimarisha Kinga ya Mwili kwa kuongeza kiwango cha Immunoglobulin A (IgA), ambayo husaidia kupambana na Magonjwa. Tafiti pia zinaonesha kuwa tendo hili likifanyika asubuhi huongeza Homoni za Kiume (Testosterone) kwa wanaume, kuboresha afya ya Moyo na Misuli. Aidha, huchochea mzunguko mzuri wa damu na kuimarisha Nishati kwa siku nzima.

Faida hizi hufanya tendo la Ndoa linalofanyika Asubuhi kabla ya Kuanza majukumu yako kuwa na athari chanya kwa afya ya mwili na Akili.

Baada ya saa kadhaa za usingizi, mwili hupoteza maji kupitia jasho na kupumua. Kunywa maji mara tu baada ya kuamka huusa...
10/02/2025

Baada ya saa kadhaa za usingizi, mwili hupoteza maji kupitia jasho na kupumua. Kunywa maji mara tu baada ya kuamka huusaidia mwili kurudi katika hali nzuri, kusafisha sumu kupitia figo, na kuimarisha mmeng’enyo wa chakula.

Pia, maji huongeza umakini kwa kuufanya ubongo ufanye kazi vizuri na kusaidia kudhibiti uzito kwa kupunguza njaa.

Unashauriwa kunywa glasi 1-2 za maji asubuhi kwa afya bora. Hata hivyo, maji hayo hayatakiwi kuwa ya baridi sana.

Utafiti wa Chuo Kikuu cha Muhimbili uliochapishwa kwenye Jarida la MDPI, Septemba 8, 2022 ukihusisha Uchunguzi kwenye ma...
10/02/2025

Utafiti wa Chuo Kikuu cha Muhimbili uliochapishwa kwenye Jarida la MDPI, Septemba 8, 2022 ukihusisha Uchunguzi kwenye machinjio ya Shekilango na Manzese uligundua viwango vya juu vya dawa za Kuua Vimelea (Antibiotics) kwenye Kuku wa Kisasa wanaochinjwa na kuuzwa, hali inayoweza kuchangia Usugu wa vimelea

Hali hii inaweza kufanya magonjwa k**a UTI, Nimonia, Kaswende, Kifua Kikuu na Kisonono kuwa magumu kutibika, na kuongeza vifo na mzigo wa kiafya na kiuchumi kwa Jamii.

Tuchukue hatua. Tufuatilie ubora wa nyama tunayokula na tuepuke matumizi holela ya Dawa za Antibiotics kwa Wanyama ili tujiepushe na Janga hili linaloua watu takriban Milioni 5 kila Mwaka.

Mlonge ni mmea wenye virutubisho zaidi ya 90 vinavyofaa kwa Afya ya Binadamu Majani yake yana vitamini A, C na Madini Ch...
10/02/2025

Mlonge ni mmea wenye virutubisho zaidi ya 90 vinavyofaa kwa Afya ya Binadamu Majani yake yana vitamini A, C na Madini Chuma yanayosaidia kuimarisha kinga ya mwili na kuongeza Damu. Pia, mbegu na mafuta ya mlonge husaidia kuboresha afya ya ngozi na nywele kwa sababu yana Viondoasumu vinavyopambana na Sumu Mwilini.

Kwa wale wenye Shinikizo kubwa la damu (Presha) au Kisukari, Mlonge husaidia kupunguza kiwango cha Sukari na kudhibiti Presha.

Hata hivyo, kwa Wajawazito, usalama wake bado haujawekwa wazi sana hivyo ni muhimu kupata Ushauri wa Daktari kabla ya Kutumia

Tukio hili la kusikitisha limetokea Nchini Nigeria katika Hospitali ya Lebechi iliyoko Owerri, Jimbo la Imo na kuzua has...
08/02/2025

Tukio hili la kusikitisha limetokea Nchini Nigeria katika Hospitali ya Lebechi iliyoko Owerri, Jimbo la Imo na kuzua hasira kwa Watu baada ya Madaktari kuripotiwa kutazama mafunzo kwenye Mtandao wa YouTube ili wafanye Upasuaji kwa Mwanamke mwenye Uchungu wa Kujifungua hivyo kusababisha kifo chake na Mwanaye.

Mume aliyefiwa, Onyekachi Eze, alisimulia tukio hilo la kuhuzunisha na kubainisha kuwa alimpeleka mkewe hospitalini ambaye alikuwa katika uchungu wa kujifungua, ambapo Madaktari walimweleza kwamba alihitaji upasuaji wa dharura kutokana na kuvuja damu nyingi hata hivyo alishtuka alipomshuhudia daktari na wauguzi wakitazama video ya YouTube wakati wa upasuaji.

“Mbele yangu, walikuwa wakitumia simu zao kutazama video ya YouTube kuhusu jinsi ya kufanya upasuaji. Nilipoteza mke wangu na mtoto wangu wakati wa mchakato” amesema Eze.

Kwa mujibu wa Ripoti Mbalimbali, Mmiliki wa hospitali hiyo pamoja na baadhi ya Wauguzi wamek**atwa huku madaktari waliohusika na upasuaji huo wanaendelea kutafutwa baada ya kutoroka.

Usisafishe Pasi kwa Panadol ni hatari kwa Afya kwani Panadol inapoyeyuka kwa moto, hutoa gesi zenye sumu k**a formaldehy...
08/02/2025

Usisafishe Pasi kwa Panadol ni hatari kwa Afya kwani Panadol inapoyeyuka kwa moto, hutoa gesi zenye sumu k**a formaldehyde na Nitrates, ambazo zinaweza kusababisha Miwasho kwenye Macho, Koo na Ngozi, Maumivu ya Kichwa, Matatizo ya Kupumua na kwa muda mrefu, huongeza hatari ya Magonjwa Sugu k**a Saratani.

Badala ya kutumia Panadol, tumia njia salama k**a kuchanganya Baking soda na maji kutengeneza pasta laini, kisha ipake kwenye pasi iliyo baridi na uifute kwa kitambaa. Pia, unaweza kutumia Vinegar na Chumvi kusafisha mabaki ya uchafu kwa ufanisi.

Afya yako ni muhimu. Epuka kutumia kemikali zisizo salama kwenye vifaa vya nyumbani. Kwa usafi bora wa pasi bila madhara, chagua mbinu za asili na zilizo salama kwa mazingira na afya yako.

“Mara ya mwisho mimi kunywa Juisi au Soda ni Mwaka 2000. Iko hivi, kuna tofauti kubwa ya kula chungwa na kunywa juisi ya...
08/02/2025

“Mara ya mwisho mimi kunywa Juisi au Soda ni Mwaka 2000. Iko hivi, kuna tofauti kubwa ya kula chungwa na kunywa juisi ya Chungwa. Nikinywa Juisi nakunywa Sukari moja kwa moja hata k**a haijawekewa sukari. Mfano, ili nipate glasi moja ya Juisi ya Chungwa nahitaji Machungwa matano. Asubuhi umekunywa glasi moja ya juisi, hayo ni Machungwa Matano. Mchana umekunywa glasi ya pili, hayo ni machungwa 10. Jioni umekunywa glasi nyingine, yanakuwa machungwa 15 kwa siku. Kwa siku 10 ni machungwa 150, Kwa mwezi ni machungwa 450. Umekula shamba”

Prof. Janabi alitoa ushauri huu Oktoba 8, 2024 kupitia Afya Podcast ya Muhimbili TV wakati anatoa Elimu juu ya Magonjwa yasiyo ya Kuambukiza huku akisisitiza kuwa matunda huwa na sukari ya Fructose ambayo ikitumika kwa wingi inaweza kuwa na hatari kwa afya.

Alibainisha kuwa Juisi huwa na Mjumuiko wa Matunda mengi hivyo ni Muhimu kula tunda lenyewe kwani ni ngumu mtu kula matunda mengi kwa wakati mmoja, pia huwa na nyuzilishe zenye manufaa kwa afya

Wizara ya Afya imebaini wepo wa taarifa kwenye mitandao ya kijamii pamoja na vyombo vingine vya habari zikielezea uhaba ...
08/02/2025

Wizara ya Afya imebaini wepo wa taarifa kwenye mitandao ya kijamii pamoja na vyombo vingine vya habari zikielezea uhaba wa dawa za kufubaza makali ya Virus vya UKIMWI (ARV),na kwamba sasa watumiaji wanalazimika kunnua dawa hizo. Taarifa hizi ni za upotoshaji na zimeleta hofu miongoni mwa wananchi na kusababisha baadhi ya wagonjwa kuomba kupewa dawa za muda mrefu kwa ajili ya akiba, jambo ambalo si sahihi na linaweza kuathiri utunzaji na matumizi sahihi ya dawa.

Serikali kupitia Wizara ya Afya, inapenda kuwahakikishia wananchi kuwa dawa za kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI Haziuzwi na kwamba zipo za Kutosha. Watumiaji wa dawa hizi, hawana sababu ya kuwa na wasiwasi kuhusu upatikanaji wa dawa hizi. Serikali kupitia Wizara inaendelea kuwea mikakati thabiti na stahiki ili khakikisha huduma zinaendelea kutolea k**a kawaida.

Aidha, Wizara inatoa rai kwa wananchi kupuuza taarifa hizi na kwamba imetenga fedha za kununua dawa zingine ikiwa akiba iliyopo itapungua.

Kuvuta Sh**ha kunaweza kuwa na madhara makubwa kwa Wanawake hasa kwenye Afya ya Uzazi kutokana na kemikali hatari zinazo...
07/02/2025

Kuvuta Sh**ha kunaweza kuwa na madhara makubwa kwa Wanawake hasa kwenye Afya ya Uzazi kutokana na kemikali hatari zinazopatikana katika moshi wake.

Tafiti za kisayansi zinaonesha kuwa moshi wa Sh**ha una kiwango kikubwa cha Carbon Monoxide, Nikotini, Metali nzito k**a Risasi, na kemikali zinazoweza kusababisha Saratani.

Kwa wanawake, kuvuta sh**ha kunaweza kuongeza hatari ya matatizo ya Uzazi k**a vile Ugumba, Ukavu wa Uke, Mimba kuharibika au kujifungua Mtoto njiti. Pia, kemikali zinazopatikana kwenye sh**ha zinaweza kuathiri mfumo wa homoni na kuongeza hatari ya Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu.

Ingawa kitanzi ni njia salama ya uzazi wa mpango, hakilindi dhidi ya magonjwa ya zinaa k**a VVU, kisonono na kaswende. I...
07/02/2025

Ingawa kitanzi ni njia salama ya uzazi wa mpango, hakilindi dhidi ya magonjwa ya zinaa k**a VVU, kisonono na kaswende. Ikiwa mtu ana wapenzi wengi au mpenzi wake ana maambukizi, anaweza kupata magonjwa haya kwa urahisi.

Pia, kitanzi huongeza hatari ya maambukizi ya njia ya uzazi (PID) kwa Mwanamke ikiwa bakteria wataingia kupitia mlango wa kizazi. PID inaweza kusababisha maumivu makali, Kutokwa na Uchafu Ukeni au Ugumba. Vilevile, uwepo wa kitanzi unaweza kuongeza uwezekano wa kupata UTI za mara kwa mara hasa kwa wale walio na historia ya maambukizi ya njia ya mkojo.

Ni muhimu kufanya uchunguzi wa afya kabla ya kutumia kitanzi na kudumisha usafi, uaminifu kwa mpenzi mmoja, na kutumia kinga inapobidi!

Kabla ya kuanza mazoezi ya gym, ni muhimu kupima afya yako ili kuepuka hatari zisizotarajiwa. Mazoezi mazito yanaweza ku...
07/02/2025

Kabla ya kuanza mazoezi ya gym, ni muhimu kupima afya yako ili kuepuka hatari zisizotarajiwa. Mazoezi mazito yanaweza kuongeza shinikizo la damu, kuathiri moyo, Kudondoka ghafla au hata kuleta madhara kwa viungo k**a misuli na mifupa ikiwa mwili hauko tayari.

Kupima afya husaidia kugundua magonjwa yaliyofichika k**a shinikizo la damu, ugonjwa wa moyo au kisukari, ambayo yanaweza kuwa hatari wakati wa mazoezi. Pia, daktari au mtaalamu wa afya anaweza kupendekeza aina sahihi ya mazoezi kulingana na hali yako.

Linda afya yako kwa kufanya vipimo kwanza, kisha fanya mazoezi kwa usalama!

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share