
20/09/2025
Kuvaa viatu virefu kwa muda mrefu huathiri Afya taratibu bila Mhusika kugundua. Viatu hivi hubadili Jinsi unavyotembea na kusababisha Shinikizo kubwa kwenye Vidole, Kiuno, Magoti na Mgongo. Matokeo yake ni maumivu ya Miguu, Majeraha ya Misuli na hata matatizo ya Mgongo, Magoti na Kisigino yanayoweza kutokea baadaye maishani, hasa baada ya kufikia umri wa Ukomo wa Hedhi
Pia, High Heels zinaweza kufanya miguu ichoke haraka na kupunguza mzunguko wa Damu, jambo linaloweza kusababisha mishipa kuvimba na Miguu kuwa mizito.
Kwa afya bora ya miguu, inashauriwa kuvaa High Heels kwa muda usiozidi Masaa 2-4 kwa siku. Ikiwa unahitaji kuvaa kwa muda mrefu, hakikisha unapata muda wa kupumzisha miguu yako kwa kuvua viatu hivyo mara kwa mara na kufanya mazoezi ya kunyoosha miguu.