Veriafya

Veriafya ⚡Afya tu!

Kuvaa viatu virefu kwa muda mrefu huathiri Afya taratibu bila Mhusika kugundua. Viatu hivi hubadili Jinsi unavyotembea n...
20/09/2025

Kuvaa viatu virefu kwa muda mrefu huathiri Afya taratibu bila Mhusika kugundua. Viatu hivi hubadili Jinsi unavyotembea na kusababisha Shinikizo kubwa kwenye Vidole, Kiuno, Magoti na Mgongo. Matokeo yake ni maumivu ya Miguu, Majeraha ya Misuli na hata matatizo ya Mgongo, Magoti na Kisigino yanayoweza kutokea baadaye maishani, hasa baada ya kufikia umri wa Ukomo wa Hedhi

Pia, High Heels zinaweza kufanya miguu ichoke haraka na kupunguza mzunguko wa Damu, jambo linaloweza kusababisha mishipa kuvimba na Miguu kuwa mizito.

Kwa afya bora ya miguu, inashauriwa kuvaa High Heels kwa muda usiozidi Masaa 2-4 kwa siku. Ikiwa unahitaji kuvaa kwa muda mrefu, hakikisha unapata muda wa kupumzisha miguu yako kwa kuvua viatu hivyo mara kwa mara na kufanya mazoezi ya kunyoosha miguu.

Mtindi unaweza kusaidia kuondoa changamoto ya Choo Kigumu kwakuwa ni chanzo kizuri cha Probiotics (Bakteria wazuri) amba...
19/09/2025

Mtindi unaweza kusaidia kuondoa changamoto ya Choo Kigumu kwakuwa ni chanzo kizuri cha Probiotics (Bakteria wazuri) ambazo husaidia kuleta usawa wa Bakteria kwenye Tumbo, hivyo kuboresha mmeng'enyo wa chakula.

Pia, huwa na Asidi ya Laktiki (Lactic Acid) inayoweza kusaidia katika kuongeza mijongeo ya Tumbo na Utumbo hivyo kupunguza ugumu wa Choo.

Mtungi wa gesi ya kupikia unapaswa kuhifadhiwa nje ya nyumba kwa sababu za kiusalama. Hii ni kwa sababu presha ikizidi M...
18/09/2025

Mtungi wa gesi ya kupikia unapaswa kuhifadhiwa nje ya nyumba kwa sababu za kiusalama. Hii ni kwa sababu presha ikizidi Mtungi unaweza kupasuka ambaoo ikitokea hali hii nafasi ya kupona ni ndogo sana, au gesi inaweza kuvuja bila wewe kugundua, na ikiwa itajikusanya ndani ya nyumba, inaweza kusababisha mlipuko au moto mkubwa endapo itakutana na cheche au moto wa wazi.

Pia, gesi iliyovuja inaweza kuwa hatari kwa afya, kwani inapovutwa kwa muda mrefu inaweza kusababisha maumivu ya kichwa, kizunguzungu na hata kukosa hewa. Ikiwa mtungi wa gesi unahifadhiwa ndani, hasa kwenye maeneo yasiyo na uingizaji hewa wa kutosha, hatari hizi zinaongezeka maradufu.

Ili kuhakikisha usalama wako na wa familia yako, inashauriwa mtungi wa gesi uwekwe nje ya nyumba mahali pakavu, penye kivuli na uingizaji hewa wa kutosha. Pia, hakikisha mrija unaounganisha mtungi na jiko umefungwa vizuri, hauvuji na ubadilishwe kila baada ya Miaka 2.

Kuweka Mswaki chooni si salama kwa afya yako. Hii ni kwa sababu choo kina Bakteria na Vimelea vinavyoweza kuambukiza Msw...
17/09/2025

Kuweka Mswaki chooni si salama kwa afya yako. Hii ni kwa sababu choo kina Bakteria na Vimelea vinavyoweza kuambukiza Mswaki wako.

Pia, chooni kuna Unyevu Mwingi unaosaidia Bakteria na Fangasi kukua kwa urahisi hivyo kuwa chanzo cha Magonjwa ya kinywa na meno.

Ili kulinda afya yako, ni vyema kuhifadhi Mswaki mahali Pakavu na penye hewa safi, mbali na Choo.

Wanawake Wajawazito, hasa katika miezi ya mwisho ya Ujauzito, mara nyingi hukumbana na changamoto ya kujinyoa sehemu za ...
16/09/2025

Wanawake Wajawazito, hasa katika miezi ya mwisho ya Ujauzito, mara nyingi hukumbana na changamoto ya kujinyoa sehemu za siri kutokana na ukubwa wa tumbo na ugumu wa kufikia maeneo hayo. Ingawa kunyoa si jambo la lazima kiafya, wengine huona ni muhimu kwa sababu za usafi au maandalizi ya kujifungua.

Ili kuwasaidia, Mjamzito anaweza kutumia mbinu mbalimbali. Moja ni kutumia kioo cha Mkononi ili kuona vizuri sehemu anazotaka kunyoa. Pia, anaweza kutumia mashine ya kunyoa (trimmer) badala ya wembe wa kawaida ili kuepuka michubuko au pia kuomba msaada kutoka kwa Mumewe au Mchumba wake, ambaye anaweza kumsaidia kwa uangalifu na kwa kuzingatia usafi.

Muhimu zaidi ni kuhakikisha usafi na kutumia njia salama ili kuepuka maambukizi au madhara yoyote kwenye ngozi, hasa katika kipindi hiki ambacho kinga ya mwili wa Mjamzito huwa dhaifu.

Daktari aitwaye Suhail Anjum (44), raia wa Pakistan, ameripotiwa kuondoka katikati ya upasuaji kwenda kufanya mapenzi na...
14/09/2025

Daktari aitwaye Suhail Anjum (44), raia wa Pakistan, ameripotiwa kuondoka katikati ya upasuaji kwenda kufanya mapenzi na nesi, tukio hilo lilitokea katika hospitali ya Manchester.

Daktari alisema alikuwa anaenda "kupumzika kidogo", lakini badala yake akaenda kukutana kimapenzi na nesi ndani ya hospitali hiyo. Kwa bahati nzuri, mgonjwa hakupata madhara kwa sababu upasuaji uliendelea na madaktari wengine waliokuwepo.

Kwa sasa, daktari huyo amerudi Pakistan, na hajarejea tena kazini Uingereza. Tume ya madaktari bado inachunguza k**a anastahili kuendelea na kazi ya Udaktari.

Kuvaa Sidiria kwa muda mrefu, hasa ikiwa inabana sana, kunaweza kusababisha maumivu ya Mgongo na kuzuia mtiririko mzuri ...
14/09/2025

Kuvaa Sidiria kwa muda mrefu, hasa ikiwa inabana sana, kunaweza kusababisha maumivu ya Mgongo na kuzuia mtiririko mzuri wa Damu. Hii hutokea kwa sababu Sidiria inayobana inaweza kushinikiza misuli ya mabega na mgongo na kusababisha maumivu ya muda mrefu. Pia, inaweza kuathiri mzunguko wa damu kifuani na maeneo ya karibu, jambo linaloweza kusababisha usumbufu na uchovu wa misuli.

Ili kuepuka matatizo haya, ni vyema kuchagua sidiria yenye saizi sahihi na isiyobana sana. Pia, inapendekezwa kuvua sidiria unapopumzika nyumbani au wakati wa kulala ili kuruhusu mwili kupumzika.

Ikiwa unapata maumivu ya mgongo mara kwa mara, jaribu kufanya mazoezi ya kunyoosha mgongo na mabega mara kwa mara.

"Unajua kwanini watu wanafunga Kwaresma, unajua kwanini Waislamu wanafunga mwezi wa Ramadhan, Shaaban na miezi mingine? ...
11/09/2025

"Unajua kwanini watu wanafunga Kwaresma, unajua kwanini Waislamu wanafunga mwezi wa Ramadhan, Shaaban na miezi mingine? Kwasababu hata huyo aliyetuumba hakutaka tule ovyo. Kwa mfano asububi, nina uhakika mmeona hata nyumbani kwenu mnapata shida sana kuwapa watoto chakula asubuhi, lazima muwalazimishe na watoto wanakuwa hawataki. Unajua kwanini? Sasa mimi nakueleza kidaktari. Asubuhi ni kipindi ambacho ile homoni ya njaa inaitwa Ghrelin ipo chini kabisa, hamna mtu mwenye njaa asubuhi. Wewe leo umekunywa chai si kwamba ulikuwa na njaa, ni kwa sababu ni asubuhi, ni Mazoea"

Prof. Janabi, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika alizungumza haya Upendo Media, Oktoba 8, 2024 ambapo alisisitiza umuhimu wa kutunza afya kwa kula mlo bora.

Aidha, aliwaasa vijana kutokupuuzia tabia ya Kutunza afya kwa kula vizuri na kufanya Mazoezi kwani magonjwa Mengi yanayoonekana uzeeni hutengenezwa wakati wa Ujana.

Kwa mara ya kwanza duniani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limetoa taarifa inayoonesha kuwa Wa...
11/09/2025

Kwa mara ya kwanza duniani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limetoa taarifa inayoonesha kuwa Watoto na vijana wenye miaka 5-19 wenye Viribatumbo ni wengi kuliko wale wenye uzito mdogo.

Taarifa hii ya Septemba 9, 2025, pamoja na mambo mengine imetaja sababu za kuongezeka kwa Viribatumbo kuwa ni ulaji wa vyakula vingi vya Haraka 'Fast food', Unywaji wa vinywaji vya Viwandani vyenye Sukari za nyongeza pamoja na vyakula vilivyoongezewa Kemikali vinavyouzwa kwenye Maduka makubwa (Supermarkets)

Ni muhimu kwa wazazi kulinda watoto kwa kuwapatia vyakula vyenye virutubisho kwani Viribatumbo husababisha Kuoza meno, Presha, Kisukari pamoja na Magonjwa mengine yasiyo ya kuambukiza yanayoweza kuhatarisha maisha ya sasa na baadae.

Mswaki unapaswa kubadilishwa kila baada ya miezi 3 ili kuhakikisha usafi wa kinywa na meno. Baada ya muda, nyuzi zake hu...
09/09/2025

Mswaki unapaswa kubadilishwa kila baada ya miezi 3 ili kuhakikisha usafi wa kinywa na meno. Baada ya muda, nyuzi zake huchakaa na kushindwa kusafisha vizuri, huku zikiwa na bakteria wanaoweza kusababisha kuoza kwa meno na magonjwa ya fizi.

Kubadilisha mswaki hupunguza harufu mbaya ya kinywa, huimarisha afya ya fizi, na kuzuia maambukizi.

Nguo ya ndani inapaswa kubadilishwa kila baada ya miezi 6-12 kwani baada ya muda hukusanya bakteria na unyevunyevu vinavyoweza kusababisha maambukizi.

Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Jagiellonian unaonesha kuwa baba wenye mabinti wana uwezekano wa kuishi muda mrefu ...
08/09/2025

Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Jagiellonian unaonesha kuwa baba wenye mabinti wana uwezekano wa kuishi muda mrefu zaidi, ambapo kila binti mmoja anaweza kuongeza takribani wiki 74 katika maisha yao.

Utafiti huo ulitathmini takwimu kutoka kwa zaidi ya watu 4,300 na kubaini kuwa idadi ya watoto wa kiume haina athari k**a hiyo kwenye urefu wa maisha ya baba.

Aidha, matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa na mabinti kunahusiana na ustawi bora wa kihisia, maisha yenye furaha na kujiamini zaidi kwa baba.

Tafiti mbalimbali zinabainisha kuwa upo uwezekano wa Mtu kupata Kiharusi kutokana na Jeraha linalosababishwa na 'Love Bi...
08/09/2025

Tafiti mbalimbali zinabainisha kuwa upo uwezekano wa Mtu kupata Kiharusi kutokana na Jeraha linalosababishwa na 'Love Bite'. Tafiti hizo zinaeleza kuwa Love Bite ikiwekwa wenye mshipa wa Carotid shingoni huweza kusababisha chembechembe za damu kuzuiwa kufika kwenye Ubongo.

Mathalani, utafiti mmoja unamueleza Mwanamke mwenye miaka 35, aliyetokwa na damu kwenye mshipa wa Carotid baada ya kupata 'Love Bite' upande wa shingo, alikumbwa na kiharusi upande wa kulia wa mwili wake.

Kadhalika, mwaka 2010 nchini New Zealand, Mwanamke wa miaka 44 aligundulika kuwa na chembechembe za damu kwenye shingo, baada ya kupata 'Love Bite', na alikumbwa na kupooza mkono wa kushoto.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share