Matmedia

Matmedia Sports,entertainment,&Media news company

Siku zimepungua, Masaa yanayoyoma dakika zinakimbia sekunde nazo si haba zinashika kasi, Zile siku ambazo hututoa kimaso...
09/09/2025

Siku zimepungua, Masaa yanayoyoma dakika zinakimbia sekunde nazo si haba zinashika kasi,

Zile siku ambazo hututoa kimasomaso machizi soka,walevi wa kabumbu mateja wa kandanda zimegonga hodi, Lupaso huwa siyo uwanja tena hugeuka mbingu kwa siku hizi za Simba day na kileleni kwenye wiki ya wananchi

Udambwi na utamu wa Soka ambalo hutandazwa pale kwa Mkapa huwa ni kitu cha ziada sana ila watu huwa na uchu wa kuvijua vikosi vyao vya msimu, kuziona timu zao ambazo zilizama 'ndichi' kwa ajili ya Pre season kwa zaidi ya siku 30

K**a mnavyojua Soka na Muziki ni kopo na mfuniko
'Machizi' soka huwa tunatamani kupata burudani za A-listed artist kwenye siku zetu hizi za burudani, hii huwa ni zaidi ya Sikukuu kwetu

September 10,2025 Jumatano ni Siku ya Simba, Simba day:
Ukiachana na Show zitakazooneshwa na mtaalamu Babajar, Maema,Mpanzu na Sowah, kuna show ya mkali wa Show zote mjini, yaani mmaliza Pawa za masela na masinyirita

Wengi hatujamshuhudia Mbosso akiwa anazunguka kuimbia watu wengi hasa machizi soka kwenye stadium kubwa k**a Lupaso tena akiimbia timu yake kabisa ya damu yaani Simba SC, sasa nadhani atawaonesha, siandiki sana,

September 12,2025 Kilele cha wiki ya Wananchi,
Huku nyoka wote watatoka pangoni kwa sauti ya Zuhura, nyoka hao watakuwa na jukumu la kwenda kumjibu Zuhura Amanda ndiyo nani?

Kabla ya Ecua kuvunja nyonga za watu, basi zuhura atatunyonga kwanza juukwani tukiinama na kuinuka kisha tutaramba asali then kila mtu atapata nyumba ndogo

Hii ni zaidi ya burudani, nasema hivi kwa sababu wote tuna experience na kwenye show za aina hii, wote tulimuona kwenye Simba Day 2023 ambapo alirambiasha asali machizi soka wote pale Lupaso mwaka ule

SIJUI WEWE UNAISUBIRI SIKU GANI HAPA

Katika Soka Mara nyingi linapikuja suala la kuhoji ubora au ukubwa wa mchezaji huwa kunaibuka hoja kadhaa zinazotetea au...
09/09/2025

Katika Soka Mara nyingi linapikuja suala la kuhoji ubora au ukubwa wa mchezaji huwa kunaibuka hoja kadhaa zinazotetea au kudhihirisha ukubwa na ubora wa nyota huyo,

Moja ya hoja huwa ni Kuitwa katika timu ya taifa, yaani National Team, mchezaji akiwa anaitwa national team wengi hutafsiri kuwa mchezaji huyo ni bora na ni mkubwa,

Pacomé Zouzoua ni moja ya Nyota wenye uwezo mkubwa sana katika ligi namba 04 kwa ubora barani Afrika, NBC Premier League,

Ukiulizwa swali kuwa Pacome ni bora, jibu bila shaka ni ndio, Pacome ni mchezaji mkubwa? Jibu obvious litakuwa ni ndio,

SWALI: Kwa nini haitwi timu ya taifa ya Ivory Coast, au tukubaliane Pacome siyo mchezaji bora wala siyo mchezaji mkubwa, yaani tuna mu exaggerate, tuna m hype, yaani anapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa, kwamba ni mchezaji mdogo sana!

Au kwa sababu...
ANACHEZA LIGI DHAIFU:
Tukubaliane kuwa Ligi yetu siyo ligi shindani inayoweza kutoa mchezaji wa kucheza timu ya Ivory Coast, I vory Coast wana nyota lukuki wanaotoka ligi zenye ushindani mkubwa k**a EPL,League One, Bundes Liga na Serea A, hivyo NBC PL haitoshi kumpeleka Pacome National Team

ANA UWEZO WA KAWAIDA SANA:
Pengine Pacome anaonekana mkubwa kwa aina ya soka la Tanzania, hana wapinzani wakubwa, pengine waandishi na media zinamkuza tu hana kiwango cha kucheza National Team k**a akina Franck kessie, Sebastian Haller Seko Fana na wengine wengi

UMRI:
Inawezekana Pacome ni mchezaji mzuri, lakini umri wake unasababisha kocha kutomuita na kuita vijana wengine k**a akina Simon Adingra ambao bado wana umri mdogo, hivyo kocha haoni future kwa Pacome katika timu ya taifa

TUPE SABABU YAKO

Mipango BABA
25/05/2025

Mipango BABA

Kuna siku niliwahi kulisema hili na nitaendelea kulisema tena na tena, Mimi sio chawa wala sio King'ang'a lakini mimi pi...
28/02/2025

Kuna siku niliwahi kulisema hili na nitaendelea kulisema tena na tena, Mimi sio chawa wala sio King'ang'a lakini mimi pia sio saa mbovu ila nitatumia vidole vyangu kuwaambia ukweli juu ya hiki ninachoeleza hapa chini,

Who is the best artist between Diamond Platnumz and Ali Kiba?
Hili swali niliamua kuuliza AI ambayo vijana wa kileo wanaiabudu zaidi kuliko bongo zao, nilipewa majibu mengi sana lakini kifupi niliambiwa;

Kila msanii ni mzuri kulingana na wewe utakavyosikiliza na kupendelea aina za muziki wao kwani Ali ni mzuri kwenye loyal and romantic tone na Diamond ni mzuri kwenye Choreography performance na Globally Diamond ni mzuri zaidi yaani ame cross border zaidi kutokana na aina ya muziki wake lakini Ali yupo local anafanya flavor za ndani zaidi,

Majibu ya AI yakanipa nguvu ya kuja kuwathibitishia ule ukweli kuwa Ali Kiba kimataifa hajulikani na hatakaa ashinde tuzo yoyote asipobadilika, yaani huyo King ni King wa Mburahati ila sio King wa Lagos au wa Cape town City kiufupi Ali Kiba kimataifa hana utofauti na Best Naso

Mkasa uliotokea kwenye Trace Music Awards ni uthibitisho mwingine kuwa Ali asijifananishe na Diamond kimataifa,
Wakati Diamond na Rema wakiwa ndio watumbuizaji wakuu Ali aliorodheshwa kwenye watumbuizaji wengine sawa na Abigal Chams, wakati Rema na Diamond wakifanyiwa booking ya Hotel ghari zaidi Ali alilala na wasanii wengine k**a Lodge tu, wakati Rema na Diamond wakipewa dk 15-20 za kuperform Ali alipewa dk 2-4 sawa na Marioo, Harmonize na madogo wengine hata treatment aliyopewa Ali na Diamond kwenye tuzo hizo ilikuwa k**a mbingu na ardhi,

Cha kushangaza Ali aligoma kupanda stejini na kuondoka kwa madai yeye ni msanii mkubwa alipaswa kufanyiwa k**a alivyofanyiwa Diamond Platnumz!

Najaribu kufikiria hili jambo angefanya media zingeandika sana kuwa dogo anadharau kadharau Tuzo lakini kiba bado anapewa 'hype' na ameandaliwa tamasha lingine huko Zanzibar

Mashabiki na media za Tanzania zungumzeni ukweli, Ali Kiba sio msani

Chama lako namba ngapi?
22/10/2024

Chama lako namba ngapi?

KNOW THAT: Baada ya mkutano wa Simba Oktoba 6 Mohammed Dewji atakutana na uongozi wa Kiungo wa zamani wa Yanga SC anayek...
03/10/2024

KNOW THAT: Baada ya mkutano wa Simba Oktoba 6 Mohammed Dewji atakutana na uongozi wa Kiungo wa zamani wa Yanga SC anayekipiga Azam FC kwa sasa Feisal Salum kukamilisha mazungumzo ya upatikanaji wa saini yake dirisha dogo Linalotarajiwa kufunguliwa Desemba 15,

Feisal amebakiza mkataba wa msimu mmoja pekee na wauza ukwaju, huku akiweka wazi hawezi kuongeza mkataba mpya klabuni hapo labda wamlipe kiasi cha Tsh Milioni 70

Mwekezaji huyo wa Simba amekiri kuwa yupo tayari kwa gharama zozote zile Feisal acheze Simba mwezi Januari

Releasing Clause ya Feisal kwa sasa ni Tsh 450Milioni ambapo mwezi December itashuka hadi Ts150Milioni.

Elie Mpanzu amesaini Simba SC miaka mitatu, Winga huyo raia wa Congo ataanza kuitumikia Simba mwezi Januari baada ya dir...
30/09/2024

Elie Mpanzu amesaini Simba SC miaka mitatu, Winga huyo raia wa Congo ataanza kuitumikia Simba mwezi Januari baada ya dirisha dogo kufunguliwa

Timu zilizopiga pasi nyingi ligikuu
30/09/2024

Timu zilizopiga pasi nyingi ligikuu

Mshambuliaji wa Simba SC Jean Charles Ahoua amehusika kwenye mabao sita kati ya mabao 10 ambayo Simba SC imefunga mpaka ...
29/09/2024

Mshambuliaji wa Simba SC Jean Charles Ahoua amehusika kwenye mabao sita kati ya mabao 10 ambayo Simba SC imefunga mpaka sasa

Amecheza jumla ya dakika 289 kwenye mechi nne ambapo amefunga mabao mawili na kutoa pasi za mwisho kwa maana ya Assist nne

Kumbuka msimu wa 2023/24 alikuwa MVP wa Ivory Coast

Msimamo kwenye Top 8 ya   mpaka sasa
29/09/2024

Msimamo kwenye Top 8 ya mpaka sasa

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255769407971

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Matmedia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Matmedia:

Share