Dayocha

Dayocha tunauza nguo zote za kike na kiume katika hii page yetu
Tunakuletea mzigo ulipo ndio unalipia Kwa wak

Just love, sikucheza nao utotoni ila ndio washikaji wa ukubwani. Maisha yanatukutanisha na watu tofauti na kututenganish...
29/06/2024

Just love, sikucheza nao utotoni ila ndio washikaji wa ukubwani. Maisha yanatukutanisha na watu tofauti na kututenganisha pia kila nyakati inasababu ila cha msingi kaa kwenye script tu husipoteze focus tu❤️❤️

🦅*12 Kanuni ngumu za maisha kwa wanaume*:🦅 1. Hakuna anayejali, fanya kazi kwa bidii zaidi. 2. Utawakera watu wengi unap...
25/02/2024

🦅*12 Kanuni ngumu za maisha kwa wanaume*:🦅

1. Hakuna anayejali, fanya kazi kwa bidii zaidi.
2. Utawakera watu wengi unapoanza kufanya yaliyo bora kwako.
3. Watakupuuza hadi watakapokuhitaji.
4. Kila kitu kinaboresha unapoamua kutojali tena.
5. Mambo yanayovunja moyo wako ni yale yale yanayofungua macho yako.
6. Wakati mwingine unahitaji kuacha kuona mema kwa watu na kuanza kuona kile wanachokuonyesha.
7. Watu wengine hawatakuunga mkono kamwe, kwa sababu wanaogopa kile unachoweza kuwa.
8. Watu watakuangusha katika maisha haya, ahadi zitavunjwa, na unapaswa kutarajia kidogo kutoka kwa wengine na kujiamini zaidi kwako mwenyewe.
9. Kuwa mtu mzuri, lakini usipoteze muda kuthibitisha hilo.
10. Jikumbushe: Ikiwa ilikuwa rahisi, kila mtu angefanya hivyo.
11. Ikiwa ni muhimu kwako utapata njia. Ikiwa sivyo, utapata kisingizio.
12. Ikiwa wanafanya k**a wanaweza kuishi bila wewe, wasaidie kufanya hivyo.

Ilikuwa ni Miaka 90'sHii ilitokea Mitaa ya San Francisco Nchini-Marekeni..Kulikuwepo na library Moja Maarufu sana ambapo...
20/02/2024

Ilikuwa ni Miaka 90's

Hii ilitokea Mitaa ya San Francisco Nchini-Marekeni..

Kulikuwepo na library Moja Maarufu sana ambapo Watu Wengi Walikuwa wanaenda kujisomea Siku za weekend

Siku Hiyo kijana Erick nae alienda kujisomea pamoja na Kutafuta Connection

Mbali mbali ya Vijana wenzie...
Baada ya Kuingia Tu akatuta Watu ni Wengi halafu kumetulia Kimyaaa...Kila Mtu yupo Busy
Akatupa Jicho Kulia...akagongana macho Kwa macho na Komwe la Binti Mmoja Mrembo mno...
Erick akanyooka Moja Kwa Moja Mpaka Kwenye
Ile meza alokaa yule Binti...
Alipofika akamnong'oneza yule Binti sikioni...
"Hey... Naweza kukaa Hapa Pembeni Yako?"
Yule Binti akajibu Kwa Sauti Kubwa...
"Unasemaje we kaka?... Mimi Siwezi Kwenda Kulala Kwako"
Watu oooooh Library nzima macho

Kwa Erick Huku wakimshangaa...
Basi Kwa Aibu Erick kimya kimya akaenda Kukaa Meza ya Nyuma ya Binti
Baada ya DKK 3 yule Binti akamgeukia Erick Kisha akamnong'oneza Akamwambia...
"Mimi nasoma Psychology Kwahiyo najua Wanaume Huwa wanawaza Nini"
Nina Uhakika Utakuwa umezalilika si Ndio?....
Erick akajibu na yeye Kwa Sauti Kubwa...
Unasemaje Wewe?...yaani Unataka $200 Kwa Usiku Mmoja Tu...Hapana aisee Hiyo ni Kubwa Sana"
Watu oooooh... macho yote Kwa yule Binti
Aibu Zote kwake...
Erick akamgeukia Kisha akamnong'oneza Akamwambia...
"Mimi Nasoma Sheria... Kwahiyo najua Jinsi ya kuwaingiza Watu Hatiani"

LESSON: Mtu akimwaga Mboga...Wewe Mwaga Ugali usikae kinyonge Utafedheheshwa"

Sio kila unae muona mkimya alizaliwa hivyo HAPANA .wenginge wanavyovipitia  vimewabadilisha kuwa hivyo.
09/02/2024

Sio kila unae muona mkimya alizaliwa hivyo HAPANA .wenginge wanavyovipitia vimewabadilisha kuwa hivyo.

25/01/2024
Tulipewa mamlaka ya kukanyaga nyoka, nng'e na vyote vitaambavyo, believe in you bro.God bring/give confidence in you not...
06/10/2023

Tulipewa mamlaka ya kukanyaga nyoka, nng'e na vyote vitaambavyo, believe in you bro.
God bring/give confidence in you not fear and failure. Tembea kifua mbele k**a unaamini hili

05/10/2023

Sikiliza sauti ya ndani yako, inanguvu sana 🙃🙃

KUNA NGUVU NA MAMLAKA KATIKA MAZUNGUMZO UKIWA UMEKAA.Kila mwanaume anatakiwa kuongea au kufanya maamuzi akiwa amekaa.Hac...
09/07/2022

KUNA NGUVU NA MAMLAKA KATIKA MAZUNGUMZO UKIWA UMEKAA.
Kila mwanaume anatakiwa kuongea au kufanya maamuzi akiwa amekaa.Hacha kuongea na mkeo au watoto wako ukiwa umesimama maana hawatakueshimu.Anza kujifunza kuongea ukiwa umekaa maana unapowaita watoto au mkeo wakikukuta umekaaa wasipokaa husiongee chochote kaa kimya. Kuna nguvu katika ukimya zaidi ya maneno .hakuna mwanamke anayeweza kupigwa na mwanaume aliyekaa hata siku moja
Mfundishe mkeo kukaa chini anapoongea na wewe pia epuka maongezi kipindi umesimama na mkeo.ukimwita mkeo akakaa katika kiti kidogo na wewe umekaa katika kiti kikubwa hata unapowaita watoto wakija lazima watakaa katika balaza chini. hii inamaana kuwa ni amri katika ukaaji hata kimamlaka. Kwa wazee na vijana wa k**amo wananielewa nachomaanisha maana wengi wazee wetu walikuwa na sehemu maarumu za kukaa na kutolea maamuzi.
Ushari kwa vijana wa leo nenda dukani nunuwa kiti kizuri na meza yake ambayo utakuwa unakaa wewe tu na si vinginevyo. Hata ukiitaji maji utakuwa unaletewa hapo pia hata matokeo ya watoto wako unapokelea hapo hapo na maamuzi mengine pia unafanyia hapo.
Siku njema na wikiend njema

15/05/2022

*SAUTI YAKO NDIO UTAMBULISHO*
Sauti yako ndio utambulisho wako japo wengi wetu katika jamii kitu pekee katika "mwonekano wa mwili". Je tunafikilia kuhusu "mwonekano wa sauti" ...
Katika "mwonekano wa mwili" naweza kununuwa tisheti, naweza kununuwa suluali, naweza kununuwa suti nzuri lakini siwezi kununuwa mwonekano wa sauti yako.
Hii ni ngumu pia kwa upande wa vipofu huwa wanatumia mwonekano wa sauti kumtambuwa mtu maana hawaoni.
Jumapili njema

01/01/2022

Siku ya jana ilikuwa hivyo, usiku mwema

Kofia &mkona & kimtandio hichoBei 30000 tuMawasiliano 0654295523
27/12/2021

Kofia &mkona & kimtandio hicho
Bei 30000 tu
Mawasiliano 0654295523

Tunachukuwa nafasi hii kuwatakia Christmas  njema wote wanapage yetu
24/12/2021

Tunachukuwa nafasi hii kuwatakia Christmas njema wote wanapage yetu

24/11/2021

Habarini za majukumu wadau wa page yetu,
Tunatanguliza shukurani za dhati pia mtuwie radhi za kutokuwepo kwa kipindi sasa mtandaoni

Mzigo wa pensi Bei 20000Mawasiliano 0654295523Free delivary kwa dar na mikoani tunatuma kwa uaminifu tu
30/08/2021

Mzigo wa pensi
Bei 20000
Mawasiliano 0654295523
Free delivary kwa dar na mikoani tunatuma kwa uaminifu tu

5G NI NINI?KWANINI ILIHUSISHWA NA UVICO 19 PAMOJA  NA LOCKDOWN?Nawasalimu kwa jamuhuri ya muungano wa  Tanzania wanaukur...
07/05/2021

5G NI NINI?KWANINI ILIHUSISHWA NA UVICO 19 PAMOJA NA LOCKDOWN?

Nawasalimu kwa jamuhuri ya muungano wa Tanzania wanaukurasa wetu wa DAYOCHA. Ngoja twende kwenye mada husika nini maana ya 5G?
5G ni mtandao wa kizazi cha tano katika teknolojia ya mawasiliano. Huku herusi "G" ikiwa imesimama badala ya "Generation" ikimaanisha kizazi cha tano.katika taaruma ya mawasiliano tulianza na 1G ,2G,3G,4G na sasa inasemek**a kuna baba lao linakuja 5G.
Teknolojia ya 1G, au kizazi cha kwanza cha data ya simu, ilianza kutumiwa 1991.

Teknolojia ya 2G ilianza pia kutumika katika kipindi hicho, ikiwa k**a ndugu wa 1G.
Teknolojia hii ya 1G sana ilikuwa analogu ambayo ilimuwezesha mtumiaji kuweza kupiga simu tu na simu za wakati huo zilikuwa k**a hizi hapa Motorola za antena.

Kisha 2G ikaja na uwezo wa kutuma ujumbe mfupi au arafa

Teknolojia ya 2G ambayo pia huitwa teknolojia ya SMS iliwezesha watu kutuma ujumbe mfupi.

Ungeweza pia kutuma ujumbe wenye picha, ambao uliitwa MMS (multimedia messaging service).

Na pia simu za wakati huo zilikuwa na teknolojia ya
GSM(Global System for Mobile communication),
GPRS(General packet Radio Service),
EDGE(Enhanced Data Rates For GSM Evolution) mfano ni k**a zile nokia

Kupiga simu kwa video kuliwezekana 2001
3G na kasi yake ya data ilianza kutumika wakati ambao simu za kwanza aina ya smartphone zilianza kuuzwa madukani.

Huduma yake ya mtandao haikuwa ya kasi sana lakini iliwezesha huduma ya mtandao kupatikana bila kutumia nyaya. Angalau ilikuwa hatua fulani.

Na watu waliweza kupiga simu za video
ili kufahamu kasi yake au mwendo wake wa upole ulivyokuwa, iwapo ungetaka kupakua filamu ya ucheshi ya David Brent: Life on the Road kutoka kwenye iTunes, ingekuchukua saa tano kupakua faili hiyo ya 4.26GB. Japo hadi sada kuna baadhi ya watu bado wanatumia simu za 3G sijuwi wanakwama wapi kutafu za 4G.

2010 teknolojia ya 4G ikaanza kutumika

Teknolojia hii ya kasi iliwezesha kuanza kupatikana kwa michezo mingi kwenye simu na ya kiwango cha juu.

Filamu ambayo ingekuchukua saa tano kuipakua kwa teknolojia ya 3G sasa inaweza ikakuchukua dakika 8 pekee kwa teknolojia ya 4G.
Lakini 4G haipatikani maeneo yote, hata katika mataifa yaliyoendelea.

Afrika Mashariki, utaipata katika baadhi ya maeneo ya miji mikubwa. Hapa kwenye 3G na 4G ndipo simu janja zilipoanza kutumika katika mawasiliano .

5G ndiyo mwendo kasi!

Hii ndiyo ya kasi zaidi kwa sasa.
Tume ya Mawasiliano ya Ulaya inakadiria kwamba kati ya mwaka 2020 na 2030, utaweza kupakua filamu moja ya HD ya saa moja kwa sekunde sita pekee.
Sasa twende kwenye swali letu la awali kuhusu 5G,
Nimesikiliza na kusoma maelezo ya waanzilishi na wainjilisti wa nadharia njama ya 5G ili kuelewa msingi wa taharuki wanayoijenga. Mengi wanayoongea ni uongo, uzushi, ya kuungaunga, na hayana usahihi wowote kisayansi wala kiimani. Nadharia hii imeanzishwa na wataalamu wa nadharia njama (conspirancy theorists - wawili wakiwa ni waingereza) na kudakwa na baadhi ya watumishi “wenye majina” k**a hoja ya mahubiri yao. Hivyo wamechukua hoja ya 5G na kuitumia k**a ilivyo au kwa kuitohoa kujengea hoja za chanzo na malengo ya Covid-19. Nitaje kwa kifupi baadhi ya hoja zilizoko kwenye nadharia njama ya 5G.
👉Taswira inajengwa kwamba kuna mkakati wa watu ambao wanaleta teknolojia ya 5G kwa lengo la kuitawala dunia na hasa kutufanya sisi wanadamu wote kuunganishwa kwenye mtandao mmoja ili kuweza kutaribiwa. Mkakati huu unapewa majina mengi lakini mojawapo ni mbinu ya kufanikisha kinachoitwa “New World Order (NWO)”. NWO ni nadharia njama inayodai kuna kundi la siri lenye nguvu kuliko mataifa yote litakaloitawala dunia nzima kibabe.
UDHAIFU: wanaoaminisha nadharia hii hawataji watu hao ni kina nani, wako nchi gani, na iwapo ni wa dunia hii au sayari nyingine. Ukiachilia kutajwa kwa baadhi ya viongozi wakuu wa baadhi ya nchi na dini kubwa, nadharia hii inabaki kuwa yakufirika na imekuwepo kwa muda mrefu.

👉Hoja inajengwa kwamba vifaa vya teknolojia ya 5G vina mionzi mikali yenye madhara kwenye miili yetu. Katika kupambana nayo, miili yetu inatengeneza virusi wa Corona.
UDHAIFU: Moja, hakuna ushahidi wa kisayansi wowote juu ya hili. Pili, k**a miili yetu inatengeneza virusi wa Corona tunapopigwa na mionzi ya 5G, kwa nini basi tusingekua tunaugua wote kwenye eneo lenye 5G? Tatu, kwa nini watu wanaoathirika wanapona?

👉Wakati huohuo wanadai Covid-19 inasambazwa kwa watu kupitia vipimo tunavyofanyiwa kujua iwapo tuna maambukizi. Lengo kubwa la kuingiziwa virusi hivi ni ili dunia nzima iwe na maambukizi kisha kupitishwe taratibu/sheria inayomtaka kila mtu lazima apewe chanjo ya kumkinga na Covid-19. Kupitia chanjo hiyo tutaingiziwa “chip” ndogo ya mawasiliano kwenye miili yetu (mithili ya line ya simu yako) itakayowezesha watu hao wasiojulikana kutufuatilia k**a vile mitambo ya kompyuta. Pia, mtu hataweza kupata visa kuingia nchi nyingine iwapo hajathibitisha kua na una kinga ya Covid-19.
UDHAIFU: Moja, tuna ushahidi kutoka nchi nyingi watu kuambukizwa na kueonesha dalili (wengine hadi kufariki) kabla ya kupimwa. Pili, ili uweze kupachika chip ya kielekroniki ifanye kazi na kuweza kusafirisha data na mfumo wa mwili, ni lazima ipachikwe mahili maalumu na kuunganishwa na mfumo wa mawasiliano wa mwili. Wanaohubiri nadharia hii hawatuelezi ni kwa jinsi gani chanjo tutakayopewa (ama vidonge au kimiminika) itaingiza chip mwilini na ikafanye kazi.

👉Wakristo wanatahadharishwa kwamba 5G ni mpango wa shetani na Covid-19 ni vita dhidi yao. Wengine wanakwenda mbali zaidi kudai Covid-19 imetengenezwa kwa lengo la kuangamiza waafrika ila waliotengeneza wamekosea ikawaathiri wao wenyewe.
UDHAIFU: Hoja hii ni dhaifu k**a zingine maana ni ya kufikirika.

👉Katika kujenga hoja zao, baadhi ya manabii wa njama hii wanasema virusi sio viumbe halisia bali wanatengenezwa kwa malengo mabaya.
UDHAIFU: Huu ni uongo ulioopitiliza kwani wanasayansi wa viorolojia wanatuambia kuna aina takribani 5,000 ya virusi wa asili duniani. Sifa kubwa ya virusi ni kutokua na uwezo wa kuishi wenyewe bila kuwa ndani au juu ya kiumbe kingine. Hivyo wanaweza kuishi kwa wanadamu, wanyama, ndege, samaki, mimea na hata viumbe vidogo k**a bakteria. Hata hivyo wataalamu wa bayoteknolojia wanaweza kutengeneza virusi kwa njia za kimaabara kwa malengo mbalimbali.

👉Wanajenga hoja kwamba kirusi cha Corona ni kipya na hajawahi kuwepo. Moja ya filamu ya kijapani iliyotengenezwa 2018 ina kipengele wanachotaja visuri wa Corona hivyo kipengele hiki kinatumika kuthibitisha kwamba Corona ni mkakati wa silaha za kibalojia.
UDHAIFU: Hoja hii inadhirisha jinsi upotoshaji huu usivyo na mashiko. Virusi wanaosababisha Covid-19 (yaani SARS-CoV-2), ni kafamilia kamoja tu kati ya familia karibu 60 za ukoo wa Coronavirus. Wana dada yao anaitwa SARS-CoV-1 aliyesababisha mlipuko wa SARS kule China mwaka 2002/2004 lakini ukadhibitiwa. Pia wana binamu naitwa MERS-Cov aliyelipuka kule uarabuni 2012 na kudhibitiwa pia.
👉asante wote pia unaruhusiwa kuchangia

*HISTORIA YA WAMANDA *Wamanda ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Njombe, Wilaya ya Ludewa. Vijiji ma...
01/05/2021

*HISTORIA YA WAMANDA *
Wamanda ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Njombe, Wilaya ya Ludewa.
Vijiji maarufu manda ni Igalu, Ilela, Iuilo, mbongo, masasi, ngelenge,Nsungu,kipingo,lihanguli.
Wenyeji wa Manda ni kabila la Wamanda na lugha yao ya asili ni Kimanda. Lugha hiyo hufanana sana na lugha ya Kingoni na ina maneno mengi ya Kiingereza mfano monire inayoendana na morning pia mbatata ni neno la kimanda likimaanisha viazi vitamu pia hata kibaiyolojia lina maana hiyo hiyo.
Wamanda wanapatikana katika wilaya za Ludewa, Mbinga na Nyasa kuanzia Lituhi, Ndongosi na kata za jirani upande wa wilaya ya Nyasa.
Pia wako katika Mkoa wa Ruvuma, Wilaya ya Mbinga. Katika wilaya ya Ludewa Wamanda wanapatikana katika kata za Manda, Ruhuhu, Luilo, Iwela, Mkomang'ombe, Ludewa na Masasi. Katika mkoa wa Ruvuma wanapatikana zaidi kaskazini mwa wilaya ya Mbinga.
Nimeandika hii sababu ya baadhi ya watu katika historia ya mwanzo kusema baadhi ya watu sio wangoni wakiwemo wamanda na wamatengo k**a hukusoma historia ya mwanzo "Historia na asili ya Wangoni" basi hipo hapa hapa gusa 👉 Dayocha

Wamanda kwa kiasi kikubwa wanaongea Kimanda, lugha yenye mchanganyiko wa Kingoni na Kinyasa kwa mawasiliano pia Ngoma za asili za wakazi wa Manda ni Mganda, Kihoda na Ligambusi.

Kiasili Wamanda ni Wangoni, ila, kutokana na mtengano wa kijiografia watu hao wametofautiana katika matamshi na baadhi ya misamiati. Natumaini zolanda inkomabakosi na abdul abubakar mndewa tunaelewana hapo kuhusu na . Kimanda mtu tunasema "mundu" kingoni sijuwi k**a inatofautiana na hilo neno maana ni kibantu naomba majibu sehemu ya comment wangoni wa songea maana mnatutenga wamanda.

Wamanda walio wengi ni Wakristo wa madhehebu ya kianglikana na Kikatoliki sababu ya kuwa na shule nyingi za kipindi hicho cha miaka ya nyuma. Kuna idadi ndogo sana ya Wamanda wanaoendelea kufuata dini asilia za Kiafrika. Hata hivyo, pamoja na kufuata Ukristo, Wamanda wengi bado wana mazoea ya kuendelea kuienzi mizimu na mahoka. Haya sasa najuwa kuna baadhi ya watu nimewaacha hapa kwenye mahoka ila msijali kuna watu watafafanua sehemu ya comment hapo chini nakutegemea faraja renatusi na thomas thomee na wamanda wengine.

Wakati wa ukoloni na mara baada ya uhuru Wamanda wengi walifanikiwa kusoma na kuwa na elimu nzuri wakapata nafasi nzuri serikalini. Mfano wa Wamanda waliofanikiwa kufikia nafasi za juu nchini Tanzania ni pamoja na hayati Horace Kolimba mbunge wa ludewa toka mwaka 1995 hadi 1996, Crispin Mponda, na Valieth aliyekuwa mbunge wa kwanza wa wilaya ya Ludewa kuanzi mwaka 1965 hadi 1970. Hawa ni baadhi bila kumsahau shangazi yangu mpendwa hayati magreth mlesa chale aliyekuwa diwani viti maarumu pale ludewa.

Kwa sasa kiwango cha elimu kwa Wamanda kipo chini sana kwa sababu mbalimbali, zikiwemo upungufu wa walimu katika shule za kata na hali ngumu ya uchumi inayosababisha wanafunzi wengi washindwe kumaliza japo kidato cha nne, au wakimaliza wanamaliza kwa madaraja ya chini sana, na hivyo kushindwa kuendelea.
Hili hata mimi pia nimelishuhudia maana nimesoma pale shule ya SEKONDALI MANDA kulikuwa na changamoto za walimu sababu ya mazingira shule ilipo ipo milimani na maji shida sana. Hali inayopelekea walimu wengi kutoka sehemu nyingine tofauti na kule kukimbia sababu ya usalama wa maji yanayoletwa na wanafunzi toka ziwa nyasa au mitoni kipindi cha mvua.Hila kwa sasa jitiada zinafanyika kumejengwa mabweni kule kule shule ya watoto wa k**e.

Wilaya ya Ludewa, pamoja na kujaliwa kuwa na utajiri mkubwa wa makaa ya mawe na chuma, wananchi wake bado wana hali mbaya ya kiuchumi na kwa ujumla Wamanda wanategemea misaada ya ndugu zao wanaoishi katika maeneo ya mijini kwa kiwango kikubwa.

Shughuli kuu za uchumi wa Wamanda ni pamoja na uvuvi wa samaki na ukulima wa mazao madogomadogo.kwenye uvuvi hapo kuna baadhi ya samaki maarufu sana ziwa nyasa k**a mbasa,ngumbu,mbufu,mbelele,likeru,makuku,ngorokoro,utapi,matuvi,nsenjere,masangalafu, sipa na samaki wengine ukiweza wataje hapo kwenye comment chini. Pia kwa wakazi wa dar es salaam unaweza kupata baadhi ya samaki wabichi kabisa toka ziwa nyasa na unga wa muhogo asilia kuna bro anauza ukiitaji nicheki nitaakuunganisha nae.

Chakula kikuu cha Wamanda ni ugali wa muhogo na samaki.ugali wa muhogo umegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni bututu ambayo ni miogo ya kuanika kisha unasaga kupata unga pia kuna kondowoli ni miogo inaanikwa kwa muda kisha inarainika na kuanikwa ikiwa imeponda na kusagwa kupata unga.

Reebok ya kijanja pia zinapatikana hapaMawasiliano 0654295523Free delivary kwa dar na mikoani tunatuma kwa uaminifu tu
29/04/2021

Reebok ya kijanja pia zinapatikana hapa
Mawasiliano 0654295523
Free delivary kwa dar na mikoani tunatuma kwa uaminifu tu

Address


Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Telephone

+255625531599

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dayocha posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Dayocha:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Opening Hours
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share