N-point

N-point nPOiNT is an Online content platform which delivers content across a range of smart devices.
(1)

It offers content beyond news, guaranteeing the best user experience to its customers.

Vikosi vya ulinzi na usalama visiwani Zanzibar vimeanza rasmi hii leo zoezi la kupiga kura ya mapema, ikiwa ni sehemu ya...
28/10/2025

Vikosi vya ulinzi na usalama visiwani Zanzibar vimeanza rasmi hii leo zoezi la kupiga kura ya mapema, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika kesho, Oktoba 29.

Kura ya mapema huwaruhusu maafisa wa usalama kutekeleza haki yao ya kidemokrasia kabla ya siku ya uchaguzi mkuu, ili waweze kushiriki kikamilifu katika majukumu ya ulinzi wakati wa zoezi hilo.

Kura ya mapema hufanyika katika vituo maalum vilivyotengwa huku waangalizi wa uchaguzi na mawakala wa vyama vya siasa wakifuatilia kwa karibu kuhakikisha uwazi na uhalali wa mchakato huo.

Ndege ndogo iliyokuwa imebeba watu 12 imeanguka katika eneo la kaunti ya Kwale, pwani ya Kenya, na kusababisha vifo vya ...
28/10/2025

Ndege ndogo iliyokuwa imebeba watu 12 imeanguka katika eneo la kaunti ya Kwale, pwani ya Kenya, na kusababisha vifo vya watu wote waliokuwa ndani, kwa mujibu wa taarifa kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Kenya (KCAA).

Mkurugenzi Mkuu wa KCAA, Emile Arao, amethibitisha kuwa ndege hiyo yenye nambari ya usajili 5Y-CCA ilikuwa imebeba watalii na ilikuwa ikielekea Kichwa Tembo, eneo la Maasai Mara, kutoka Diani, kabla ya kuanguka muda mfupi baada ya kupaa.

Picha na video zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha ndege hiyo ikiwa imeteketea kwa moto mkubwa, huku moshi mzito ukipanda angani. Mashuhuda waliokaribia eneo la tukio wamesema waliona ndege ikishuka kwa kasi kabla ya kulipuka mara ilipogonga ardhi.

Timu za polisi, zimamoto, na watoa huduma za dharura zilikimbilia eneo la tukio mara tu baada ya ajali hiyo kutokea, wakianza juhudi za kuzima moto na kuokoa manusura, ingawa baadaye ilibainika hakuna aliyeweza kuokolewa.

Sababu kamili ya ajali hiyo bado haijajulikana. KCAA imesema uchunguzi wa kiufundi umeanzishwa ili kubaini chanzo cha ajali hiyo, huku uchunguzi wa awali ukilenga hali ya hewa, matengenezo ya ndege, na mawasiliano ya mwisho ya rubani kabla ya ajali.

Wakazi wa eneo la Kwale wameelezea huzuni kubwa kufuatia tukio hilo, wakisema ni mojawapo ya ajali mbaya zaidi za ndege kuwahi kutokea katika eneo hilo kwa miaka ya karibuni. Serikali imetoa wito wa utulivu huku familia za waathirika zikipatiwa msaada wa kisaikolojia na usaidizi mwingine wa dharura.

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara amechaguliwa kwa muhula wa nne kwa ushindi mkubwa katika uchaguzi wa marudio, kuli...
28/10/2025

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara amechaguliwa kwa muhula wa nne kwa ushindi mkubwa katika uchaguzi wa marudio, kulingana na matokeo ya muda yaliyotangazwa Jumatatu, matokeo ambayo yalitarajiwa kwa kiasi kikubwa baada ya wapinzani wake wakuu kuonekana kutokuwa na ushawishi.

Alassane Ouattara mwenye umri wa miaka 83 alipata asilimia 89.77% ya kura zilizopigwa.

Mtangulizi wake, Laurent Gbagbo, alikataa kukiri kushindwa katika kinyang'anyiro kilichopita, na kusababisha vita vya miezi minne vilivyoua takriban watu 3,000.

Waziri wa zamani wa Biashara Jean-Louis Billon, ambaye alikubali kushindwa na Ouattara siku ya Jumapili, alipata asilimia 3.09% ya kura, huku mke wa rais wa zamani Simone Gbagbo akipata asilimia 2.42%, kulingana na matokeo yaliotolewa kwenye televisheni ya serikali na Ibrahime Coulibaly-Kuibiert, rais wa tume ya uchaguzi.

Huduma za kivuko kati ya mji wa kibiashara wa Tanzania wa Dar es Salaam na Zanzibar zitasimamishwa Oktoba 29, 2025, waka...
28/10/2025

Huduma za kivuko kati ya mji wa kibiashara wa Tanzania wa Dar es Salaam na Zanzibar zitasimamishwa Oktoba 29, 2025, wakati nchi hiyo itakapokuwa na uchaguzi mkuu.

Waendeshaji pekee, Azam Marine na Zan Fast Ferries wametangaza kuwa hakuna feri zitakazoendesha shughuli zake katika mwelekeo wowote hadi Oktoba 30.

Katika taarifa tofauti, makampuni hayo mawili yamesema uamuzi wa kusimamisha huduma hizo ulifanywa ili kuwezesha ushiriki wa wapiga kura katika uchaguzi.

Vivuko vinavyoendeshwa na wawili hao, husafirisha karibu abiria 10,000 kila siku kati ya Dar es Salaam na Zanzibar.

Mabrouk Hussein, msafiri wa kawaida alisema "Nashangaa. Kwa nini iwe hivyo? Itakuwaje ikiwa mtu anahitaji kusafiri kwa ajili ya mazishi au matibabu?

Hii si haki, inaonekana ina madhumuni ya kisiasa. Kwa nini sasa? Sio kila mtu anapenda kupiga kura.

Baadhi ya makampuni ya mabasi ya umbali mrefu pia yametangaza kuwa huduma za kwenda na kutoka Dar es Salaam zitasitishwa.

Siku ya uchaguzi, baadhi ya mabasi hayataendesha hadi miji mikubwa k**a Mwanza, Tarime, Kilimanjaro, Arusha, Tabora, Bukoba na Kigoma.

Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa) kimesema kusimamishwa kwa shughuli za usafiri kunalenga kuwawezesha wafanyakazi wa usafirishaji na abiria kupiga kura zao.

Hata hivyo, Shirika la Haki za Abiria limekosoa uamuzi huo na kudai kuwa shirika la wamiliki limeshindwa kuzingatia wajibu wa kijamii na familia.

Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masijala Ndogo ya Dar es Salaam imeahirisha Kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa (CHADEMA...
24/10/2025

Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masijala Ndogo ya Dar es Salaam imeahirisha Kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa (CHADEMA), Tundu Lissu hadi Novemba 3, 2025, baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuendelea kutokana na kukosekana kwa Shahidi.

Wakili wa Serikali Mkuu Renatus Mkude aliieleza Mahak**a kuwa upande wa Jamhuri ulikuwa tayari umeshatoa ushahidi kupitia mashahidi watatu, lakini shahidi wa tatu, Mkaguzi wa Polisi na Mtaalamu wa Uchunguzi wa Kielektroniki Samwel Kaaya, alishindwa kuwasilisha vielelezo vyake vya flash disk na memory card baada ya Mahak**a kukataa kuvipokea.

“Kwa sasa hatuna shahidi mwingine aliye tayari kutoa ushahidi kwa kuwa waliopangwa wanatoka nje ya Dar es Salaam na wanahitaji maandalizi zaidi. Kwa mujibu wa kifungu cha 302 cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA), tunaomba ahirisho,” alisema Mkude.

Kwa mujibu wa Wakili huyo wa Serikali, tarehe 3 Novemba 2025 ilikuwa tayari imepangwa katika ratiba ya kesi hiyo, hivyo aliomba shauri hilo liendelee siku hiyo.

Hata hivyo, Lissu alipinga ombi hilo la kuahirishwa akidai kuwa sababu zilizotolewa na upande wa Jamhuri hazina msingi wa kisheria.

Kutokana na hatua hiyo, Jaji Ndunguru, alisema Mahak**a imezingatia hoja za pande zote mbili na kubaini kuwa ombi la kuahirisha lina msingi wa kisheria kwa kuwa upande wa mashtaka haujawahi kukosa shahidi tangu shauri lianze, hivyo kesi inaahirishwa hadi Novemba 3, 2025.

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara anawania muhula wa nne katika uchaguzi wa siku ya Jumamosi, akiahidi kuendeleza uk...
24/10/2025

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara anawania muhula wa nne katika uchaguzi wa siku ya Jumamosi, akiahidi kuendeleza ukuaji thabiti huku wakosoaji wakilaani kile wanachoeleza k**a jitihada za serikali yake za kukandamiza upinzani.

Uchaguzi katika nchi hiyo mzalishaji mkubwa wa kakao duniani unawakutanisha Ouattara, 83, dhidi ya mawaziri wawili wa zamani wa serikali pamoja na mke wa zamani na msemaji wa zamani wa mtangulizi wake, Laurent Gbagbo.

Ouattara ndiye mgombea pekee anayeungwa mkono na chama chenye nguvu cha kisiasa, na hivyo kumfanya kuwa kipenzi wengi.

Wapinzani wengine wawili mashuhuri, Gbagbo na Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Credit Suisse Tidjane Thiam, walizuiwa kushiriki.

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kusitisha mara moja mazungumzo yote ya kibiashara na Canada, akitaja tangazo la...
24/10/2025

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kusitisha mara moja mazungumzo yote ya kibiashara na Canada, akitaja tangazo la televisheni lililotumia sauti ya Rais wa zamani Ronald Reagan akipinga sera za ushuru k**a kichocheo cha uamuzi huo.

Kupitia chapisho kwenye mtandao wake wa Truth Social, Trump alisema tangazo hilo, lililodhaminiwa na serikali ya jimbo la Ontario, limeonyesha “mwenendo wa kukera” unaolenga kuingilia masuala ya ndani ya Marekani.

“Kwa kuzingatia tabia yao isiyokubalika, MAZUNGUMZO YOTE YA KIBIASHARA NA KANADA YAMEKOMA KUANZIA SASA,” aliandika Trump Alhamisi usiku.

Rais huyo ameweka kodi ya asilimia 35 kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka Kanada, ingawa ameidhinisha msamaha kwa bidhaa fulani zilizo chini ya Makubaliano ya Biashara Huria ya Amerika Kaskazini (USMCA) mkataba wa kibiashara kati ya Marekani, Kanada na Mexico alioufanyia marekebisho katika muhula wake wa kwanza.

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wakubaliana kuisaidia Ukraine kifedha katika kipindi kingine cha miaka miwili.Lakini hata hiv...
24/10/2025

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wakubaliana kuisaidia Ukraine kifedha katika kipindi kingine cha miaka miwili.

Lakini hata hivyo wameshindwa kutoa mamilioni ya fedha za Urusi zilizozuiwa ili kutoa ufadhili wa ulinzi wa nchi hiyo

Katika mkutano wao wa jana viongozi hao waliahirisha uamuzi wao wa kutumia kiasi ya Euro bilioni 140 za mali ya Urusi zinazoshikiliwa nchini Ubelgiji hadi hapo Desemba.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameeleza mkutano huo wa Ubelgiji kwamba hatua hiyo italeta matokeo chanya. '' Ningependa kuwashukuru viongozi wote wa Ulaya kwa mosimamo yao thabiti kupitia vikwazo waliyoweka, alisema.

Mkutano huo wa Brussels ulifanyika jana wakati kukitarajiwa kufanyika mkutano mwingine huko London ambako Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer anatarajiwa kuwahimiza viongozi wa Ulaya kuongeza kupeleka vifaa vya kijeshi nchini Ukraine.

Mama wa taifa wa kwanza wa Ghana Nana Konadu Agyeman-Rawlings ameripotiwa kufariki dunia akiwa na umri wa miaka 76.Taaar...
23/10/2025

Mama wa taifa wa kwanza wa Ghana Nana Konadu Agyeman-Rawlings ameripotiwa kufariki dunia akiwa na umri wa miaka 76.

Taaarifa zinasema amefariki mapema leo Alhamisi, 23 Oktoba, katika Hospitali ya Ridge huko Accra.

Shirika la serikali la Utangazaji la Ghana limeshirikisha ujumbe kwenye Jukwaa la X, kutangaza kufo chake.

Nana Konadu Agyeman-Rawlings alikuwa mama wa taifa wa kwanza kutoka Juni 4, 1979, hadi Septemba 24, 1979, chini ya Baraza la Mapinduzi la Wanajeshi (AFRC), na tena kutoka Desemba 31, 1981, hadi Januari 6, 1993, chini ya Baraza la Ulinzi la Kitaifa (PNDC).

Aliendelea kuhudumu k**a mwanamke wa kwanza kutoka Januari 7, 1993, hadi Januari 6, 2001, na kutamatisha muda mihula miwili chini mfumo mpya wa demokrasia wa kaunti.

Ujumbe wa salamu za rambirambi unaendelea kutumwa kwa haraka katika mitandao ya kijamii kufuatia taarifa za kifo chake.

23/10/2025

Mahak**a Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam, imeikataa ripoti ya uchunguzi wa uhalisia wa picha mjongeo (video clip) ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, anayekabiliwa na kesi ya uhaini, yenye maudhui yanayodaiwa kuwa ya uhaini.

Upande wa mashtaka katika kesi hiyo jana Jumatano, Oktoba 22, 2025 kupitia shahidi wake wa tatu iliiomba mahak**a iipokee ripoti hiyo kuwa kielelezo cha ushahidi wa upande wa mashtaka.

Hata hivyo, Lissu aliweka pingamizi dhidi ya ripoti hiyo isipokewe akidai shahidi huyo hana mamlaka ya kisheria kuiwasilisha mahak**ani wala kuiandaa ripoti hiyo kwa kuwa si mtaalamu wa uhalifu wa kimtandao.

Licha ya upande wa mashtaka kupinga hoja zake kuwa hazina mashiko kisheria, lakini Mahak**a katika uamuzi wake leo Alhamisi Oktoba 23, 2025 imekubaliana na pingamizi lake baada ya kuridhia na hoja zake, hivyo ikaikataa ripoti hiyo ikieleza kuwa shahidi huyo hana mamlaka ya kisheria kuwasilisha ripoti hiyo kwa kuwa si mtaalamu wa masuala ya uhalifu mtandao.

23/10/2025

Tume ya Kitaifa ya Uwiani na Maridhiano nchini Kenyac(NCIC) imemtaka Gavana wa Nyeri, Mutahi Kahiga, kutoa maelezo rasmi kuhusu kauli zake zilizozua utata kuhusu kifo cha aliyekuwa kinara wa ODM Raila Odinga.

Kauli hizo zimezua hasira kubwa nchini Kenya, hasa baada ya Kahiga kusema kuwa kifo cha Odinga ni “mpango wa Mungu” ili kanda ya Mlima Kenya ipate faida kutoka kwa rasilimali za serikali ambazo zilikuwa zikitumika sehemu nyingine.

Kahiga alidai kuwa makubaliano ya kisiasa kati ya Rais William Ruto na marehemu Odinga yalibadilisha vipaumbele vya maendeleo ya serikali kuelekezwa zaidi katika kanda ya Nyanza, hali inayodaiwa kumfanya mkoa wa Mlima Kenya kupoteza fursa za kimaendeleo.

Tume ya NCIC imesema kuwa kauli hizo ziliharibu kwa kiasi kikubwa juhudi zilizofanywa kudumisha amani na mshik**ano wa kitaifa, na kwamba Gavana Kahiga anapaswa kuwajibishwa kwa kuwa ni mtu anayeongoza katika nafasi ya umma.

Katika taarifa yao ya Jumatano, Tume ilionya kuwa kauli k**a hizo si tu zinahuzunisha kumbukumbu za shujaa wa taifa, bali pia zinaweza kuchochea migogoro ya kikabila na mivutano ya kijamii wakati taifa linapolia kiongozi wake wa zamani.

23/10/2025

Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza rasmi vikwazo vipya dhidi ya baadhi ya makampuni makubwa ya mafuta kutoka Urusi, hatua inayolenga kuongeza shinikizo kwa serikali ya Rais Vladimir Putin kufuatia kuendelea kwa mvutano wa kisiasa.

Vikwazo hivyo vinahusisha kufungia mali za makampuni kadhaa na kuzuia biashara ya mafuta kati ya Urusi na washirika wake wa kimataifa.

Hatua hiyo imesabisha kupanda kwa bei ya mafuta duniani, huku wachambuzi wakionya kuwa inaweza kuongeza gharama za nishati katika nchi nyingi.

Serikali ya Urusi imelaani hatua hiyo, ikidai kuwa Marekani inajaribu kutumia nguvu za kiuchumi k**a silaha ya kisiasa.

Hata hivyo, Ikulu ya Marekani imesisitiza kuwa vikwazo hivyo ni sehemu ya juhudi za kulinda maslahi ya kimataifa na kudhibiti ufadhili wa kijeshi wa Urusi.

Address

Kimweri Street
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when N-point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to N-point:

Share