N-point

N-point nPOiNT is an Online content platform which delivers content across a range of smart devices.
(1)

It offers content beyond news, guaranteeing the best user experience to its customers.

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu imeahirishwa hadi Jul...
15/07/2025

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu imeahirishwa hadi Julai 30, 2025.

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kesi hiyo baada ya Jamhuri kuomba ahirisho ili kusubiri maamuzi ya Mahak**a Kuu ya kuwapa ulinzi mashahidi.

Unaweza Kutufuatilia Kupitia:
TWITTER: ://twitter.com/npointtz
INSTAGRAM: ://instagram.com/npointtz
FACEBOOK: ://www.facebook.com/n-point
Fuatilia matangazo ya moja kwa moja kupitia Akaunti yetu ya Youtube na mitandao mingine ya kijamii.

Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kusitisha mabilioni ya dola ya ruzuku zinazotolewa kwa kampuni za Tesla na Space...
03/07/2025

Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kusitisha mabilioni ya dola ya ruzuku zinazotolewa kwa kampuni za Tesla na SpaceX zinazomilikiwa na bilionea Elon Musk kufuatia mvutano unaoendelea kati yao ambapo hii ni baada ya Musk kukosoa vikali mswada mpya wa kodi na matumizi ya Serikali unaolenga kufuta ruzuku za ununuzi wa magari ya umeme hatua inayotajwa kuathiri moja kwa moja kampuni ya Tesla.

Trump amenukuliwa akisema kuwa bila ruzuku hizo, Musk atahitaji kufunga biashara na kurudi nyumbani Afrika Kusini, kauli iliyozua mjadala mpana nchini humo na kwa upande wake, Musk hakusita kujibu kwa maneno makali akisema, “Zuia kila kitu sasa.”

Aidha mabishano haya yameibuka wakati ambapo Seneti ya Marekani imepitisha mswada huo kwa kura chache tu huku soko la hisa la Tesla likiripotiwa kushuka kwa asilimia kubwa ambayo ni ishara ya wasiwasi kwa wawekezaji kuhusu mustakabali wa kampuni hiyo.


Unaweza Kutufuatilia Kupitia:
TWITTER: ://twitter.com/npointtz
INSTAGRAM: ://instagram.com/npointtz
FACEBOOK: ://www.facebook.com/n-point
Fuatilia matangazo ya moja kwa moja kupitia Akaunti yetu ya Youtube na mitandao mingine ya kijamii.

Mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Ureno, Diogo Jota, ameripotiwa kufariki dunia katika ajali mbaya ya gari i...
03/07/2025

Mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Ureno, Diogo Jota, ameripotiwa kufariki dunia katika ajali mbaya ya gari iliyotokea nchini Hispania, karibu na eneo la Zamora, kaskazini magharibi mwa nchi hiyo na kwa mujibu wa shirika la habari la EFE la Hispania, ajali hiyo ilitokea siku ya Jumanne na imethibitishwa na vyanzo kadhaa vya karibu na familia.

Jota, mwenye umri wa miaka 28, alikuwa mmoja wa wachezaji muhimu wa Liverpool tangu alipojiunga na klabu hiyo mwaka 2020 akitokea Wolverhampton Wanderers kwa ada ya zaidi ya pauni milioni 40 vile vile alijizolea umaarufu mkubwa kutokana na kasi, uwezo wa kufunga na nidhamu uwanjani na kabla ya tukio hili la kusikitisha Jota alikuwa ameoa wiki chache zilizopita na alikuwa na familia ndogo yenye furaha pamoja na watoto wake watatu.

Habari za kifo chake zimepokewa kwa mshtuko mkubwa na mashabiki wa soka duniani kote huku wengi wakituma salamu za rambirambi kupitia mitandao ya kijamii na klabu ya Liverpool, mashabiki wake pamoja na jamii ya soka kwa ujumla wanakumbuka mchango mkubwa wa Jota katika mchezo huo na kuomboleza kuondokewa na mchezaji aliyeacha alama isiyofutika.

Unaweza Kutufuatilia Kupitia:
TWITTER: ://twitter.com/npointtz
INSTAGRAM: ://instagram.com/npointtz
FACEBOOK: ://www.facebook.com/n-point
Fuatilia matangazo ya moja kwa moja kupitia Akaunti yetu ya Youtube na mitandao mingine ya kijamii.

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imeahirisha kusikiliza mashtaka mawili yanayomkabili Mwenyekiti wa ...
02/07/2025

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imeahirisha kusikiliza mashtaka mawili yanayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu.

Katika shtaka la kwanza la uhaini, Mahak**a imeahirisha kesi hiyo baada ya kubainika kuwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) haijatoa uamuzi wa kuendelea au kutokuendelea na shauri hilo. Hakimu ameipangia kesi hiyo kusikilizwa tena Julai 15. Je, serikali itaendelea na kesi hiyo?

Unaweza Kutufuatilia Kupitia:
TWITTER: ://twitter.com/npointtz
INSTAGRAM: ://instagram.com/npointtz
FACEBOOK: ://www.facebook.com/n-point
Fuatilia matangazo ya moja kwa moja kupitia Akaunti yetu ya Youtube na mitandao mingine ya kijamii.

12/05/2025
11/05/2025
Mkutano wa Injili Ulioandaliwa na Kanisa la wa Adventista Wa Sabato Tanzania , Umefunguliwa leo rasmi Katika Kanisa la  ...
10/05/2025

Mkutano wa Injili Ulioandaliwa na Kanisa la wa Adventista Wa Sabato Tanzania , Umefunguliwa leo rasmi Katika Kanisa la . Mkutano Huu Utakuwa MBASHARA kupitia Channel Yetu ya YouTube . Karibu uweze kubarikiwa na mafundisho mbalimbali Kutoka kwa Watumishi wa MUNGU. —- HUBIRI KUU || MASOMO YA FAMILIA || MASOMO YA AFYA || IJUE SHERIA!!!

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anauita "wakati wa kihistoria" kwa Kanisa Katoliki, na anapanua "ujumbe wa udugu". "Nao...
09/05/2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anauita "wakati wa kihistoria" kwa Kanisa Katoliki, na anapanua "ujumbe wa udugu". "Naomba papa huyu mpya awe wa amani na matumaini," anasema.

Rais wa Poland Andrzej Duda ametoa "pongezi zake za dhati", akiandika kwenye mitandao ya kijamii: "Huu ni wakati wa kusisimua sana kwa jumuiya ya Kanisa Katoliki na kwa ulimwengu mzima. Nchini Poland, tunaipitia kwa hisia na matumaini makubwa."

Rais wa Tume ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen pia ametoa pongezi zake. Anasema: "Tunatamani kuwa papa aongozwe na hekima na nguvu, anapoongoza jumuiya ya Kikatoliki na kuutia moyo ulimwengu kupitia kujitolea kwake kwa amani na mazungumzo."

Waziri mkuu wa Canada Mark Carney anasema katika chapisho kwenye X: "Ninatoa sala zangu na kumtakia heri Baba Mtakatifu Leo XIV katika kuchaguliwa kwake." "Wakati wa changamoto za kimataifa, papa aendeleze misheni ya mshik**ano, huruma na utu kwa wote," Carney alisema.

 : Moshi mweupe umeonekana ukifuka kutoka kwenye bomba la moshi katika Kanisa la Sistine Chapel, ni wazi mchakato wa upi...
08/05/2025

: Moshi mweupe umeonekana ukifuka kutoka kwenye bomba la moshi katika Kanisa la Sistine Chapel, ni wazi mchakato wa upigaji kura umekamilika na makadinali wamemchagua mrithi wa Papa Francis.

Bado hatujui ni nani amechaguliwa, lakini itaonekana wazi watakapotokea kwenye roshani ya Kanisa la Sistine, ndani ya k**a saa moja.

Beki wa kulia wa Uingereza, Trent Alexander-Arnold, amethibitisha kuwa ataondoka na kuikacha mabingwa wa Ligi Kuu ya Uin...
05/05/2025

Beki wa kulia wa Uingereza, Trent Alexander-Arnold, amethibitisha kuwa ataondoka na kuikacha mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza, Liverpool, mwishoni mwa msimu.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye amekuwa klabuni hapo tangu akiwa na umri wa miaka sita, mkataba wake unamalizika Juni 30 na anatarajiwa kujiunga na Real Madrid.

"Baada ya miaka 20 katika Klabu ya Soka ya Liverpool, sasa ni wakati wangu wa kuthibitisha kuwa nitaondoka mwishoni mwa msimu," Alexander-Arnold alitangaza kwenye mitandao ya kijamii.

"Huu ni uamuzi mgumu zaidi ambao nimewahi kufanya maishani mwangu."

Alexander-Arnold ni mmoja wa wachezaji watatu mashuhuri ambao mikataba yao Anfield inamalizika msimu huu wa joto.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when N-point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to N-point:

Share