The Chanzo

The Chanzo Uchambuzi, maoni, uchunguzi na habari zenye kugusa jamii
(1)

Mtandao Warudishwa, Watanzania Waomboleza Vifo vya Wapendwa WaoHuduma ya mtandao imerudishwa jioni ya Novemba 03, 2025, ...
04/11/2025

Mtandao Warudishwa, Watanzania Waomboleza Vifo vya Wapendwa Wao

Huduma ya mtandao imerudishwa jioni ya Novemba 03, 2025, baada ya huduma ya huduma hiyo kusitishwa na serikali toka Oktoba 29, 2025, baada ya kuibuka kwa maandamano yaliyosambaa katika miji na majiji ya Tanzania.

Huduma ya mtandao imerudishwa ikiwa ni masaa machache toka uapisho wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na makamu wake, Emmanuel Nchimbi.

Sehemu kubwa ya jumbe ambazo zinaendelea kusambazwa mtandaoni ni zile za watu kuomboleza juu ya wapendwa wao waliofariki kwa kupigwa risasi na watumishi wa vyombo vya ulinzi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania.

Shughuli za mazishi zimeshafanyika katika baadhi ya maeneo, hasa kwa kuzingatia mila na taratibu za kidini. Huku wengine wakiendelea kupanga misiba, hasa kutokana na ugumu uliotokea wa kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine.

Picha na video mbalimbali zinazo onesha majeraha ya watu waliofariki kwa kupigwa risasi pia zimeendelea kuwekwa mitandaoni. Sehemu kubwa ya picha hizo za kuogofya zikionesha vijana wa takribani miaka 17 mpaka 25.

Bado hakuna idadi rasmi ya watu waliofariki, baadhi ya mashirika ya kimataifa tayari wametoa angalizo kuwa idadi ya waliofariki inaweza kuwa kubwa.

Katibu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa tamko la kusisitiza juu ya umuhimu wa ustahimilivu.

"Nimesikitishwa na hali inayoendelea Tanzania, ikihusisha ripoti za vifo na watu kuumizwa katika maandamano," ameeleza Guterres. "Natoa wito kwa wote kuwa na ustahimilivu, kukataa vurugu na kushiriki katika mazungumzo jumuishi na yenye kujenga ili kuzuia kuendelea kwa hali ya mvutano."

Serikali kupitia Waziri wa Mambo ya Nje, Mahmoud Thabit Kombo imeeleza kuwa nguvu kiasi ilitumika kuwadhibiti waaandamanaji.

Msigwa: Watumishi wa Umma Wafanyie Kazi Nyumbani Kasoro Wenye Majukumu ya Kazi Yanayowataka KuwepoMsemaji Mkuu wa Serika...
30/10/2025

Msigwa: Watumishi wa Umma Wafanyie Kazi Nyumbani Kasoro Wenye Majukumu ya Kazi Yanayowataka Kuwepo

Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Gerson Msigwa ametoa taarifa kuwa watumishi wote wa umma nchini Tanzania kufanyia kazi nyumbani siku ya Oktoba 30, 2025 isipokuwa wale ambao majukumu yao yanawahitaji kuwepo eneo la kazi.

Katika taarifa ya Msigwa ambayo imetoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi na kuchapwa kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram amesema uamuzi huo ni kufuatia angalizo la kiusalama lililotolewa na Jeshi la Polisi kwa wakazi wa Dar es Salaam.

“Aidha, waajiri katika Sekta Binafsi wanashauriwa kuzingatia tahadhari hiyo na kuwaruhusu watumishi wao nao kufanya kazi nyumbani,” imeeleza taarifa hiyo.

Imeeleza pia wananchi wasio na ulazima wa kutoka kwenye makazi yao wanashauriwa kufanyia shughuli zao nyumbani.

Oktoba 29, 2025 jioni mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IJP Camillus Wambura alitoa amri kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam kutotoka nje kuanzia saa 12 jioni, k**a angalizo kufuatia vurugu kuripotiwa kwenye baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam siku ya zoezi la kupiga kura.

Ripoti mbalimbali zinaonesha kuwa yamefanyika maandamano maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mbeya, Arusha, Songwe na Shinyanga.

29/10/2025

Namna kiwanda hiki cha taka rejeshi Kigoma kilivyotoa fursa kwa vijana.

29/10/2025

Mwinyi, Othman wapiga kura Zanzibar.

29/10/2025

Wagombea wa Urais kutoka vyama mbalimbali wakiwemo CCM, CUF na CCK wakishiriki katika zoezi la kupiga kura.

29/10/2025

Waandamanaji wamejitokeza katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam. Majira ya saa tano asubuhi waandamanaji hao walikuwa maeneo ya Tip Top Manzese, ambapo Polisi nao walifika na kujaribu kufanya jitihada za kuwatuliza.

28/10/2025

Kesi ya Vigogo wa CHADEMA Yaendelea Mahak**a Kuu: Uamuzi Kutolewa Novemba 4, 2025

Dar es Salaam. Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imeendelea leo Jumanne, Oktoba 28, 2025, kusikiliza kesi ya jinai namba 48250 ya mwaka 2025, iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Said Issa Mohamed, pamoja na wenzake Ahmed Rashid Khamis na Maulidah Anna Komu dhidi ya vigogo wa CHADEMA wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Bara John Wegesa Heche.

Kesi hii iliyofunguliwa kwa hati ya dharura inasikilizwa mbele ya Jaji Awamu Mbagwa, ambapo leo mahak**a imeendelea na usikilizwaji wa mapingamizi yaliyowasilishwa na wajibu maombi, pamoja na kuanza kusikiliza kesi ya msingi.

Wajibu maombi, akiwemo John Mnyika, Brenda Rupia, Rose Mayemba, Gervas Lyenda, Twaha Mwaipaya, Hilda Newton, Katibu Mkuu, na Bodi ya Wadhamini wa CHADEMA, wanadaiwa kukiuka amri ya Mahak**a Kuu iliyotolewa Juni 10, 2025, iliyowazuia kufanya shughuli za kisiasa na kiutendaji kwa mwavuli wa chama hicho.

28/10/2025

Familia ya Eliza yenye watoto wenye ugonjwa wa Selimundu yawashukuru Watanzania kwa msaa.

Unaweza kuwasiliana nao kupitia namba 0684601059.

28/10/2025

CCM wahitimisha kampeni Mwanza.

28/10/2025

ACT Wazalendo walalamikia mapungufu kura ya mapema Zanzibar, Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yawatoa hofu.

28/10/2025

Wasimamizi wa uchaguzi Mtwara wasisitizwa kuwapa kipaumbele watu wenye mahitaji maalumu.

28/10/2025

Kura ya mapema yafanyika Zanzibar.

Address

Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Chanzo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to The Chanzo:

Share