The Chanzo

The Chanzo Uchambuzi, maoni, uchunguzi na habari zenye kugusa jamii
(1)

Mahak**a Kuu ya Zanzibar imewapeleka rumande watuhumiwa sita wanaokabiliwa na tuhuma ya mauaji ya Sheikh Jabir Haidar Ja...
09/07/2025

Mahak**a Kuu ya Zanzibar imewapeleka rumande watuhumiwa sita wanaokabiliwa na tuhuma ya mauaji ya Sheikh Jabir Haidar Jabir, tukio lililozua gumzo kubwa katika jamii ya Zanzibar mwishoni mwa mwezi Mei.

Watuhumiwa hao ni Salum Manja Ame (23), Idrisa Kijazi Kasim (41), Ali Mohamed Ali (30), Ali Machano Haji (30), Zahor Khamis Ali (54), na Mohamed Hassan Jongo (38). Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Mahak**a ya Zanzibar, wote ni wakazi wa Zanzibar na wanashtakiwa kwa kosa la kumuua kwa makusudi Sheikh Jabir Haidar Jabir, kinyume na kifungu namba 179 na 180 vya Sheria ya Adhabu namba 6 ya mwaka 2018.

Wakili kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, ndugu Anuwar Saaduni, aliiambia Mahak**a kuwa watuhumiwa hao walishirikiana kwa makusudi katika kupanga na kutekeleza mauaji hayo. Tuhuma zinaeleza kuwa tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 27 Mei 2025 majira ya saa tatu usiku katika eneo la kisiwani, ambapo Sheikh Jabir aliuawa kwa kutumia silaha ya moto.

Katika kikao cha kusikilizwa kwa shtaka hilo, watuhumiwa wote walikana mash*taka dhidi yao. Hata hivyo, kutokana na uzito wa kesi hiyo, Mahak**a Kuu mbele ya Jaji Khadija Shamte Mzee imeahirisha kesi hiyo hadi tarehe 16 Julai 2025, ambapo itatajwa upya kwa hatua zinazofuata za kisheria.

09/07/2025

Biteko: Kutofautiana kimaoni si uhalifu

"Ni vyema tuendelee kuhimiza maelewano uvumilivu wa kisiasa na utamaduni wa kuheshimu tofauti za maoni. Kutofautiana kimaoni si uhalifu, mtu kuwaza hivi kinyume na unavyowaza wewe si dhambi," ameeleza Naibu Waziri Mkuu, Doto Biteko.

Na kuongeza: "Dhambi ni kuamini kuwa unachoamini wewe ndiyo sahihi tu na wanachoamini wenzio siyo sahihi. Na kwamba anayeamini kinyume na wewe basi huyo zawadi yake ni matusi na kudhalilishwa hilo si sawa tuheshimiane tu. Anayeamini kuwa Yanga ni timu bora muache amini hivyo, na yule anayeamini Simba ni timu bora muache aamini hivyo. Muhimu wote tunaamini katika soka."

Biteko Ameyasema hayo leo Julai 09, 2025, alipokuwa akifungua mkutano wa serikali wa wadau wa habari kujadili mchango wa sekta ya habari katika kufanikisha uchaguzi mkuu 2025.

08/07/2025

Chalamila Kwa Viongozi wa Dini: 'Serikali Haipokei Vitisho'

"Serikali haipokei vitisho, serikali inapokea ushauri. Vitisho sio sehemu yake, sasa ukibadilisha ushauri kuwa vitisho serikali inaweza kutisha zaidi halafu ikapitiliza," anaeleza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila.

"Lakini ukipeleka k**a ushauri, inaupokea na inautekeleza vizuri sana. Kwa hiyo ninyi viongozi wetu wa dini, tuendelee kutambua kwamba lugha ni hisia, lugha ni utamaduni, lugha ni mshik**ano."

08/07/2025

Mwigulu atoa hoja mabango yawekwe kwenye miradi: ‘Kwa hisani ya walipa kodi Tanzania’

"Na niliongea na CG [Kamishna TRA] nikamwambia nenda kwenye miradi yote ambayo imejengwa kwa kodi za Watanzania piga bango hapo kwamba jengo hili, daraja hili limejengwa kwa kodi za Watanzania," anaeleza Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba

"Kwa sababu hii ni heshima kwa Watanzania wote, ni heshima kwa uhuru wa Tanzania. Kuliko tunakuwa na jengo tunakuwa na mradi mkubwa k**a wa Busisi umejengwa kwa kodi za Watanzania hauna tangazo hilo. Halafu unakuta choo matundu manne ya choo tunaambiwa imejengwa kwa msaada wa hisani ya watu wa Marekani."

08/07/2025

Jumuiya ya Maridhiano yasema wao siyo wapambe: ‘Tunaungana na Serikali kipindi cha uchaguzi’

08/07/2025

Nyerere 1985: Tumekubaliana tunataka serikali ya hiari

08/07/2025

Mwalimu Nyerere alivyokutana na Stonehouse mwaka 1960

08/07/2025

China yatoa msaada wa vifaa vya matibabu vya zaidi ya shilingi milioni 200, kuwezesha kutoa huduma Zanzibar

05/07/2025

Shekhe aibua sakata la kesi ya Tundu Lissu wakati wa uzinduzi wa jengo jipya la kanisa la Mwamposa.

"Mtu anasema tukinukishe, haya kukishanuka hapa wewe unaenda wapi?" anaeleza Shekhe Mohammed Mawinda

04/07/2025

Zitto: Thamani ya uhai imepotea Tanzania, taifa halithamini utu

"Katika nchi yetu thamani ya uhai wa binadamu inapotea, tumekuwa taifa ambalo halithamini utu, halithamini uhai. Kila mtu sasa hivi anaona ana uwezo wa kutesa mtu, wa kutoa uhai wa mtu na hakuna kitakachomtokea, taifa gani hili tunajenga taifa? Taifa la namna gani hili tunalolijenga?"

Azimio TFF Lilitakiwa Lifute Uchaguzi 2025Na Angetile OsiahNi kawaida ya jumuiya, au taasisi yeyote, kuweka kwenye katib...
04/07/2025

Azimio TFF Lilitakiwa Lifute Uchaguzi 2025

Na Angetile Osiah

Ni kawaida ya jumuiya, au taasisi yeyote, kuweka kwenye katiba yake vipindi vya uchaguzi kwa ajili ya kupata viongozi, ama walewale waliopo madarakani waendelee, au kuingiza sura mpya.

Hii imewekwa ili kuwe na ushindani, au kusiwepo na kubwweteka, kwa viongozi wanaopewa dhamana ya kuongoza kwa kuwa pale wanapobweteka tu na mambo kuenda mrama, wapigakura hushtuka na kusubiri kipindi cha uchaguzi ili watumie haki yao kufanya mabadiliko.

Hata kwenye nchi za chama kimoja, bado uchaguzi ni kitu muhimu ili jamii iweze kusonga mbele. Hata kwenye nchi zenye utawala wa kifalme, bado kuna taratibu zinazowekwa kwa ajili ya wananchi kuchagua Serikali inayojihusisha na maisha yao ya kila siku.

Ingia https://thechanzo.com/2025/07/04/azimio-tff-lilitakiwa-lifute-uchaguzi-2025/

Address

Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Chanzo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to The Chanzo:

Share