The Chanzo

The Chanzo Uchambuzi, maoni, uchunguzi na habari zenye kugusa jamii
(1)

07/10/2025

Mbaroni kwa kijiunganishia umeme kinyemela, kutumia umeme bila kuulipia.

Tukiruhusu Ukatili Utawale Tanzania, Tutawezaje Kuwa na Nchi ya Amani?Niliwahi kufundisha shule fulani ambapo, mara moja...
07/10/2025

Tukiruhusu Ukatili Utawale Tanzania, Tutawezaje Kuwa na Nchi ya Amani?

Niliwahi kufundisha shule fulani ambapo, mara mojamoja, mwalimu mkuu wake aliamua kwamba, kutokana na utundu au uzembe fulani, wanafunzi wapewe extra drill. Ndiyo.

Sijawahi kuwepo jeshini, lakini walimu wenzangu waliniambia kwamba ni hiyohiyo waliyopitia wengine wakiwa JKT. Lakini baadaye walikiri kwamba baadhi ya adhabu walizotoa zilikuwa zimepigwa marufuku jeshini, hasa kwa wanawake, na hii ilikuwa shule ya wasichana.

Na extra drill sio mchezo. Sikujua. Sasa kwa kuwa walimu wote walitakiwa kushiriki kutoa hiyo extra drill, ikabidi niwemo na mimi. Wanafunzi walikimbizwa, wakaviringishwa kwenye mchanga, na hata kulazimika kulala kwenye mifereji yenye maji baridi sana, wakarushwa hata kichura.

Hadi wanafunzi karibu wote walikuwa wanalia, wengine wanatoa udenda k**a vile wanataka kufa, wanashindwa kusimama, lakini wanapigwa viboko hadi wasimame na kuanguka tena.

Wengine walizimia, wengine walipelekwa zahanati baadaye lakini adhabu iliendelea … iliendelea … iliendelea hadi baada ya masaa, mwalimu mkuu, ambaye ninao uhakika alikuwa anaangalia akiwa nyumbani kwake maana nyumba ilikuwa ndani ya eneo la shule, hadi akatoka.

Dah maigizo!

Alitukimbilia sisi walimu akihema maana hakuwa mwembamba, akiasa: “Jamani walimu, inatosha, inatosha, jamani, maskini wanafunzi inatosha.”

Ni yeye aliyeagiza iwepo extra drill. Ni yeye aliyeangalia ikifanyika. Na sasa anajidai mwenye huruma sana na kuwasihi walimu waache. “Jamani imezidi,” alitwambia. “Sikujua, basi, basi, basi walimu naomba mwache.” Halafu anawageukia wanafunzi, akiwaambia: “Poleni, poleni, nendeni mkapumzike.”

Yaani ionekane walimu ndio washenzi, yeye mtakatifu. Sijui wanafunzi wangapi walitambua hilo, lakini mimi binafsi nilisikia kichefuchefu mbele ya unafiki wa aina hii.

https://thechanzo.com/2025/10/06/tukiruhusu-ukatili-utawale-tanzania-tutawezaje-kuwa-na-nchi-ya-amani/

07/10/2025

Mgombea urais wa chama cha MAKINI aahidi kugawa bodaboda na ardhi bure kwa vijana.

07/10/2025

Samia: Tunaomba kazi-tulinde, tuheshimishe utu wa Mtanzania

07/10/2025

Manispaa ya Mtwara Mikindani yajipanga kutokomeza 'zero' kidato cha nne.

Polisi: Tunamtafuta Augustino Polepole Atoe Maelezo na Kuthibitisha Tuhuma AlizotoaDodoma. Jeshi la Polisi Tanzania lime...
07/10/2025

Polisi: Tunamtafuta Augustino Polepole Atoe Maelezo na Kuthibitisha Tuhuma Alizotoa

Dodoma. Jeshi la Polisi Tanzania limesema pamoja na kuendelea na uchunguzi wa tuhuma za kutekwa kwa Humphrey Polepole zilizotolewa Oktoba 6, 2025 na aliyejitambulisha kuwa ndugu yake aitwaye Augustino Polepole, Jeshi hilo limesema linamtafuta ndugu huyo wa Polepole ili aweze kuwapatia ushirikiano.

Katika taarifa iliyotolewa leo Jumanne, Oktoba 7, 2025, imeeleza kuwa Polisi inamtaka Augustino Polepole aweze kutoa maelezo yake na uthibitisho wa shutuma alizotoa kwamba kuna afisa wa Jeshi la Polisi amehusika katika kumteka ndugu yake.

Mapema siku ya Jumatatu, Oktoba 6, 2025 ilisambaa video kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha Augustino Polepole ambaye alijitambulisha kuwa ni kaka wa Humphrey Polepole akieleza kuwa nyumba aliyokuwa anaishi Humphrey Polepole iliyopo Ununio jijini Dar es Salaam ilivamiwa usiku wa kuamkia siku hiyo na ndugu yake aliyekuwa akiishi humo kutekwa.

Sambamba na hilo Jeshi la Polisi limesema kwamba wanamhitaji Augustino ili kuthibitisha kuwa Humphrey Polepole alikuwa ni mpangaji ama mkazi wa nyumba inayotajwa kuwa utekaji huo umefanyika.

Humphrey Polepole ambaye amewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi na Cuba, hivi karibuni baada ya kujiuzulu nafasi ya ubalozi nchini Cuba Julai 13, 2025 alikuwa mkosoaji mkubwa wa mwenendo wa Serikali na chama chake cha CCM.

Katika ukosoaji wake Polepole aliibua tuhuma mbalimbali ambazo Jeshi la Polisi liliwahi kumpa wito Septemba 15, 2025 wa kufika katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai kutoa maelezo na ushahidi wa tuhuma mbalimbali ambazo amekuwa akizitoa kupitia mitandao ya kijamii.

07/10/2025

Lissu Alivyofikishwa Mahak**ani Leo, Anatarajia Kumhoji Shahidi wa Jamhuri

Dar es Salaam. Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu inaendelea leo katika Mahak**a Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam ambapo leo inatarajiwa Lissu atamuuliza maswali shahidi wa Jamhuri.

Lissu anakabiliwa na sh*taka la uhaini linaloelezwa kuwa ni kinyume na Sheria ya Kanuni ya Adhabu kifungu cha 39 (2) d kosa analodaiwa kulifanya Apili 3, 2025.

06/10/2025

Humphrey Polepole: Former Ambassador and Government Critic Reportedly Abducted

06/10/2025

Lissu kumhoji shahidi wa Jamhuri kesho, hii ni baada ya kuwasilisha ushahidi wake mbele ya Mahak**a.

06/10/2025

Hotuba ya Magufuliyatumika k**a kibwagizo kampeni za Urais za CCM Zanzibar, Dk aahidi neema kwa vijana na wazee.

06/10/2025

Onesmo Dirisha: Mwanafunzi wa UDOM aliyegeuza likizo kuwa fursa ya kipato kupitia sanaa ya uchoraji.

06/10/2025

Wamachinga Mtwara walia na changamoto ya kupata mikopo kwa wakati.

Address

Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Chanzo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to The Chanzo:

Share