23/08/2025
Mhubiri na mwimbaji wa nyimbo za injili Elisha Juma ametekwa na watu wenye silaha waliomfuata wakiwa na Landcruiser nyeupe mnamo Agosti 19, 2025.
Shuhuda wa tukio hilo anaeleza kuwa mmoja wa watekaji hao, kijana wa takribani miaka 20, alifika studio ambapo mhubiri huyo hurekodi nyimbo zake akijifanya kuwa ni msanii wa Hip hop.
Baada ya Elisha kufika, wengine wawili walifika na Landcruiser na kumchukua na kutokomea naye toka Agosti 19, 2025.
Elisha ni mhubiri wa dini ya Kikristo maeneo ya kanda ya ziwa, hivi karibuni amepata umaarufu katika mitandao kupitia nyimbo zake za kiharakati ikiwemo wimbo wa 'Wajinga ndio watatiki'.