The Chanzo

The Chanzo Uchambuzi, maoni, uchunguzi na habari zenye kugusa jamii
(1)

23/08/2025

Pamoja na mifumo ya uandikishaji wapiga kura Kuunganishwa na NIDA, INEC yaeleza kuwa haihusiani na upigaji Kura.

INEC imefafanua haya ikijibu tuhuma zilizotolewa na Kada wa Chama cha Mapinduzi, Humphrey Polepole

Saving Mothers and Babies: Tanzania Leads with AI and Care at Health SummitBy Valentina ThomasThis October, Dar es Salaa...
23/08/2025

Saving Mothers and Babies: Tanzania Leads with AI and Care at Health Summit

By Valentina Thomas

This October, Dar es Salaam will host the 12th Annual Tanzania Health Summit, bringing together over 2,000 health leaders from over 20 countries. What began as a national platform is now shaping regional policy, drawing global institutions like the WHO, the Africa CDC, and AfDB. The conversations will centre on one theme: how data and technology can transform health systems across Africa.

For Tanzania, the timing is perfect. The country has been quietly proving that digital innovation is not just a theory but a life-saving reality. Now, its story—of mothers surviving childbirth and newborns given a fighting chance—is capturing continental attention.

Read https://thechanzo.com/2025/08/23/saving-mothers-and-babies-tanzania-leads-with-ai-and-care-at-health-summit/

23/08/2025

ACT Wazalendo ni 'Project'? Othman Ajibu Madai ya Polepole.

23/08/2025

ACT Wazalendo wanamaanisha nini wanaposema wanataka 'mamlaka kamili ya Zanzibar'?

23/08/2025

Mhubiri na mwimbaji wa nyimbo za injili Elisha Juma ametekwa na watu wenye silaha waliomfuata wakiwa na Landcruiser nyeupe mnamo Agosti 19, 2025.

Shuhuda wa tukio hilo anaeleza kuwa mmoja wa watekaji hao, kijana wa takribani miaka 20, alifika studio ambapo mhubiri huyo hurekodi nyimbo zake akijifanya kuwa ni msanii wa Hip hop.

Baada ya Elisha kufika, wengine wawili walifika na Landcruiser na kumchukua na kutokomea naye toka Agosti 19, 2025.

Elisha ni mhubiri wa dini ya Kikristo maeneo ya kanda ya ziwa, hivi karibuni amepata umaarufu katika mitandao kupitia nyimbo zake za kiharakati ikiwemo wimbo wa 'Wajinga ndio watatiki'.

23/08/2025

Sakata la mwanachama wa ACT-Wazalendo Monalisa Ndala kupinga uteuzi wa Lugaha Joelson Mpina kuwa mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ACT-Wazalendo kwa sasa linasubiri umamuzi wa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Akizungumza baada ya kuitikia wito wa Msajili, Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Ado Shaibu amesema suala hilo limebaki kwa msaji wa siasa, kwani wao k**a chama wameshafafanua juu ya uhalali wa mchakato wa uteuzi na katika hatua ya sasa hawana maelezo ya ziada.

“Suala la uteuzi wa Luhaga Joelson Mpina kuwa mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umefuata taratibu zote za uteuzi wa wagombea wa chama chetu," amesema Ado.

Kwa upande wake Ndala ambaye hakutaka kuzungumza chochote baada ya kikao na Msajili, ni mjumbe wa Mkutano Mkuu uliompitisha Mpina kuwa mgombea urais.

22/08/2025

Nyerere alivyosimulia TANU ilivyoitisha mfungo wa nchi nzima

22/08/2025

Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA (BAZECHA) Susan Lyimo amesema kuwa chama chake kinadai mabadiliko ya msingi katika mfumo wa uchaguzi ikiwemo kuwepo na Tume huru kweli ya uchaguzi.

Lyimo ameyasema hayo katika mkutano wake kwa njia ya mtandao uliofanyika leo Agosti 22, 2025

22/08/2025

Wadau wasisitiza uwajibikaji wimbi la uchimbaji wa madini ya makaa ya mawe, wataka maslahi ya wananchi yatangulizwe kwanza.

22/08/2025

Unaona hizi video zina uhalisia au hazina?

Address

Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Chanzo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to The Chanzo:

Share