Mazoea TV

Mazoea TV Sports, Fun &
Entertainment

Tumeanzisha group kwa ajili yetu sote kuchati na kupeana habari na uchambuzi wa mambo mbali mbali yakiwemo ya soka. Kila...
11/05/2025

Tumeanzisha group kwa ajili yetu sote kuchati na kupeana habari na uchambuzi wa mambo mbali mbali yakiwemo ya soka. Kila mtu anaweza kuingia. Kujiunga tumia link hii hapa 👉🏽 https://chat.whatsapp.com/EHoSjWJPWzBEuNNI5yqs2N

Au Sms WhatsApp- +255752689460

Niseme nini zaidi ya shukrani! Asante wote na tuendelee kuisapoti Mazoea Media You Tube, sasa tuna wafuasi 30K+ Hii ni k...
02/05/2025

Niseme nini zaidi ya shukrani! Asante wote na tuendelee kuisapoti Mazoea Media You Tube, sasa tuna wafuasi 30K+ Hii ni kubwa sana katika kipindi kifupi toka tumerudi rasmi. Asanteni sana

Asanteni🙏 Endeleeni kutupa sapoti MAZOEA MEDIA pale You Tube🙏
19/03/2025

Asanteni🙏 Endeleeni kutupa sapoti MAZOEA MEDIA pale You Tube🙏

Imagine mtu mmoja ndo anasubiriwa hapo ifike 10,000 au 10K subscribers!!! Jamani!!! Lakini mnatisha sana huko You Tube.
19/02/2025

Imagine mtu mmoja ndo anasubiriwa hapo ifike 10,000 au 10K subscribers!!! Jamani!!! Lakini mnatisha sana huko You Tube.

Milloud Hamdi kocha mpya wa Yanga, alikuwa akiiandaa Singida kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi, ameondoka hata hajao...
04/02/2025

Milloud Hamdi kocha mpya wa Yanga, alikuwa akiiandaa Singida kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi, ameondoka hata hajaonyesha makeke.

TAARIFA KWA UMMA📌
04/02/2025

TAARIFA KWA UMMA📌

Kumekuwa na mshtuko mkubwa katika mazoezi ya Young Africans Sports Club wakati kikosi hicho kikijiandaa kwa mchezo wa Li...
04/02/2025

Kumekuwa na mshtuko mkubwa katika mazoezi ya Young Africans Sports Club wakati kikosi hicho kikijiandaa kwa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya KenGold, utakaochezwa katika Uwanja wa KMC Complex, jijini Dar es Salaam. Kocha Sead Ramovic ametangaza kuwa huo utakuwa mchezo wake wa mwisho kabla ya kuondoka klabuni hapo, baada ya kupokea ofa kutoka CR Belouizdad ya Algeria. Ramovic anachukua nafasi ya Abdelkader Amrani aliyeachana na klabu hiyo mwezi uliopita.

Tangu achukue nafasi ya ukocha tarehe kumi na tano, mwezi wa kumi na moja, mwaka elfu mbili ishirini na nne, Ramovic ameiongoza Young Africans Sports Club kwa siku themanini na moja. Katika muda huo, ameiongoza timu katika mechi kumi na tatu kwenye mashindano yote, akishinda michezo tisa, kutoka sare mara mbili na kupoteza miwili. Kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, ameshinda mechi zote sita, akifunga mabao ishirini na mbili na kuruhusu mawili pekee.

Katika mashindano mengine, Ramovic ameiongoza Young Africans Sports Club kwenye mechi moja ya Kombe la Shirikisho, akishinda mabao matano kwa sifuri, na michezo sita ya Ligi ya Mabingwa Afrika, akishinda miwili, sare mbili na kupoteza miwili. Timu yake imefunga mabao matano na kuruhusu sita kwenye mashindano hayo ya kimataifa.

Tangazo lake la kuondoka liliwashtua wachezaji na mashabiki, kwani hakukuwa na dalili za awali kuhusu uamuzi huo. Amewaaga wachezaji, akiwataka kupambana kushinda mchezo wa kesho na kuhakikisha timu inatetea ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Nafasi yake itachukuliwa na Abdihamid Moallin, ambaye alijiunga na Young Africans Sports Club k**a Mkurugenzi wa Ufundi mwezi wa kumi na moja, mwaka elfu mbili ishirini na nne, akitokea KMC. Moallin ana uzoefu wa kuiongoza Azam na KMC k**a kocha mkuu katika vipindi tofauti.

Ramovic ameacha alama kwa matokeo mazuri, ikiwemo ushindi wa mabao manne kwa sifuri dhidi ya Tanzania Prisons na Kagera Sugar, ushindi wa mabao matano kwa sifuri dhidi ya Copco na Fountain Gate, na ushindi wa mabao matatu kwa moja dhidi ya TP Mazembe. Hata hivyo, alipata changamoto katika mechi za kimataifa, akipoteza michezo miwili dhidi ya MC Alger na Al Hilal.

Kwa ujumla, mchango wake Yanga ni mkubwa na hii inazua maswali.

Kwa takwimu hizi kipa bora vita ni mbichi mno, tusubiri mechi zilizobaki angalau nusu tutaanza kuona mwelekeo halisi. Sa...
04/02/2025

Kwa takwimu hizi kipa bora vita ni mbichi mno, tusubiri mechi zilizobaki angalau nusu tutaanza kuona mwelekeo halisi. Sahivi bado tusimalize maneno

Credits: Leonard Musikula

04/02/2025
Tabora United huenda ikakumbana na changamoto k**a ilivyokuwa mwanzoni mwa msimu ilipopoteza kwa mabao manne kwa sifuri ...
29/01/2025

Tabora United huenda ikakumbana na changamoto k**a ilivyokuwa mwanzoni mwa msimu ilipopoteza kwa mabao manne kwa sifuri dhidi ya Simba Sports Club. Ikiwa zimesalia siku nne kabla ya mchezo wao wa Februari mbili kwenye Ligi Kuu ya NBC, wachezaji wao saba waliosajiliwa katika dirisha dogo bado hawajapata leseni.

Wachezaji hao ni Jean Noel, Akandwanaho, Cedric Zemba, Mwanengo, Fikirini, Chobwedo na Yasin Mustafa. Hata hivyo, wanne wazawa taratibu zao zimekamilika na wanatarajiwa kupatiwa leseni kabla ya mchezo huo.

Kwa upande wa wachezaji wa kigeni, klabu inapaswa kulipa zaidi ya shilingi milioni ishirini kwa ajili ya vibali vyao vya kufanya kazi na kuishi nchini ili wapate leseni. Changamoto hii siyo kwa sababu ya kunyimwa leseni makusudi, bali ni kutokana na Tabora United kutokamilisha malipo hayo.

Kujua zaidi, ingia You Tube search MAZOEA MEDIA au tumia link kwenye bio.

Inaelezwa kuwa timu nne maarufu barani Afrika, Orlando Pirates (Afrika Kusini), MC Alger (Algeria), Wydad Casablanca (Mo...
28/01/2025

Inaelezwa kuwa timu nne maarufu barani Afrika, Orlando Pirates (Afrika Kusini), MC Alger (Algeria), Wydad Casablanca (Moroko), na Al Ahly Benghazi (Libya), zimeonyesha nia ya kumsajili kiungo wa Yanga SC, Stephan Aziz Ki, raia wa Burkina Faso.

Aziz Ki, ambaye amekuwa mhimili mkubwa wa kikosi cha Yanga SC kwa takribani miaka mitatu, anatajwa kuwa na nafasi ya kuondoka ili kukabiliana na changamoto mpya katika taaluma yake ya soka. Ripoti mbalimbali zimeeleza kuwa nyota huyo anatafakari hatma yake huku vilabu vikubwa vikimvizia.

Kiungo huyo wa kimataifa ameonyesha kiwango cha hali ya juu katika mashindano ya ndani na kimataifa, hali iliyovutia vilabu hivyo vinavyotafuta huduma zake. Itasubiriwa kuona iwapo Yanga SC itafanikiwa kumshawishi kuendelea kubaki au kuruhusu kipaji hicho kuondoka.

Kujua zaidi, ingia You Tube search MAZOEA MEDIA au tumia link kwenye bio.

Address

Dar Es Salaam
16102

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mazoea TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share