Space Online Tv

Azizi ki wallpaper ya simu yake ameweka picha yake ya ndoa picha hiyo huyo aziz ki pamoja na mke wake kipenzi ambae ni H...
08/10/2025

Azizi ki wallpaper ya simu yake ameweka picha yake ya ndoa picha hiyo huyo aziz ki pamoja na mke wake kipenzi ambae ni Hamisa Mobetto

🟣Inaonesha kuwa wawili hawa wana mapenzi ya kweli kabisa na wanapendana hadi raha. Je wewe Wallpaper ya Simu yako umeweka picha gani?

Umegundua Nini Kutoka Kwenye Picha Hii Ya Poshy Queen ?
08/10/2025

Umegundua Nini Kutoka Kwenye Picha Hii Ya Poshy Queen ?

SIKU MBILI ZILITOSHA KUMKUBALI ROTIMIMwanamuziki wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee ameweka wazi kuwa ilimchukua siku mbili tu...
08/10/2025

SIKU MBILI ZILITOSHA KUMKUBALI ROTIMI

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee ameweka wazi kuwa ilimchukua siku mbili tu kuweza kutambua kuwa Rotimi ni mwanaume wake wa maisha.

"Ilinichukua siku mbili tu, Kujua huyu (Rotimi) ni mwanaume ambaye nitakuwa naye katika kipindi chote cha maisha yangu." - Vanessa Mdee.

Vanessa alisema hayo miezi kadhaa baada ya kuweka wazi uhusiano wake na Rotimi aliyejizolea umaarufu kupitia tamthilia ya Power.

SIJAPATA MWANAUME WA KUNITOSHELEZARapa wa k**e nchini Rosa ree anasema kuwa kwa sasa hataki kabisa kujihusisha na mahusa...
08/10/2025

SIJAPATA MWANAUME WA KUNITOSHELEZA

Rapa wa k**e nchini Rosa ree anasema kuwa kwa sasa hataki kabisa kujihusisha na mahusano ya aina yoyote kwa sababu anaona kabisa kuwa tangu aanze kuwa katika mahusiano hajapata mwanaume wa kumtoshleza wala kumpa changamoto bado.

Rosa Ree anasema kuwa ni kweli kuwa kwa sasa amekuwa na ndoto za kuja kuolewa baadae lakini hii haimfanyi hatamani kuwa katika mahusiano kwa sasa kwa sababu aliwahi kuumizwa sana na mapenzi hapo awali hivyo ilimfanya kuvunjika moyo.

"Sio kwamba sijawahi kuwa katika mahusia, Nilishawahi kuumizwa sana na ndio maana hata sasa nimeamua kukaa pembeni katika maswala hayo, Kiikubwa ni kwamba sijapata bado mwanaume anaeweza kunichallenge kifupi mwanaume ambae anaweza kuwa kidume, Akanitisha mpaka nikasema hapa kweli nimepata kidume."

"Sio kwamba wanitishe wanipige, hapana lakini awe na ile vission na intelligence kwa sababu nimetembea sehemu nyingi na kuona kabisa mwanaume huyu hajielewei kabisa."- Amefunguka Rosa Ree.

Hata hivyo Rosa ree anakiri kuwa watu wengi wamekuwa wakijudge sana muonekano wake na kuona k**a vile haweizi kujihusisha na mahusaino kitu ambacho sio kweli kwa sababu hata yeye ni mwanamke.

"NILISTAHILI KUOLEWA NA AZIZ KI."Mwanamuziki  wa Bongo Fleva Agness Suleiman Kihamba  [ AggyBaby ] ameonyesha kutokupend...
08/10/2025

"NILISTAHILI KUOLEWA NA AZIZ KI."
Mwanamuziki wa Bongo Fleva Agness Suleiman Kihamba [ AggyBaby ] ameonyesha kutokupendezwa na kitendo cha Aziz Ki kumuoa Hamisa Mobeto na amedai kuwa heshima yake aliyoijenga alipaswa kupata ndoa kabla ya Hamisa.

"Hadi leo nashindwa kuelewa Aziz Ki aliona nini kwa Hamisa hadi kufikia maamuzi ya kumuoa. Hivi hakutuona sisi wanawake wenye heshima zetu hapa mjini, Jamani Kweli mimi ni wakutanguliwa kuolewa na Hamisa mobeto..!!!" ~Amefunguka AggyBaby.

Ibraah Tz ameibua gumzo mitandaoni baada ya kufunguka kuhusu tukio la ukarimu alilofanyiwa na muigizaji maarufu Kajala k...
08/10/2025

Ibraah Tz ameibua gumzo mitandaoni baada ya kufunguka kuhusu tukio la ukarimu alilofanyiwa na muigizaji maarufu Kajala katika kipindi ambacho alikuwa anakabiliwa na changamoto za kifedha.

Akizungumza kupitia mahojiano na East Africa Radio, Ibraah alieleza kwa ucheshi lakini pia kwa kuguswa jinsi Kajala alivyojitokeza kumsaidia bila kusita.

"Kajala aliona hali yangu ilivyo, kwa hiyo akaenda pale pale kwenye kitita cha msela (Konde) akachota 20k akanipitishia dirishani. Shukurani sana shem kajala," alisema Ibraah.

NILIMUACHIA NYUMBA NZIMA MAMA QAYLLAHMwanamuziki /Mwanasiasa Nurdin Bilal maarufu k**a [Shetta] ameweka wazi jinsi alivy...
08/10/2025

NILIMUACHIA NYUMBA NZIMA MAMA QAYLLAH

Mwanamuziki /Mwanasiasa Nurdin Bilal maarufu k**a [Shetta] ameweka wazi jinsi alivyokuwa akiishi na Mama Qayllah baada ya kuachana kwao.

"Ilikuwa ni hatua ngumu sana kwangu ukifikiria ni mwanamke ambaye tumeishi naye miaka tisa na tuna watoto wawili naye, Nakumbuka siku tuliyoachana mimi ndio niondoka nyumbani na mabegi yangu tu niliamua kuacha kila kitu nikaanze maisha Mapya."

"Pia nashukuru sasa tumebaki k**a wazazi katika kilea watoto na tumekuwa tukitoka nao Out wakati mwingine lengo ni kufanya watoto wetu wasijisikie vibaya na waone uwepo wa wazazi wote katika kuwalea."- Alifunguka Shetta.

Mimi nime anza kuzungumziwa tangu nikiwa mtoto mdogo na kila ninapo enda sehemu huwa nateka attention ya watu. Kwa sasa ...
07/10/2025

Mimi nime anza kuzungumziwa tangu nikiwa mtoto mdogo na kila ninapo enda sehemu huwa nateka attention ya watu. Kwa sasa singumziwi sana mitandaoni k**a hapo kabla kwanza chakwanza siku hizi nipo sana bize

Arafu management yangu inanisimamia vizuri sana ndio maana hauoni nikizungumziwa mitandaoni k**a kipindi cha nyuma kilicho pita

Kwakuwa nilianza kuzungumziwa tangu nikiwa mtoto hizi attention za ukubwa ni hazinipi shida na sihangaiki nazo. Najua nimetoka wapi na nahitaji kwenda wapi

Amefunguka Hamisa Mobeto baada ya kuulizwa na mwandishi kuwa kwanini siku hizi Hamisa Mobeto hazungumziwi sana kwenye mitandao ya kijamii

Inasemekana msanii wa muziki wa Bongo Fleva Harmonize tangia atoke kimapenzi na Sanchi Ameshuka sana kimuziki je!  Unahi...
07/10/2025

Inasemekana msanii wa muziki wa Bongo Fleva Harmonize tangia atoke kimapenzi na Sanchi Ameshuka sana kimuziki je!
Unahisi nini kinamkwamisha...?🤔

"NIMEACHANA NAO BADO WANANIPENDA."Msanii wa filamu za Bongo Movie na mjasiriamali Diva Jacqueline Wolper ameibuka na kud...
07/10/2025

"NIMEACHANA NAO BADO WANANIPENDA."
Msanii wa filamu za Bongo Movie na mjasiriamali Diva Jacqueline Wolper ameibuka na kudai kuwa katika Mahusiano yake yote ambayo amewahi kuwa nayo wanaume anaoachana nao bado wanakuwa wanampenda.

Wolper amefunguka kuwa katika maisha yake yote anapokuwa anaachana na wanaume aliokuwa nao Kwenye Mahusiano wote wanakuwa bado wanamuhitaji licha ya yeye kuwatema na kutowahitaji tena.

"Ujue mimi kila nikiachana na mwanaume anakuwa bado ananipenda, pale nilikimbia kwa sababu nikiachana na boyfriend, huwa sipendi niendelee kuwasiliana naye wala kusogeleana naye, sipendi kusalimiana na X."

"Ilishawahi kutokea X ananihitaji kwa ajili ya mambo ya kibiashara lakini kwa sababu nakuwa sihitaji kabisa kuwasiliana nao nili-crash halafu nikakosa dili, hilo ni pepo ambalo ninalo nadhani nitamwambia Mchungaji aniombee.” ~Amefunguka Jacqueline wolper.

"NILIKUTANA NA MKE WANGU SIKU YA NDOA."~Staa wa filamu za kibongo Issa M***a [Cloud 112] ameweka wazi namna alivyokutana...
07/10/2025

"NILIKUTANA NA MKE WANGU SIKU YA NDOA."
~Staa wa filamu za kibongo Issa M***a [Cloud 112] ameweka wazi namna alivyokutana kwa mara ya kwanza na mke wake siku ya ndoa yao.

"Mimi na mke wangu tulitongozana kwenye simu tu, Tukawa tunawasiliana sana lakini hatukuwahi kukutana Mubashara kwa mara ya kwanza tunaonana ilikuwa ni siku mbili kabla ya ndoa yetu." ~Amefunguka Cloud 112.

Burudani nchini Tanzania imepata gumzo jipya baada ya taarifa zisizo rasmi kuibuka zikidai kuwa Huddah Nai, maarufu kwa ...
07/10/2025

Burudani nchini Tanzania imepata gumzo jipya baada ya taarifa zisizo rasmi kuibuka zikidai kuwa Huddah Nai, maarufu kwa mtindo wake wa kipekee na maisha ya kifahari, anajiandaa kuingia kwenye ndoa na Kiungo Mshambuliaji wa Yanga SC, Pacome Zouzoua.

Mashabiki wa soka na wafuasi wa mitandao ya kijamii wamejibu taarifa hizi kwa mchanganyiko wa kicheko na mshangao, huku wengi wakisema:

“Kama ndoa hii itatimia, Pacome atakuwa amepata mke kweli kweli… 😂😂😂😂”

Pacome, ambaye ni kipaji kinachoshika nafasi muhimu kwenye Yanga SC, na Huddah, ambaye amejulikana k**a mtu wa hadhi na mtindo, wameshika vichwa vya habari vya burudani, huku mvutano wa mashabiki ukijumuisha maoni ya kutegemea taarifa rasmi.

Mitandao Yazidi Kuwaka Moto – Uhusiano wa Huddah na Pacome Waibua Hisia Kali
Wengi wanashangaa na kujiuliza k**a jozi hii itathibitishwa rasmi, huku wengine wakihimiza muunganiko wa mitindo na soka k**a jambo la kuvutia litakaloongeza mvuto wa burudani na michezo nchini.

Hata hivyo, taarifa rasmi kutoka kwa jozi hiyo au familia zao bado haijafahamika, na mashabiki wanashauriwa kusubiri kwa hamu taarifa ya kweli kabla ya kuhitimisha chochote.

Address

Ubungo External
Dar Es Salaam

Telephone

+255764944226

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Space Online Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Space Online Tv:

Share