Telebongo

Telebongo Karibu Tuongee Filamu!

02/01/2026

Je, anahusiks?

18/12/2025

Siku ya jana, mwongozaji wa filamu kutoka India, S.S Rajamouli siku ya jana alipata fursa ya kuongea na mwongozaji mkubwa wa filamu duniani, James Cameron, yule aliyefanya Titanic, Terminator 2, Avatar, Alien, True Lies n.k.

Mwamba James anataka awepo wanavyoendelea ku-shoot filamu ya VARANASI.

10/12/2025

Hizi ni filamu nzuri za Bollywood ambazo haziongelewi sana. Ukipata wasaa zitazame, uta-enjoy mno.

SHABIKI ALIPOTAKA KUMPONZA GOVINDAGovinda alikuwa moja ya mastaa wakubwa zaidi Bollywood miaka ya 1990 na 2000, umaarufu...
10/12/2025

SHABIKI ALIPOTAKA KUMPONZA GOVINDA

Govinda alikuwa moja ya mastaa wakubwa zaidi Bollywood miaka ya 1990 na 2000, umaarufu wake ukiwaficha hata mastaa wakubwa wa tasnia hiyo, akiwemo Amitabh Bachchan!

Mashabiki vijana walikuwa tayari kufanya chochote ili tu wamuone au kupata sahihi yake, wakifurika kwenye sets za filamu na matukio aliyohudhuria.

Mmoja kati ya hao alikuwa Santosh Rai, shabiki mkubwa wa Govinda ambaye mwaka 2008 alitembelea seti ya filamu ya "Money Hai Toh Honey Hai" huko jijini Mumbai, akitumaini kumuona staa wake kipenzi. Wakati wa picha kurekodiwa, alikaa kimya nyuma ya waigizaji na watu wa nyuma ya kamera akitazama kwa hamu kila kinachoendelea, bila kujua kuwa tukio hilo la ndoto yake lingegeuka kuwa la kushtua.

Kile kilichoanza k**a ziara ya kawaida kati ya shabiki na msanii wake, kiligeuka ghafla kuwa tukio la kushtusha baada ya Govinda kupoteza uvumilivu na kumpiga Santosh kofi mbele ya kila mtu. Kofi hilo lilikuwa fedheha kubwa kwa Santosh, ambaye alikuwa akimuabudu nyota huyu wa "Dostana".

Wakati Govinda akisema kwamba shabiki huyo “alileta kero kwa wacheza muziki wa kike” wakati wa ku-shoot, Santosh alisimulia upande tofauti kabisa wa tukio.

Akizungumza na Rediff, Santosh alisema: “Fikiria kupigwa na mtu uliyemchukulia k**a mungu.”

Kilichofuata kilikuwa kesi ya kisheria iliyodumu kwa miaka 9, ikirudi kwenye vichwa vya habari kila ilipofufuliwa. Santosh Rai aliwasilisha kesi ya kushambuliwa, akidai haki na fidia kwa aibu aliyopata.

Hatimaye kesi ilifika Mahak**a kuu, ambako majaji hawakusita kumkemea Govinda. Kwa mujibu wa Rediff, mahak**a ilimwambia Govinda, “Tuna-enjoy filamu zako, lakini hatuwezi kuvumilia wewe kumpiga mtu.”

Kadri kesi ilivyoendelea, timu ya wanasheria wa Govinda ilijaribu kuimaliza kwa njia ya maelewano, wakitoa msamaha na fidia ya rupia laki tano. Mahak**a ilibainisha kwamba angeweza kushtakiwa ikiwa Santosh angekataa msamaha huo, na angekabiliwa na kifungo cha hadi miaka miwili kwa vitisho na shambulio.

Mwaka 2017, Govinda aliomba msamaha hadharani kwa Santosh Rai, akitoa tamko la toba bila masharti na kutaka kutoa fidia ya fedha. Lakini Santosh alikataa fedha hizo, akiiambia Hindustan Times: “Nilitaka hak

09/12/2025

Sharmila Tagore ni mwigizaji mashuhuri wa India kutoka kwenye ukoo wa kifahari wa Kibengali wa Tagore.Anajulikana kwa mc...
08/12/2025

Sharmila Tagore ni mwigizaji mashuhuri wa India kutoka kwenye ukoo wa kifahari wa Kibengali wa Tagore.

Anajulikana kwa mchango wake wa kipekee katika filamu za Kibengali na Kihindi kuanzia Apur Sansar, Kashmir Ki Kali, Mausam, Aradhana, Amar Prem na Chupke Chupke.

Sharmila aligeuka kuwa nyota mkubwa wa Bollywood, akipata umaarufu kupitia ushirikiano wake na Rajesh Khanna na kuvunja miiko iliyokuwepo wakati huo (k**a kuvaa bikini kwenye An Evening in Paris).

Aliolewa na Mansoor Ali Khan Pataudi, Nawab kutoka Pataudi, akasilimu na kuchukua jina Ayesha Sultana.

Huyu ndiye mama wa waigizaji Saif Ali Khan na bibie Soha Ali Khan.

Leo ametimiza miaka 81.

Happy birthday to SHARMILA TAGORE.

08/12/2025

Mwigizaji nguli Dharmendra angekuwa anatimiza miaka 90 siku ya leo.

Familia ya Deol wamemkumbuka kwa upendo na posti za hisia.

Mtoto wake mkubwa Sunny Deol, binti yake Esha Deol kutoka ndoa yake ya pili na mke wake mwigizaji Hema Malini na mpwa wake Abhay Deol, ambaye pia ni mwigizaji, wametumia Instagram kumkumbuka huyu gwiji wa Bollywood katika siku hii maalum.

Sunny Deol ame-share hii video na kuandika jinsi anavyomkumbuka baba yake.

Ameandika, “Leo ni siku ya kuzaliwa ya baba yangu. Papa yuko daima nami, ndani yangu, nakupenda papa. Nakukumbuka.”

Happy Heavenly birthday to DHARAM SINGH DEOL.

WAIGIZAJI AMBAO HAWAJWAHI KUWA KWENYE NDOA.AKSHAYE KHANNA: Anaamini ndoa siyo vitu vyake, anasikia fahari kuendelea kuwa...
07/12/2025

WAIGIZAJI AMBAO HAWAJWAHI KUWA KWENYE NDOA.

AKSHAYE KHANNA: Anaamini ndoa siyo vitu vyake, anasikia fahari kuendelea kuwa single.

ABHAY DEOL: Ameamua kutofunga ndoa na kutoweka hadharani maisha yake binafsi.

UDAY CHOPRA: Mziwanda wa familia ya Yash Chopra, ameamua kukaa mbali na uigizaji pamoja na ndoa.

AMEESHA PATEL: Ameamua kuweka nguvu kwenye kazi na kujipenda, akiishi kwa furaha akiwa single.

KARAN JOHAR: Mwamba aliyekuletea Kuch Kuch Hota Hai, Ae Dil Hai Mushkil, Kal Ho Na Hoo, Kabhi Kushi Kabhie Gham n.k Hana ndoa ingawa ni baba wa watoto wa kupandikiza (Surrogacy).

SUSHMITA SEN: Ingawa amewaasili mabinti wawili lakini yeye hajafunga ndoa.

SALMAN KHAN: Mseja wa dunia huyu, ambaye Hana hata mtoto mmoja. Dunia bado inasubiri ndoa yake.

TABU:Ameschagu kujitegemea huku akiisha maisha ya kujipangia nini anafanya na nini hafanyi.

Itazame hii!
30/05/2025

Itazame hii!

Subscribe ili kupata recaps za movies kutoka sehemu mbalimbali duniani.Pia kuna historia, stori na mikasa mikali ya waigizaji, filamu na watu walio nyuma ya ...

22/01/2025

Van Damme

Address

Ubungo
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Telebongo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Telebongo:

Share