28/10/2024
PART 1:Wengi hasa wafuatiliaji wa soka katika miaka ya 1990s mpaka 2000s wanamfahamu mtu anaitwa Ronaldo Luís Nazário de Lima, alikuwa maarufu kwa jina la Ronaldo, mchezaji wa zamani wa vilabu vya Inter Milan, Barcelona, Real Madrid, PSV, Corinthians na timu ya taifa ya Brazili ambaye kwa sasa ni mfanyabiashara mkubwa na mmiliki wa timu ya La liga ya Real Valladolid.
Alikuwa mshambuliaji mahiri akitwaa kombe la dunia na Brazil mwaka 2002 na kutwa a tuzo ya mchezaji bora wa dunia mara 3. Wengi wanadhani jina la Ronaldo wa sasa limetokana na umaarufu wa Ronaldo wa zamani, la hasha Ronaldo wa sasa jina lake lina historia tofauti.
Cristiano Ronaldo Dos Santos Aveiro alizaliwa mwaka Februari 5, mwaka 1985 huko Funchal katika visiwa vya Madeira, kwa mama Maria Doroles Dos Santos Aveiro na marehemu baba yake Jose Dinis Aveiro.
Alipozaliwa tu baba yake akampatia jina la Ronaldo akimuona k**a Ronald Reagan (Rais wa Marekani) ajae.
Wakati huo baba yake hakuwa na wazo kabisa kuhusu mwanae kuwa mwanasoka, alimpenda sana Rais Reagan, ambaye wakati Ronaldo anazaliwa ndio alikuwa ametoka kuapishwa kuwa rais katika awamu yake ya pili ya uongozi
Google
Ronaldo ni mtoto wa mwisho katika familia ya watoto watatu waliozaliwa na wazazi wake, mwingine ni Maria Dolores mwenye fani ya upishi na Jose Denis Aveiro ambaye ni askari wa zamani, mtunza bustani na mtunza vifaa. Ana ndugu wengine wakubwa kaka yake Hugo, na dada zake wawili Elma na Liliana Cátia "Katia".
Katika utoto wake, Ronaldo alikuwa anadekezwa na kudeka kupita kiasi. Kuna wakati ndugu zake hasa kaka zake walilazimika kubeba makosa yake. Alijiliza na kujilalamisha kitoto kila alipoona amekosea, na kwa huruma zao ndugu zake wakubwa walibeba makosa yake mbele ya wazazi wao.
Baba yake José, alifariki mwaka 2005 Ronaldo akiwa na miaka 20 tu, huku mama yake akitibiwa saratani ya matiti mwaka 2007, ingawa anaendelea vyema sasa.