17/08/2026
Wakili wa Kujitegemea na Mteteezi wa Haki za Binadamu, Peter Madeleka, ameachiwa kwa dhamana leo Agosti 17, 2026, baada ya kushikiliwa kwa takriban siku tatu katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central) jijini Dar es Salaam.
Upatikanaji wa dhamana hiyo umethibitishwa na Wakili Paul Kisabo kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), aliyekuwa akifuatilia mchakato huo.
Akizungumza kwa njia ya simu, Kisabo ameeleza kuwa licha ya mteja wao kutofikishwa mahak**ani ndani ya saa 24 k**a sheria inavyoelekeza, Jeshi la Polisi hatimaye limeridhia kumpa dhamana kupitia Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa (ZCO).
Taratibu hizo zilikamilishwa majira ya mchana baada ya Madeleka kudhaminiwa na watu watatu, wakiwemo Wakili Kisabo pamoja na ndugu zake wawili.
“Asubuhi niliamkia Central Police Station na kukutana na ZCO kuomba dhamana ya Wakili Madeleka, ambapo aliniambia nirudi saa nane mchana. Tuliporejea, amekubali adhaminiwe na watu watatu mimi na ndugu zake wawili. Dhamana ipo wazi na tumemdhamini,” ameeleza Wakili Kisabo.
Kuhusu hatua za kisheria, Kisabo amebainisha kuwa msisitizo wao mkuu ulikuwa ni kupata dhamana ya polisi ili mteja wao awe nje wakati taratibu zingine zikiendelea.
Wakili Madeleka alik**atwa Agosti 14, 2026, majira ya saa 9:30 alasiri katika viunga vya Mahak**a ya Uhujumu Uchumi (Mikocheni B) akitekeleza majukumu yake. Polisi walieleza kuwa alik**atwa kwa tuhuma za kudharau amri za Mahak**a Kuu zilizotolewa Julai 27 na Agosti 13, 2026 hatua iliyotokea saa chache baada ya kutangaza nia ya kufungua kesi kupinga zuio la Msajili wa Mahak**a linalowazuia mawakili kufanya mahojiano na vyombo vya habari maeneo ya mahak**a.