Gilly Bonny Tv

Gilly Bonny Tv Independent Media.
(3)

Wakili wa Kujitegemea na Mteteezi wa Haki za Binadamu, Peter Madeleka, ameachiwa kwa dhamana leo Agosti 17, 2026, baada ...
17/08/2026

Wakili wa Kujitegemea na Mteteezi wa Haki za Binadamu, Peter Madeleka, ameachiwa kwa dhamana leo Agosti 17, 2026, baada ya kushikiliwa kwa takriban siku tatu katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central) jijini Dar es Salaam.

​Upatikanaji wa dhamana hiyo umethibitishwa na Wakili Paul Kisabo kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), aliyekuwa akifuatilia mchakato huo.

Akizungumza kwa njia ya simu, Kisabo ameeleza kuwa licha ya mteja wao kutofikishwa mahak**ani ndani ya saa 24 k**a sheria inavyoelekeza, Jeshi la Polisi hatimaye limeridhia kumpa dhamana kupitia Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa (ZCO).

​Taratibu hizo zilikamilishwa majira ya mchana baada ya Madeleka kudhaminiwa na watu watatu, wakiwemo Wakili Kisabo pamoja na ndugu zake wawili.

“Asubuhi niliamkia Central Police Station na kukutana na ZCO kuomba dhamana ya Wakili Madeleka, ambapo aliniambia nirudi saa nane mchana. Tuliporejea, amekubali adhaminiwe na watu watatu mimi na ndugu zake wawili. Dhamana ipo wazi na tumemdhamini,” ameeleza Wakili Kisabo.

​Kuhusu hatua za kisheria, Kisabo amebainisha kuwa msisitizo wao mkuu ulikuwa ni kupata dhamana ya polisi ili mteja wao awe nje wakati taratibu zingine zikiendelea.

​Wakili Madeleka alik**atwa Agosti 14, 2026, majira ya saa 9:30 alasiri katika viunga vya Mahak**a ya Uhujumu Uchumi (Mikocheni B) akitekeleza majukumu yake. Polisi walieleza kuwa alik**atwa kwa tuhuma za kudharau amri za Mahak**a Kuu zilizotolewa Julai 27 na Agosti 13, 2026 hatua iliyotokea saa chache baada ya kutangaza nia ya kufungua kesi kupinga zuio la Msajili wa Mahak**a linalowazuia mawakili kufanya mahojiano na vyombo vya habari maeneo ya mahak**a.

17/08/2026

Wananchi wa kata ya Twangoma jijini Dar es Salaam wameiomba Serikali kuwajengea daraja la kudumu eneo la Goloka B kwa Kibajaji, kwani lililopo sio salama na linahatarisha usalama wa watu hususani kipindi cha mvua.

Akiongea Mara baada ya kukagua daraja hilo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ameagiza TARURA, kufanya ukaguzi na kutoa tathimini kwenye eneo la daraja hilo k**a panafaa kujengwa daraja jipya au wapendekeze eneo jingine litakalokuwa linaungana na barabara ili daraja hilo liweze kujengwa kwa haraka.

Chalamila ametoa maagizo hayo Leo Agosti 17,2026 alipokuwa kwenye ziara ya kukagua ujenzi wa barabara ya Masaki iliyopo Toangoma pamoja na ya Ndunguru iliyopo Kibondemaji Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, huku akiwataka wananchi kuwa watulivu wakati zoezi hilo likiwa linaendelea.

17/08/2026

VIDEO 📹

17/08/2026

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert John Chalamila, leo Agosti 17, 2026, ametoa agizo la kuk**atwa kwa dereva yeyote atakayepaki lori katika maeneo ya service road bila kufuata utaratibu.

Chalamila ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Temeke, ambapo amekagua hali ya matumizi ya barabara na kubaini malori yakipaki katika maeneo yasiyoruhusiwa.

Amesema tabia hiyo inasababisha usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara, ikiwemo kuzuia njia na kuathiri matumizi sahihi ya miundombinu hiyo.

Kutokana na hali hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa amewaagiza viongozi na vyombo vinavyohusika kuhakikisha agizo hilo linatekelezwa na dereva yeyote atakayekiuka utaratibu wa maegesho ya malori katika service road anachukuliwa hatua.

Chalamila amesema hatua hiyo inalenga kurejesha utaratibu katika matumizi ya barabara na kuhakikisha miundombinu ya barabara inatumika kwa usalama na kwa manufaa ya watumiaji wote.

17/08/2026

Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Asemewe Taifa, Geofrey Kiliba, amewataka vijana na Watanzania kwa ujumla kuweka mbele amani, maridhiano na ushirikiano kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Akizungumza katika mkutano na vijana, Kiliba amesema uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan umeendelea kusisitiza umuhimu wa maridhiano na kuwataka Watanzania kutumia mazungumzo katika kutatua tofauti zao.

Kiliba amesema wito wa maridhiano unalenga kuwaunganisha Watanzania na kuweka mazingira ya amani na utulivu kwa ajili ya maendeleo.

“Huyu mama kwa ustahimilivu na unyenyekevu wake kila itwapo leo anatoa wito wa maridhiano... Njooni tukawe meza moja tuzungumze, kuna mahala tumekoseana njooni tusamehane,” alisema Kiliba.

Amesema hakuna sababu ya msingi inayopaswa kuzuia juhudi za maridhiano, akisisitiza kuwa mazungumzo yana nafasi muhimu katika kujenga amani, upendo, umoja na mshik**ano.

“Hakuna sababu yoyote ya kimsingi ndani ya dunia hii, na hakuna mtu yeyote anayeweza kuwa na hekima ya kukupa hoja za kimsingi za kukupa mbadala wa maridhiano,” alieleza.

Kiliba pia amewataka vijana kuendelea kushiriki katika shughuli za maendeleo na kulinda umoja wa taifa, huku akitoa wito wa kumuunga mkono Rais Samia katika juhudi za kusukuma mbele maendeleo ya Tanzania.

17/08/2026

VIDEO 📹

17/08/2026

"Jayrutty afanye kazi yake, Wenzake waliopita hawakuleta fujo, lakini kwanini tangu alipoingia yeye kuwa mzabuni wa Simba kumekuwa na fujo?"

17/08/2026

Huu hapa muonekano wa Uwanja uliopo jijini Arusha utakaotumika kwenye michuano ya AFCON mwakani 2027.

17/08/2026

Klabu ya Singida Black Stars imefanikiwa kupata uwanja wa kufanyia mazoezi katika Manispaa ya Bukoba kwa ajili ya maandalizi ya mwisho kuelekea mchezo wake dhidi ya Kagera Sugar FC.

Kupitia taarifa yake, Singida Black Stars imesema kikosi hicho kitafanya mazoezi katika uwanja huo kesho, yakilenga maandalizi ya kiufundi kabla ya kukutana na Kagera Sugar.

“Tume fanikiwa kupata uwanja wa kufanyia mazoezi mwisho hapa mjini Bukoba, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mwisho kuelekea mchezo wetu dhidi ya Kagera Sugar FC,” imeeleza taarifa hiyo.

Klabu hiyo imeongeza kuwa mazoezi hayo yatazingatia maandalizi ya kiufundi kwa ajili ya mchezo huo.

Singida Black Stars pia imewashukuru wenyeji wake kwa ushirikiano walioutoa katika kuwezesha timu hiyo kupata mazingira ya kuendelea na maandalizi yake mjini Bukoba.

Address

Sinza Makaburini
Dar Es Salaam
1110111101(2)

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gilly Bonny Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share