Gilly Bonny Tv

Gilly Bonny Tv Independent Media.
(4)

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Juma Mkomi, amewahamasisha watumishi wa umma ...
09/10/2025

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Juma Mkomi, amewahamasisha watumishi wa umma kote nchini kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Akizungumza katika kikao cha tatu cha Baraza la Nane la Wafanyakazi kilichofanyika jijini Dodoma kwa siku mbili, Mkomi alisema licha ya kutokuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa, ana mapenzi na ustawi wa taifa, hivyo ni muhimu kwa kila Mtanzania mwenye sifa ya kupiga kura, hasa watumishi wa umma, kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika mchakato huo wa kidemokrasia.

"Nawaomba wenzangu watumishi wa umma tujitokeze kwa wingi siku ya Oktoba 29 kwenda kupiga kura huu ni wajibu wetu wa kikatiba na njia ya kushiriki moja kwa moja katika maamuzi ya nchi yetu," alisema Mkomi.

Aidha, alibainisha kuwa hata viongozi wa kisiasa wamekuwa wakihamasisha familia zao kujitokeza kupiga kura, hivyo ni vyema pia kwa wafanyakazi wa umma kuwa mstari wa mbele katika kushiriki kwa amani na utulivu.

"Niwaombe wajumbe wa baraza hili na watumishi wote, tusiwe nyuma. Tuwe mfano wa kuigwa katika kujenga demokrasia kwa kushiriki uchaguzi," alisisitiza.

Kauli hiyo imekuja wakati nchi ikijiandaa kwa uchaguzi ambao unatarajiwa kushirikisha wananchi katika kuchagua viongozi watakaowakilisha maeneo yao, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha utawala bora na ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya maendeleo.

Mkurugenzi wa Nishati safi  ya kupikia, Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, ametoa wito kwa shule zote nchini  kuhakiki...
09/10/2025

Mkurugenzi wa Nishati safi ya kupikia, Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, ametoa wito kwa shule zote nchini kuhakikisha zinaachana na matumizi ya kuni na badala yake kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwemo gesi, majiko banifu, na mkaa mbadala.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya nishati safi ya kupikia inayotekelezwa chini ya mpango wa CookFund katika Mkoa wa Mwanza, Mlay amesema kuwa shule nyingi bado zinategemea kuni k**a nishati ya dharura, hali inayochangia uharibifu wa mazingira na madhara kwa afya ya watumiaji.

“Katika ziara hii nimebaini Shule nyingi zinatumia kuni k**a nishati ya dharura hivyo nitoe wito kwa uongozi wa shule mkishirikiana na Afisa Elimu kuanza kutumia mkaa mbadala ambao ni rafiki kwa mazingira na unachangia katika kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa." Amesema Mlay

Aidha, Bw. Mlay amepongeza baadhi ya shule ambazo tayari zimeanza kutumia nishati safi, ambazo hazifadhiliwi na mradi wa Cookfund ikiwemo shule ya Sekondari ya wavulana Musabe pamoja na Shule ya Msingi Buhongwa A akizitaja kuwa mfano bora kwa taasisi nyingine nchini.

Amesema matumizi ya nishati safi huchangia kwa kiasi kikubwa kulinda afya ya wanafunzi na walimu dhidi ya magonjwa ya mfumo wa upumuaji, yanayosababishwa na moshi kutoka kwa kuni na mkaa wa kawaida.

“Tunapongeza juhudi za shule zinazohamia kwenye nishati safi ya kupikia kwani hii hatua ni kubwa katika kulinda afya, mazingira na hata kuongeza ufanisi wa shughuli za kila siku shuleni hivyo nitoe wito kwa shule zote ambazo bado hazijaanza kutumia nishati safi ya kupikia, kuanza kutumia nishati safi kwani ni nafuu na zinaokoa muda." Ameongeza Bw. Mlay

vilevile, Mlay amehimiza Serikali za Mitaa, Wakuu wa Shule na wadau wa elimu kushirikiana kwa karibu katika kuhakikisha taasisi za elimu zinapata vifaa vya kisasa vya kupikia kwa kutumia nishati safi.

Amesisitiza kuwa mradi wa CookFund na mipango mingine ya kitaifa iko tayari kusaidia shule zinazotaka kuhamia kwenye mfumo huo wa kisasa wa kupikia ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia 2024 - 2034 ambao unalenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2034, asilimia 80

09/10/2025

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amewaonya baadhi ya makada wa chama hicho wanaowaunga mkono wagombea wa vyama vya upinzani, akisema wasitarajie CCM itashindwa.

Makada wanaozungumziwa na Dkt Samia, ni baadhi ya waliokuwa watiania wa nafasi mbalimbali kwa tiketi ya chama hicho, lakini vikao havikuwapitisha.

Dkt Samia ametoa onyo hilo leo, Alhamisi Oktoba 9, 2025 katika hotuba yake mbele ya wananchi wa Musoma mkoani Mara, katika mkutano wake wa kampeni za urais.

“Najua ndani ya Mara hapa kuna watu wamenunanua na katika kununa kwao wanasaidia wagombea wa vyama vya upinzani, ili waikomoe CCM.

“Tunataka kuwaambia CCM haikomoki na katika kuthibitisha hilo, niwaombe ndugu zangu Oktoba 29 tutoke wote kwa pamoja tukachague CCM,” amesema Dkt Samia.

09/10/2025

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amesema katika Mkoa wa Mara pekee, atafufua bandari zisizotumika, kufikisha mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) Mjini Musoma na kuuendeleza uwanja wa ndege.

Dkt Samia ametoa ahadi hizo leo, Alhamisi Oktoba 9, 2025 katika hotuba yake mbele ya wananchi wa Musoma, mkoani Mara, katika mkutano wake wa kampeni za urais.

Amesema anatambua kuna haja ya Mkoa wa Mara kuwa na Uwanja wa Ndege na kwamba atauendeleza ili ufikie kiwango cha kutua ndege kubwa za kibiashara.

Kuhusu bandari iliyoacha kutumika, amesema itafufuliwa na iliyopo itaendelezwa, ili MV Mwanza itakayosafirisha abiria na mizigo kutoka Mwanza hadi Mara na meli nyingine kubwa zitie nanga.

Dkt Samia pia ameahidi kujenga SGR kutoka Bandari ya Tanga, kupitia Moshi, Arusha hadi Musoma na inatarajiwa kuleta mapinduzi ya kiuchumi ndani ya mkoa huo.

“Ndugu zangu Wana Mara lililobaki hapa twendeni tukachague CCM ili tuliyoyasema hapa tukayafanyie kazi,” amesema.

09/10/2025

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amesema dhamira ya Serikali yake katika miaka mitano ijayo ni kumwezesha kila mwananchi kiuchumi kwa kuchukua hatua mbalimbali zitakazolifanikisha hilo.

Miongoni mwa hatua hizo kwa mujibu wa Dkt Samia, ni kujenga masoko na stendi katika maeneo mbalimbali, zitakazotumika na wananchi kufanya biashara na hatimaye kujipatia kipato.

Dkt Samia ametoa ahadi hiyo leo, Alhamisi Oktoba 9, 2025 alipozungumza na wananchi wa Musoma mkoani Mara, katika mkutano wake wa kampeni za urais.

Jambo lingine aliloahidi kulifanya kumwezesha mwananchi kiuchumi ni kutenga Sh200 bilioni kwa ajili ya uwezeshaji wa biashara ndogondogo ili zikue nao wajipatia kipato na kuimarisha ustawi wao.

Sio hayo tu, Dkt Samia amesema katika miaka mitano hiyo, atarasimisha biashara zisizo rasmi, ili wafanyabiashara wake wapate haki, fursa na neema zote k**a wanazozipata wengine na kukuza vipato vyao.

Utoaji wa ruzuku ya mbolea, chanjo kwa mifugo ni mambo mengine aliyoyaahidi Dkt Samia ili kumwezesha mwananchi kiuchumi na kuimarisha vipato vyao.

09/10/2025

"Waingereza wana msemo wao unasema vitendo vinaongea kwa sauti zaidi kuliko maneno, maelezo yaliyotolewa hapa na Wagombea wa Ubunge wa Majimbo na Viti maalumu wamewasilisha mawazo ya ukweli juu ya vitendo ambavyo vimefanyika chini ya Uongozi wako na kwakweli wala sio kwa Musoma tu, kwa Tanzania nzima
.. Sasa wapo watu wanatuuliza, CCM ninyi mnachuana na nani? Majibu yetu ni rahisi tu, kuna Vyama 19 vilivyoandikishwa na kati yake Vyama 17 vina wagombea Urais na Kimoja kina wagombea Ubunge peke yake na kingine kiliweka mpira kwapani. Sasa CCM sisi tufanyaje, sisi tunagombea na waliokubali kuingia kwenye mchezo. Wale walioogopa mchezo hatuna la kuwasaidia kwasababu sheria haimalizimishi mtu kugombea wala hakuna sheria inayosema Chama fulani lazima kigombee. Wamekataa kanuni za mchezo wakatoka, nchi lazima iende haiwezi kusimama.

"Na kusema kwamba uchaguzi hautokuwepo ni ndoto ya mchana na ndoto za mchana ni mbaya kwasababu unaweza ukaota dunia imeungana na ardhi kumbe hakuna kitu. Niwaambie Musoma na Tanzania, uchaguzi utakuwepo tarehe 29 na utakuwa wa amani na utulivu, wala msisikilize maneno yaliyoko kwenye mtandao, maana kwenye mtandao nako kuna mambo ukiyasikiliza utafikiri ni muvi ya kihindi ambayo mwenye kucheza hiyo muvi anakufa halafu anafufuka tena anaendelea."- Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania bara, Ndugu Stephen Wasira, kwenye kampeni za Dkt. Samia Suluhu Hassan Musoma Mjini leo Oktoba 09, 2025.

09/10/2025

"Nasimama mbele yenu ndugu zangu kwa heshima na taadhima naombeni kura zenu zote kwa Mama yetu Samia Suluhu Hassan, ni mwanamke aliyetuheshimisha wanawake. Mama Samia sio fisadi, Mama Samia sio mwizi na ndio maana wanawake wa Mkoa wa Mara tunathubutu kusema mitano tena inakustahili Mama.
.... Tulikwenda wanawake kutoka kila Kata za Mkoa wa Mara nyumbani kwa Mama Samia anapoishi yeye na Mama yake mzazi. Tulikwenda kuangalia, na wanawake wa kila Kata za Mkoa wa Mara ni mashuhuda Mama, walidhani watakutana na maghorofa, wanawake wakakuta nyumba anayoishi Mama yako mzazi, Mhe. Mwenyekiti wetu ni k**a nyumba anayoishi Mama yangu mimi, Muuza dagaa."- Agnes Marwa, Mbunge mteule wa viti Maalum Mkoa wa Mara, akizungumza kwenye Kampeni za Dkt. Samia Suluhu Hassan Musoma Mjini leo Oktoba 09, 2025.

09/10/2025

Mgombea wa urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amesema anapoomba ridhaa ya kuwaongoza Watanzania kwa nafasi ya urais, haendi kujifunza, kwa sababu tayari anaujua uongozi kutokana na uzoefu wake.
Katika msisitizo kuhusu hilo, Dkt Samia amewasihi Watanzania wasichague viongozi kutoka upinzani, kwa kuwa hawana uzoefu wa kuiongoza nchi na majimbo, hivyo watakwenda kujifunza.
Dkt Samia ameeleza hayo, leo Alhamisi Oktoba 9,2025 wakati akizungumza na wananchi wa Bunda mkoani Mara, katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika wilayani humo, katika mwendelezo wa kusaka, huku akiwataka Watanzania kujitokeza Oktoba 29 kupiga kura.
“Nataka niwaambie jambo moja katika uendeshaji wa nchi, hakuna majaribio... mpe nchi yule ambaye, unayemuamini na ataendesha vema na maslahi ya wananchi yatapatikana,”

“Ukiangalia kwetu Tanzania, chama kitakachofanya kazi na maslahi ya wananchi yatapatikana ni Chama cha Mapinduzi peke yake, wengine bado... Mkiwapa wengine iwe Serikali au jimbo wanawenda kuwafuja au kuwapoteza,” ameeleza.

Dkt Samia ameongeza kuwa, “Kwa sababu kwanza watajifunza, lakini ukimpa jimbo asiyekuwa CCM anakwenda kuongea na nani, anakwenda kuongea nani au kumwomba maji au barabara nani? Kwa sababu mwenye Serikali ni Chama cha Mapinduzi yeye ni mpinzani,” ameeleza.

Dkt Samia amewaomba wananchi wa Bunda, kutocheza na suala hilo...akiwasihi kuwachagua wagombea wa CCM kuanzia ngazi ya udiwani hadi urais ili safari ya maendeleo iendelee.
“Nataka kuwaambia msidanganywe, msidanganyike, maendeleo na maslahi yenu yatatokana na Serikali ya Chama cha Mapinduzi,” amesisitiza Dkt Samia.

Katika mkutano huo, Dkt Samia amewaahidi wananchi wa Bunda, iliyomuisha majimbo ya Bunda Mjini na Vijijini pamoja na Mwibara kuwa awamu ijayo Serikali itaongeza nguvu kwenye sekta ya uvuvi.
“Ilani yetu kwa miaka ijayo inazungumza tuweke viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi, pale ambapo tutaona mengi yakutosheleza,”amesema Dkt Samia.
Kuhusu barabara, Dkt Samia amewaambia wananchi wa Bunda kuwa barabara ya Nyamuswa hadi Bulamba kilomita 54, akiahidi kuongeza nguvu ili kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa watu na bidhaa.

“Tutakwenda kuongeza bajeti kwa Tanroads na Tarura ili kujenga barabara nyingi kwa kiwango cha kupitika kwa mwaka mzima,wakati wote iwe jua au mvua,” ameeleza.

09/10/2025

Mgombea wa urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amewaahidi wananchi wa Simiyu kuendeleza kasi ya uboreshaji wa sekta ya afya, ikiwemo kuongeza nguvu katika huduma za mama na mtoto.
Dkt Samia ameeleza hayo, leo Oktoba 9,2025 Alhamisi wakati aliposimama kuzungumza na wananchi wa Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu katika mwendelezo wa kampeni za kusaka kura.
“Tutaendelea na kasi ileile ya huduma za afya, tutajenga vituo vya afya na zahanati zaidi na tunakwenda kuboresha hospitali ya wilaya kwa kujenga jengo kubwa la mama na mtoto, ili huduma ziendelee kwa kiasi kikubwa,”
“Mimi ni mama, najua masuala ya kujifungua kazi yake, huduma zinazotakiwa, hivyo naweka nguvu huko kwa mama na mtoto,” amesema Dkt Samia.
Mbali na hilo, Dkt Samia ambaye ni Mwenyekiti wa CCM amewaambia wananchi Lamadi, kuwa atakwenda kuongeza shule za sekondari na msingi, sambamba na vyuo vya ufundi wa Veta ili vijana kupata mafunzo ya ufundi yatakayowaweza kujiajiri na kuajiriwa.
“Kwenye maji kazi kubwa imefanyika, tunatambua baadhi ya maeneo kuna miundombinu imechakaa, inahitaji kufanyiwa kazi, nimeongozana na Waziri wa Maji (Jumaa Aweso) amesikia tunakwenda kuifanyia kazi,”
“Tunakwenda kumaliza vitongoji vilivyobaki katika sekta ya umeme, Ilani iliyopita iliagiza kupeleka umeme kwenye vijiji tu sasa, tumejiongeza hadi vitongoji. Mkituchagua tena tunakwenda kumaliza vitongoji,” amesema Dkt Samia.
*Ujenzi wa barabara hautasimama*
Katika mkutano huo, Dkt Samia amewaahidi Watanzania kuwa ujenzi wa Barabara unaondelea katika maeneo mbalimbali hautasimama, akisema miundombinu hiyo itajengwa k**a ambavyo imeanishwa katika Ilani.
*Ahadi ya soko*
Katika mazungumzo yake, Dkt Samia alikumbushia ahadi yake ya ujenzi wa soko, alipofanya ziara wilayani humo, miezi iliyopita akisema akiahidi lazima atekeleze.
“Nilitenga fedha za kujenga soko la hapa Lamadi, lakini uongozi wa halmashauri unabishana lijengwe Lamadi au Nyashimo, ndio maana soko halikujengwa. Lakini ahadi yangu bado iko palepale, madiwani wakielewana,” ameeleza Dkt Samia.
Hata hivyo, Dkt Samia amesisitiza kuwa ahadi yake, soko lijengwe Lamadi na stendi ya mabasi ijengwe eneo la Nyashimo,kupitia mradi wa uboreshaji wa miji utakaofanya shughuli hizo.
*Tujitokeza Oktoba 29*
Dkt Samia amewaomba wananchi wa Simiyu waliojindikisha katika Daftari wa Wapigakura kujitokeza kushiriki mchakato huo.
“Kama ni baba au mama wa familia, hakikisha kila aliyejiandikisha katika nyumba yako anajitokeza kupiga kura,”
“Kama ni balozi hakikisha watu wa eneo lako, wote walioandikishwa wametoka kupiga kura. Tukakigie kura CCM, bado tuna mengi tunayahitaji,” amesema Dkt Samia.

Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) tarehe 9 Oktoba, 2025 wametoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia...
09/10/2025

Watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) tarehe 9 Oktoba, 2025 wametoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa Walimu na Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Nyangaka, iliyopo Halmashauri ya Bariadi Mji pamoja na kuhamasisha kuhusu matumizi sahihi ya nishati ya umeme shule hapo.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo; Bi. Jaina Msuya, Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi, amesema nishati safi ya kupikia ni dhana inayotumika kuelezea na kubainisha nishati na teknolojia sahihi ambapo kwa pamoja hutoa moshi wenye kiwango kidogo cha sumu pale zinapotumika kwa usahihi.

“Nishati safi ya kupikia hupimwa kwa ufanisi katika muda mfupi, urahisi wa kutumia, upatikanaji, usalama, unafuu (Bei ya matumizi kila siku) na isiyowaweka Watumiaji katika mazingira hatarishi na yenye sumu” ameeleza Bi. Jaina.

Ametolea mfano matumizi ya majiko ya umeme, gesi pamoja na majiko banifu yanayotumia mkaa na kuni mbadala pamoja kuni na mkaa kidogo na kuongeza kuwa teknolojia hizo zinapatikana ingawa zinahitaji kiwango kikubwa cha fedha ya kununua.

“Licha ya gharama ya kununulia teknolojia za nishati safi kuwa juu mfano jiko la umeme la ‘induction’ lakini ukiwa na jiko hili, unatumia chini ya uniti moja ya umeme ambayo kwa bei ya TANESCO (Mjini inauzwa shilingi 356.24) na (Kijijini inauzwa shilingi 122); unakuwa umepika na kuivisha chakula, wakati huu kopo la mkaa ni zaidi ya shilingi 1,000 na utahitaji kununua zaidi ya kopo moja kwa ajili ya kupika chakula cha siku moja kwa familia ya watu watatu,”amesema Bi. Jaina.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shula ya Msingi Nyangaka Bi. Theresia Chuwa ameishukuru REA kwa kuendesha mafunzo hayo ya vitendo kwa Wanafunzi wa shule hiyo na kuongeza kuwa yametoa fursa ya Wanafunzi kujifunza na watayakumbuka kwa kuwa yametolewa kwa vitengo.

“Tunashukuru kwa kuwa mchakato wa kujifunza unachukua muda na ni Imani yetu, kuwa Wanafunzi wamepata kitu na wataendelea kujifunza na kuwa Mabalozi wa kesho wa nishati safi ya kupikia kwenye jamii na familia zao” amesema Mwalimu Theresia.

Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, leo Alhamisi Oktoba 9, 2025, imesikiliza maombi ya dharura nam...
09/10/2025

Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, leo Alhamisi Oktoba 9, 2025, imesikiliza maombi ya dharura namba 24511 ya mwaka 2025 yaliyofunguliwa na Humphrey Polepole kupitia kwa wakili wake Peter Kibatala dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na wenzake wanne.

Kesi hiyo, inayosikilizwa chini ya Jaji Mfawidhi Salma Maghimbi, inahusiana na kutoweka kwa Polepole katika mazingira yanayoelezwa kuwa tata, jambo lililozua mjadala mkubwa mitandaoni, ndugu zake wakidai kuwa ametekwa.

Katika hoja zake, Wakili Peter Kibatala aliomba Mahak**a kutoa amri ya haraka ili wajibu maombi wamlete Polepole mahak**ani mara moja, wakati wakisubiri kusikilizwa kwa hoja za pande zote.

Hata hivyo, Wakili wa Serikali Mwandamizi Faraja Nguka alipinga ombi hilo, akieleza kuwa maombi hayo hayatekelezeki kwa kuwa kiapo cha Kibatala hakijaonesha wazi ni nani anayemshikilia Polepole, na kwamba kiapo hicho kimekiri mleta maombi kuchukuliwa na watu wasiojulikana.

Nguka aliongeza kuwa, katika maelezo ya Kibatala, kuna tuhuma kwamba Polepole huenda anashikiliwa na mjibu maombi namba tano, ambaye ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ZPC).

Akijibu hoja hizo, Wakili Kibatala alifafanua kuwa amewataja wajibu maombi wote kwa kuwa wanawakilisha Jamhuri, hivyo wote wanapaswa kumleta Polepole mahak**ani. Aliongeza kuwa mjibu maombi wa tano amesisitizwa zaidi kutokana na taarifa za awali alizozipokea kutoka kwa ndugu wa Polepole, Godfrey na Augustino Polepole, ambazo zimeenea mitandaoni na katika vyombo vya habari.

Kesi hiyo inatarajiwa kuendelea baada ya Mahak**a kupitia hoja za pande zote mbili kabla ya kutoa maamuzi kuhusu hatima ya maombi hayo.

09/10/2025

Mgombea wa Nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kutotekelezwa kwa ahadi yake ya Ujenzi wa soko Lamadi Wilayani Busega Mkoani Simiyu kumetokana na mivutano ya Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo, waliokuwa wakivutana kutaka kubadilisha eneo la ujenzi wa soko hilo k**a ilivyokuwa ahadi yake wakati alipofanya ziara eneo hilo.

Dkt. Samia ameyasema hayo leo Alhamisi Oktoba 09, 2025 akiwa kwenye Mkutano wake wa Kampeni kwenye Viwanja vya Kituo cha Mabasi Lamadi na kuagiza kuwa ni muhimu soko hilo likajengwa sehemu aliyoahidi na ikiwa Madiwani wanataka soko hilo lijengwe Nyashimo, basi yatumwe maombi mengine ya kutaka soko huko.

"Niliahidi na k**a mnavyojua Samia Suluhu akiahidi anatekeleza, nilitenga fedha za kujenga soko hapa Lamadi lakini ni Uongozi wa Halmashauri (Madiwani) wanabishana Lamadi au Nyashimo. Soko lile halikujengwa lakini ahadi yangu ipo palepale, Madiwani watakapoelewana litajengwa na ahadi yangu wakati ule ilikuwa ni soko lijengwe Lamadi k**a kuna mahitaji ya soko Nyashimo hilo ni ombi lingine." Amekaririwa akisema Dkt. Samia.

Kulingana na Dkt. Samia soko hilo pamoja na ujenzi wa Kituo cha mabasi Nyashimo vitatekelezwa chini ya Mradi wa uendelezaji Miji Tanzania maarufu k**a TACTIC, Akisema mara baada ya Madiwani kukubaliana, mradi huo utaanza kutekelezwa kwani fedha tayari zimetengwa.

Dkt. Samia pia ameeleza mafanikio makubwa ya utekelezaji wa Ilani ya mwaka 2020/25 ya Chama chake, akiomba kura kwa wananchi wa eneo hilo na kusema Chama Cha Mapinduzi ni muhimu kikachaguliwa kwasababu kinawafahamu vyema wananchi wa Lamadi, kikiwa na uzoefu na masuala ya Uongozi wa serikali tofauti na Vyama vingine ambavyo vitataka muda mkubwa wa kujifunza na kujua fedha zinapopatikana ili kutekeleza miradi ya maendeleo.

Address

Sinza Makaburini
Dar Es Salaam
1110111101(2)

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gilly Bonny Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share