Gilly Bonny Tv

Gilly Bonny Tv Independent Media.
(4)

07/08/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, amefanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya miradi ya upanuzi wa vituo vya kupokea, kupoza na kusambaza umeme vya Dege, Gongolamboto na Ubungo vilivyopo jijini Dar es Salaam yenye lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme kwa wakazi wa Dar es Salaam, Pwani na mikoa ya jirani kutokana na ongezeko la mahitaji ya umeme.

Katika kituo cha Dege, upanuzi unahusisha usimikaji wa transfoma mpya yenye uwezo wa 120MVA, kutoka 60MVA ya awali. Pia, mradi unajumuisha ujenzi wa njia za kusambaza umeme za kilovoti 33. Utekelezaji wake umefikia asilimia 56 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Aprili 2026.

Kituo cha Gongolamboto pia kinahusisha usimikaji wa transfoma mpya yenye uwezo wa 125MVA kutoka 50MVA ya awali ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 80 , wakati kituo cha Ubungo kinapanuliwa kwa usimikaji wa transfoma yenye uwezo mkubwa wa 300MVA.

Akizungumza leo Agosti 07 , 2025 baada ya ukaguzi huo Bw. Twange amebainisha kuwa miradi hiyo mitatu ni ya kimkakati kwa sababu inalenga kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika na wa kutosha kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam na maeneo ya jirani.

“Hii ni sehemu ya kuhakikisha kuwa miundombinu ya TANESCO inaimarishwa ili kukidhi mahitaji ya sasa na ya baadae, hasa katika mikoa yenye shughuli nyingi za kiuchumi k**a Dar es Salaam,” amesema Bw. Twange.

Ameongeza kuwa Dar es Salaam ni mkoa mkubwa unaochangia kwa kiasi kikubwa katika ukusanyaji wa mapato ya serikali na TANESCO, hivyo kuwa na huduma ya umeme wa uhakika ni msingi wa kuendesha shughuli za kiuchumi, kijamii na utoaji huduma muhimu k**a elimu na afya.

Bw. Twange amewapongeza Wahandisi na Wasimamizi wa miradi hiyo kwa uwajibikaji na weledi, licha ya kufanya kazi katika mazingira yenye changamoto. Ameeleza kufurahishwa kwake na kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo, akisema inazingatia muda uliowekwa katika mikataba.

“Ninayo furaha kusema kuwa kazi zinaendelea vizuri. Nawahakikishia wakazi wa Dar es Salaam hususani wa Kigamboni kuwa, changamoto za umeme wanazokumbana nazo hivi sasa zitaisha mara tu miradi hii itakapokamilika,” amesisitiza.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kituo cha redio cha RAC1, hali ndani ya klabu ya FC Barcelona inazidi kuwa tete, baada ya k...
07/08/2025

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kituo cha redio cha RAC1, hali ndani ya klabu ya FC Barcelona inazidi kuwa tete, baada ya kudaiwa kuwa Rais wa klabu hiyo, Joan Laporta, "hataki tena kusikia kuhusu Marc-André ter Stegen."

Ripoti zinaeleza kuwa uhusiano kati ya Laporta na kipa huyo wa muda mrefu wa Barcelona "umedorora vibaya na kuvunjika kabisa" – ikimaanisha kwamba kuna mgawanyiko mkubwa ndani ya uongozi wa klabu hiyo kuhusu mustakabali wa mchezaji huyo.

Ter Stegen, ambaye amekuwa nguzo muhimu ya safu ya ulinzi ya Barcelona kwa miaka kadhaa, sasa anaonekana kuwa katika hatihati ya mustakabali wake Camp Nou – huku ikielezwa kuwa uongozi hautaki tena kujadili au kujihusisha naye kwa namna yoyote.

Hii ni habari inayokuja wakati Barcelona inaendelea na mipango ya mabadiliko makubwa ndani ya kikosi chake na uongozi wake, kufuatia msimu mgumu uliopita.

Kampuni ya vifaa vya kielektroniki ya Haier imetangaza rasmi kusaini mkataba wa udhamini wa miaka mitatu na klabu ya Yan...
07/08/2025

Kampuni ya vifaa vya kielektroniki ya Haier imetangaza rasmi kusaini mkataba wa udhamini wa miaka mitatu na klabu ya Yanga SC, wenye thamani ya Shilingi Bilioni 3.3.

Kupitia mkataba huo, kampuni ya Haier itapata haki ya kuweka logo yake upande wa kushoto kwenye mkono wa jezi ya wachezaji wa Yanga, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuimarisha ushirikiano wa kibiashara kati ya pande hizo mbili.

Mkataba huo mpya utaanza rasmi kufanya kazi kuanzia msimu wa 2025-2026, na unatarajiwa kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya klabu hiyo kongwe nchini Tanzania.

Haier imekuwa miongoni mwa makampuni makubwa ya kielektroniki duniani, na udhamini huu unaonyesha nia yake ya kuendelea kuwekeza katika michezo barani Afrika, hasa Tanzania.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA); Mhandisi, Hassan Saidy amesema inawezekana hadi mwaka 2034 Watanzan...
07/08/2025

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA); Mhandisi, Hassan Saidy amesema inawezekana hadi mwaka 2034 Watanzania zaidi ya asilimia 80 wakawa wanatumia nishati safi ya kupikia kwa kuwa Serikali imeweka mipango madhubuti sambamba na uwekezaji mkubwa uliofanywa.

Mhandisi, Saidy ameongeza kuwa pamoja na jitihada za makusudi za Serikali ili kuhakikisha kila Mtanzania anatumia nishati safi ya kupikia ametoa angalizo la kila Mtanzania kuchagua aina ya nishati safi ambayo anaimudu kulingana na uwezo wake kiuchumi kwa kuwa fursa ya kuchagua kwa ajili ya matumizi ipo.

Mhandisi, Hassan Saidy ametoa wito huo, hivi karibuni wakati alipofanya ziara ya kutembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na mabanda mengine ya Taasisi za Wizara ya Nishati katika viwanja vya maonesho ya Kimataifa vya Nane Nane 2025, Nzuguni Jijini Dodoma.

Mhandisi, Saidy amesema Serikali kupitia REA na Wadau mbalimbali imeanza kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi kivitendo katika kipindi cha miaka minne hadi sasa na kuongeza kuwa juhudi hizo pamoja uwekezaji wa rasilimali fedha; muda na teknolojia umeongeza mwamko kwa Wananchi kuendelea kutumia teknojia za nishati safi ambazo zinapatikana licha ya kwamba zinategemea na hali ya uchumi wa Watu.

Ametoa mfano kuwa matumizi ya gesi n umeme yanaonekana sana mijini kutokana na upatikanaji wake pamoja na uwezo wa Watu wa mijini kiuchumi ukilinganisha na vijijini ingawa Watu wa vijijini wanayo fursa ya kununua majiko banifu ambayo yameboreshwa ambayo kwa kiasi kikubwa yanatumia nishati ya mkaa na kuni kidogo lakini bado ni salama kwa afya za Watu na mazingira.

“Nishati safi, mfano umeme, gesi ya majumbani na gesi asilia, mkaa mbadala, kuni mbadala na gesi vunde. Matumizi ya aina hizi za nishati yanategemea na hali za uchumi wa Watu; kwa sababu hiyo Watu watumie aina hizi za nishati kulingana na uwezo wao kiuchumi.

“Nitoe mfano, REA kwenye utekelezaji wa Miradi ya Nishati Safi ya Kupikia, imeliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kuanza kutumia nishati safi ya kupikia kwenye kambi 22 Tanzania Bara. Mradi huo umegharimu shilingi bilioni 5; REA pia imewesha maeneo 211 ya Jeshi la Magereza kutumia nishati safi ya kupikia kwa gha

07/08/2025

Wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) pamoja na wadau mbalimbali wa hifadhi ya jamii wametakiwa kutumia mifumo ya kidijitali inayotolewa na Mfuko huo ili kupata huduma kwa haraka, ufanisi na bila usumbufu wowote popote walipo.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF, Bi. Lulu Mengele, wakati wa Maonesho ya Wakulima ya Nanenane yanayofanyika kitaifa jijini Dodoma, ambapo NSSF inashiriki kikamilifu katika Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kinga ya Jamii pamoja na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika upatikanaji wa huduma.

Kwa upande wake, Meneja wa Wananchi Waliojiajiri wa NSSF, Bi. Rehema Chuma, amesema Mfuko umeweka mazingira rafiki kwa wananchi waliojiajiri kuweza kujiunga na kuchangia NSSF kwa njia rahisi na ya kidijitali, jambo ambalo limeongeza mwamko wa kujihifadhi kwa wengi katika kundi hilo muhimu. Huku naye Meneja wa NSSF Mkoa wa Dodoma, Yahya Mudhihir, ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa waajiri wote kuhakikisha wanawasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati ili kuimarisha ustawi wa wanachama wao na kuepuka adhabu zitokanazo na ucheleweshaji wa michango.

Maonesho ni jukwaa muhimu katika mkakati wa elimu kwa umma ambao unawezesha kuifikia jamii moja kwa moja na kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa kinga ya jamii katika maisha yao ya sasa na ya baadaye.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba  amefungua mafunzo ya wataalam kutoka taasisi mbalimbali nchini ...
07/08/2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amefungua mafunzo ya wataalam kutoka taasisi mbalimbali nchini yanayohusu usanifu, utengenezaji na ufungaji wa mifumo ya Nishati ya Jua na matumizi yake.

Matumizi hayo ni kuchemsha, kupika, kupoza maji pamoja na kukausha mazao kwa kutumia nishati ya Jua.

Akifungua mafunzo hayo jijini Dar es Salaam, Mhandisi Mramba amesema mafunzo kuhusu teknolojia ya nishati ya Jua yanaenda sambamba na vipaumbele vya taifa katika Dira 2050 ambapo Dira hiyo inagusia mikakati ya kuendeleza matumizi ya nishati jadidifu nchini.

"Nishati Jadidifu ikiendelezwa kikamilifu itakuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi, itapunguza utegemezi katika nishati isiyosafi ikiwemo kuni na kuongeza upatikanaji wa huduma za nishati kwa njia ya kisasa zaidi." Amesema Mhandisi Mramba

Mramba amewaasa washiriki wa mafunzo hayo kuwa makini na kuzingatia kile kinachofundishwa ili kiweze kuleta tija nchini.

Vilevile, Mhandisi Mramba ameeleza kuwa Tanzania inajivunia ushirikiano wake na mashirika mbalimbali ya Kimataifa katika kuendeleza Sekta ya Nishati ikiwa ni pamoja na kufanikisha mafunzo mbalimbali ya kuwajengea uwezo wataalam.

Mafunzo hayo ya Nishati ya Jua yanayojulikana k**a SOLTRAIN + yameandaliwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Kituo Mahiri cha Matumizi Bora ya Nishati na Nishati Jadidifu (SACREEE) ambacho kipo chini ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi zilizo Kusini mwa Afrika ( SADC).

Jumla ya washiriki 40 kutoka taasisi mbalimbali wanahudhuria mafunzo hayo ya siku mbili wakiongozwa na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga.

07/08/2025

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ameungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuunga mkono timu ya taifa ya soka, Taifa Stars, kwa kutoa mchango wa shilingi milioni 20. Mchango huo umetolewa kufuatia ushindi wa bao 1–0 dhidi ya Mauritania kwenye AFCON mchezo uliopigwa jijini Dar es Salaam.

RC Chalamila amesema mchango huo ni sehemu ya kutambua na kuhamasisha juhudi za vijana wa Taifa Stars, pamoja na kuunga mkono jitihada za Rais Samia katika kuendeleza michezo nchini. Ushindi huo umeongeza matumaini ya Tanzania kufuzu mashindano hayo, huku morali ya wachezaji ikiongezeka kutokana na hamasa hiyo ya kitaifa.

Umoja wa Mataifa imeshutumu waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda kwa mauaji ya raia zaidi ya mia tatu mashariki mwa J...
07/08/2025

Umoja wa Mataifa imeshutumu waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda kwa mauaji ya raia zaidi ya mia tatu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Ofisi yake ya haki za binadamu imesema waathiriwa ni pamoja na wanawake arobaini na nane na watoto kumi na tisa.

Pia ililaani shambulizi dhidi ya raia lililotekelezwa na makundi mengine yenye silaha katika eneo hilo.

Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa UN, Volker Turk, amesema ameshutuka kwamba licha ya mpango wa kusitisha mapigano hivi karibuni uliosainiwa huko Qatar, vurugu upande wa mashariki ya Congo zimeongezeka.

Kulingana na UN, ofisi yake imepokea taarifa za moja kwa moja kuhusu wapiganaji wa M23 kuwauwa raia mia tatu na kumi na tisa kwa kipindi cha wiki mbili mwezi uliopita.

Waathiriwa wengi walikuwa wakulima wanaojishulisha na upanzi wakati huu wa msimu wa upandaji.

There was some optimism after a recent Washington brokered peace deal between Rwanda and Congo.

Hata hivyo, afisa mwandamizi wa M23 ametupilia mbali ripoti hiyo akisema ni propaganda.

Kulikuwa na matumaini ya kupungua kwa ghasia katika eneo hilo baada ya mpango wa hivi karibuni wa amani ulioongozwa na Marekani kati ya Rwanda na Congo lakini UN inasema raia wanaendelea kukabiliwa na athari mbaya za mgogoro huo.

ACT Wazalendo imemuidhinisha rasmi bwana Luhaga Mpina kuwa mmoja wa wagombea wa Urais atakayechuana na Rais Samia Suluhu...
07/08/2025

ACT Wazalendo imemuidhinisha rasmi bwana Luhaga Mpina kuwa mmoja wa wagombea wa Urais atakayechuana na Rais Samia Suluhu Hassan wa CCM kwenye uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu.

Uamuzi huo umefikiwa na Halmashauri Kuu ya ACT wazalendo jijini Dar es Salaam, ambayo ilipendekeza majina mawili, Aaron Kalikawe na Luhaga Mpina.

Majina hayo yaliyopendekezwa yaliwasilishwa kwa Mkutano Mkuu Taifa kwa ajili ya kupigiwa kura, ambapo katika mkutano huo, Mpina alichaguliwa kwa kishindo kwa kupata kura 559 sawa na asilimia 92.3 ya kura zote 610 zilizopigwa.

Luhaga Mpina amemshinda Mgombea mwenzake Kalikawe aliyepata kura 46 sawa na asilimia 7.7 na sasa atapeperusha bendera ya ACT katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, mgombea mwenza akiwa Bi. Fatma Ferej.

Kwa upande wa Zanzibar, Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo Othman Masoud Othman amechaguliwa kuwa Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kupata kura 606 za ndiyo sawa na asilimia 99.5 ya kura zote halali 609.

06/08/2025

Luhaga mpina amewaambia wajumbe wa chama Cha Act Wazalendo k**a watampa ridhaa ya kugombea Urais basi atapamabana na utekaji na mauaji ya watu nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dk. Samia Suluhu Hassan amesema amepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha...
06/08/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dk. Samia Suluhu Hassan amesema amepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mheshimiwa Job Yustino Ndugai, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rais Samia ametoa pole kwa familia, wanachama wote wa Chama Cha Mapinduzi, watumishi wa Bunge na Wabunge wote aliotumikia nao akiwa Spika wa Bunge, wananchi wa Kongwa, ndugu jamaa na marafiki.

Amewataka watanzania kuungana kwa pamoja kumuombea kwa Mwenyezi Mungu na kuwaombea familia, ndugu, jamaa na marafiki uvumilivu, faraja na moyo wa ibada katika kipindi hiki kigumu.

06/08/2025

Rashida Omari, mwenyekiti wa chama Cha Act Wazalendo Jimbo la Handeni Vijiji amehoji juu ya usalama wa Wananchi wakati wa Kulinda kura kwenye uchaguzi mkuu huku vitendo Vya kikatili Zaidi ya Wananchi wa chama hicho vikishamili.

Address

Sinza Makaburini
Dar Es Salaam
1110111101(2)

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gilly Bonny Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share