Gilly Bonny Tv

Gilly Bonny Tv Independent Media.
(3)

Jeahi la Polisi Mkoa wa Arusha limekanusha vikali taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikituhumu uwepo wa ...
14/06/2026

Jeahi la Polisi Mkoa wa Arusha limekanusha vikali taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikituhumu uwepo wa askari polisi aliyepigwa mkoani humo, likitaja maudhui hayo kuwa ni ya uongo na yenye lengo la kuchochea taharuki katika jamii.

​Ufafanuzi huo umetolewa leo, kupitia taarifa rasmi kwa umma iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, kufuatia kusambaa kwa picha mjongeo (video) iliyochapishwa na mwanaharakati Maria Sarungi ikidai kuwa tukio hilo limetokea mkoani humo.

​Jeshi hilo limebainisha kuwa hakuna tukio lolote la namna hiyo lililotokea ndani ya Mkoa wa Arusha na uchunguzi wa awali unaonyesha wazi kuwa video hiyo ilichukuliwa maeneo mengine nje ya nchi, kisha kuwekewa maneno ya uongo ili kuaminisha umma vibaya.

​"Tunawaomba wananchi kupuuza taarifa hiyo, kwa kuwa mtu huyo amekuwa akiandaa na kusambaza maudhui ya uongo, uchonganishi na kutaka kuleta taharuki kwa jamii jambo ambalo ni kinyume na makuzi, mila, desturi na mifumo ya kisheria," amesema Kamanda wa Polisi mkoani humo kupitia taarifa hiyo.

​Mbali na kukanusha, jeshi hilo limetoa onyo kali kwa watu wote wenye tabia ya kuandaa, kusambaza taarifa za uongo, na kupandikiza chuki ili kuchonganisha jamii, likisisitiza kuwa vitendo hivyo ni kinyume cha sheria za nchi na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayebainika kukiuka taratibu hizo.

14/06/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linamshikilia Filbert Philimon (23), mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. John's, kwa tuhuma za kuwaua kwa kuwachoma moto wanawake wawili, Rebeka James na Felister Peter, ndani ya chumba walichokuwa wakiishi katika mtaa wa Kikuyu jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, mtuhumiwa anadaiwa kununua lita mbili za petroli ambazo alizitumia kutekeleza tukio hilo, huku chanzo kikitajwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Tukio hilo lilitokea usiku wa tarehe 7 Juni 2026, na baada ya tukio mtuhumiwa alidaiwa kutoroka kabla ya kuk**atwa baadaye katika Stendi ya Mabasi ya Magufuli jijini Dar es Salaam alipokuwa akijaribu kuondoka.

Jeshi la Polisi limesema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea huku hatua za kisheria zikichukuliwa dhidi ya mtuhumiwa.

14/06/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkataba wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Barabara ya Kitusha–Kinampanda–Kisana–Kisiriri umeshasainiwa, hatua inayofungua njia ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo unaotarajiwa kubadilisha shughuli za usafiri na uchumi katika maeneo ya Wilaya ya Iramba.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo, Jumapili Juni 14, 2026, wakati akizungumza, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Tarafa ya Kinampanda katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Kinampanda, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Amesema Serikali imekamilisha hatua muhimu ya upatikanaji wa fedha za mradi huo na kwamba changamoto iliyobaki sasa ni kukamilisha taratibu za kumpata mkandarasi atakayetekeleza ujenzi huo.

“Leo tunavyoongea, mkataba wa upatikanaji wa fedha umeshasainiwa. Kwa hiyo fedha si tatizo tena. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Halmashauri ambao walishuhudia kusainiwa kwa mkataba huo,” amesema Dkt. Mwigulu.

14/06/2026
14/06/2026

VIDEO 📹

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa timu yake ya wanasheria ipo tayari kikamilifu kusimamia ukwel...
14/06/2026

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa timu yake ya wanasheria ipo tayari kikamilifu kusimamia ukweli na haki katika shauri la kisheria linalohusu mali za chama hicho, linalotarajiwa kutajwa kesho Jumatatu katika Mahak**a Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

​Msimamo huo umetolewa leo Jumapili, Juni 14, 2026, kupitia taarifa rasmi kwa umma iliyosainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa chama hicho, Brenda Rupia, ikihusu mwenendo wa kesi hiyo ya mali za chama iliyofunguliwa dhidi yao na Saidi Issa Mohamed akishirikiana na mwenzake.

​Rupia amebainisha kuwa shauri hilo limepangwa kuja mahak**ani hapo kwa ajili ya kutajwa kuanzia saa 3:00 asubuhi, huku akisisitiza kuwa msimamo wa Chadema umekuwa imara na thabiti wakati wote katika kulinda rasilimali na mali zote ambazo ni jasho la wanachama na wananchi wanaokiunga mkono chama hicho.

​"Kazi ya kulinda chama na rasilimali zake ni jukumu letu sote. Tunatoa wito kwa viongozi, wanachama, na wapenzi wa Chadema kujitokeza kwa wingi mahak**ani kesho Jumatatu asubuhi ili kuonyesha mshik**ano na ufuatiliaji wa karibu wa shauri hili muhimu kwa mustakabali wa mali za chama chetu," amesema Rupia kwenye taarifa hiyo.

​Kesi hiyo inayovuta hisia za wanachama wengi inatarajiwa kuanza hatua za kutajwa huku viongozi wa chama hicho wakihamasisha utulivu na mshik**ano wa kisheria ili kuhakikisha rasilimali zote za chama kikuu cha upinzani nchini zinabaki salama chini ya uangalizi wa kisheria.

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkataba wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Barabara ya Kitusha–Kina...
14/06/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkataba wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Barabara ya Kitusha–Kinampanda–Kisana–Kisiriri umeshasainiwa, hatua inayofungua njia ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo unaotarajiwa kubadilisha shughuli za usafiri na uchumi katika maeneo ya Wilaya ya Iramba.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo, Jumapili Juni 14, 2026, wakati akizungumza, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Tarafa ya Kinampanda katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Kinampanda, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Amesema Serikali imekamilisha hatua muhimu ya upatikanaji wa fedha za mradi huo na kwamba changamoto iliyobaki sasa ni kukamilisha taratibu za kumpata mkandarasi atakayetekeleza ujenzi huo.

“Leo tunavyoongea, mkataba wa upatikanaji wa fedha umeshasainiwa. Kwa hiyo fedha si tatizo tena. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Halmashauri ambao walishuhudia kusainiwa kwa mkataba huo,” amesema Dkt. Mwigulu.

Amesema barabara hiyo itaanzia Kitusha, kupita Kinampanda, Galangala, Kisana na kuunganishwa na Kisiriri kabla ya kuelekea Sibiti, hatua itakayorahisisha mawasiliano na usafirishaji wa watu na bidhaa katika ukanda huo.

Waziri Mkuu amesema mradi huo utatekelezwa kwa kiwango cha kisasa na unatarajiwa kuwa miongoni mwa barabara bora zaidi mkoani Singida.

“Barabara hii huenda ikawa moja ya barabara bora kuliko zote hapa mkoani Singida. Itakuwa ni barabara ya kisasa kweli kweli,” amesema.

Akitoa ufafanuzi wa hatua za utekelezaji wa mradi huo, Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Singida, Mhandisi Claver Mwinuka amesema tayari mchakato wa kumpata mshauri elekezi unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.

Amesema baada ya kukamilika kwa michoro na nyaraka za zabuni, Serikali itaanza mchakato wa kumpata mkandarasi huku matarajio yakiwa ni mkandarasi huyo kupatikana ifikapo mwezi Septemba mwaka huu.

Mhandisi Mwinuka amesema barabara hiyo ina urefu wa kilometa 38.5 na itajengwa kwa upana wa mita 9.5, tofauti na barabara nyingi za TARURA ambazo hujengwa kwa upana wa mita 8.5.

Aidha, amesema barabara hiyo itakuwa na taa zaidi y

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, amedai kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu y...
14/06/2026

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, amedai kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Jonathan Lema, anavuta malipo ya shilingi milioni 15 kila mwezi kwa ajili ya kuratibu na kuhamasisha vurugu na maandamano nchini.

​Kihongosi ametoa madai hayo mazito leo, Jumapili, Juni 14, 2026, kupitia ukurasa wake rasmi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, akimtaja mwanasiasa huyo na kumfananisha na "mpiga ramli" anayetumia vijana wa Kitanzania k**a mtaji wa kisiasa wakati familia yake ikiishi maisha salama nje ya nchi.

​Mwenezi huyo amebainisha kuwa, Lema ameiweka familia yake nchini Canada ambako watoto wake wanasoma na kufurahia maisha, ilihali yeye anabaki nchini kuwashawishi watoto wa wenzake kuingia barabarani kufanya fujo na maandamano yanayoweza kuhatarisha amani.

​"Huyu jamaa bwana hana tofauti na mpiga ramli. Yaani yeye amepeleka familia yake Canada inafurahia maisha, watoto wanasoma Canada na kila mwezi yeye analipwa milioni 15 kwa kazi ya kuleta vurugu katika nchi. Bila aibu anahamasisha watoto wa wenzake wafanye maandamano ilihali watoto wake hataki washiriki fujo," amesema Kihongosi.

​Kihongosi ametoa changamoto kuwa, k**a mwanasiasa huyo ana dhamira njema na anachokipigania, anapaswa kuirejesha familia yake kutoka Canada ili iingie mstari wa mbele kwenye vurugu hizo, na k**a akikataa basi Watanzania wajue ni utapeli wa kisiasa na waendelee kufanya kazi halali za kujenga uchumi wao.

​Mwishoni mwa ujumbe wake, Kihongosi amewajibu wale wanaotaka Mwenezi wa CCM asizungumze, akisisitiza kuwa yeye ni mtumishi wa chama aliye kwenye majukumu yake ya kikatiba, akimalizia kwa kusema kuwa siasa ni sayansi inayotegemea mikakati na hoja na si vurugu.

FULL-TIME I   Simba SC 2-1 Pamba Jiji FC Mpanzu ⚽️Libasse Gueye ⚽️Tegis ⚽️
14/06/2026

FULL-TIME I

Simba SC 2-1 Pamba Jiji FC

Mpanzu ⚽️
Libasse Gueye ⚽️

Tegis ⚽️

Address

Sinza Makaburini
Dar Es Salaam
1110111101(2)

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gilly Bonny Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share