24/07/2025
Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amemuagiza mkandarasi anayejenga mradi wa maji kutoka chanzo cha mto Kiwira mkoani Mbeya kampuni ya China Railway Construction Engineering Group kuharakisha utekelezaji wa mradi huo.
Mradi wa Kiwira unatarajia kuzalisha lita milioni 117 kwa siku zitakazowezesha Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya kuzalisha lita milioni 190 kutoka lita milioni 74,240 za sasa.
Chanzo hicho kitatosheleza maji katika jiji la Mbeya na mji wa Mbalizi hadi mwaka 2045 ambapo miji hiyo inatarajiwa kuwa na wakazi zaidi ya milioni moja nukta tank.
Waziri Aweso amesema mradi huo unabeba matumaini makubwa kwa wananchi wa Mbeya kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye anatambua changamoto wanayopitia akina mama mkoani hapo.
Amesema anaridhishwa na kasi ya utekelezaji katika eneo la chanzo lakini bado upo umuhimu wa kuongeza kasi ili mradi huo ukamilike Desemba 2025 k**a ilivyoainishwa katika mkataba.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mbeya, Langael Akyoo amesema CCMi mkoani inaridhihwa na jitihada zinazofanywa na serikali kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi. Amesema wataendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Maji ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.
Waziri Aweso pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Wazjiri wako katika ziara ya kukagua miradi ya maji katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.