Gilly Bonny Tv

Gilly Bonny Tv Independent Media.
(3)

24/07/2025

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amemuagiza mkandarasi anayejenga mradi wa maji kutoka chanzo cha mto Kiwira mkoani Mbeya kampuni ya China Railway Construction Engineering Group kuharakisha utekelezaji wa mradi huo.

Mradi wa Kiwira unatarajia kuzalisha lita milioni 117 kwa siku zitakazowezesha Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya kuzalisha lita milioni 190 kutoka lita milioni 74,240 za sasa.

Chanzo hicho kitatosheleza maji katika jiji la Mbeya na mji wa Mbalizi hadi mwaka 2045 ambapo miji hiyo inatarajiwa kuwa na wakazi zaidi ya milioni moja nukta tank.

Waziri Aweso amesema mradi huo unabeba matumaini makubwa kwa wananchi wa Mbeya kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye anatambua changamoto wanayopitia akina mama mkoani hapo.

Amesema anaridhishwa na kasi ya utekelezaji katika eneo la chanzo lakini bado upo umuhimu wa kuongeza kasi ili mradi huo ukamilike Desemba 2025 k**a ilivyoainishwa katika mkataba.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mbeya, Langael Akyoo amesema CCMi mkoani inaridhihwa na jitihada zinazofanywa na serikali kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi. Amesema wataendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Maji ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

Waziri Aweso pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Wazjiri wako katika ziara ya kukagua miradi ya maji katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

24/07/2025

Mchungaji wa kanisa la kiinjili la kilutheri Samweli karao aongoza ibaada ya mazishi ya aliekuwa katibu wa CHADEMA wilaya ya Arumeru Albert .E.Mollel huku akiwaeleza Viongozi wa chadema kuwa Hali wanayopitia nchini inaonekana na wamazidi kuwaombea wapite salama katika kipindi hiki Cha kampeni.

Aidha mchungaji Mollel alisisitiza kuwepo Kwa Siasa nchini inayoruhusu Vyama vingi Kwa matendo na si Kwa nadharia tu.

Kumekuwa na kauli zinazojaribu kuaminisha watu kuwa maisha yao yako mikononi mwao pekee. Kauli k**a hizi zinaweza kuhama...
24/07/2025

Kumekuwa na kauli zinazojaribu kuaminisha watu kuwa maisha yao yako mikononi mwao pekee. Kauli k**a hizi zinaweza kuhamasisha mtu kujituma, lakini pia zinaweza kuficha ukweli wa msingi: maendeleo ya mtu binafsi hayawezekani katika mazingira magumu ambayo yanatokana na uzembe wa serikali.

Mtu anawezaje kufanikisha ndoto zake bila elimu bora, afya ya uhakika, barabara zinazopitika, umeme wa uhakika, usalama na ajira? Hayo yote yanategemea serikali.

Rwanda imejipanga upya baada ya janga kubwa la kihistoria kupitia mipango ya serikali. Leo hii, Kigali ni moja ya miji safi zaidi Afrika. China imewatoa watu zaidi ya milioni 800 kutoka umasikini kwa sababu ya sera madhubuti za serikali. Nchi k**a Sweden na Finland zimejenga mifumo imara ya kijamii ambapo serikali inahakikisha kila raia anapata huduma bora bila ubaguzi.

Kauli za "jibebe" haziwezi kuchukua nafasi ya wajibu wa serikali. Serikali bora huandaa mazingira yatakayomwezesha mtu binafsi kufanikiwa kwa haki, usawa na heshima.

Tanzania haiwezi kufanikiwa kwa juhudi binafsi pekee bila mwelekeo na wajibu wa wazi kutoka kwa serikali. Haki ya kupata maisha bora si zawadi – ni wajibu wa taifa kwa raia wake.

Tudai uwajibikaji. Tukatae propaganda.

24/07/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, amefanya ziara ya kikazi tarehe 23 Julai 2025 kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Tanzania - Zambia (TAZA) katika Mkoa wa Iringa na Njombe maneo ya ujenzi wa njia ya umeme na vituo vya kupoza umeme vya Tagamenda na Kisada.

Katika ziara hiyo, Bw. Twange alitoa maelekezo kwa wasimamizi wa mradi kuhakikisha ujenzi wa njia za kusafirisha umeme pamoja na vituo vya kupokea, kupoza na kusambaza umeme unakamilika kwa wakati k**a ilivyoainishwa kwenye mikataba, huku akisisitiza kuwa usimamizi thabiti ni muhimu ili kuleta tija na kuhakikisha wananchi wananufaika kwa wakati.

“Simamieni wakandarasi vizuri katika kutekeleza ujenzi wa miradi hii. Msisimamie kwa mazoea, bali kwa weledi na kasi ili tija ya miradi hii ionekane na wananchi wapate huduma kwa wakati,” alisisitiza Bw. Twange.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwapongeza wasimamizi kwa juhudi zinazofanyika hadi sasa licha ya changamoto zinazojitokeza katika usimamizi wa miradi mikubwa, aliwataka kuendelea kutumia kipindi hiki kisicho na mvua kufanya kazi kwa kasi ili mradi ukamilike kwa ufanisi k**a ilivyopangwa na Serikali.

Katika ziara hiyo, Bw. Twange pia alitembelea miradi ya upanuzi wa vituo vya kupokea na kusambaza umeme katika Kituo cha Cotex (Iringa) na Kituo cha Makambako (Njombe), ambavyo tayari vimekamilika kwa kiasi kikubwa na kuanza kutoa huduma kwa wateja.

Alieleza kuwa hali ya umeme katika mikoa hiyo sasa imeboreshwa kwa kiwango kikubwa, huku miundombinu ikiwa na uwezo mkubwa wa kuhudumia mahitaji ya sasa na ya baadaye.

“Nimefurahishwa na utekelezaji wa miradi hii ya vituo vya kupoza umeme katika mikoa ya Iringa na Njombe. Kwa sasa tuna uwezo mkubwa wa kuhudumia wateja wengi zaidi kuliko hapo awali,” alieleza Bw. Twange.

Akihitimisha ziara hiyo ya siku mbili, Bw. Twange alionesha kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi wa TAZA, ambapo hadi sasa ujenzi wa njia za kusafirisha umeme umefikia zaidi ya asilimia 60, na ujenzi wa vituo vya kupoza umeme upo kwenye asilimia 31. Alisisitiza dhamira ya TANESCO kuendelea kusimamia miradi kwa ufanisi ili kutimiza malengo ya kitaifa ya upatikanaji wa umeme wa uhakika.

Mchezaji wa klabu ya Manchester Uniteda anaekipiga Kwa mikopo katika klabu ya Fc Barcelona, Marcus Rashford, amezungumzi...
24/07/2025

Mchezaji wa klabu ya Manchester Uniteda anaekipiga Kwa mikopo katika klabu ya Fc Barcelona, Marcus Rashford, amezungumzia hali ya sasa ndani ya klabu hiyo na kuelezea uhusiano wake wa karibu na timu hiyo ya kihistoria ya England.

Akizungumza katika mahojiano, Rashford alisema:

“Hali ya Manchester United kwa sasa ni kwamba klabu inapitia kipindi cha MABADILIKO, na hiki kimekuwa kinaendelea kwa muda sasa.”

Rashford amejiunga na klabu ya Barcelona Kwa mkopo wa muda Mrefu huku mahusiano na klabu yake hiyo yakielezwa kutokuwa mazuri.

“Sina jambo lolote la kusema vibaya kuhusu Manchester United. Nafikiri klabu hii imekuwa sehemu muhimu, si tu katika taaluma yangu ya soka, bali pia katika maisha yangu kwa ujumla.”

Rashford, ambaye ni zao la akademia ya Manchester United na ameichezea timu hiyo tangu akiwa mtoto.

Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa maeneo ambayo yamepata fedha nyingi kupitia mradi wa kuimarisha ubora wa Elimu ya sekonda...
24/07/2025

Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa maeneo ambayo yamepata fedha nyingi kupitia mradi wa kuimarisha ubora wa Elimu ya sekondari nchini SEQUIP ambapo umepokea zaidi ya Bilioni 36.596

Fedha hizo ambazo zimetolewa na serikali zimetumika kujenga shule mpya 41 za Sekondari ambazo miongoni mwake ni pamoja na Shule 1 ya wasichana, Shule 1 ya kanda ya Wavulana, Shule za kata 36, Shule 1 ya Amali ya Mkoa, na Shule 2 za Amali za kata.

Hayo yamebainishwa na Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Mwl Vicent Kayombo ambapo amesema kuwa fedha hizo pia zimetumika kujenga Madarasa 77, Matundu ya Vyoo 119, Maabara 19, Mabweni 22, na Nyumba za Walimu 22.

Mwl Kayombo amesema kuwa mkoa wa Dodoma umejenga shule mpya ya wasichana Manchali kwa gharama ya Shilingi Bilioni 4.450 sambamba na ujenzi wa shule mpya ya Amali ya mkoa iliyojengwa katika kijiji cha Manchali wilayani Chamwino kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.6

Mwl Kayombo ameishukuru serikali inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi katika mkoa wa Dodoma kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ambazo zitapunguza umbali wa wanafunzi kwenda shuleni ikiwa ni pamoja na kuondokana na vishawishi njiani, na kuongeza muda wa wanafunzi kujisomea.

JIBU K**A SALUM
23/07/2025

JIBU K**A SALUM

23/07/2025

Makamu Mwenyekiti wa chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Heche amewaambia viongozi wawchadema na Wananchi waliohudhuria ibaada ya mazishi ya aliekuwa katibu wa CHADEMA wilaya ya Arumeru Albert .E.Mollel kuwa ukiwa kiongozi wa Umma unapaswa kukubali ukosoaji na si kuwakandamiza wakosoaji.

23/07/2025

Makamu Mwenyekiti wa chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Heche amewaambia viongozi wawchadema na Wananchi waliohudhuria ibaada ya mazishi ya aliekuwa katibu wa CHADEMA wilaya ya Arumeru Albert .E.Mollel kuwa ni Bora kutengeneza jina Bora maishani k**a alivyofanya katibu huyo mpaka siku ya kifo chake.

23/07/2025

Mchungaji wa kanisa la kiinjili la kilutheri Samweli karao aongoza ibaada ya mazishi ya aliekuwa katibu wa CHADEMA wilaya ya Arumeru Albert .E.Mollel huku akiwaonya viongozi wa kisiasa dhidi ya kutumia msiba huo kwa malengo ya kisiasa.

Akihubiri mbele ya umati ya watu huko ngangaramtoni jijini arusha,asisitiza kuwa msiba huo ni ibaada takatifu ya Mungu sio Mahalia pa kampeni au kauli za kisiasa.

23/07/2025

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, amemwagiza Mkandarasi kutoka Kampuni ya Larsen & Toubro Limited kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wa maji wa miji 28 unaoendelea Rujewa kwa kufanya kazi usiku na mchana pamoja na kuongeza idadi ya wafanyakazi katika eneo la mradi.

Waziri Aweso ametoa agizo hilo leo Julai 23, 2025, wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa kimkakati ambao unalenga kusambaza maji kutoka Mbarali - Rujewa - Wanging’ombe mpaka Makambako.

Amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tayari ametoa zaidi ya shilingi bilioni 130 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo, hivyo hakuna sababu yoyote ya mkandarasi kuchelewesha kazi.

"Mkandarasi hana kisingizio chochote. Fedha zipo, Serikali imeshatekeleza wajibu wake. Tunataka kuona kazi inafanyika kwa kasi usiku na mchana hadi mradi ukamilike kwa wakati," amesema Waziri Aweso.

Waziri Aweso amesisitiza umuhimu wa wakandarasi kuwashirikisha vijana wa eneo hilo kwa kuwapa ajira ili wawe sehemu ya mradi unaotekelezwa katika maeneo yao, hatua ambayo pia inalenga kuinua maisha yao kiuchumi.

Mradi huo wa maji wa miji 28 unaotarajiwa kukamilika mwezi Oktoba 2025, ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama katika maeneo mbalimbali nchini.

Viongozi wa Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA) wamesema hawataunga mkono mipango yoyote ya kupanua matumizi ya tekno...
23/07/2025

Viongozi wa Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA) wamesema hawataunga mkono mipango yoyote ya kupanua matumizi ya teknolojia ya VAR ili kujumuisha maamuzi yanayohusu mipira ya kona na utoaji wa kadi za njano za pili.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka The Times na The Sunday Times, UEFA imesisitiza kuwa kuongeza mamlaka ya VAR katika maeneo hayo kutavuruga zaidi mtiririko wa mchezo na kuongeza mijadala isiyoisha kuhusu uamuzi wa waamuzi.

Hatua hii imepokelewa kwa shangwe na mashabiki wengi wa soka waliokuwa wakihofia kuwa VAR inaweza kuwa chanzo cha kuharibu ladha ya mchezo. "Naamini nazungumza kwa niaba ya wengi tunaposema, asante sana kwa uamuzi huu!" aliandika shabiki mmoja kwenye mitandao ya kijamii huku akiongeza emoji za kushangilia.

Kwa sasa, VAR inaruhusiwa kutumika katika maamuzi makuu manne tu: mabao, penalti, kadi nyekundu za moja kwa moja, na makosa ya kumtambua mchezaji aliyehusika.

UEFA inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuweka teknolojia k**a chombo cha kusaidia waamuzi, si kuchukua nafasi yao kabisa.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gilly Bonny Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share