29/11/2025
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limeendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya kijamii ili kuimarisha usalama na kudhibiti uhalifu, ambapo limekutana na maafisa usafirishaji wa Kanda ya Igoma, Wilaya ya Nyamagana.
Akizungumza katika mkutano huo, leo Novemba 29 2025, eneo la Ndama Kata ya Igoma, K**anda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa, ameeleza kufurahishwa na ushiriki wa kundi hilo, huku akisisitiza umuhimu wa kuzingatia elimu ya usalama barabarani waliyopewa.
Amesema ongezeko la ajali za barabarani linatokana na uzembe wa baadhi ya waendesha vyombo vya moto hivyo akataka kila mmoja kuwajibika ipasavyo kukomesha ajali hizo.
Amesisitiza kuwa utii wa sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani ni wajibu wa kila mtumiaji wa barabara huku akiwaonya dhidi ya makosa hatarishi k**a vile kuendesha bila kofia ngumu, kupuuza taa za barabarani, kubeba abiria zaidi ya mmoja, kuendesha bila leseni au mafunzo rasmi ya udereva.
"Makosa haya yamekuwa chanzo cha vifo na ulemavu kwa watumiaji wa barabara,” amesema K**anda Mutafungwa.
Aidha, amewakumbusha wananchi wa Mkoa wa Mwanza kuepuka kujihusisha na vurugu k**a zilizotokea tarehe 29 Oktoba 2025, akisisitiza kuwa matatizo yoyote ya kisheria yashughulikiwe kwa kufuata taratibu badala ya kujichukulia sheria mkononi.
“Kupitia elimu na ushirikiano, tumeweza kuzuia uhalifu mkubwa uliokuwepo awali,” amesema.