Gilly Bonny Tv

Gilly Bonny Tv Independent Media.
(3)

Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesema wananchi wa Venezuela wameondokana na kile alichokitaja kuwa ni udikteta wa N...
03/01/2026

Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesema wananchi wa Venezuela wameondokana na kile alichokitaja kuwa ni udikteta wa Nicolás Maduro, akieleza kuwa hatua hiyo ni chanzo cha faraja kwa watu wa nchi hiyo.
Kupitia ujumbe aliouchapisha katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X, Macron alisema Maduro alidhuru heshima ya wananchi wake kwa kunyakua madaraka na kukanyaga haki na uhuru wa msingi wa binadamu.

Rais huyo wa Ufaransa amesisitiza kuwa mchakato wa mpito wa uongozi nchini Venezuela unapaswa kufanyika kwa amani, kwa misingi ya kidemokrasia na kwa kuheshimu matakwa ya wananchi.

Aidha, Macron ameeleza matumaini yake kuwa Rais Edmundo González Urrutia, aliyechaguliwa mwaka 2024, ataweza kusimamia haraka mchakato huo wa mpito kwa lengo la kurejesha utawala wa kidemokrasia nchini humo.

Macron amebainisha kuwa kwa sasa anaendelea kufanya mazungumzo na washirika wa Ufaransa katika ukanda wa Amerika ya Kusini kufuatilia maendeleo ya kisiasa nchini Venezuela.

Amesisitiza kuwa Serikali ya Ufaransa ipo macho na imejipanga kikamilifu, hasa katika kuhakikisha usalama wa raia wake waliopo nchini Venezuela, kutokana na hali ya sintofahamu inayoendelea.

FULL-TIME:  Muembe Makumbi  0-1 Simba SC Mohammed Bajaber ⚽️
03/01/2026

FULL-TIME:

Muembe Makumbi 0-1 Simba SC

Mohammed Bajaber ⚽️

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa nchi yake iko tayari kufanya mashambulizi mengine dhidi ya Venezuela iwapo ...
03/01/2026

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa nchi yake iko tayari kufanya mashambulizi mengine dhidi ya Venezuela iwapo itahitajika, akisisitiza kuwa Marekani itasimamia nchi hiyo hadi pale mpito salama wa uongozi utakapoweza kufanyika.

Kauli hiyo imetolewa muda mfupi baada ya operesheni kubwa ya kijeshi iliyofanyika usiku wa kuamkia leo katika mji mkuu wa Venezuela, Caracas.

Akizungumza na wanahabari, Trump alisema operesheni hiyo ilitekelezwa kwa kutumia nguvu “kubwa na ya kutisha” ya kijeshi kupitia anga, ardhi na baharini.

Aliielezea k**a moja ya mashambulizi yenye ufanisi na nguvu zaidi katika historia ya kijeshi ya Marekani, akiongeza kuwa hakuna mwanajeshi wa Marekani aliyepoteza maisha wala kifaa chochote cha kijeshi kuharibiwa.

Trump alisema lengo kuu la operesheni hiyo lilikuwa kumk**ata Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, pamoja na mkewe, lengo ambalo amesema limefanikiwa. Alimtaja Maduro k**a “dikteta haramu” na kumshutumu kwa kuhusika na uingizaji wa kiasi kikubwa cha dawa za kulevya nchini Marekani, pamoja na kuongoza mtandao wa Cartel de los Soles, madai ambayo Maduro amekuwa akiyakanusha.

Rais huyo wa Marekani alisema awali walikuwa wamejiandaa kufanya wimbi la pili la mashambulizi, wakiamini lingeweza kuhitajika. Hata hivyo, kutokana na mafanikio ya operesheni ya kwanza, alisema huenda hatua hiyo isihitajike kwa sasa, ingawa alisisitiza kuwa Marekani iko tayari kuchukua hatua kubwa zaidi endapo hali italazimisha.

Aliongeza kuwa Nicolás Maduro na mkewe wanasafirishwa kuelekea Marekani, huku uamuzi ukitarajiwa kufanyika kuhusu kushtakiwa kwao kati ya New York na Miami. Trump aliwahakikishia Wavenezuela walioko Marekani kuwa mateso yao yatafikia mwisho.

MAPUMZIKO:  Muembe Makumbi  0-1 Simba SC Mohammed Bajaber ⚽️
03/01/2026

MAPUMZIKO:

Muembe Makumbi 0-1 Simba SC

Mohammed Bajaber ⚽️

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na Balozi wa Jamhuri ya Muung...
03/01/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amekutana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Luteni Jenerali (Mst) Yacoub Mohamed, katika Ofisi Ndogo ya Waziri, jijini Dar es Salaam.

Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kujadili fursa mbalimbali za ajira zilizopo katika nchi za Falme za Kiarabu, kutathmini changamoto zinazojitokeza, pamoja na kuweka mikakati ya kuboresha upatikanaji na usimamizi wa fursa za ajira kwa Watanzania.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Sangu amesema Serikali itaendelea kushughulikia changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika ajira za nje ya nchi kwa kuboresha mifumo ya usimamizi wa mawakala wa ajira, kuhakikisha utekelezaji wa sheria na kulinda maslahi ya wananchi.

Mhe. Sangu amemshukuru Balozi Yacoub kwa kuwasilisha mapendekezo muhimu kwa Wizara, ambayo yataisaidia kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za ajira katika nchi za Falme za Kiarabu.

Kwa upande wake, Mhe. Balozi Yacoub amemshukuru Waziri kwa ushirikiano mzuri uliopo kati ya Wizara na Ubalozi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kikao hicho kilifanyika tarehe 3 Januari, 2026 jijini Dar es Salaam, na kiliwahusisha watumishi kutoka Wizara pamoja na Ubalozi wa Tanzania nchini Falme za Kiarabu.

MWISHO

03/01/2026

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipatia shilingi milioni 500 Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kwa kufanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora kwenye michuano ya Mataifa Afrika (AFCON) inayoendelea nchini Morocco

Taarifa hiyo imetolewa leo Januari 03, 2026 na Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alipozungumza kwa njia ya simu na wachezaji pamoja na benchi la Ufundi la timu hiyo kupitia Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Paul Makonda.

Waasi wanaohusishwa na kundi la Islamic State wameua angalau watu 15 katika vijiji vitatu mashariki mwa Jamhuri ya Kidem...
03/01/2026

Waasi wanaohusishwa na kundi la Islamic State wameua angalau watu 15 katika vijiji vitatu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, maafisa wa eneo hilo wamesema.

Mashambulizi hayo yalitokea usiku wa Alhamisi katika wilaya ya Lubero, mkoani Kivu Kaskazini, yakilenga zaidi raia.

Kundi la Allied Democratic Forces (ADF), lililoanza k**a waasi nchini Uganda lakini baadaye kujikita katika misitu ya mashariki mwa Congo tangu mwishoni mwa miaka ya 1990, linatambuliwa na Islamic State k**a tawi lake.

Kwa mujibu wa Macaire Sivikunula, mkuu wa eneo la Bapere ambako vijiji vilivyoshambuliwa vipo, raia tisa waliuawa katika kijiji cha Kilonge, raia wawili katika kijiji cha Katanga, huku raia wawili na wanajeshi wawili wakiuawa katika kijiji cha Maendeleo.

Alisema waasi hao waliwaua waathiriwa wengi kwa kutumia silaha za jadi k**a mapanga, ingawa pia kulikuwa na mapigano ya risasi kati ya waasi na wanajeshi katika kijiji cha Maendeleo.

Afisa wa jeshi anayesimamia Lubero, Alain Kiwewa, alisema baadaye Ijumaa kuwa idadi ya waliothibitishwa kufariki imefikia 16.

Msemaji wa jeshi la Congo, Luteni Marc Elongo, alisema wanajeshi wa serikali wanaendelea kuwafuatilia waasi, bila kutoa maelezo zaidi.

Kwa upande wake, Kakule Kagheni Samuel, kiongozi wa mashirika ya kiraia katika eneo la Bapere, alisema waasi hao pia walichoma nyumba kadhaa katika maeneo hayo.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kulinda amani nchini Congo, MONUSCO, lilisema Novemba kuwa waasi wa ADF waliua raia 89 ndani ya wiki moja katika mashambulizi mfululizo.

Mwezi Septemba, ADF ilidai kuhusika na shambulizi lililoua zaidi ya watu 60 wakati wa mazishi mashariki mwa Congo.

Maafisa wa eneo hilo wamesema mazishi ya waathiriwa wa mashambulizi ya karibuni bado hayajaanza kwa sababu wanangoja wanajeshi kulinda usalama wa eneo, wakihofia waasi hao wanaweza kuwavamia raia wakati wa shughuli za mazishi na kuua tena.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Marekani imefanya “mashambulizi makubwa” dhidi ya Venezuela na kwamba imemk**ata R...
03/01/2026

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Marekani imefanya “mashambulizi makubwa” dhidi ya Venezuela na kwamba imemk**ata Rais wa nchi hiyo, Nicolás Maduro, pamoja na mke wake.

Katika taarifa aliyochapisha kwenye mtandao wa Truth Social, Trump alisema: “Marekani imefanikiwa kutekeleza mashambulizi makubwa dhidi ya Venezuela na kiongozi wake, Rais Nicolás Maduro, ambaye yeye pamoja na mke wake wamek**atwa na kusafirishwa nje ya nchi.”

Trump aliongeza kuwa operesheni hiyo ilifanyika kwa kushirikiana na vyombo vya usalama vya Marekani, akisema maelezo zaidi yatatolewa baadaye. Pia ametangaza kutakuwa na mkutano na waandishi wa habari lbaadaye katika makazi yake ya Mar-a-Lago.

Hadi sasa, serikali ya Venezuela haijatoa tamko rasmi kuthibitisha au kukanusha madai hayo ya kuk**atwa kwa maduro.

Maafisa wameiambia CBS News, mshirika wa BBC nchini Marekani, kwamba Maduro, amek**atwa na kikosi cha Delta Force cha jeshi la Marekani. Delta Force ni kikosi cha juu kabisa cha jeshi la Marekani kinachojihusisha na operesheni za kupambana na ugaidi.

Makamu wa Rais wa Venezuela, Delcy Rodríguez, amesema serikali yake haijui mahali alipo Rais Nicolás Maduro wala mkewe, ...
03/01/2026

Makamu wa Rais wa Venezuela, Delcy Rodríguez, amesema serikali yake haijui mahali alipo Rais Nicolás Maduro wala mkewe, Cilia Flores, kufuatia madai ya Marekani kwamba wamek**atwa baada ya mashambulizi makubwa ya kijeshi.

Akizungumza kupitia televisheni ya taifa, Rodríguez alidai kuwa Marekani inapaswa kutoa “uthibitisho wa uhai” wa Rais Maduro na mke wa rais, akisema serikali ya Venezuela ina wasiwasi mkubwa kuhusu hatima yao.

“Tunaitaka serikali ya Marekani kutoa uthibitisho wa uhai wa Rais Maduro na Mama wa Taifa. Rais alikuwa tayari ametuonya kuwa hali k**a hii inaweza kutokea,” alinukuliwa akisema, kwa mujibu wa Shirika la Habari la Venezuela.

Rodríguez aliongeza kuwa raia wameanza kufahamu kwamba rais alikuwa ametoa maelekezo ya wazi kwa vyombo vya ulinzi kuanza kutekeleza mipango yote ya kulinda taifa kwa mshik**ano kamili.

Wakati huo huo, Waziri wa Ulinzi wa Venezuela, Vladimir Padrino López, alitangaza awali kwamba vikosi vya kijeshi vya nchi hiyo vitasmabazwa katika maeneo yote ya nchi.

Katika hotuba ya video kwa taifa, Padrino López alitoa wito wa mshik**ano wa kitaifa mbele ya kile alichokiita “uvamizi mbaya zaidi kuwahi kufanywa dhidi ya Venezuela”, akisema jeshi linafuata maelekezo ya Rais Maduro ya kuhamasisha vikosi vyote vya ulinzi.

“Wametushambulia, lakini hawatatutawala,” alisema waziri huyo wa ulinzi, huku akisisitiza kuwa Venezuela itapinga uwepo wowote wa majeshi ya kigeni katika ardhi yake.

Taarifa hizi zinafuatia mashambulizi ya Marekani yaliyolenga maeneo ya kijeshi mjini Caracas na sehemu nyingine za nchi, huku hali ya sintofahamu ikiendelea kuhusu hatima ya uongozi wa Venezuela.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Jeshi la Marekani limefanikiwa kufanya mashambulizi yaliyowezesha kumk**ata Rais w...
03/01/2026

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Jeshi la Marekani limefanikiwa kufanya mashambulizi yaliyowezesha kumk**ata Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ambaye alikuwa mbioni kukimbia Venezuela kwenda nje ya nchi hiyo akiwa na Mkewe.

Trump amesema taarifa zaidi kuhusu kuk**atwa kwa Maduro zitatolewa baadaye.

Mashambukizi hayo yanafanyika wakati ambapo mvutano kati ya Marekani na Venezuela uko katika kiwango cha juu, huku Marekani ikiendelea na mashambulio dhidi ya boti mwendokasi katika bahari ya Carribean, ambazo inadai zinabeba dawa za kulevya.

Trump amesema Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, hakuingia madarakani kwa njia halali na anahusika moja kwa moja na biashara ya dawa za kulevya nchini Venezuela na kuingiza dawa hizo Marekani na maeneo mengine Duniani.

Hata hivyo Serikali ya Venezuela inasema hatua za hivi karibuni za Marekani ikiwa ni pamoja na kuk**ata meli za mafuta ni jaribio la kumfanya Rais Maduro aondolewe madarakani na kudhibiti rasilimali za mafuta za nchi hiyo.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linachunguza tukio la mauaji ya Evans Andrea Mohamed, mwenye umri wa miaka 51, dereva wa ...
03/01/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linachunguza tukio la mauaji ya Evans Andrea Mohamed, mwenye umri wa miaka 51, dereva wa gari na mkazi wa Mtaa wa Mnyampala, Kata ya Nyamanoro, Wilaya ya Ilemela.

Tukio hilo lilitokea tarehe 01 Januari 2026, majira ya saa 1:00 asubuhi, katika Mtaa wa Kileleni, Kata ya Kitangiri, Wilaya ya Ilemela. Marehemu aliuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali usoni na kichwani na mtu au watu ambao bado hawajafahamika.

Mwili wa marehemu ulikutwa katika mtaa huo wa Kileleni na kuchukuliwa na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure, kwa ajili ya uchunguzi wa kitabibu. Baada ya uchunguzi kukamilika tarehe 02 Januari 2026, mwili wa marehemu ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kina ili kuwabaini wahusika, kubaini mazingira ya tukio hili la mauaji, na kuchukua hatua stahiki za kisheria dhidi ya wahusika watakaobainika.

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wote wenye taarifa zitakazosaidia kufanikisha uchunguzi huu kuwasilisha taarifa hizo katika kituo chochote cha Polisi kilicho karibu ili ziweze kufanyiwa kazi kwa haraka na wahalifu wak**atwe na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

03/01/2026

Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema Bwawa la Kidunda Linakwenda kumaliza changamoto ya maji katika mikoa mitatu ambapo wakati wa Kiangazi mikoa hiyo hupata Changamoto ya Maji.

Address

Sinza Makaburini
Dar Es Salaam
1110111101(2)

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gilly Bonny Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share