Gilly Bonny Tv

Gilly Bonny Tv Independent Media.
(4)

29/11/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limeendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya kijamii ili kuimarisha usalama na kudhibiti uhalifu, ambapo limekutana na maafisa usafirishaji wa Kanda ya Igoma, Wilaya ya Nyamagana.

Akizungumza katika mkutano huo, leo Novemba 29 2025, eneo la Ndama Kata ya Igoma, K**anda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa, ameeleza kufurahishwa na ushiriki wa kundi hilo, huku akisisitiza umuhimu wa kuzingatia elimu ya usalama barabarani waliyopewa.

Amesema ongezeko la ajali za barabarani linatokana na uzembe wa baadhi ya waendesha vyombo vya moto hivyo akataka kila mmoja kuwajibika ipasavyo kukomesha ajali hizo.

Amesisitiza kuwa utii wa sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani ni wajibu wa kila mtumiaji wa barabara huku akiwaonya dhidi ya makosa hatarishi k**a vile kuendesha bila kofia ngumu, kupuuza taa za barabarani, kubeba abiria zaidi ya mmoja, kuendesha bila leseni au mafunzo rasmi ya udereva.

"Makosa haya yamekuwa chanzo cha vifo na ulemavu kwa watumiaji wa barabara,” amesema K**anda Mutafungwa.

Aidha, amewakumbusha wananchi wa Mkoa wa Mwanza kuepuka kujihusisha na vurugu k**a zilizotokea tarehe 29 Oktoba 2025, akisisitiza kuwa matatizo yoyote ya kisheria yashughulikiwe kwa kufuata taratibu badala ya kujichukulia sheria mkononi.

“Kupitia elimu na ushirikiano, tumeweza kuzuia uhalifu mkubwa uliokuwepo awali,” amesema.

29/11/2025

“Tabia ya nikija kwenye ziara, maji yanatoka, nikiondoka yanakatika ikome” Waziri Aweso aionya DAWASA
“Sitakaa na mtendaji wa DAWASA anayefanya kazi kwa uzembe na kuichafua Sekta ya Maji, asiyetaka kufanya kazi atupishe” , Aweso ameonya.

Padri wa Kanisa la Anglican, Dikoni Edwin Achi, aliyetekwa pamoja na mkewe na binti yao Oktoba 28 katika jimbo la Kaduna...
29/11/2025

Padri wa Kanisa la Anglican, Dikoni Edwin Achi, aliyetekwa pamoja na mkewe na binti yao Oktoba 28 katika jimbo la Kaduna, ameuwawa baada ya kukaa takriban mwezi mmoja akiwa mateka, amesema Askofu Mkuu Henry Ndakuba. Mkewe na binti yao bado wanashikiliwa.

Vita vya watekaji nyara kaskazini mwa Nigeria vimeongezeka hivi karibuni, ikiwemo utekaji wa wasichana 25 jimbo la Kebbi na zaidi ya wanafunzi 300 na walimu kutoka shule ya Kikatoliki ndani ya jimbo la Niger.

Rais Bola Tinubu ameagiza mamlaka za polisi kuajiri askari 50,000 na kuahirisha safari zake za nje kupambana na hali hiyo.

Ndakuba ameitaka serikali na vyombo vya usalama kubaini na kufichua waliokuwa nyuma ya watekaji na kuomba haraka kuachiliwa kwa mke na binti wa Achi. Marekani pia imeonesha wasiwasi juu ya watekejaji na mauaji hayo.

Papa Leo XIV, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, ametembelea Msikiti wa Sultan Ahmed (Blue Mosque)—moja ya alama kubwa...
29/11/2025

Papa Leo XIV, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, ametembelea Msikiti wa Sultan Ahmed (Blue Mosque)—moja ya alama kubwa za historia ya Uturuki, uliojengwa kati ya 1609–1616.

Katika ziara hiyo, Papa aliungana na viongozi wa dini ya Kiislamu nchini humo na kusali akiwa ndani ya msikiti huo maarufu, hatua iliyoonekana k**a ishara ya amani, maelewano ya kidini na kuheshimiana.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Boniface Simbachawene ametoa wito kwa wananchi na hususani Vijana wa Tanza...
29/11/2025

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Boniface Simbachawene ametoa wito kwa wananchi na hususani Vijana wa Tanzania kudumisha amani na kuepuka kupanga, kuratibu ama kushiriki kwenye maandamano, akisema kwamba Tanzania bado inakabiliwa na athari kubwa zilizosababishwa na matukio ya Uvunjifu wa amani ya siku ya uchaguzi Mkuu na baada ya uchaguzi huo wa Oktoba 29, 2025.

Waziri Simbachawene amesema hayo usiku wa Ijumaa Novemba 28, 2025 katika burudani ya amani iliyofanyika kwenye Soko la Nyama Choma la Kumbilamoto, Kata ya Vingunguti wilayani Ilala mkoani Dar es Salaam akibainisha kuwa maandamano hayo yalisababisha vifo, uharibifu wa mali za serikali na mali binafsi pamoja na kusimama kwa shughuli za kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Simbachawene ameonya kuwa zipo taarifa za mipango ya maandamano mapya yanayotarajiwa kufanyika Desemba 9, 2025, akisisitiza kuwa Serikali haitaruhusu kutokea kwa vurugu nyingine na kuwaomba wananchi kutotumika na kuchochewa kurudia makosa yaliyopita.

Akirejea athari za maandamano ya Oktoba 29, Waziri Simbachawene amewataka vijana kufahamu gharama kubwa za uharibifu wa miundombinu, ikiwemo kuchoma vituo vya mabasi ya mwendokasi- mradi alioutaja kuwa umejengwa kwa ajili ya wananchi wasio na uwezo wa kumiliki magari. Amefafanua kuwa miradi hiyo inagharimiwa na kodi pamoja na mikopo ambayo vizazi vijavyo vitapaswa kuilipa.

Akizungumzia umuhimu wa amani, Waziri Simbachawene amesema Tanzania inaonekana kuonewa wivu kutokana na mafanikio yake, hivyo wananchi wanapaswa kuepuka kuvuruga misingi ambayo imeijengea nchi heshima na utulivu wa miaka mingi. Ameongeza kuwa baadhi ya majirani wa Tanzania wamekumbwa na migogoro kwa muda mrefu, akisisitiza kuwa wananchi wanapaswa kujifunza kutokana na changamoto za mataifa hayo.

“Na leo hii nilikuwa na mkutano mkubwa sana wa utatu kati ya Tanzania, Burundi na UNHCR (Shirika la kuhudumia wakimbizi duniani), tunafikiria namna ya kuwarudisha wakimbizi wale wa Burundi kurudi kwao maana wamekaa hapa karibu miaka 40…sasa tunafikiria warudi kwao kwa sababu masharti ya ukimbizi yameisha hawataki kuondoka, tunafikiria kutumia ushawishi wa nguvu ili waweze kuondoka. K**a wakimbizi hawataki kuo

29/11/2025

Sehemu ya Alichokisema Rais wa Shirikisho la Soka nchini TFF Wallace Karia ambaye ni rasmi katika uchaguzi Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) ambao unafanyika leo Jijini Dar es Salaam.

29/11/2025

Waislamu kutoka wilaya za Rufiji na Kibiti wamefanya ibada ya kuchinja wanyama na dua maalum kuelekea Mwenyezi Mungu, wakiuombea taifa la Tanzania kuondokana na mabalaa na vurugu. Ibada hii imefanywa kuashiria kuungana na malezi ya wazee wao ya kumwelekea Mungu kwa ajili ya amani na usalama.

Wakizungumza wakati wa dua na ibada ya kuliombea taifa, walisema lengo ni kuombea viongozi, hasa Rais, kupata nguvu ya kutatua matatizo ya taifa na kuhakikisha vurugu za kisiasa hazirudi. Pia, waliomba Mwenyezi Mungu awashughulikie wale wote waliokuwa sehemu ya machafuko ya uchaguzi, na kuondoa nguvu za uovu.

Waislamu hao wametoa wito wa umoja, kutokukengeushana, na kumtumainia Mwenyezi Mungu katika kujenga amani na mshik**ano wa taifa.

29/11/2025

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) ameitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kukamilisha Mradi wa Maji wa Msumi wenye thamani ya takribani Shilingi Bilioni 1.9 ndani ya miezi mitatu.

Waziri Aweso ametoa maelekezo hayo katika mkutano wa hadhara akihutubia wakazi wa eneo la Msakuzi, Wilaya ya Ubungo, jijini Dar es Salaam.

Waziri Aweso amesema kazi ya utekelezaji wa mradi huo ni lazima ifanyike kwa saa 24 ili ukamilike haraka na kumaliza kero ya huduma ya maji kwa wanachi.

Amemuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri kuidhinisha kiasi cha shilingi milioni 500 kwa DAWASA ndani ya siku saba ili kukamilisha kazi zilizobaki.

“Nikutie moyo Mbunge wa Jimbo la Kibamba, Mhe. Angela Kairuki mradi huu nitausimamia kwa karibu na tukimaliza vikao vya Bunge mwezi Februari, 2026 tunakuja wote kuuzindua”, Aweso amesema.

Katika ziara hiyo Waziri Aweso ameambatana na Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, ametoa kauli nzito akisisitiza kuwa anahitaji kiongo...
29/11/2025

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, ametoa kauli nzito akisisitiza kuwa anahitaji kiongozi atakayechaguliwa ndani ya Bodi ya Ligi (TPLB) awe mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi naye kwa ushirikiano, si chanzo cha migogoro.

Akizungumza kuhusu nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, ambayo kikanuni hukaimu pia nafasi ya Makamu wa Rais wa Pili wa TFF, Karia amesema kuwa ni muhimu kiongozi huyo awe na uwezo wa kuendana na mwelekeo wa shirikisho katika kusimamia na kuendeleza soka la Tanzania.

“Mniletee mtu ambaye anaweza kufanya kazi na mimi. Mwenyekiti wa Bodi ya TPLB kwa nafasi yake atakuwa Makamu wa Rais wa Pili wa TFF, hivyo nileteeni mtu anayeweza kufanya kazi na mimi, sio mtu atakayekuja kuvurugana na mimi,” amesema Karia.

29/11/2025

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Mhe. Peter Masindi, amesema mradi wa umeme unaozalishwa kwa nguvu ya jua ni kielelezo cha ongezeko la uzalishaji wa umeme nchini ikiwa ni dhamira ya Serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kutaka kuongeza uzalishaji umeme hadi kufikia jumla ya megawati 8000 ifikapo mwaka 2030.

Mhe. Masindi aliyasema hayo Novemba 28, 2025, alipoambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, kukagua maendeleo ya Mradi wa kuzalisha umeme wa jua unaotekelezwa wilayani humo.

Amesema mradi huo sio tu utakuwa na faida kwa wananchi wa Mkoa wa Sinyanga pekee bali hadi katika mikoa ya Jirani ambapo pia amesema zaidi ya wananchi 1,200 waliokuwa wakiendesha shughuli zao katika eneo la Mradi tayari wamelipwa fidia na kwamba jamii imeupokea mradi kwa mtazamo chanya na imekuwa mstari wa mbele kulinda miundombinu.

“Mradi huu ni tegemeo kwa wananchi wa Kishapu wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha miundombinu inalindwa. Wameuelewa Mradi na wanaufurahia," alisema Mhe. Masindi.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, ameeleza kuwa mradi huo ni miongoni mwa miradi ya kielelezo inayotakiwa kukamilika ndani ya siku 100 tangu kuapishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameelekeza kiasi cha shilingi bilioni 118 kwa ajili ya utekelezaji wake.

Vilevile, alimuagiza mkandarasi anayetekeleza mradi kuhakikisha unakamilika ifikapo Januari 15, 2026, akibainisha kuwa haitatolewa nyongeza ya muda na kwamba kinyume chake hatua za kisheria zitachukuliwa.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji limesema mwanamke anayesambazwa mitandaoni akidaiwa kutekwa na watu wanaodaiwa k...
29/11/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji limesema mwanamke anayesambazwa mitandaoni akidaiwa kutekwa na watu wanaodaiwa kujitambulisha k**a askari wa Kibiti, Winfrida Charles Malembeka, hajakumbwa na tukio la utekaji bali amek**atwa kwa tuhuma za kuchapisha na kusambaza taarifa za uchochezi na kuhamasisha vurugu kupitia mitandao ya kijamii.

Katika taarifa iliyotolewa Novemba 28, 2025 na K**anda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Protas Mutayoba, imeelezwa kuwa Winfrida alik**atwa katika maeneo ya Kibiti Mjini na kwa sasa anaendelea kushikiliwa na jeshi hilo mpaka taratibu za kisheria zikamilishwe.

“Anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuchapisha na kusambaza taarifa za uchochezi, kuhamasisha vurugu na maandamano tarehe 09/12/2025 kupitia mitandao ya kijamii akishirikiana na watu wengine”, imeeleza taarifa hiyo.

Aidha, jeshi hilo limetoa wito kwa wananchi kuepuka kuchapisha na kusambaza taarifa za kichochezi zinazoleta taharuki kwa jamii, likisisitiza kuwa halitasita kumchukulia hatua za kisheria mtu yeyote atakayebainika kufanya vitendo hivyo.

Watumishi wa Jeshi la Magereza mkoa wa Dodoma, tarehe 25 Novemba, 2025 wamepokea majiko ya gesi ya sahani mbili pamoja n...
29/11/2025

Watumishi wa Jeshi la Magereza mkoa wa Dodoma, tarehe 25 Novemba, 2025 wamepokea majiko ya gesi ya sahani mbili pamoja na mitungi yake ya kilo 15 zaidi ya 15,000 kutoka kwa Msambazaji; kampuni ya Lake Oil Tanzania ambapo ni uwezeshaji wa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) k**a sehemu ya jitihada ili kuchochea matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Akipokea majiko hayo pamoja na mitungi yake, kwa niaba ya Mkuu wa Gereza la Msalato mkoani Dodoma, Kaimu Mrakibu wa Gereza la Msalato; Tumaini Mgongo ameishukuru Serikali kwa kufikisha teknolojia za nishati safi ikiwemo majiko ya gesi ya sahani mbili pamoja na mitungi yake ya kilo 15 na kuongeza kuwa Askari na Watumishi wa Gereza la Msalato watayatumia na kuwa mabalozi wa nishati safi.

“Ninaahidi kwa niaba ya Watumishi wa Magereza kuwa, tutayatumia majiko haya na tutakuwa mabalozi kwa Wananchi wengi katika kutumia gesi k**a chanzo cha nishati safi ya kupikia, majumbani mwetu” alisema Kamishna Mgongo.

Kwa upande wake Mtaalam wa Nishati na Jinsia kutoka REA; Dkt. Joseph Sambali amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeendelea kuwezesha, kuhamasisha na kutoa elimu juu ya umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa Wananchi wakiwemo Watumishi wa Magereza ili kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa Mwaka 2024/2034 ambao unasisitiza angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.

“Tukio la leo ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia na ni matumaini yetu kuwa baada ya Serikali kusambazia Magereza majiko haya pamoja na mitungi ya gesi, watafikiwa Jeshi la Magereza pamoja na Taasisi zingine” alisema Dkt. Sambali.

REA kwa kushirikiana na Magereza wameendelea kuwafikia Watumishi wa Jeshi hilo ambapo, tarehe 25 Novemba, 2025 ilikuwa ni zamu ya Magereza mkoa wa Dodoma ambapo jumla ya majiko ya gesi ya sahani mbili na mitungi yake 15,068 imeanza kusambazwa mkoani humo ambapo usambazaji umezinduliwa rasmi katika Gereza la Msalato.

Address

Sinza Makaburini
Dar Es Salaam
1110111101(2)

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gilly Bonny Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share