JikoPoint

JikoPoint Chombo cha kwanza cha habari za mtandaoni kuhusu chakula na nishati safi ya kupikia.

Pata maujanja ya namna ya kutumia vifaa na nishati mbalimbali safi za kupikia kupitia kwenye mitandao ya kijamii na kwenye tovuti yetu.

30/04/2026

Virutubisho vina umuhimu mkubwa kwa mama mjamzito kwa sababu humsaidia kuwa na afya njema na kuhakikisha mtoto anayekua tumboni anakua vizuri.

Lishe bora humpa mama nguvu za kutosha, humkinga dhidi ya magonjwa na upungufu wa damu, na pia husaidia mwili wake kuhimili mabadiliko yanayotokea kipindi cha ujauzito.

29/04/2026

Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, ametoa wito kwa vijana, wanawake na wawekezaji nchini kuchangamkia kilimo cha tufaha, akieleza kuwa zao hilo lina fursa kubwa ya kiuchumi na uwezo wa kupunguza utegemezi wa matunda hayo kutoka nje ya nchi.

Chongolo amesema kwa muda mrefu Tanzania imekuwa ikiagiza tufaha kutoka nje licha ya kuwa na maeneo yenye uwezo mkubwa wa kuzalisha zao hilo kwa viwango vya kimataifa, hususan katika Kanda ya Kaskazini, Kati pamoja na Nyanda za Juu Kusini.

Hayo ameyasema Aprili 28, 2026 wakati akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2026/2027 bungeni jijini Dodoma.

Amesema hadi Machi 2026, Tanzania iliingiza kutoka nje takribani tani 1,481.98 za tufaha, hali inayoonyesha mahitaji makubwa ya zao hilo ndani ya nchi.

Kwa mujibu wa Chongolo, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imepanga kuhamasisha wakulima kuongeza uzalishaji wa tufaha katika mwaka wa fedha 2026/2027 ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na kuongeza mapato ya wakulima.

“Kilimo hiki si tu alama ya mabadiliko ya kifikra bali ni chanzo kipya cha kukuza uchumi wa mkulima mmoja mmoja, hususan vijana na wanawake, pamoja na kuliingizia Taifa fedha za kigeni,” amesema Chongolo.

29/04/2026

Tanzania imeendelea kuimarisha usalama wa chakula nchini baada ya kiwango cha utoshelevu wa chakula kufikia asilimia 130, hatua inayotokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya chakula pamoja na ukuaji wa sekta ya kilimo nchini.

Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, amesema hayo Aprili 28, 2026 wakati akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa Chongolo, uzalishaji wa mazao ya chakula katika msimu wa kilimo wa 2024/2025 umefikia tani milioni 23.78, kutoka tani milioni 22.8 zilizozalishwa katika msimu wa 2023/2024 ikiwa ni ongezeko la asilimia 4.3.

22/04/2026

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuwa baada ya kumaliza majukumu yake ya urais na kustaafu, atakuwa mlezi wa Umoja wa Babalishe na Mamalishe Tanzania (Umalita).

Rais Samia Suluhu Hassan ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Mamalishe na Babalishe lililofanyika jijini Dar es Salaam Aprili 21,2026.

22/04/2026

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mama na Baba Lishe Tanzania (Umalita), Julieth Malata, amewasilisha kilio cha wanachama wake mbele ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akitaja ukosefu wa mitaji na miundombinu mibovu k**a vikwazo vikuu vinavyokwamisha ustawi wa sekta hiyo nchini.

Malita aliyekuwa akizunguimza Aprili 22, 2026 katika hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Mama lishe na Baba lishe lililofanyika jijini Dar es Salaam, amesema upatikanaji wa mikopo yenye masharti nafuu bado ni kitendawili, hali inayowafanya wengi kushindwa kuendeleza biashara zao na kubaki katika lindi la umaskini licha ya mchango wao mkubwa katika uchumi wa nchi.

30/03/2026

Mbaazi ni mbegu ndogo ndogo za kijani zinazoliwa zinazopatikana kwenye kundi la Pisum.
Badala ya kula maandazi, chapati au mkate wakati wa asubuhi, basi wewe tumia mbaazi.
Kwa sababu mbaazi zina
1. Protini
2. Wanga
3. Nyuzinyuzi
4. Madini chuma
5. Magnesiamu, fosforasi na potasiamu
6. Folate (Vitamin B9)
7. Vitamini A na C

(Picha|Canva)

30/03/2026

Mbaazi ni mbegu ndogo ndogo za kijani zinazoliwa zinazopatikana kwenye kundi la Pisum.
Badala ya kula maandazi, chapati au mkate wakati wa asubuhi, basi wewe tumia mbaazi.
Kwa sababu mbaazi zina
1. Protini
2. Wanga
3. Nyuzinyuzi
4. Madini chuma
5. Magnesiamu, fosforasi na potasiamu
6. Folate (Vitamin B9)
7. Vitamini A na C

(Picha|Canva)

14/03/2026

Dk Omari Mwangaza, ambaye ni Daktari Mratibu wa Tiba na Magonjwa Yasiyoambukiza kutoka halmashauri ya manispaa ya kinondoni anaeleza kuwa ni muhimu kuzingatia aina ya mafuta yanayotumika katika mapishi ya vyakula.

Anaeleza kuwa mafuta yanayotumika kwenye biashara ni tofauti na yanayotumika nyumbani.

WHO yatoa mwongozo mpya wa lishe mashuleni kudhibiti unene uliopitilizaShirika la Afya Duniani (WHO) limetoa mwongozo mp...
28/01/2026

WHO yatoa mwongozo mpya wa lishe mashuleni kudhibiti unene uliopitiliza

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa mwongozo mpya wa kimataifa wa lishe mashuleni, unaoziitaka nchi wanachama kuimarisha mazingira ya lishe shuleni ili kudhibiti ongezeko la unene uliopitiliza na kukabiliana na changamoto ya utapiamlo kwa watoto.

Uzito au unene uliopitiliza hufafanuliwa k**a mkusanyiko usio wa kawaida au wa kupita kiasi wa mafuta mwilini ambao unaweza kuweka afya hatarini ikichangiwa zaidi na mtindo mbovu wa maisha, ulaji usiozingatia kanuni za afya na tabia bwete.

Takwimu za WHO zinakadiria kuwa mwaka 2024 takribani watoto milioni 35 walio chini ya umri wa miaka mitano duniani kote walikuwa na uzito uliopitiliza suala linaloweka afya zao rehani.

Hali ni mbaya zaidi kwa watoto na vijana milioni 188 wenye umri wa kwenda shule ambao waliripotiwa na WHO kuwa na unene uliopitiliza, sawa na mtoto mmoja kati ya 10, idadi iliyozidi kwa mara ya kwanza watoto wenye uzito pungufu.

WHO inapendekeza shule ziweke kanuni za lazima zitakazohamasisha upatikanaji wa vyakula vyenye afya. Picha/Canva.

Kutokana na uwepo wa changamoto hiyo, January 27, 2026, WHO ilitoa mwongozo wa lishe mashuleni utakaohakikisha vyakula na vinywaji vinavyotolewa shuleni, pamoja na vinavyopatikana katika mazingira yanayozunguka shule, ni vyenye afya na lishe bora.

“Uzito kupita kiasi na unene uliokithiri kwa watoto vinaendelea kuongezeka duniani, huku utapiamlo bado ukiwa changamoto ya kudumu. Shule ziko mstari wa mbele katika kukabiliana na mzigo huu maradufu wa utapiamlo,” inaeleza sehemu ya taarifa ya WHO.

Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus aliyekuwa akizunngumza alisema kuwa lishe shuleni ina athari ya moja kwa moja katika afya na maendeleo ya watoto.

“Chakula ambacho watoto hula shuleni kinaweza kuathiri uwezo wao wa kujifunza na kuwa na madhara ya muda mrefu kwa afya na ustawi wao. Lishe sahihi shuleni ni msingi wa kuzuia magonjwa baadaye maishani,” alisema.

Takribani mtoto mmoja kati ya 10 duniani ana unene uliopitiliza. Shule zinaweza kuwa sehemu ya kutatua tatizo hili. Picha/ Canva.

Katika muktadha wa kitaifa, baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania, tayari zina miongozo ya chakula cha shule inayolenga kuboresha lishe kwa wanafunzi kupitia Mpango wa Taifa wa Chakula Shuleni (NSFG).

Mpango huo unazingatia Sera ya Afya ya mwaka 2007, Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 na Mpango wa Taifa wa Sekta Jumuishi wa Miaka Mitano wa Utekelezaji wa Lishe 2016/17 hadi 2020/2.

Kwa mujibu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, utoaji wa huduma za chakula shuleni huchangia kuboresha afya ya wanafunzi, kupunguza utoro, kuongeza usikivu darasani na kuinua kiwango cha ufaulu.

WHO inakadiria kuwa zaidi ya watoto milioni 466 duniani hupata chakula kupitia programu za chakula shuleni jambo linaloimarisha afya ya akili na kuimarisha uwezo wao wa kimasomo.

Kuongeza vyakula vyenye afya na kupunguza vyenye sukari na mafuta yasiyo na afya ni hatua muhimu ya kuwalinda watoto. Picha/ Canva.

Hata hivyo, shirika hilo linaonya kuwa bado kuna upungufu wa taarifa kuhusu ubora wa lishe ya chakula hicho, hali inayoweza kusababisha changamoto za kiafya.

Katika mwongozo wake mpya, WHO inapendekeza shule ziweke kanuni za lazima zitakazohamasisha upatikanaji wa vyakula vyenye afya na kupunguza matumizi ya vyakula vyenye sukari nyingi, chumvi na mafuta yasiyo na afya, pamoja na kudhibiti mbinu za kibiashara zinazowalenga watoto.

Kwa sasa, nchi 104 zina sera za chakula chenye afya mashuleni huku karibu robo tatu zikiwa na vigezo vya lazima vya kuongoza muundo wa chakula cha shule huku nchi 48 pekee zikizuia matangazo ya vyakula vyenye sukari nyingi, chumvi au mafuta yasiyo na afya.

21/12/2025

From store to your door! Hivi ndivyo tunavyopeleka mzigo wako salama kila siku. December hii tunafanya delivery bure Dar es Salaam!

Karibu Jikosokoni tukuhudumie, piga simu namba 0677 088 088 kuweka oda yako au nunua kupitia WhatsApp Ghala 0744 419 420, kwa bidhaa zaidi tembelea tovuti yetu ya www.jikosokoni.co.tz.

20/12/2025

Sikukuu za mwisho wa mwaka ndio hizoo zimekaribia, je umejipangaje kudhibiti gharama za chakula na vinywaji zinazoweza kutumika msimu huu?

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na nukta Jikopoint kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka bei ya bidhaa nyingi za chakula na vinywaji hupanda zaidi suala linaloacha maumivu kwa watu wengi hususani wenye kipato cha kati.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when JikoPoint posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to JikoPoint:

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share