08/03/2026
Kiungo mahiri wa Simba SC, Yusuph Kagoma, ameongeza mkataba wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo yenye maskani yake Msimbazi.
Uongozi wa Simba Sports Club umeamua kumuongezea mkataba mchezaji huyo kufuatia kiwango kizuri anachoendelea kukionesha ndani ya kikosi hicho.
Hatua hiyo inaonesha wazi kuwa benchi la ufundi lina imani na mchango wa Kagoma katika mipango ya sasa na ya baadaye ya timu hiyo katika mashindano ya ndani na kimataifa.
Mashabiki wa Simba wana matumaini kuwa kuendelea kubaki kwa Kagoma kutaimarisha zaidi safu ya kiungo ya wekundu hao wa Msimbazi.
゚viralシfypシ゚viralシalシ